MSHAMBULIAJI wa KImataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic amekuwa akihusishwa na kutaka kutua Manchester United ili kuungana na Kocha wake wa zamani, Jose Mourinho, lakini wakala wake wamesema klabu atakayojiunga nayo itashangaza wengi.Wakala wa mchezaji huyo, Mino Raiola, alisema Straika huyo ambaye mkataba wake na PSG imeisha hakuna anayejua atatua wapi na hivyo mashabiki wasubiri kushtukizwa tu.
Nahodha huyo wa Sweden mwenye miaka 34, kwa sasa anaendelea na maandalizi ya kuiongoza timu yake katika michuano ya Fainali za Kombe la Ulaya itakayoanza Juni 10 nchini Ufaransa.
"Sidhani kama atajiunga na United, na wala hakuna anayelala Sweden kwa sasa hakuna anayejua kitakachotokea," alisema Raiola.
Wakala huyo alisema bila shaka mwisho wa yote watu watashangazwa na maamuzi ya mkali huyo kwa klabu atakayojiunga nayo kwa msimu ujao.
"Bado hatuajamua, lakini itashangaza wengi mwishowe. Watu wanazungumza kuhusu United, ila ukweli utafahamika tu na ndio maana hatusemi mengi kwa waandishi wasubiri waone wenyewe," alisema wakala huyo.

KLABU YA Tottenham Hotspur imetangaza kuwa itacheza mechi zake za Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani kwenye Uwanja wa Wembley.
WAKALA wa beki kisiki wa Barcelona, Dani Alves amekanusha taarifa kuwa mteja wake amesaini mkataba wa awali na Juventus, japo amekiri kuwa mabingwa hao wa Italia na klabu nyingine zinamwinda mchezaji huyo.
Benitez Akisaini Mkataba huo wa kumweka Newcastle United Miaka 3
Wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari juu ya kuongeza Miaka 3 kuifundisha Klabu hiyo ya Newcastle United
Kwenye Mkutano na Waandishi huko St. James Park




