STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 21, 2015

Ivory Coast, Cameroon Chupuchupu, wenyeji kujaribu tena leo

Vita ya Ivory Coast na Guinea ilikuwa hivi
Seydou Keita wa Mali akichuana na mchezaji wa Cameroon
MALABO, Guinea ya Ikweta
VIGOGO vya soka barani Afrika, Ivory Coast na Cameroon zimeanza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, Afcon 2015 kwa kuponea chupuchupu vipigo toka kwa wapinzani wao katika mechi zao tofauti za Kundi D, zilizochezwa kwenye uwanja wa Malabo, mjini Malabo.
Ivory Coast walicheza mapema na Guinea katika mechi ya Kundi D, walinusurika kipigo toka kwa Guinea wakiwa pungufu baada ya nyota wake, Gervinho kulimwa kadi nyekundu katika kipindi cha pili kwa kuchomoa bao dakika 18 kabla ya pambano lao kumalizika.
Guinea walionyesha kandanda safi wakiwabana nyota wa Ivory Coast walioongozwa na nahodha wake, Yaya Toure, Mchezaji Bora wa Afrika kwa mwaka wa nne mfululizo, walitangulia kupata bao dakika ya 36 kupitia kwa Mohammed Yattara.
Hata hivyo Ivory Coast ilipambana na kurejesha bao hilo dakika ya 72 kupitia mtokea benchi Seydou Doumbia na kuipa pointi moja muhimu kigogo hicho kilichokuwa kikipewa nafasi kubwa kushinda pambano hilo na miongoni mwa zinazopewa nafasi ya kubwa bingwa.
Katika pambano jingine lililofuata Cameroon ililazimika kusubiri hadi dakika ya 84 kuchomoa bao mbele ya wapinzani wao Mali waliokuwa wakiumana nao kwenye uwanja wa Malabo.
Shujaa wa Cameroon alikuwa ni beki Ambroise Oyongo aliyefunga bao la kusawazisha baada ya Mali kutangulia kupata bao katika dakika ya 71 kupitia kwa Sambou Yatabare.
Katika mfululizo wa michuano ya fainali hizo za 30, timu za kundi A leo zitashuka dimbani kuumana ambapo wenyeji Guinea ya Ikweta itakuwa dimbani kujiuliza na Burkina Faso, huku Gabon wakipepetana na Kongo wakati kesho kutakuwa na mechi za kukata na shoka kwa timu za Kundi B, Zambia kupepetana na Tunisia kabla ya Cape Verde kupepetana na DR Congo katika mechi zitakazochezwa kwenye uwanja wa Ebebiyin, mjini Ebebiyin.
Katika mechi za kwanza kwa timu za kundi hilo kila moja iliambulia sare ya bao 1-1, Zambia ikitoshana nguvu na DR Congo na Tunisia na Cape Verde zilishindwa kutambiana.
Ijumaa kutakuwa na mechi za kundi C ambapo Ghana itashuka tena dimbani mjini Mongomo kuumana na Algeria baada ya kutoka kupokea kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Senegal ambayo itashuka dimbani kucheza na Afrika Kusini.

Kocha Aston Villa asisitiza Benteke haendi kokote

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2012/11/27/article-2239412-163DB1CE000005DC-38_634x375.jpgMENEJA wa klabu ya Aston Villa, Paul Lambert amesema mshambuliaji wao nyota, Christian Benteke haondoki klabu hapo, hata kama kuna tatizo la ufungaji katika kikosi chake.
Klabu ya Villa ndfiyo timu yenye idadi ndogo ya magoli katika Ligi Kuu ya England na imekuwa ikidaiwa kuwa huenda ikaachana na Benteke ili kusajili mchezaji mwingine mkali wa kutatua tatizo jilo la ufungaji.
Hata hivyo, Lambert amesema kuwa hakuna mahali kokote mshambuliaji huyo atakapokwenda licha ya kikosi chake kushika nafasi ya 15 katika msimamo wa ligi pointi tatu juu ya eneo la hatari ya kushuka daraja.
Kikosi hicho cha Villa hakijafunga bao lolote katika mechi tano zilizopita za karibuni ikiwa na mabao 11 katika mechi 22 walizocheza, lakini Lambert amesema bado wanamhitaji Benteke.
Pia kocha huyo alimsifia Benteke akisema kuwa ni mmoja wa washambuliaji bora barani Ulaya na kwamba klabu yao haiwezi kumuacha kirahisi licha ya kasi yake ya kufumania nyavu kupungua baada ya kutoka kwenye majeraha.
Mshambuliaji huyo kutokla Ubelgiji, amefunga mabao mawili tu msimu huu katika mechi 13 alizoichezea timu yake na amekuwa akidaiwa kunyemelewa na baadhi ya klabu katika dirisha la usajili linaloendelea.

