STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 13, 2010

Cheka, Maugo kumaliza Ubishi Dar






MABONDIA Francis Cheka 'SMG' na Mada Maugo 'King Maugo Jn' wanatarajia kumaliza ubishi baina yao watakapopigana kwenye ukumbi wa PTA jijini Dar es Salaam badala ya uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro.
Mratibu wa pambano hilo, Kaike Siraju, aliiambia MICHARAZO mapema leo kuwa, pambano la wababe hao wawili litafanyika Dar na sio Morogoro kama alivyokuwa akitaka iwe na kuingia kwenye mzozo na Mada Maugo.
Maugo, anayeshikilia taji la ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, alitishia kutopigana na Cheka kama pambano hilo lingehamishiwa Morogoro.
Siraju, alisema wameangalia mambo mengi kabla ya kusitisha uamuzi wa kulibakisha pambano hilo Dar na kueleza kuwa maandalizi kwa ujumla yanaendelea vema ikiwemo mabondia wote kuendelea kujifua.
"Maandalizi ya pambano la Cheka na Maugo, yanaendelea vema na litafanyika Dar kama ilivyokuwa awali, baada ya jaribio la kulihamishia Moro kushindikana," alisema Siraju.
Siraju alisema pambano hilo la uzani wa Middle la raundi nane lisilo la kuwania Mkanda litakalofanyika Januari Mosi, mwakani, likisindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi.
Mratibu huyo aliitaja michezo ya utangulizi siku hiyo ni pamoja na pambano kati ya Mshihiri Kidira atakayezidunda na Deo Njiku, Jafari Majid dhidi ya Juma Afande na Hussein Mbonde atakayezichapa na Cosmas Cheka.
Michezo mingine ni ile ya Simba wa Tunduru ataonyeshana kazi na Albert Mbena, Arafati ‘Ngumi Jiwe’ atapambana na Juma Kihio wakati Sadik Momba atafunga kazi na Smoo Njiku.
Michezo yote hiyo inasimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO na ni maalum kwa kukata mzizi wa fitina baina ya mabondia hao wanaotambiana kila mmoja akitamba ni bora kuliko mwenzie.

Mwisho

BREAKING NEWS-DK REMMY IS NO MORE


MWANAMUZIKI maarufu nchini aliyewahi kutamba na bendi za Makasy na Super Matimila kabla ya kuhamia kwenye muziki wa Injili, Ramadhani Mtoro Ongalla 'Dk Remmy' amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa tatizo la Ini, bado tunafuatilia kujua taratibu za mazishi yake.
Dk Remmy atakumbukwa kwa vibao vyake matata kama Nataka Mtoto, Siku ya Kufa, Muziki Sio Uhuni, Mambo kwa Soksi, Mrema, Mariam, Mwanza na kadhalika....!
Mungu Ilaze Roho ya Marehemu Mahali Pema. Amin