STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 16, 2013

Waislam waitana Dar kuhusiana kupigwa risasi, kukimbizwa Segerea akiwa mgonjwa kwa Sheikh Ponda


SIKU moja tu baada ya jeshi la Polisi 'kumtorosha' kininja Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania akiwa bado akiuguza jehara la kupigwa risasi alipokuwa amelazwa Hospitali ya Muhimbili (MOI), Waislam wameitana kwa ajili ya kutoa tamko na kuamua la kufanya kutokana na kadhia hiyo.
Sheikh Ponda anadaiwa kupigwa risasi na Polisi mkoani Morogoro mara baada ya kumaliza kuzungumza na Waislam katika Kongamano la Wahadhiri wa Kiislam mkoani humo kwa kilichoelezwa kwamba anasakwa kwa kauli za kichochezi visiwani Zanzibar, ambapo awali Polisi waliruka kuwepo kwa tukio hilo kabla ya baada ya kudai ililazimika kupiga mabomu ya machozi na risasi baridi baada ya kuzuiwa na wafuasi wa Ponda wasimkamate Sheikh wao.
Sheikh huyo alipata huduma ya kwanza mjini humo kabla ya kuletwa Muhimbili, ambapo Polisi walitangaza kumtia mbaroni kisha juzi kusomewa mashtaka akiwa kitandani kabla ya jana kuondolewa kinyemela akiwa bado mgonjwa na kuifanya familia kuiachia Jumuiya ya Kiislam kuamua la kufanya.
Hivyo Waislam kupitia Jumuiya hiyo wameitisha kongamano kubwa litakalofanyika siku ya Jumapili kwenye viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke jijini Dar es Salaam ambapo kutakuwa na ajenda moja tu isemayo 'KWANINI SERIKALI YA CCM IMEMPIGA RISASI SHEIKH PONDA?'
Kongamano hilo pia linatarajiwa kufichua mambo mengine kadhaa dhidi ya dhuluma wanazofanyiwa Waislam wa Tanzania kabla ya kufanyika maandamano makubwa jijini Dar es Salaam na mikoani kupigwa udhalili wanaodaiwa kufanyiwa na serikali ya CCM.
Kwa mujibu wa vipeperushi vilivyosambazwa karibu msikiti yote mikubwa jijini Dar na hasa ile ya harakati imesema kongamano hilo litafanyika kuanzia saa 8 mchana na kuwahimiza waislam popote walipo kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kutoa maamuzi mazito yasiyotarajiwa kwa kilichoelezwa kuchoshwa na unyonge.
Kipeperushi hicho kinasema kuwa Waislam watajitahidi kupambana na hali hiyo ya unyonge kwa gharama yoyote ili amani ya kweli iweze kupatikana.
"Polisi waliotaka kumuua Sheikh Ponda, sasa wanamteka toka Muhimbili hadi Segerea akiwa bado mgonjwa, ili mfumo wa kuwakandamiza Waislam na kuwapendelea Wakristo (Mfumo Kristo) uweze kudumu na waweze kuikalia Zanzibar kinyume na matakwa ya Wazanzibar" Sehemu ya Kipeperushi hicho kinasomeka hivyo.
"Kwamba Wakristo waendelee kupoewa fedha na serikali chini ya Mkataba (MoU), wanedelee kupendelewa Baraza la Mitihani, Waendelee kupata nafasi nyingi za ajira na utawala serikalini, waendelee kuwafanya wasilam kuwa Raia wa daraja la pili, waendelee kuwazuia Waislam kutekeleza dini yao na kuwabana wasijiendeleze, ili waendelee kuwaweka Masheikh magerezani bila ya Haki. Shime Waislam"
Kipeperushi hicho kinaongeza kikionyesha kimetolewa na Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania ambalo Sheikh Ponda Issa Ponda ndiye kiongozi wake.
Katika Wahubiri wa Kiislam wametahadharisha serikali kwa kudai kuwa hata kama itaamua kumdhuru Sheikh Ponda na 'kutowesha' kabisa bado haiwezi kuwarudisha nyuma Waislam kudai haki zao kna kudai njia ya kufanya waislam watulie ni kupewa haki zao na kutendewa usawa kama wenzao wa dini nyingine.
Khatibu aliyehutubia swala ya Ijumaa msikiti Mwenge mchana wa leo, alisema waislam hawawezi kunyamaza kwa kukamatiwa au kudhuriwa kwa viongozi wao kwa madai kuwa Uislam ni dini iliyokamilika na inayoongozwa kwa mujibu wa Qur'an na mafgundisho ya Mtume Muhammad (SAW).
"Yu wapi Mtume na kipenzi cha Mwenyezi Mungu (SW), kuondoka kwake kumeuzima uislam> Hapana, makhalifa na maulamaa wangapi wamepita na uislam umebaki hivyo hivyo na nguvu zake, hivyo hata Ponda akiuwawa na masheikh wengine watafutiliwa mbali bado haiwezi kuuzima Uislam na kuwanyamzisha waislam kulilia na kutetea haki zao," alisema Khatibu huyo.
"Jambo la muhimu kwa serikali itambue na tunajua mpo vibaraka wake humu ndani nendeni mkawaambie mabosi wenu kuwa waislam HATUTANYAMAZA KUDAI HAKI ZETU mpaka iache DHULUMA kwa WAISLAM na UPENDELEO kwa WAKRISTO," alisisitiza.
Kipeperushi cha kongamano hilo la Jumapili litakalofanyika Viwanja vya Mwemba Yanga ni hiki hapa:

