STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 2, 2014

Mkwasa, Pondamali rasmi Yanga, Ruvu yambeba Olaba

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhTXi3WHN12cf8ydSpE-fPtnYQJPurRJ22H6JNFYml5gvQRweEVHouVGPOI60fMLbZqjBDgCdv7coaNCZdquECswYZVgIIy8lazwc8J3wFiZ4x-HiUg6aVMW1OGD5TogH0Kdb_sGSwFxg/s1600/PONDAMALI+JUMA.JPG
Pondamali akiwa na kaseja
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyhILGXEPzcg08Ou6VWhyphenhyphenGQ_bEGVRsjHkUwM-95WMFyKgoa3AmSEp0pQFl7LDHsP8AUvz0B1SdcA1_DqHCjiLzsmNFvGJVgE7hf4UYU6HgdkrfVXUq4_nOTvCDcVKeGrucIGKzxSSwSOHl/s1600/Charles-Boniface-Mkwasa1.jpg
Charles Boniface Mkwasa 'Master'

WAKATI klabu ya Ruvu Shooting ikimtangaza kocha wa zamani wa Mtibwa Sugar, Tom Olaba kuwa kocha wao mkuu kuchukua nafasi ya Charles Boniface Mkwasa 'Master', Yanga yenyewe imetangaza makocha wake wapya kuimarisha benchi lake la ufundi.
Nyota wa zamani wa klabu ya Yanga na Taifa Stars, Mkwasa na Juma Pondamali ndiyo waliotangazwa rasmi kuwa makocha wa Yanga wakati zoezi la kusakwa kocha mkuu likiendelea.
Kwa mujibu wa taarifa makocha hao wote watakuwa wasaidizi na wataanza kibarua chao kesho kuchukua nafasi za makocha Fred Minziro na Razak Siwa kutimuliwa hivi karibuni. Huku nafasi ya daktari wa timu nafasi imerudi mikononi mwa Dk Sufian Juma kumrithi Dk Nassor Matuzya naye aliyeondolewa klabuni hapo.
Baada ya kuondokewa na kocha wake, Ruvu Shooting yenyewe imemtangaza Mkenya Tom Olaba kuwa kocha mkuu baada ya kusaini naye mkataba wa muda mfupi wakati akijipanga kumpa mkataba wa muda mrefu kuifundisha timu yao.
Kwa mujibu wa taarifa ya Afisa habari wa Ruvu, Masau Bwire ni kwamba tayari kocha huyo ameshaanza kibarua tangu jioni ya leo.
Taarifa rasmi ya Yanga kuhusu uteuzi wa makocha na daktari wa kuchukua nafasi ya watu wa benchi la ufundi lililotimuliwa ni:
Uongozi wa Young Africans SC umepata warithi wa nafasi tatu za benchi la ufundi (Charles Boniface Mkwasa, Juma Pondamali na Dr. Suphian Juma), huku wakiendelea na mchakato kumpata kocha mkuu ambaye atachukua nafasi ya mholanzi Ernie Brandts aliyesitishiwa mkataba wake mwishoni mwa mwaka 2013.
Charles Boniface Mkwasa "Master" aliyekua kocha mkuu wa timu ya Ruvu Shooting katika mzunguko wa kwanza anachukua nafasi ya aliyekua kocha msaidizi Fred Felix "Minziro" ambaye muda wake umemalizika mwishoni mwa mwaka 2013.
Mkwasa ambaye aliichezea Young Africans miaka ya 80's kwa kiwango cha hali juu pia alishawahi kuwa Kocha Mkuu/Msaidizi kwa kikosi cha Jangwani kwa vipindi tofauti jambo ambalo linamfanya aiwe mgeni katika mitaa ya Twiga na Jangwani.
Kocha wa makipa wa timu ya Taifa Tanzania "Taifa Stars" Juma Pondamali "Mensah" anachukua nafasi ya aliyekua kocha wa makipa mkenya Razaki Siwa ambaye pia alistishiwa mkataba wake mwishoni mwa mwaka 2013.
Pondamali golikipa aliyeichezea Yanga miaka ya 80's kwa kwa kiwango cha hali ya juu hata kufikia kuwa katika kikosi cha Tanzania kilichoshiriki mashindano ya Mataifa Afrika nchini Nigeria mwaka 1980, sio mgeni katika timu ya Young Africans kwani awali alishwahi kuwa kocha msaidizi kwa vipindi tofauti.
Dr Suphian Juma anachukua nafasi ya Dr Nassoro Matuzya ambaye pia alisitishiwa ajira yake mwishoni mwa mwaka 2013 pamoja benchi la Ufundi.
Mara baada ya kuwapata viongozi hao watatu wa Benchi la Ufundi kikosi cha Young Africans kesho kitaanza mazoezi jioni katika Uwanja wa Bora Kijitonyama kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na mashindano ya Kimataifa huku kocha Mkwasa akiongoza benchi hilo la Ufundi mpaka atakapopatikana kocha mkuu ambaye watafanya watafanya kazi kwa pamoja.

