STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 21, 2014

Matokeo ya Kidato cha Nne 2013 yatangazwa

Kaimu Katibu Mkuu wa baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dk. Charles Msonde akisoma matokeo ya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2013 Dar es Salaam jana. 


Idadi ya ufaulu mtihani kidato cha nne mwaka jana  imeongezeka kutoka 185,940  hadi kufikia 235, 225, ikilinganishwa na mwaka 2012.
Vile vile watahiniwa 151,187 kati ya 404,083 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana wamepata ‘divisheni’ ziro.

Hata hivyo,  idadi ya waliopata daraja sifuri imepungua ikilinganishwa na mwaka 2012 ambapo wanafunzi 240,903 kati ya 397,132 waliambulia daraja hilo na kusababisha hamaki iliyoshinikiza viongozi wa sekta ya elimu kuwajibishwa.

Matokeo hayo yalitangazwa jana jijini Dar- es- Salaam na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la  Mitihani (Necta), Dk. Charles Msonde, aliyeongeza kuwa idadi ya ufaulu kwa mwaka jana ilipanda ikilinganishwa na mwaka 2012.

Ongezeko hilo la watahiniwa 49,285 waliofaulu zaidi mwaka huo, limefanya kiwango cha ufaulu kupanda kwa asilimia 58.25 ikilinganishwa na hali ilivyokuwa  mwaka 2012.

“Jumla ya watahiniwa  404,083 sawa na asilimia 94. 48 waliofanya mtihani huo, wanafunzi 151,187 ambao ni  asilimia 42.91 walishindwa mtihani.” Alisema Dk. Msonde na kuongeza kuwa wasichana waliofaulu ni 106,792 sawa na asilimia 56.73,  wavulana ni 128,435 sawa na asilimia 59.58.

Watahiniwa  waliofaulu  moja kwa moja kutoka shuleni ni 201,152 sawa na asilimia 57.09, wasichana wakiwa 90,064 sawa na asilimia 55.49 na wavulana ni 111,088 sawa na asilimia 58.45.

Alisema idadi ya wanafunzi  wa kujitegemea ilikuwa   34,075 sawa na asilimia 66.23 ikilinganishwa na  ya mwaka 2012 ambao idadi yao ilikuwa 2,619.

Watahiniwa wa mtihani wa Maarifa(QT), waliofaulu ni 6,529 sawa na asilimia ikilinganisha na watahiniwa 5,984  wa  mwaka 2012.

Akitangaza matokeo hayo mbele ya wanahabari alisema watahiniwa  walioandikishwa kufanya mtihani huo mwaka jana walikuwa 427,679, kati yao wasichana ni  199,123 sawa na asilimia 46.56.

Wavulana walikuwa ni 228,556 sawa na asilimia 53.44, huku watahiniwa wa shule wakiwa 367,163 na watahiniwa wa kujitegemea wakiwa 60,516.

Alisema kati ya watahiniwa 427,679 waliosajiliwa kufanya mtihani huo, 404,083 sawa na asilimia 94.48 walifanya mtihani huo na watahiniwa 23,596 sawa na asilimia 5.52 hawakufanya mtihani huo.

Kwa watahiniwa wa shule 367,163 waliosajiliwa , 352,614 sawa na asilimia 96.04 walifanya mtihani, wasichana wakiwa 162,412 sawa na asilimia 96.07 na wavulana ni 190,202 sawa na asilimia 96.0.

Pia alisema watahiniwa 14,549 sawa na asilimia 3.96 hawakufanya mtihani.

Aidha aliongeza kuwa kwa upande wa watahiniwa wa kujitegemea 60,516 waliosajiliwa  kufanya mtihani huo, 51,469 sawa na asilimia 85.05 walifanya mtihani huo, na watahiniwa  9,047 sawa na asilimia 14.95 hawakufanya mtihani.

Alisema  kwa  watahiniwa  18,217 wa mtihani wa maarifa (QT),  waliosajiliwa, 15,061 sawa na asilimia 82.68 walifanya mtihani huo na 3,156 sawa na asilimia 17.32 hawakufanya mtihani.

