STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 6, 2013

Tottenham Hotspur yakiona cha moto nyumbani, Arsenal yapunguzwa kasi

 Ravel Morrison
TIMU ya Tottenham Hotspur wakiwa nyumbani kwao White Hart Lane, London ya Kaskazini wamekiona cha moto baada ya kukanidkwa mabao 3-0 na wageni wao, West Ham United katika mechi ya Ligi Kuu ya England iliyomalizika hivi punde, huku Arsenal ikipunguzwa kasi kwa kulazimishwa sare ya 1-1 ugenini.
Vijana hao wa Andre Villa Boas walishindwa kabisa kufurukuta katika pambano hilo ambalo lilishuhudiwa hadi mapumziko kukiwa hakuna mbabe.
Kipindi cha pili kilipoanza, wenyeji walianza kusulubiwa kwa kutanguliwa kufungwa bao la kwanza kupitia kwa Winston Reid dakika ya 66 na dakika sita baadaye Ricardo Tav Te akaongeza la pili kabla ya Ravel Morrison kuongeza la tatu dakika ya 79 lililowanyong'onyesha Spurs.
Nayo Arsenal baada ya ushindi wa mechi tano mfululizo katika ligi hiyo ilirejea kileleni mwa msimamo jioni hii baada ya kulazimisha sare ya 1-1 na West Bromwich Albion uwanja wa ugenini na kuiengua Liverpool iliyokuwa imekalia nafasi ya kwanza kwa tofauti ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Wenyeji walitangulia kubata bao dakika ya 42 lililofungwa na Claudio Yacob, bao lililodumu hadi mapumziko.
Jack Welshire aliisawazishia vijana wa Arsene Wenger katika dakika ya  63 na kuifanya Arsenal kuambulia pointi moja na kufikisha pointi 16 sawa na Liverpool lakini ikiwa na mabao mengi ya kufunga kuliko vijogoo hao wa Anfield.

Chemsha Bongo! Kama unawakumbuka ebu wataje majina yao

Wawili kati ya hao bado wapo wapo ndani ya klabu hii ni akina nani na ukiweza taja nafasi zao

Didier Kavumbagu, Peter Michael wamfukuza Amisi Tambwe kimya kimya


Tambwe aliyenyoosha kidole anayeoongoza kwa mabao Ligi Kuu
Didier Kavumbagu (kushoto) akishangilia mabao yake na wachezaji wenzke wa Yanga
WASHAMBULIAJI Didier Kavumbagu wa Yanga na Peter Michael wa Prisons-Mbeya wanamfukuza kimya kimya mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe baada ya kila mmoja leo kutupia bao moja moja na kufikisha idadi ya mabao manne.
Kavumbagu aliyekuwa mfuingaji namba mbili msimu uliopiota alifunga bao lake jioni hii wakati Yanga wakiilaza Mtibwa mabao 2-0 na Michael akifunga bao pekee lililoizamisha Mgambo JKT mjini Tanga na kufikisha nusu ya mabao aliyonayo Tambwe anaongoza akiwa na mabao nane mpaka sasa.
Naye kiungo mshambuliaji nyota wa Yanga na Taifa Stars, Mrisho Ngassa ameanza kufungua akaunti yake ya mabao baada ya leo kufunga bao likiwa ni goli la kwanza kwa msimu huu ambapo alikosa mechi sita za ligi hiyo kutokana na adhabu aliyokuwa akiitumikia kwa kusaini mikataba katika klabu mbili za Simba na Yanga.
Mpaka sasa jumla ya mabao 101 yameshatinga wavuni wakati ligi ikiwa kwenye raundi ya saba, huku Simba ikiendelea kuongoza kwa kufunga mabao mengi ikiwa na mabao 16 ikifuatiwa na Yanga yenye 13.
Timu yenye safu butu ya ushambuliaji ni Mgambo JKT ikiwa na mabao mawili tu, huku kwa kipigo cha leo imeporomoka hadi nafasi ya 13 ikiipokea Prisons iliyopata ushindi wake wa kwanza na kuipeleka hadi nafasi ya 11.
Kwsa matokeo ya mwishoni mwa wiki ni kwamba Simba imeendelea kukaa kileleni ikiwa na pointi 15 ikifuatiwa na Yanga kisha JKT Ruvu zenye pointi 12 kila moja, kisha timu nne za Azam, Mbeya City, Coastal Union na Kagera zikifuatia zikiwa na pointi 11, huku Ashanti ikiendelea kuzibeba timu zote kwa kuwa na pointi mbili mpaka sasa licha ya kucheza mechi saba.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea Jumatano kwa mechi itakazozikutanisha timu za Rhino Rangers vs Mbeya City, mjini Tabora, huku Oljoro JKT itawalika Ruvu Shooting jijini Arusha, huku Azam itaikaribisha Mgambo JKT uwanja wa Chamazi na Mtibwa Sugar itaonyeshana kazi na JKT Ruvu Manungu, Morogoro.