Polisi Arusha katika kashfa, wanakwaya 6 wadaiwa kupigwa bomu na askari

https://fbcdn-sphotos-b-a.akamaihd.net/hphotos-ak-ash4/395583_170893516406261_293707556_n.jpg
Majeruhi wa bomu la Mei 6 kanisa la Mtakatifu Mfanyakazi jijini Arusha
 HABARI ambazo zimeripotiwa muda mfupi uliopita na kituo cha redio cha Wapo kimeeleza kuwa wanakwaya sita wa Kanisa Katoliki mkoani Arusha wamejeruhiwa kwa kilichoelezwa kupigwa bomu na askari wakati wakitoka kanisani usiku wa mkesha wa mwaka mpya.
Inadaiwa wanakwaya hao walikuwa katika makundi na ghafla wakitokea kanisani na kuvamiwa na gari la doria la Polisi na kisha kupigwa na bomu lililowafanya wanguke na kujikuta miili yao ikiwa imechanwachanwa na kulowa damu na kukimbizwa hospitalini na kulazwa huku wengine kuwaliokuwa nao kuruhusiwa kurudi majumbani.
Askofu Lobulu amenukuliwa akisikitishwa na kitendo hicho na kuhoji vipi kanisa katoliki liandamwe na mashambulizi ya mabomu akirejea tukio la Mei 6 kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi kupigwa bomu na kuua watu kadhaa na kujeruhiwa wengine kibao.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amesema atatoa ufafanuzi wa tukio hilo kesho kwenye mkutano wa wanahabari, huku akisema anajua ni wanawake wawili tu ndiyo waliojeruhiwa katika tukio ambalo hata hivyo hakupenda kulizungumza kwa kina kwa madai atafanya hivyo kesho.
Tukio hili liemkuja huku jeshi la Polisi likishuhudia likipata IGP mpya Ernest Mangu na naibu wake, Abdulrahman Kaniki, na pia mkoa huo ukiwa kuna matukio ya milipuko ya bomu likiwemo lile la kwenye mkutano wa CHADEMA.
Tusubiri kupona kesho RPC Sabas atuweke sawa juu ya ukweli wa tukio hilo la fungua mwaka 2014.

Simba yaidonyoa Leopards kimoja Mapinduzi Cup

Haruna Shamte akimtoka mchezaji wa AFC Leopards

Kikosi cha Simba kilichoshinda jana
Leopards waliopigwa kimoja na Simba (Picha zote:ZanziNews)
 KLABU ya Simba bila ya kocha wake mkuu., Mcroatia Zdavko Logarusic usiku wa jana iliwapa raha mashabiki wake baada ya kuwatungua AFC Leopards ya Kenya kwa bao 1-0 katika mfululizo wa michuano yta Kombe la Mapinduzi iliyoanza jana visiwani Zanzibar.
Bao pekee la Simba liliwekwa kimiani na kiungo nyota, Amri Kiemba aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Awadh Juma 'Maniche' katika dakika ya 77 na kuipa Simba ushindi huo ikiwa chini ya kocha msaidizi, Suleiman Matola.
Michuano hiyo inayoshirikisha timu 12 inatarajiwa kuendelea jioni ya leo kwenye viwanja viwili vilivyopo Unguja na Pemba.