Kwa upande wa ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja , alisema kwa watahiniwa wa shule unaonyesha kuwa jumla ya watahiniwa 74,324 sawa na asilimia 21.09 wamefaulu katika daraja la I hadi la III wakiwamo wasichana 27,223 sawa na asilimia 16.77 na wavulana 47.101 sawa na asilimia 24.

Dk. Msonde alisema takwimu za matokeo zinaonyesha kuwa ufaulu katika masomo yote umepanda kwa asilimia kati ya 0.61 na 16.72 ikilinganishwa na mwaka 2012.

Alisema watahiniwa wamefaulu zaidi masomo ya Kiswahili kwa asilimia 67.77 na somo ambalo wamefaulu kwa kiwango cha chini ni Hesabu kwa asilimia 17.78.

Kwa mujibu wa Necta wanafunzi waliong’ara ni Robina Nicholaus, Sarafina Mariki, Abby Sembuche   na  Janeth Urassa  wa Sekondari ya Wasichana ya Marian.

Wengine ni  Magreth Kakoko na Angel Ngulumbi wa   St. Francis, Joyceline Marealle wa Sekondari ya  Canossa,   Sunday Mrutu  wa Sekondari ya Anne Marie,  Nelson Rugola na Emmanuel Mihuba Sekondari ya  Kaizirege .

Kadhalika, shule zilizofanya vizuri zaidi  na kuingia katika kumi bora  katika kundi la shule zenye watahiniwa 40 ni  shule ya wasichana ya St. Francis, Shule ya wavulana na Marian, shule ya wasichana ya Feza, shule ya Precious Blood, Canossa, Shule ya wasichana ya Marian, shule ya wasichana ya Anwarite, Abbey, Rosminini na Shule ya Seminari ya Don Bosco.

KUANGALIA MATOKEO YA MITIHANI


Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) uliofanyika Novemba 2013 unaweza kuyaona kwa  kubofya hapa MATOKEO

Golden Bush, Pugu Veterani kuonyeshana kazi kesho

Wazee wa 'dozi' Golden Bush Veterani
BAADA ya kimya cha muda mrefu, wakali wa soka la maveterani, Golden Bush kesho inatarajiwa kushuka dimba la Kines majira ya asubuhi kuvaana na wazee wenzao, Pugu Veterani katika mchezo wa kirafiki.
Golden Bush ambayo imekuwa ikiwasasambua wapinzani wao kwa vipigo kikubwa, mechi hiyo ya kesho dhidi ya Pugu ni kama marudiano kwani walishakutana mwishoni mwa mwaka jana na mchezo kushindwa kumalizika kutokana na kugotokea fujo, huku Pugu wakiwa wamepigwa kimoja.
Kwa mujibu wa Msemaji wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' katika pambano hilo wanatarajia kuwashikisha adabu wapinzani wao.
Ebu soma tambo wa wakali hao hapo chini mwenyewe;
Hi Wadau
 
Kwa muda mrefu kidogo nimekuwa kimya kwasababu ya majukumu ya kila siku ambayo kwa namna moja ama nyingine ilikuwa taabu kupata nafasi ya kuto matokeo huku ukizingatia kwamba timu yetu sasa hivi imekuwa ikitoa vipigo vya goli kuanzia 5 kwenda mbele. Ukipona sana 4.
 
Kesho vijana watukutu kutoka Pugu wakiongozwa machezaji mwenye maneno mengi Sele Thomas watakuwa wageni wetu katika uwanja wa St James Park, ikumbukwe game ya mwisho tuliwafunga goli moja lakini mpira uliisha dakika ya 88 pale walipoanzisha vurugu na kutuharibia game yetu. Kesho tumejipanga umpya ili kuhakikisha tunawakoma kwa kuwapa goli nyingi kama wenzao wa Stakishari walipigwa 6, Kigogo fresh 5, Mtongani 9, Mwanyamala 5 na wengine ambao siwakumbuki lakini wek kwenye akili yako kuwa walifungwa sichini ya goli 4 au 5.
 