Msimamo wa Ligi hiyo baada ya mechi za wikiendi hii ni kama ifuatavyo;
                                   P   W  D  L  F  A  GD  PTS
1. Simba                      7    4   3   0 16  5  11   15
2. Yanga                      7    3   3   1  13  7   6   12
3. JKT Ruvu                7    4   0   3   8   5   3    12
4. Kagera Sugar          7    3   2   2   8   5    3   11
5. Azam                      7    2   5   0   9   6   3   11
6. Mbeya City             7    2   5   0   8   6   2    11
7. Coastal Union         7    2   5   0   6   3   3   11
8. Ruvu Shooting         7   3   1   3   7   5   2    10
9.  Rhino Rangers        7   1   4   2   7   8   -1   7
10.Mtibwa Sugar         7   1  4   2   5   8    -3   7
11.Prisons                    7   1  4   2   4   9   -5   7
12. Oljoro                   7   1   2   4   4   8   -4   5
13.Mgambo                7   1   2   4   2  11  -9   5
14.Ashanti                 7    0   2   5   4  15 -11  2

Wafungaji:
8- Tambwe Amisi (Simba)
4- Didier Kavumbagu (Yanga)
3- Jerry Tegete (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Kipre Tchetche (Azam), Peter Michael (Prisons), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Paul Nonga (Mbeya City), Themi Felix (Kagera Sugar)
2- Jonas Mkude (Simba), Jerry Santo, Haruna Moshi (Coastal Union), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Mwagani Yeya (Mbeya City), Hamis Kiiza (Yanga), Machaku Salum (JKT Ruvu)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla,(Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki, Ramadhani Singano (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva, Mrisho Ngassa (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku, Kamana Salum, Hussein Abdallah (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris,  John Bocco, Joseph Kimwaga (Azam), Steven Mazanda, Richard Peter (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Shaaban Susan, Jerome Lembeli, Cosmas Ader, Said Dilunga (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally, Shaaban Nditti, Shaaban Kisiga (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu, Tumba Swedi, Paul Maono,            (OG) (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Godfrey Wambura, Clement Douglas (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary, Paul Malipesa, Expedito Kiduko (Oljoro JKT)

Mauaji ya Sheikh Rogo na wenzake yaiweka Mombasa roho juu

Sheikh Abou Rogo enzi za uhai wake. Mwanaharakati huyu wa Kiislama aliuwawa mwaka jana na juzi mrithi wake Ibrahim Rogo na wenzake waliuwawa kama alivyouwawa yeye kwa kupigwa risasi
HALI ya amani katika mji wa Mombasa imezidi kuwa tete, kutokana na makundi ya vijana wenye hasira kali kuendeleza machafuko katika viunga mbalimbali vya mji huo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na BBC, jumla ya watu wanne wamepoteza maisha katika machafuko hayo, baada ya makundi ya vijana hao kupambana na askari wa kutuliza ghasia.


