STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 9, 2015

Barcelona wapaa kileleni kwa kuua 6, Messi apiga 'hat-trick' ya 24

Messi akifurahia kufunga baio
Messi akifanya vitu vyake
Messi ni shiida
Akijiandaa kufunga penati iliyozaa bao lake la kwanza
Barcelona wakipongezana
Suarez akishangilia bao lake

MSHAMBULIAJI Nyota wa Argentina, Lionel Messi alifunga hat trick ya 24 ya La Liga, huku Luis Suarez akifunga mabao mawili wakati Barcelona wakiizamisha Rayo Vallecano.
Ushindi huo umeifanya Barcelona kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Hispania, La Liga wakiishusha Real Madrid ambayo Jumamosi ilifungwa ugenini na Deportivo la Coruna.
Barcelona walianza kuandika bao la kwanza dakika ya tano kupitia kwa Luis Suarez akimalizia kazi nzuri ya Xavi kabla ya Gerrard Pique kufunga la pili dakika ya 49.
Messi alianza kuandika karamu yake ya mabao kwa kufunga bao la tatu la Barcelona kwa mkwaju wa penati dakika ya 56 kabla ya kuongeza jingine dakika ya 63 na 68.
Bao la sita la Barcelona lilifungwa dakika za lala salama na Suarez akimaliza kasi nzuri ya Messi.
Rayo Vallecano walipata bao lao la pekee la kufutia machozi katika dakika ya 81 kwa mkwaju wa penati kupitia Bueno.

Arsenal, Man Utd ni vita tupu leo FA, Liverpool yabanwa

http://soccer.indonewyork.com/wp-content/uploads/2015/03/mufc-arsenal-fa-cup-3-15.jpegLONDON, England
TIMU za Manchester United na Arsenal leo zinakutana katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la FA.

Tayari kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amekiri kuwa mchezo huo utakuwa mgumu kutokana na uzoefu wa timu hizo katika mashindano hayo. Timu hizo ndizo zilizotwaa taji hilo mara nyingi.

Wenger alisema anaamini timu itakayoibuka na ushindi leo ndio itakuwa bingwa wa kombe hilo.

Mchezo huo utapigwa kuanzia saa 4:45 usiku kwa majira ya Afrika Mashariki.

“Ninauona huu ni mchezo mgumu na utakaotoa sura halisi ya ubigwa hasa ikizingatiwa kuwa atakayeibuka mshindi ndiye anayeweza kutwaa taji hili mwishoni, “alisema kocha huyo.

Aidha, nahodha wa Manchester United, Wayne Rooney atacheza mchezo huo huku akiwa na kumbukumbu ya mataji tisa, lakini katika vikombe hivyo, halipo la FA.

Rooney akiwa na timu hiyo mwaka 2005 wakati timu yake hiyo ilipocheza na Arsenal pamoja na mwaka 2007 ilipocheza na
Chelsea, haikuweza kushinda kombe hilo.

“Kwa miaka mingi hatujafikia hatua ya kucheza fainali kwa mchezo huu tunaweza kuondoa gundu na kufikia fainali kirahisi na kulitwaa taji hilo, ”alisema alisema Rooney.
Katika mechi nyingine ya michuano hiyo iliyochezwa usiku wa kuamkia leo, Liverpool ilibanwa nyumbani na Blackburn na sasa watarudiana kupata mshindi wa kuungana na timu ya Aston Villa iliyotangulia kwa kuilaza West Bromwich Albion.

Simba waitafuna Yanga Taifa, Okwiiiiii aleta maafa

Okwi (25) akishangilia bao na wachezaji wenzake

Raha ya ushindi
Elias Maguli akimtoka beki wa Yanga aliyeanguka
Na Rahma Junior
BAO pekee la kiufundi lililofungwa na Emmanuel Okwi katika dakika ya 51 limeiwezesha Simba kuizima Yanga katika pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara.
Okwi, raia wa Uganda alifunga bao hilo baada ta kupenyezewa pande safi na Ibrahm Ajibu na kumchungulia kipa Ally Mustafa Barthez aliyekuwa ametoka eneo lake la kujidai na kupiga 'mashine' ya umbali wa mita 27 na kuiandikia Simba bao hilo.
Bao hilo liliwafanya wapenzi wa Yanga kulala mapema na kuwafanya viongozi na wanachama wa Yanga waliokuwa wakitamba mapema kwamba Simba si saizi yao kuzima simu zao.
Ushindi huo umeifanya Simba kuendelea kuwatesa Yanga ambao walitoka kuwtaungua kwenye mechi ya Nani Mtani Jembe 2 Desemba mwaka jana.
Simba imefikisha pointi 26 kwa ushindi huo na kushika nafasi ya tatu ikiwaengua Kagera Sugar, japo Yanga wanaendelea kuongoza msimamo wakiwa na pointi 31, moja zaidi ya Azam waliopo nafasi ya pili.
Dalili za Simba kuitambia Yanga zilianza kuonekana mapema kwenye uwanja wa Taifa, baada ya timu yao ya vijana U20 kuwanyuka wa Yanga mabao 4-2.
Katika mchezo huo Haruna Niyonzima alitolewa uwanjani kwa kadi Nyekundu baada ya kupewa kadi ya njano ya pili kwa kupiga mpira huku filimbi ya mwamuzi Martin Saanya wa Morogoro, ikiwa imepulizwa. 
Vikosi vilikuwa hivi:
SIMBA SC: Ivo Mapunda, Kessy Ramadhan, Mohhamed Hussein, Hassan Isihaka, Juuko Murshid, Abdi Banda/Simon Sserunkuma, Ramadhani Singano, Jonas Mkude, Ibrahim Ajib/ Elias Maguli, Said Ndemla na  Emanuel Okwi.
YANGA SC: Ally Mustafa,Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub, Kelven Yondani, Said Juma, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Amis Tambwe, Mrisho Ngassa/ Khap Sherman na Danny Mrwanda/ Hussein Javu.

AIBU! Mtoto mwingine albino akatwa kiganja Rukwa

http://ak2.picdn.net/shutterstock/videos/3573986/preview/stock-footage-close-up-of-bloody-knife-with-blood-dripping.jpg 
MATUKIO ya Ukatili dhidi ya albino yanaendelea kuwa tishio nchini Tanzania baada ya mtoto wa miaka sita kukatwa kiganja cha mkono.
Shambulio hilop jipya limetokea mkoani Rukwa kusini magharibi mwa nchi hiyo.
Mtoto huyo kiume Baraka Cosmas alikuwa amelala na mama yake mzazi wakati wahalifu hao walipovamia nyumba yao.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Rukwa Jackob Mwaruanda amesema kwa sasa mtoto huyo anapata matibabu hospitali na hali yake inaendelea vizuri.
Polisi inaendelea na uchunguzi kubaini wahusika.
Shambulio hilo linajitokeza wiki moja tu baada ya watuhumiwa wanne kuhukumiwa adhabu ya kifo kwa mauaji ya albino.
Pia ni muda mfupi baada ya Rais Tanzania Jakaya Kikwete kukemea mauaji ya albino, ambao viungo vyao hutumika katika shughuli za kishirikina kwa imani potofu kuwa zinasaidia kuleta utajiri na madaraka.
Kadhalika kukiwa kumeanzishwa kampeni maalum ya 'Inatosha' kukomesha mauaji hayo ya albino ambayo yameitia aibu Tanzania katika usoa wa dunia.