Maajabu! Mama ajifungua kichanga na 'chura' huko Chunya

Mtoto aliyezaliwa pamoja na kiumbe cha ajabu kinachofanana na chura
Mtoto akiwa na afya tele
Hiki ndicho kiumbe kilchotoka tumboni pamoja na mtoto mchanga kwa mama Matrida picha hii mara baada ya kutenganishwa na mtoto huyo
Kushoto ni Matrida Erick (20) aliyejifungua mtoto pamoja na kiumbe hicho cha ajabu akiwa na mkunga Agripina Sikanyika aliyembeba mtoto wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kujifungua kwa mkunga huyo
Hapa ndipo  kwa mkunga Agripina Sikanyika Matrida alipojifungulia watoto hao
Mkunga huyo akionyesha mkeka unaotumika kuwatandikia wajawazito wanaokuja kujifungulia katika  kliniki yake

Mkunga akionyesha vibali vinavyothibitisha ruhusa aliopewa na Serikali kwa ajili ya kutoa huduma ya kuwazalisha akina mama wajawazito.

Mwanamke mmoja anayejulikana kwa jina la MATRIDA ERICK  mwenye umri  wa miaka ishirini mkazi wa magamba ,wilaya ya chunya ,amejifungua mtoto jinsi ya kiume na wakati huohuo na chura.

Mkunga aliyemzalisha bi AGGRIPINA SIKANYIKA mkazi wa MBUYUNI wilaya ya chunya amesema tukio hilo limetokea majira ya saa tisa alasiri agosti 13 mwaka huu,mara  mwanamke huyo kufikishwa kwa mkunga huyo na mumewe aitwaye BUNDALA JOSEPHAT ISANDU mwenye umri wa miaka thelathini na tano

MATRIDA amesema huo ni uzao wake wanne  na kwamba alishangazwa na kiumbe hicho ingawa wakati anajifungua hakupata tatizo  lolote na pia alifurahia kupata mtoto wa kiume mwenye afya na alisikitishwa kupata hicho kiumbe ambacho kilikuwa na miguu ya mbele yenye vidole vinne na miguu ya nyuma vidole vitano vya binadamu.

Kwa upande wake AGGRIPINA amesema mtoto alikuwa katika kondo lake na chura alikuwa katika kondo lake la nyuma la uzazi wa mwanamke huyo na pia ameeleza kuwa hilo ni tukio la tatu ambapo la kwanza  mwanamke alijifungua kichwa cha ng’ombe mwaka jana na la pili mwaka huu mwezi wa tano ambapo mwanamke alijifungua chura badala ya binadamu kwa hiyo hili ni tukio la tatu  hivyo hakushangazwa na tukio hilo.

Hata hivyo mume wa Matrida amesema katika familia yao hilo ni tukio la kwanza na kwamba limewashangaza.
Baada ya tukio hilo mkunga alimtafuta mwenyekiti wa kijiji cha MBUYUNI bwana CONRAD WAMBOKA ambaye alimtaarifu mtendaji wa kijiji MICHAEL SANZIMWA ambao walishuhudia tukio hilo na walimwamuru mkunga huyo kuondoa kiumbe hicho ‘’CHURA’’ kwenye kondo la uzazi.

Aidha chura hicho kilikufa na ndugu siku moja baadae ambapo ndugu walikabidhiwa na taratibu za mila zilifuatwa.
Baadhi ya ndugu wamehusisha kitendo hicho na imani za kishirikina zilizokithiri huko wilayani chunya.  

Na Ezekiel Kamanga  Mbeya yetu

Tiketi za Yanga, Azam kuuzwa kesho asubuhi lengo kukwepa 'vishoka'


Na Boniface Wambura
TIKETI  kwa ajili ya mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Yanga na Azam itakayochezwa kesho (Agosti 17 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zitaanza kuuzwa saa 3 asubuhi.

Vituo vitakavyouza tiketi hizo Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Barber Shop iliyoko Sinza Madukani.

