STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 6, 2013

Tottenham Hotspur yakiona cha moto nyumbani, Arsenal yapunguzwa kasi

 Ravel Morrison
TIMU ya Tottenham Hotspur wakiwa nyumbani kwao White Hart Lane, London ya Kaskazini wamekiona cha moto baada ya kukanidkwa mabao 3-0 na wageni wao, West Ham United katika mechi ya Ligi Kuu ya England iliyomalizika hivi punde, huku Arsenal ikipunguzwa kasi kwa kulazimishwa sare ya 1-1 ugenini.
Vijana hao wa Andre Villa Boas walishindwa kabisa kufurukuta katika pambano hilo ambalo lilishuhudiwa hadi mapumziko kukiwa hakuna mbabe.
Kipindi cha pili kilipoanza, wenyeji walianza kusulubiwa kwa kutanguliwa kufungwa bao la kwanza kupitia kwa Winston Reid dakika ya 66 na dakika sita baadaye Ricardo Tav Te akaongeza la pili kabla ya Ravel Morrison kuongeza la tatu dakika ya 79 lililowanyong'onyesha Spurs.
Nayo Arsenal baada ya ushindi wa mechi tano mfululizo katika ligi hiyo ilirejea kileleni mwa msimamo jioni hii baada ya kulazimisha sare ya 1-1 na West Bromwich Albion uwanja wa ugenini na kuiengua Liverpool iliyokuwa imekalia nafasi ya kwanza kwa tofauti ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Wenyeji walitangulia kubata bao dakika ya 42 lililofungwa na Claudio Yacob, bao lililodumu hadi mapumziko.
Jack Welshire aliisawazishia vijana wa Arsene Wenger katika dakika ya  63 na kuifanya Arsenal kuambulia pointi moja na kufikisha pointi 16 sawa na Liverpool lakini ikiwa na mabao mengi ya kufunga kuliko vijogoo hao wa Anfield.

No comments:

Post a Comment