STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 2, 2014

Manchester Man 'nyanya' kwa Tottenham

Adebayor akifuka juu kuupiga mpira uliozaa bao la kwanza la Spurs
Adebayor akiifungia Spurs bao la kuongoza
Oyoooooo! vijana wa Spurs wakishangilia bao lao la pili
MASHETANI Wekundu wamezidi kumweka pabaya kocha wake, David Moyes baada ya jana kupokea kipigo cha mabao 2-1 wakiwa nyumbani  mbele ya vijana wa Tottenham Hotspur.
Manchester Utd ambayo msimu huu imekuwa 'urojo' ilipokea kipigo hicho ikiwa ni mara ya kwanza baada ya kipindi kirefu kufungwa na Spurs nyumbani kwake.
Mabao ya Emmanuel Adebayor aliyefunga kipindi cha kwanza kwenye dakika ya 34 na jingine la Eriksen la dakika ya 66 yalitosha kuizamisha Mashetani hao.
Bao la kufuitia machozi la vijana wa Moyes lilifungwa dakika moja baada ya Spurs kupata bao lao la pili kupitia kwa Danny Welbeck.
Kipigo hicho kimeifanya Man Utd iporomoke kutoka nafasi ya sita hadi ya saba na kuipisha Spurs kuwa juu yao kwa tofauti ya pointi tatu.
Spurs ambayo imekuwa na matokeo mazuri tangu ilipomtimua AVB na kupewa Tim Sherwood imekusanya pointi 37 huku Man Utd ikiwa na 34. dakika ya 67. Timu zote zikicheza mechi 20 kila moja.

No comments:

Post a Comment