Katika vituo hivyo tiketi zitauzwa katika magari maalumu. Magari yote yanayouza tiketi yatahamia uwanjani saa 7 kamili mchana.

Viingilio katika mechi hiyo ni sh. 7,000 kwa viti vya rangi ya kijani na bluu wakati viti vya rangi ya chungwa ni sh. 10,000. Watakaiongia viti vya VIP C watalipa sh. 15,000, viti vya VIP B ni sh. 20,000 wakati VIP A watalipa sh. 30,000.

Ajali tena! Watatu wafa baada ya magari mawili kugongana na Trekta



TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI -AJALI
MNAMO TAREHE 15.08.2013 MAJIRA YA  SAA 20:30HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA CHIMBUYA BARABARA YA  MBEYA/TUNDUMA WILAYA YA  MBOZI MKOA WA MBEYA. GARI T.765 BBA AINA YA  SCANIA LILILOKUWA LIKITOKEA MBEYA MJINI KUELEKEA TUNDUMA LILIENDESHWA NA DEREVA AMBAYE BADO HAJAFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE LILIGONGA  TREKTA AMBALO HALIJAFAHAMIKA NAMBA ZA USAJILI KISHA KULIGONGA GARI ACP 8839 AINA YA  SCANIA  MALI YA  KAMPUNI YA  USAFIRISHAJI YA  DHANDHO LILILOKUWA LIKITOKEA TUNDUMA KUELEKEA MBEYA MJINI DEREVA WA GARI HILO BADO KUFAHAMIKA. KATIKA AJALI HIYO WATU WATATU  WAWILI KATI YAO WALIKUWA KATIKA GARI T.765 BBA NA MMOJA NI DEREVA WA TREKTA  AMBAO HAWAJATAMBULIKA MAJINA WALA MAKAZI YAO,  WOTE WANAUME WALIFARIKI DUNIA PAPO HAPO.  AIDHA WATU WAWILI  WALIOKUWA KATIKA GARI ACP 8839 AMBAO PIA HAWAJATAMBULIKA WALIJERUHIWA NA WAMELAZWA  KATIKA HOSPITALI YA  RUFAA MBEYA.  MIILI YA  MAREHEMU IMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA  SERIKALI VWAWA WILAYA YA  MBOZI. CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO KWA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUSHA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
 
Mkuu wa wilaya ya Mbozi Dk. Michael Kadeghe akiwa na Mkuu wa Polisi wilaya ya Mbozi Ally Wendo katika eneo la ajali leo asubuhi



Mabaki ya lori
 



Mabaki ya trekta






TFF yamlilia Mtangazaji Radi ABM- Dodoma

Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa mwandishi wa habari za michezo wa Radio ABM ya Dodoma, Gracemo Bambaza kilichotokea Agosti 14 mwaka huu katika Hospitali ya Ocean Road, Dar es Salaam.

Msiba huo ni mkubwa katika sekta ya habari na mpira wa miguu kwani Bambaza kwa kipindi chote akiwa mwandishi alikuwa akifanya kazi nasi, hivyo mchango wake katika mpira wa miguu tutaukumbuka daima.

Bambaza aliyezaliwa mwaka 1973 na ambaye pia aliwahi kufanya kazi katika vituo vya redio vya Wapo cha Dar es Salaam na Pride cha Mtwara amesafirishwa jana (Agosti 15 mwaka huu) kwenda Karagwe mkoani Kagera kwa ajili ya mazishi.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Bambaza, ABM Radio na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Mungu aiweke roho ya marehemu Bambaza mahali pema peponi. Amina

Dk Mwakyembe azidi kuwasha moto sakata dawa za kulevya, atimua mtandao uliopo JNIA



SOURCE-MTAA KWA MTAA BLOG

Kumekucha Copa Coca Cola, mipira fulana zamwaga kama njugu kwa timu shiriki


SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa shukrani kwa kampuni ya Coca Cola kwa kukabidhi fulana 800 na mipira 100 kwa ajili ya ngazi ya mashindano ya vijana wenye umri chini ya miaka 15 ngazi ya mikoa yanayoanza Septemba Mosi mwaka huu.

Coca Cola ndiyo inayodhamini mashindano hayo yaliyoanzia ngazi ya wilaya ambapo mwaka huu yatachezwa kwa kanda na baadaye fainali itakayochezwa kuanzia Septemba 7-14 mwaka huu jijini Dar es Salaam ikishirikisha mikoa 16 itakayokuwa imefanya vizuri katika ngazi ya kanda.
Kila mkoa utapata fulana 25 na mipira mitatu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya timu zao kwa ajili ya michuano hiyo ngazi ya kanda itakayomazika Septemba 6 mwaka huu.