Habari kutoka nchini humo zinaeleza kuwa machafuko hayo yametokea siku moja baada ya kifo cha Sheikh Ibrahim Omar ‘Rogo’, aliyeuawa kwa kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana.

Katika shambulizi hilo, pia washirika watatu wa Sheikh Rogo nao wamepoteza maisha papo hapo, huku Salim Adbi akinusurika katika shambulizi hilo.

Kwa mujibu wa taarifa zaidi kutoka mjini Mombasa, vijana wenye hasira kali wameteketeza kanisa moja katika ghasia za juzi. 

Sheikh Ibrahim Rogo alikuwa mhubiri katika msikiti ambao ulikuwa unatumiwa kwa mahubiri na marehemu Sheikh Aboud Rogo, ambaye pia aliuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana mwaka jana.

Sheikh Aboud Rogo alishutumiwa kutoa mafunzo yenye itikadi kali yaliyowashawishi vijana kujiunga na kikundi cha kigaidi cha Al Shabaab.

Kabla ya kifo chake, marehemu Aboud Rogo alidaiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la Al Shabaab.

Tukio la kifo cha Sheikh Ibrahim Omar ‘Rogo’ limetokea ndani ya kipindi cha wiki mbili baada ya shambulizi la kigaidi la Westgate Mall, ambapo jumla ya watu 67 walipoteza maisha.

Ibrahim Rogo alionekana kama mrithi wa marehemu Aboud Rogo, alipohutubu katika msikiti huo.

Chelsea yaifumua Norwich City, Swansea wakifa ugenini


Mshikemshike wa pambano la Chelsea na Norwich City

Chelsea
Chelsea wakipogezana baada ya kuwatungua Norwich

VIJANA wa Jose Mourinho, Chelsea jioni hii wameifumua bila huruma Norwich City baada ya kuitandika mabao 3-1, huku Swansea City ikifa ugenini kwa kulazwa na Southampton ambayo imeendeleza rekodi ya nzuri ya katika Ligi Kuu ya England.
Bao la mapema la Oscar katika dakika ya 5 na mengine ya dakika za lala salama kupitia kwa Hazard na  William yalimpa faraja Mourinho kwa kuvuna pointi muhimu tatu.
Wenyeji walipata bao lao lililokuwa la kusawazisha katika dakika ya 68  kupitia kwa Pilkington ambalo lilionekana kama lingefanya matokeo kusaliwa bao 1-1 kabla ya Chelsea kucharuka na kupata mabao mawili dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika.
Katika mechi nyingine Southampton imeendeleza libeneke kwa kuizamisha Swansea waliowafuata kwa mabao 2-0 na kuinga kwenye Nne Bora ya msimamo wa Ligi hiyo ingawa kuna mechi mbili kwa sasa zinaendelea kuchezwa zinazoweza kubadilisha msimamo ulivyo.