Baada ya game hiyo huenda tukawapata ndugu zetu ambao tumewatafuta kwa muda mrefu sana, Survey Veterans siku ya jumapili inayofuata. Game hii itakuwa na umuhimi wa pekee kabisa kwasababu tunataka tuwapige goli za mwaka mzima ili wakikataa kucheza tunakuwa na hakiba ya ushindi kibindoni, hawa jamaa nina hamu nao Survey! We acha tu.
Njooni wewe, mjomba wako na shangazi yako uone football ya kesho kuanzia saa mbili kamili asubuhi

Twiga Stars, Zambia sasa kukipiga mapema

MECHI ya pili ya Raundi ya Kwanza kuwania Kombe la Afrika kwa Wanawake (AWC) kati ya Tanzania (Twiga Stars) na Zambia (Shepolopolo) sasa itachezwa Februari 28 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam. Twiga Stars tayari ipo kambini kujiandaa kwa mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni. Twiga Stars chini ya Kocha Rogasian Kaijage inafanya mazoezi yake kwenye Uwanja wa Karume ambao ni wa nyasi za bandia kama ulivyo ule wa Azam Complex.
Shepolopolo iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mechi ya kwanza iliyochezwa Februari 14 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nkoloma jijini Lusaka.
Iwapo Twiga Stars itafanikiwa kuiondoa Shepolopolo itacheza na mshindi wa mechi kati ya Botswana na Zimbabwe. Zimbabwe ilishinda mechi ya kwanza ugenini.
Wachezaji wa Twiga Stars waliopo kambini ni Amina Ali, Anastazia Katunzi, Asha Rashid, Donisia Minja, Esther Chabruma, Etoe Mlenzi, Everine Sekikubo, Fatuma Issa, Fatuma Makusanya, Fatuma Mustafa, Fatuma Mwisendi, Fatuma Omari, Flora Kayanda, Happiness Mwaipaja, Maimuna Mkane, Mwajuma Abdallah, Mwapewa Mtumwa, Pulkeria Charaji, Sherida Boniface, Sophia Mwasikili, Therese Yona, Vumilia Maarifa na Zena Said.

Michuano ya kusaka vipaji kuanza kesho

MICHUANO ya mikoa katika mpango maalumu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuboresha Taifa Stars inaanza kutimua vumbi kesho (Februari 22 mwaka huu) kwa mechi nne.
Mechi rasmi ya ufunguzi wa michuano hiyo inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwa kati ya Ilala na Temeke. Mechi hiyo ya kundi G itachezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kuanzia saa 9.30 alasiri.
Kundi A kutakuwa na mechi kati ya Pwani na Morogoro kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi wakati Kusini Unguja na Kaskazini Unguja zitacheza kwenye Uwanja wa Mao Tse Tung mjini Unguja katika kundi H.
Kusini Pemba na Kaskazini Pemba zitacheza mechi ya Kundi I katika Uwanja wa Gombani kisiwani Pemba.
Mechi za keshokutwa (Februari 23 mwaka huu) ni Simiyu itacheza na Shinyanga mjini Bariadi katika kundi E. Nayo Ruvuma itacheza na Njombe kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea katika kundi D.
Kundi C ni Tanga na Kilimanjaro kwenye Uwanja wa Mkwakwani wakati Kagera itacheza na Geita kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba katika kundi B. Mtwara itacheza na Lindi kwenye Uwanja wa Nangwanda mjini Mtwara katika kundi F.
Wang’amuzi 40 wa vipaji tayari wamesharipoti kwenye vituo vya mechi hizo kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.

