STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 21, 2015

Liverpool chupuchupu kwa Chelsea Kombe la Ligi

Eden Hazard comfortably stroked home a penalty in the 18th minute to give Chelsea the lead against Liverpool on Tuesday night
Eden Hazard akifunga bao la penati lililowapa uongozi Chelsea kabla ya Liverpool kulirejesha
Raheem Sterling celebrates after scoring a superb equaliser for the hosts in the 59th minute in the Capital One Cup semi-final
Raheem Sterling  akishangilia bao la kusawazisha la Liverpool
Lazar Markovic (left), Can and Gerrard appeal loudly after Diego Costa appeared to handle the ball in his own box
Wachezaji wa Liverpool wakilalamika baada ya Diego Costa (10) aliyekaa chini kuonekana kuushika mpira lanoni
BAO la dakika ya 59 lililofungwa na mshambuliaji Raheem Sterling liliiokoa Liverpool isiumbuke nyumbani baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, Chelsea katika pambano la kwanza la Nusu Fainali ya Kombe la Ligi (Capital One).
Katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Anfield, wenyeji walishtukizwa baada ya Chelsea kupata penati baada ya Eden Hazard kufanyiwa madhambi na beki Emre Can na mshambuliaji huyo kutoka Ubelgiji aliukwamisha wavuni mkwaju wa adhabu hiyo katika dakika ya 18.
Bao hilo lilidumu kipindi chote cha kwanza na kipindi cha pili kilipoanza wenyeji walionyesha kucharuka kusaka bao la kusawazisha na juhudi zao zilizaa matunda baada ya Sterling kusawazisha katika dakika ya 59 mbele ya msitu wa mabeki wa Chelsea na kuwapa nafuu 'vijogoo' hao ambao wataifuata Chelsea uwanja wao wa Stanford Bridge katika mchezo wa marudiano ya nusu fainali  wiki ijayo.
Katika pambano hilo mwamuzi Martin Atkinson alilalamikiwa na wachezaji wa Liverpool kwa kuwanyima penati baada ya Diego Costa kuonyesha kuushika mpira akiwa langoni mwa timu yake.
Mshindi wa pambano hilo atafuzu fainali kucheza na mshindi wa mechi ya nusu fainali ya pili kati ya timu ya Tottenham Hotspur  na Sheffield United inayotarajiwa kuchezwa leo katika mkondo wa kwanza kabla ya kurudiana tena Alhamisi ijayo.

No comments:

Post a Comment