Yanga yalipa kisasi kwa Mtibwa, yaipumulia Simba, Mgambo yalala nyumbani

Ngassa akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao la kwanza
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga jioni imefanikiwa kulipa kisasi kwa Mtibwa Sugar kwa kuinyuka mabao 2-0 na kuwapumulia watani Simba wanaoongoza ligi wakiwa na pointi 15.
Ushindi huoi ambao ni wa pili mfulilizo kwa Yanga baada ya awali kuwa na matokeo mabaya, ulipatikana kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kufanikiwa kukata ngebe za Mtibwa waliotamba awali kuwa wangerejea ilichokifanya msimu uliopita walipoitungua Yanga 3-0 na kutimua kocha na baadhi ya viongozi.
Bao la mapema la dakika ya tano kwa winga mahiri nchini, Mrisho Ngassa na jingine dakika 19 baadaye kupitia kwa Didier Kavumbagu ambalo ni la nne kwake tangu msimu huu uanze, yalitosha kuwazima wapinzani wao ambao walilazimika kufanya mabadiliko ya wachezaji baada ya safu ya nyuma kupwaya.
Kocha Mecky Mexime alimtoa Salvatory Nteba na kumuungiza Dickson Daud kabla ya kumtoa tena Vincent Barnabas na nafasi yake kuchukuliwa na Masoud Mohammed.
Mabadiliko hayo yaliweza kuifanya Yanga ishindwe kufurukuta zaidi hadi walipomaliza dakika 45 za kwanza wakiwa na ushindi huo wa mabao 2-0, matokeo yaliyoendelea kuwepo hata katika kipindi cha pili na kuifanya Yanga ijikusanyie jumla ya pointi 12 sawa na JKT Ruvu ambayo jana iliilaza Kagera Sugar mabao 2-1, lakini mabingwa watetezi wakiwa na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Katika mchezo nwingine uliochezwa uwanja wa Mkwakwani Tanga, Mgmabo JKT ilikumbana na kipigo cha kushtukiza kutoka kwa  Prisons ya Mbeya kwa bao lililotupiwa na mfungaji mahiri wa timu hiyo ya maafande wa Magereza Peter Michael likiwa bao lake la nne msimu huu.
Ligi hiyo itaendelea tena siku ya Jumatano kwa miuchzero kadhaa wakati huo Yanga itakuwa ikianza safari ya kuifuata Kagera Sugar katika pambano lao litakalochezwa Jumamosi kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Kagera.

Hivi ndivyo dada wa Mhe Freeman Mbowe alivyozikwa mjini Moshi jana


MWENYEKITI wa Chadema Freeman Mbowe akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu dada yake,Grace Mbowe, huko Moshi jana.
 Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP Reginald Mengi akiweka shada la maua kwenye kaburi la dada wa Freeman Mbowe.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge,William Lukuvi akiweka shada la maua kwenye kaburi la dada wa Freeman Mbowe.
 Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiweka shada la maua kwenye kaburi la dada wa Freeman Mbowe. 
 
Picha na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii

Hussein Gobossi hoi kwa Adam Ngange

Bondia Adamu Ngange kushoto akipambana na Hussein Gobossy wakati wa mpambano wao wa masumbwi uliofanyika katika ukumbi wa Sonata uliopo Chanika Dar es salaam jana Ngange alishinda kwa K.O ya raundi ya nne.
Bondia Adamu Ngange kushoto akipambana na Hussein Gobossy wakati wa mpambano wao wa masumbwi uliofanyika katika ukumbi wa Sonata uliopo Chanika, Dar es salaam jana Ngange alishinda kwa K.O ya Raundi ya Nne.
Adamu Ngange katikati akiwa na kocha wake
Bondia Hussein Gobossy  kushoto akipambana na Adamu Ngange wakati wa mpambano wao wa masumbwi uliofanyika katika ukumbi wa Sonata uliopo Chanika Dar es salaam jana Ngange alishinda kwa K.O ya raundi ya nne.
Bondia Adamu Ngange akisubili kupigana na mpinzani wake
Bondia Adamu Ngange kulia akimwangalia bondia HUSSEIN GOBOSSY ambaye alikimbia ulingoni kwa kipigo kikali ambapo mvua ya makonde ilikuwa ikimwelemea.
Bondia Adamu Ngange akinyosha mikono juu baada ya mpinzani wake kuingia mitini kwa kukimbia mchezo huo

PAMBANO LA RUVU, SIMBA LAINGIZA MIL 75/-

 
Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya wenyeji Ruvu Shooting na Simba lililochezwa jana (Oktoba 5 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 75,692,000.

Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 43 la VPL msimu wa 2013/2014 lililomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya bao 1-1 walikuwa 13,395.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 17,983,902.31 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 11,546,237.29.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 9,144,357.11, tiketi sh. 3,183,382, gharama za mechi sh. 5,486,614.26, Kamati ya Ligi sh. 5,486,614.26, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,743,307.13, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 1,066,841.66 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,066,841.66.