Kanda hizo ni Mwanza itakayokuwa na timu za mikoa ya Geita, Kagera, Kigoma, Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Tabora. Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Singida inaunda Kanda ya Arusha.

Zanzibar itakuwa na Kaskazini Pemba, Kusini Pemba na mikoa miwili ya Unguja wakati Kanda ya Dar es Salaam ina Ilala, Kinondoni, Lindi, Mtwara, Temeke na mkoa mmoja wa Unguja.

Kanda ya Mbeya inaundwa na Iringa, Katavi, Mbeya, Njombe, Rukwa na Ruvuma wakati Dodoma, Morogoro, Pwani na Tanga zinaunda Kanda ya Morogoro.

Mwanza itatoa timu nne kucheza hatua ya fainali wakati kanda nyingine za Arusha timu mbili, Zanzibar (2), Mbeya (3) na Kanda ya Morogoro itaingiza timu mbili.

Wakati huo huo, semina ya makocha 32 wa timu za mikoa zitakazoshiriki michuano ya U15 FIFA Copa Coca-Cola iliyokuwa ikiendeshwa na mkufunzi Govinder Thondoo kutoka Mauritius inafungwa leo (Agosti 16 mwaka huu) saa 9 alasiri kwenye ukumbi wa Msimbazi Center, Dar es Salaam.

Uchaguzi wa TFF wapigwa 'dochi' sasa kufanyika Okt 27

Na Boniface Wambura
UCHAGUZI Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF uliokuwa umepangwa siku moja na pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, sasa umesogezwa mbele kwa wiki moja na sasa utafanyika Oktoba 26 na 27 mwa huu.
Maamuzi ya kusogezwa mbele kwa uchaguzi huo ambao tangu Desemba mwaka jana umekuwa ukipigwa danadana yaliyotolewa naKamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kuzingatia mamlaka iliyonayo katika kifungu cha 10(6) cha Kanuni za Uchaguzi za TFF na kuusogeza mbele hadi tarehe hiyo mpya.
Sababu za kusogeza mbele uchaguzi ni kutokana na ukweli kuwa Oktoba 20 mwaka huu uongozi wa TFF utakuwa na shughuli nyingi za maandalizi ya mechi ya Simba na Yanga, na hivyo haitawezekana kusimamia shughuli za Mkutano Mkuu wa Uchaguzi kwa wakati mmoja na mchezo huo.
Siku ya mwisho ya kampeni itakuwa Oktoba 25 mwaka huu. Ukiondoa  mabadiliko hayo ya tarehe ya uchaguzi wa viongozi wa TFF, ratiba ya mchakato wa uchaguzi na itabaki kama ilivyotangazwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF katika mkutano wake na waandishi wa habari Agosti 24 mwaka huu.
Pia Kamati imeamua kuwa uchaguzi wa Bodi ya Ligi utabakia kuwa Oktoba 18 mwaka huu kama ilivyopangwa awali.
Kamati imesema inaamini wahusika wote watapokea vizuri mabadiliko hayo na inasikitika kwa usumbufu utakaosababishwa na mabadiliko hayo.

Yanga yaibwaga Simba, TFF yawapa Ngassa lakini yamfungia mechi 6


Mrisho Ngassa aliyeidhinishwa Yanga, lakini atupwa 'kifungoni'
Na Boniface Wambura
KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imepitia usajili wa wachezaji wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na kumuidhinisha Mrisho Ngassa kuchezea timu ya Yanga baada ya kukamilisha usajili wake.

Hata hivyo, Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa imebaini kuwa Ngassa alisaini mkataba mwingine Simba (katika kipindi ambacho alikuwa na mkataba na Azam) ambapo anatakiwa kurejesha fedha alizopokea (sh. milioni 30) pamoja na fidia ya asilimia 50 (sh. milioni 15) ya fedha hizo kwa Simba.

Kamati pia imemfungia mechi sita za mashindano (kuanzia mechi ya Ngao ya Jamii), na anatakiwa awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi hicho cha kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza hadi atakapolipa fedha hizo.

Vilevile Kamati imepitia pingamizi zote zilizowasilishwa kuhusu usajili wa wachezaji, kukatiza mikataba ya wachezaji na kuzitaka klabu husika ziwe zimetatua masuala hayo hadi Alhamisi (Agosti 22 mwaka huu).

Kwa upande wa wachezaji wa kigeni, Kamati imeagiza wasiruhusiwe kucheza hadi watakapopata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) pamoja na vibali vya kufanya kazi nchini (work permits).

Kamati hiyo itakutana tena Ijumaa (Agosti 23 mwaka huu) ili kupata ripoti za pingamizi ilizoagiza ziwe zimefanyiwa kazi hadi Agosti 22 mwaka huu na kutoa uamuzi kwa pande ambazo hazikuafikiana.