STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 6, 2013

Yanga yalipa kisasi kwa Mtibwa, yaipumulia Simba, Mgambo yalala nyumbani

Ngassa akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao la kwanza
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga jioni imefanikiwa kulipa kisasi kwa Mtibwa Sugar kwa kuinyuka mabao 2-0 na kuwapumulia watani Simba wanaoongoza ligi wakiwa na pointi 15.
Ushindi huoi ambao ni wa pili mfulilizo kwa Yanga baada ya awali kuwa na matokeo mabaya, ulipatikana kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kufanikiwa kukata ngebe za Mtibwa waliotamba awali kuwa wangerejea ilichokifanya msimu uliopita walipoitungua Yanga 3-0 na kutimua kocha na baadhi ya viongozi.
Bao la mapema la dakika ya tano kwa winga mahiri nchini, Mrisho Ngassa na jingine dakika 19 baadaye kupitia kwa Didier Kavumbagu ambalo ni la nne kwake tangu msimu huu uanze, yalitosha kuwazima wapinzani wao ambao walilazimika kufanya mabadiliko ya wachezaji baada ya safu ya nyuma kupwaya.
Kocha Mecky Mexime alimtoa Salvatory Nteba na kumuungiza Dickson Daud kabla ya kumtoa tena Vincent Barnabas na nafasi yake kuchukuliwa na Masoud Mohammed.
Mabadiliko hayo yaliweza kuifanya Yanga ishindwe kufurukuta zaidi hadi walipomaliza dakika 45 za kwanza wakiwa na ushindi huo wa mabao 2-0, matokeo yaliyoendelea kuwepo hata katika kipindi cha pili na kuifanya Yanga ijikusanyie jumla ya pointi 12 sawa na JKT Ruvu ambayo jana iliilaza Kagera Sugar mabao 2-1, lakini mabingwa watetezi wakiwa na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Katika mchezo nwingine uliochezwa uwanja wa Mkwakwani Tanga, Mgmabo JKT ilikumbana na kipigo cha kushtukiza kutoka kwa  Prisons ya Mbeya kwa bao lililotupiwa na mfungaji mahiri wa timu hiyo ya maafande wa Magereza Peter Michael likiwa bao lake la nne msimu huu.
Ligi hiyo itaendelea tena siku ya Jumatano kwa miuchzero kadhaa wakati huo Yanga itakuwa ikianza safari ya kuifuata Kagera Sugar katika pambano lao litakalochezwa Jumamosi kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Kagera.

No comments:

Post a Comment