STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 6, 2013

Didier Kavumbagu, Peter Michael wamfukuza Amisi Tambwe kimya kimya


Tambwe aliyenyoosha kidole anayeoongoza kwa mabao Ligi Kuu
Didier Kavumbagu (kushoto) akishangilia mabao yake na wachezaji wenzke wa Yanga
WASHAMBULIAJI Didier Kavumbagu wa Yanga na Peter Michael wa Prisons-Mbeya wanamfukuza kimya kimya mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe baada ya kila mmoja leo kutupia bao moja moja na kufikisha idadi ya mabao manne.
Kavumbagu aliyekuwa mfuingaji namba mbili msimu uliopiota alifunga bao lake jioni hii wakati Yanga wakiilaza Mtibwa mabao 2-0 na Michael akifunga bao pekee lililoizamisha Mgambo JKT mjini Tanga na kufikisha nusu ya mabao aliyonayo Tambwe anaongoza akiwa na mabao nane mpaka sasa.
Naye kiungo mshambuliaji nyota wa Yanga na Taifa Stars, Mrisho Ngassa ameanza kufungua akaunti yake ya mabao baada ya leo kufunga bao likiwa ni goli la kwanza kwa msimu huu ambapo alikosa mechi sita za ligi hiyo kutokana na adhabu aliyokuwa akiitumikia kwa kusaini mikataba katika klabu mbili za Simba na Yanga.
Mpaka sasa jumla ya mabao 101 yameshatinga wavuni wakati ligi ikiwa kwenye raundi ya saba, huku Simba ikiendelea kuongoza kwa kufunga mabao mengi ikiwa na mabao 16 ikifuatiwa na Yanga yenye 13.
Timu yenye safu butu ya ushambuliaji ni Mgambo JKT ikiwa na mabao mawili tu, huku kwa kipigo cha leo imeporomoka hadi nafasi ya 13 ikiipokea Prisons iliyopata ushindi wake wa kwanza na kuipeleka hadi nafasi ya 11.
Kwsa matokeo ya mwishoni mwa wiki ni kwamba Simba imeendelea kukaa kileleni ikiwa na pointi 15 ikifuatiwa na Yanga kisha JKT Ruvu zenye pointi 12 kila moja, kisha timu nne za Azam, Mbeya City, Coastal Union na Kagera zikifuatia zikiwa na pointi 11, huku Ashanti ikiendelea kuzibeba timu zote kwa kuwa na pointi mbili mpaka sasa licha ya kucheza mechi saba.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea Jumatano kwa mechi itakazozikutanisha timu za Rhino Rangers vs Mbeya City, mjini Tabora, huku Oljoro JKT itawalika Ruvu Shooting jijini Arusha, huku Azam itaikaribisha Mgambo JKT uwanja wa Chamazi na Mtibwa Sugar itaonyeshana kazi na JKT Ruvu Manungu, Morogoro.

Msimamo wa Ligi hiyo baada ya mechi za wikiendi hii ni kama ifuatavyo;
                                   P   W  D  L  F  A  GD  PTS
1. Simba                      7    4   3   0 16  5  11   15
2. Yanga                      7    3   3   1  13  7   6   12
3. JKT Ruvu                7    4   0   3   8   5   3    12
4. Kagera Sugar          7    3   2   2   8   5    3   11
5. Azam                      7    2   5   0   9   6   3   11
6. Mbeya City             7    2   5   0   8   6   2    11
7. Coastal Union         7    2   5   0   6   3   3   11
8. Ruvu Shooting         7   3   1   3   7   5   2    10
9.  Rhino Rangers        7   1   4   2   7   8   -1   7
10.Mtibwa Sugar         7   1  4   2   5   8    -3   7
11.Prisons                    7   1  4   2   4   9   -5   7
12. Oljoro                   7   1   2   4   4   8   -4   5
13.Mgambo                7   1   2   4   2  11  -9   5
14.Ashanti                 7    0   2   5   4  15 -11  2

Wafungaji:
8- Tambwe Amisi (Simba)
4- Didier Kavumbagu (Yanga)
3- Jerry Tegete (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Kipre Tchetche (Azam), Peter Michael (Prisons), Bakar Kondo (JKT Ruvu), Paul Nonga (Mbeya City), Themi Felix (Kagera Sugar)
2- Jonas Mkude (Simba), Jerry Santo, Haruna Moshi (Coastal Union), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Saady Kipanga (Rhino Rangers), Mwagani Yeya (Mbeya City), Hamis Kiiza (Yanga), Machaku Salum (JKT Ruvu)
1- Abdi Banda, Crispian Odulla,(Coastal Union), Henry Joseph, Betram Mombeki, Ramadhani Singano (Simba), Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Simon Msuva, Mrisho Ngassa (Yanga), Iman Joel, Salum Majid, Mwalimu Musuku, Kamana Salum, Hussein Abdallah (Rhino Rangers), Gaudence Mwaikimba, Seif Abdallah, Khamis Mcha, Aggrey Morris,  John Bocco, Joseph Kimwaga (Azam), Steven Mazanda, Richard Peter (Mbeya City), Laurian Mpalile (Prisons-OG), Shaaban Susan, Jerome Lembeli, Cosmas Ader, Said Dilunga (Ruvu Shooting), Juma Luzio, Masoud Ally, Shaaban Nditti, Shaaban Kisiga (Mtibwa Sugar), Shaaban Juma, Anthony Matangalu, Tumba Swedi, Paul Maono,            (OG) (Ashanti Utd), Abdallah Bunu, Emmanuel Switta, Amos Mgisa (JKT Ruvu), Fully Maganga, Hamis Msafiri (Mgambo JKT), Seleman Kibuta, Daud Jumanne, Maregesi Marwa, Godfrey Wambura, Clement Douglas (Kagera Sugar), Shaibu Nayopa, Amir Omary, Paul Malipesa, Expedito Kiduko (Oljoro JKT)

No comments:

Post a Comment