STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 20, 2012

ZUKU TZ NA MAXCOM WAJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA MALIPO 

 Meneja  Mkazi wa Zuku Tanzania, Fadhili Mwasyeba akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana wakati wa kutia saini makubaliano ya ushirikiano baina yao na kampuni ya Maxcom, kupitia huduma ya maxmalipo. Kulia ni Mwendeshaji Mkuu wa Kampuni ya Maxcom, Ahmed Lussasi.
Mwendeshaji mkuu wa Kampuni ya Maxcom, Ahmed Lussasi akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.
Mwendeshaji Mkuu wa Maxcom, Ahmed Lussasi akizungumza, hukui maafisa wenzake kutoka Zuku Tanzania wakimsikiliza.
Mwendeshaji Mkuu wa Kampuni ya MaxCom, Ahmed Lussasi, (kulia) akionesha mashine ya Maxmalipo  wakati wa mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa kutia saini makubaliano ya Ushirikiano na Kampuni ya Zuku Pay Tv, ambapo wateja wa Zuku watalipia ada zao za mwezi kupitia huduma ya Maxmalipo. Kushoto ni Meneja  Mkazi  Zuku Tanzania, Fadhili Mwasyeba.


KAMPUNI ya Wananchi Satellite Ltd inayomiliki televisheni ya kulipia ya Zuku kikishirikiana na kampuni ya Max Com zimeingia mkataba wa kuanza kutoa huduma rahisi ya malipo kwa wateja wa televisheni hiyo kwa nchi nzima kutumia huduma ya Maxmalipo.
Uzinduzi wa huduma hizo ulifanyika jana jijini Dar es Salaam baada ya viongozi wa pande hizo mbili kusaini mkataba huo mbele ya waandishi wa habari katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond, uliopo  Ubungo.
Meneja wa Wananchi Satellite kwa hapa nchini, Fadhili Mwasyeba alisema wameamua kurahisisha huduma ili kuwapa fursa wateja wao kufanya malipo kwa njia nyepesi na ya haraka tofauti na siku za nyuma kwa kutumia Maximalipo.
"Tuna furaha juu ya ushirikiano huo mpya na utakaowajali wateja wetu wa Zuku. Ahadi yetu ni kutoa ufumbuzi rahisi kwa wateja wetu wafanyabiashara na wauzaji na ufumbuzi huui utatuwezesha kufika mbali zaidi ya matarajio ya vwateja wetu." alisema.
Aidha Mwasyeba aliongeza kuwa wakati wakiwarahisishia unafuu wa kulipa malipo ya kila mwezi kwa wateja wao, pia kampuni yao inaendelea na promosheni yao ya kuwazawadia wateja wao iitwayo Zuku Tunakuthamini-Pata Tv Bure'.
Alisema kinachotakiwa kwa wateja kuwaunganisha wateja watano kujiunga na Zuku na kulipia malipo na kisha kujishindia runinga kati ya inchi 22 na wale watakaofikisha idadi ya wateja 10 watanyakua rungina ya inchi 42 na walioungwanishwa nao wakiambulia 'offer' nyingine zinazotolewa na kampuni yao kupitia promosheni hiyo.
Naye Msimamizi Mkuu wa kampiuni Maxcom, Ahmed Lussasi, alisema kuanza kutoa huduma hiyo kwa wateja wa zuku ni fursa ya kuwapa unafuu wateja wa televisheni hiyo popote walipo nchini kutokana na kampuni yao kuwa na vituo vya malipo ya Max malipo zaidi ya 3500 nchi nzima.
"Tunajitahidi kufanya kazi kwa ufanisi kwa malipo ya ushirikiano wa kipekee na zuku ili kuwafikia wateja kwa ukaribu zaidi," alisema na kuongeza;
Tuna furaha kufanya kazi na Zuku na tunaamini huu ni mwanzo tu wa ushirikiano wa kibiashara," alisema.
Televisheni ya Zuku inatoa uchaguziu mpana wa stesheni za burudani ikiwa ni pamoja na habari, michezo na sinema, majarida na muziki ikiwa imejumuisha chaneli za kimataifa kama BBC, MTV Base. Sentanta Sports, MGM Movies na nyinginezo ka gharama nafuu kwa ubora na kiwango cha hali ya juu.
 

No comments:

Post a Comment