Ronaldo adaiwa kujituliza kwa Mtangazaji wa runinga

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo aliyetangaza kuachana na mpenzi wake wa muda mrefu mwanamitindo , Irina Shayk, amedaiwa kuangukia mikononi mwa kimwana mpya Mtangazaji wa kituo cha Televisheni chaHispania, Lucia Villalon.
Kwa mujibu vyanzo vya habari vya karibuni na mwanasoka huyo vinasema kuwa Mreno huyo aliyetoka kunyakua tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia (FIFA Ballon 'dOr) kwa mara ya pili mfululizo na tuzo ya tatu kwake kwa sasa anatoka na mtangazaji huyo.
Picha iliyomuonyesha Ronaldo akiwa na kimwana huyo wakipongezana mara baada ya nyota huyo kufanikiwa kunyakua tuzo hiyo ya Ballon d'Or akiwashinda Lionel Messi na Manuel Neuer, imedaiwa ndiyo chanzo cha hisia hizo kwamba huenda mtangazaji huyo ndiyo aliyeziba nafasi ya Irina, ambaye hakuhudhuria sherehe za utoaji wa tuzo hizo zilizofanyika nchini Uswisi.
Ronaldo alifichua juu ya tetesi ya kumwagana na Irina, aliyemudu naye katika mahusiano kwa miaka mitano na kueleza alikuwa anapaswa aache kuendelea na mambo yake baada ya tukio hilo la kumwagana na mwanamitindo huyo.
Hata hivyo vyombo vya habari vimedokeza, Ronaldo na Villalon wanatoka pamoja na ndiyo maana kimwana huyo mwishoni mwa wiki alitupia kwenye akaunti yake ya twitter ujumbe kuonyesha alikuwa akifuatilia pambano baina ya Getafe na Real Madrid lililoisha kwa Madrid kushinda mabao 3-0, mawili kati ya hayo yakifungwa na Ronaldo na jingine likitumbukizwa wavuni na Gareth Bale.

Jamie Carragher awaponda wachezaji Arsenal

http://images.dailystar-uk.co.uk/dynamic/1/photos/602000/620x/42602.jpg
Jamie Carragher
BEKI wa zamani wa klabu ya Liverpool, Jamie Carragher amewakosoa wachezaji wa Arsenal kwa kushangilia kwao baada ya kuichapa Manchester City kwa mabao 2-0 katika Uwanja wa Etihad Jumapili iliyopita.
Mabao yaliyofungwa na Santi Cazorla na Olivier Giroud yalitosha kuwapa Arsenal ushindi dhidi ya mabingwa hao wa Ligi Kuu kikiwa ni kipigo cha kwanza katika mechi 12 walizocheza.
Baada ya mchezo huo Aaron Ramsey na Alex Oxlade-Chamberlain wote walituma picha zikiwaonyesha wakishangilia katika mitandao ya kijamii jambo ambalo halijamfurahisha Carragher.
Carragher amesema haikatazwi kushangilia lakini sio timu nzima kama walivyofanya wakati hakuna taji lolote waliloshinda mpaka sasa hivyo anadhani wanapaswa kuacha.
 Carragher pia alishangazwa na aina ya mchezo uliotumiwa na meneja Arsene Wenger katika mchezo huo kwani alikuwa akizuia zaidi jambo ambalo sio kawaida yake kwani amezoea mchezo wa wazi.

Liverpool chupuchupu kwa Chelsea Kombe la Ligi

Eden Hazard comfortably stroked home a penalty in the 18th minute to give Chelsea the lead against Liverpool on Tuesday night
Eden Hazard akifunga bao la penati lililowapa uongozi Chelsea kabla ya Liverpool kulirejesha
Raheem Sterling celebrates after scoring a superb equaliser for the hosts in the 59th minute in the Capital One Cup semi-final
Raheem Sterling  akishangilia bao la kusawazisha la Liverpool
Lazar Markovic (left), Can and Gerrard appeal loudly after Diego Costa appeared to handle the ball in his own box
Wachezaji wa Liverpool wakilalamika baada ya Diego Costa (10) aliyekaa chini kuonekana kuushika mpira lanoni
BAO la dakika ya 59 lililofungwa na mshambuliaji Raheem Sterling liliiokoa Liverpool isiumbuke nyumbani baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, Chelsea katika pambano la kwanza la Nusu Fainali ya Kombe la Ligi (Capital One).
Katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Anfield, wenyeji walishtukizwa baada ya Chelsea kupata penati baada ya Eden Hazard kufanyiwa madhambi na beki Emre Can na mshambuliaji huyo kutoka Ubelgiji aliukwamisha wavuni mkwaju wa adhabu hiyo katika dakika ya 18.
Bao hilo lilidumu kipindi chote cha kwanza na kipindi cha pili kilipoanza wenyeji walionyesha kucharuka kusaka bao la kusawazisha na juhudi zao zilizaa matunda baada ya Sterling kusawazisha katika dakika ya 59 mbele ya msitu wa mabeki wa Chelsea na kuwapa nafuu 'vijogoo' hao ambao wataifuata Chelsea uwanja wao wa Stanford Bridge katika mchezo wa marudiano ya nusu fainali  wiki ijayo.
Katika pambano hilo mwamuzi Martin Atkinson alilalamikiwa na wachezaji wa Liverpool kwa kuwanyima penati baada ya Diego Costa kuonyesha kuushika mpira akiwa langoni mwa timu yake.
Mshindi wa pambano hilo atafuzu fainali kucheza na mshindi wa mechi ya nusu fainali ya pili kati ya timu ya Tottenham Hotspur  na Sheffield United inayotarajiwa kuchezwa leo katika mkondo wa kwanza kabla ya kurudiana tena Alhamisi ijayo.