STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 11, 2013

SHANGWE ZA EID KUPAMBWA NA MASHAUZI CLASSIC


Kocha Wailes ampaisha Gareth Bale

http://www.scaryfootball.com/wp-content/uploads/2013/05/gareth-bale-and-ronaldo-real-madrid-transfer-2013-zidane.png
bale akiwa amebebwa na Ronaldo
KOCHA wa timu ya taifa ya Wales, John Toshack alizungumza na kituo cha radio cha 'La Xarxa' cha Hispania kuhusu mchezaji wake Gareth Bale na akasema kwamba nyota huyohayuko mbali sana na ubora walionao Cristiano Ronaldo na Lionel Messi.
Alisema: "Sitaki kuingia katika mijadala kuhusu thamani yake, lakini ninaloweza kusema sasa ni kwamba Bale hayuko mbali sana na matawi aliyopo Cristiano Ronaldo na Messi."
Toshack pia alisema winga huyo wa zamani wa Tottenham hahusiki kwa lolote katika kiwango kikubwa cha pesa kilicholipwa ili kumhamishia Real Madrid, akisema: "Mchezaji si wa kulaumiwa kwa ada ya euro milioni 100 iliyolipwa ili kumsajili. Kama klabu mbili husika zimeafikiana bei hiyo, hayo ni makosa yao."
Pia aliwataka watu wawe wavumilivu kwa nyota huyo ili azoee mazingira mapya. "Alikuwa na bahati mbaya hakujifua katika kipindi cha kujiandaa na msimu, kutokatana na mvutano uliokuwapo baina ya Tottenham na Real Madrid, lakini Bale ni mchezaji mzuri. Hakuna sababu yoyote ya kutilia shaka uwezo wa Gareth Bale, nawahakikishia," alisema kwa kujiamini.
Kocha huyo wa Wales pia alizungumzia hali ya vipaji vinavyoibukia Real. "Kwa mfano watu kama Illarramendi, Isco au wachezaji yosso wa El Castilla (Real Madrid B), kama wakiangalia benchi la Ancelotti na Zidane linaleta matumaini. Kwa sasa ni wakati mgumu kwao kwa sababu Barcelona wanafanya vyema, huku Madrid wakiwa nyuma yao kwenye msimamo, lakini wanahitaji kupewa muda,” alisema kocha huyo Wales.