Yanga, Ruvu Shooting kesho kiama, mtanange wa Azam wapelekwa mbele

Yanga watakaovaana na Ruvu Shooting kesho
Azam baada ya kung'oka Kombe la Shirikisho wenyewe watashuka dimbani Jumapili badala ya kesho kama ratiba ilivyokuwa inaonyesha
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inaingia Raundi ya 19 kesho (Februari 22 mwaka huu) kwa mechi tano zitakazochezwa katika miji ya Dar es Salaam, Bukoba, Morogoro, Tanga na Arusha.
Yanga itakuwa mgeni wa Ruvu Shooting ya mkoani Pwani katika mechi itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Nayo Kagera Sugar inaikaribisha Rhino Rangers ya Tabora katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Uwanja wa Manungu uliopo Turiani mkoani Morogoro ndiyo utakaotumika kwa mechi kati ya Mtibwa Sugar na Ashanti United, wakati Coastal Union itaumana na Mbeya City katika mechi itakayooneshwa moja kwa moja na Azam Tv kutoka Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Maafande wa Oljoro JKT watakuwa nyumbani kupambana na Mgambo Shooting katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha.
Jumapili (Februari 23 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa ni Simba dhidi ya JKT Ruvu, mechi ambayo pia itaoneshwa moja kwa moja na Azam Tv.
Mechi kati ya Azam na Tanzania Prisons iliyokuwa ichezwe kesho (Februari 22 mwaka huu) Uwanja wa Chamazi sasa itachezwa Jumapili (Februari 23 mwaka huu) ambapo na itakuwa ‘live’.
Ligi hiyo itaendelea Jumatano (Februari 26 mwaka huu) kwa mechi moja kati ya Ashanti United na Azam itakayochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex (Chamazi).

Spurs wafa ugenini, Juve, Valencia zikitakata Ueropa League

 

WAKATI Tottenham Hotspur ikilazwa ugenini na timu ya Dnipro ya Ukraine, Juventus wameifumua Trabzonspor kwa mabao 2-0 na kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga 16 Bora ya Ligi Ndogo ya Ulaya (Europa League).
Spurs ambayo ilipoteza mkwaju wa penati uliopigwa na nahodha wake Michael Dawson ambao huenda ungewasaidia kupata sare ugenini na kuwa na kazi nyepesi kwenye mechi ya marudiano dhidi ya wapinzani wao, walifungwa bao hilo la pekee kwenye dakika ya 81 kwa mkwaju wa penati.
Penati hiyo ilitumbukizwa kimiani na Yevhen Konoplyanka na kuifanya Spurs kuwa na kazi ya kuhakikisha wanashinda mechi ya nyumbani wiki ijayo kama inataka kufuzu 16 Bora.
Katika mechi nyingine, mabingwa wa Italia waliotupwa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa, Juventus iliifumua Tarbzonspor kwa mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa mjini Turin, Italia.
Mabao ya Dani Osvaldo la dakika ya 15 na jingine la lala salama ya mchezo huo kupitia kwa Paul Pogba yaliipa uhakika Juve kuwa na kazi nyepesi kwenye mechi ya marudiano ugenini wiki ijayo.
Nayo timu ya Lazio ya Italia walipata kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Ludogorets ya Bulgaria, huku Eintracht Frankfurt  ya Ujerumani ikitoka nyuma kwa mabao mawili na kupata sare ya 2-2 dhidi ya Porto ya Ureno.
Mabao ya Ricardo Quaresma na Silvestre Varela ya kila kipindi yaliipa uongozi Porto kabla Joselu  kufunga bao moja na Alex Sandro kuisaidia wageni toka Ujerumani kwa kujifunga dakika ya 78.
Fiorentina ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Esbjerg, Sevilla ikitoka sare ya 2-2 na Maribor nayo Shakhtar Donetsk ikipata sare ya 1-1 dhidi ya Viktoria Plzen, huku Rubin Kazan waliocheza pungufu  ya mchezaji mmoja ugenini iliambulia sare ya 1-1 dhidi ya wenyeji wa Real Betis. Wageni walimpoteza nyota wao Alexander Prudnikov aliyetolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 28.
Benfica ilishinda 1-0 dhidi ya PAOK Salonika, huku  AZ Alkmaar ikishinda kama hivyo mbele ya Slovan Liberec, nazo timu za  Chornomorets na Lyon, Anzhi Makhachkala na Genk zikitoka suluhu ya kutofungana katika mechi zao mbili tofauti huku Valencia wenyewe walipata ushindi wa 2-0 dhidi ya Dynamo Kiev.