STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 29, 2014

Arsenal yainyoa kiduchu West Brom Albion nyumbani kwao

The England international rose highest to head the Gunners in front after Ben Foster failed to keep out his attempt
Danny WElbeck akiifungia Arsenal bao pekee
Arsenal players celebrate after finally breaking down West Brom with Danny Welbeck's header on the hour mark at the HawthornsBAO pekee la lililofungwa na mshambuliaji Danny Welbeck limeisaidia Arsenal kupata ushindi wa bao 1-0 ikiwa ugenini dhidi ya West Bromwich Albion.
Katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa The Hawthorns, WElbeck alifunga bao hilo kwa kichwa katika dakika ya 59 akimalizia kazi nzuri ya Santi Cazorla na kuipa ushindi huo muhimu Ze Gunnerz.
Ushindi huo umewafanya vijana wa Arsene Wenger kuchumpa hadi nafasi ya nne, ingawa mechi nyingine zinachezwa jioni hii.
Wenyeji walikaribia kusawazisha bao hilo dakika ya 80 baada ya kugongesha mwamba mkwaju wake murua ambao ulionekana kuelekea wavuni.
Kipigo hicho kimeifanya West Brom kufikisha mechi saba ikicheza nyumbani bila kupata ushindi na katika mechi ya leo mashabiki wao walishindwa kuwavumilia na kuanza kuwazomea.

Angel di Maria, Yaya Toure kuchuana World X1 2014

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/10/25/1414241023993_wps_6_Manchester_United_s_Angel.jpg
di Maria
http://www.kora.me/uploads/jpg/toot_dfc8f07f1c.jpg 
WACHEZAJI 15 wa nafasi ya kiungo wametangazwa na Shirikisho la Soka Duniani,FIFA  kwa ajili ya kupigiwa za kuchaguliwa kwenye kikosi cha dunia ambapo majina matatu pekee ndio yatashinda nafasi hiyo. 
Kikosi hicho kinachojulikana kama World XI 2014, ambacho huteuliwa kwa kura za wachezaji duniani kote kinatarajiwa kutangazwa rasmi katika sherehe za utoaji tuzo ya Ballon d’Or Januari 12 mwakani. 
Wote waliojumuishwa katika orodha hiyo ni nyota waliokuwemo katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil akiwemo mfungaji bora James Rodriquez wa Colombia pamoja na Angel Di Maria ambaye timu yake ya Argentina ilishika nafasi ya pili pamoja na Bastian Schweinsteiger anaewawakilisha mabingwa wa dunia Ujerumani. 
Cristiano Ronaldo na Lionel Messi wao wanatarajiwa kuwemo katika orodha ya washambuliaji ambayo itatolewa Desemba mosi mwaka huu, wakati wateule wa nafasi ya golikipa na mabeki wao wakiwa tayari wameshatangazwa. 
Orodha kamili ya viungo hao na timu zao ni pamoja na Xabi Alonso (Bayern Munich), Angel Di Maria (Manchester United), Cesc Fabregas (Chelsea), Eden Hazard (Chelsea), Xavi (Barcelona) na Andres Iniesta (Barcelona).
Wengine ni; Toni Kroos (Real Madrid), Luka Modric (Real Madrid), Mesut Ozil (Arsenal), Andrea Pirlo (IJuventus), Paul Pogba (Juventus), James Rodriguez (Real Madrid), Bastian Schweinsteiger (Bayern Munich), Yaya Toure (Manchester City), Arturo Vidal (Juventus)

Mke wa Idd Kipingu amwaga misaada shule za Montesory, Ulongoni

Mkurugenzi wa Zugo Gold Mining na Mwakilishi wa Wanawake, Maendeleo ya Vijana na Ajira kwa Wachezaji wa Shirikisho na Ngumi za Ridhaa Tanzania (*BFT), Zuwena Idd Kipingu akizungumza na wazazi kwenye hafla ya Mahafali ya 35 Shule ya Montesoty Nursery& Primary iliyofanyika leo
Mkurugenzi wa Zugo Gold Mining na Mwakilishi wa Wanawake, Maendeleo ya Vijana na Ajira kwa Wachezaji wa Shirikisho na Ngumi za Ridhaa Tanzania (*BFT), Zuwena Idd Kipingu akizungumza na wazazi kwenye hafla ya Mahafali ya 35 Shule ya Montesoty Nursery& Primary iliyofanyika leo

Baadhi ya wazazi waliohudhuria Mahafali ya 35 ya Shule ya Montesory wakifuatilia maonyesho ya watoto wao
Baadhi ya wazazi waliohudhuria Mahafali ya 35 ya Shule ya Montesory wakifuatilia maonyesho ya watoto wao
Baadhi ya wahitimu wa shule ya Montesory wakionyesha maonyesho ya kitaaluma
Wahitimu wa Montesory wakiimba kwenye sherehe za kuagwa zilizofanyika shuleni hapo mchana wa leo

Wanafunzi wakionyesha michezo yao ya taaluma. Hapa wanaigiza kama wapo darasani na mwalimu wao aliyekaa pembeni kushoto


Ikafuata burudani na kurudi 'magoma' hawa majamaa ni noma
Sabri Omary akionyesha umahiri wa kunengua katima mahafali hayo

Babu na wajukuu zake wakisimuliana hadithi kwa vitendo, Kuku na Bata wakimsikiliza Tembo
Kama Muuguzi vile, mmoja wanafunzi wahitimu wa Montesory akijitambulisha kuwa ni Muuguzi kwa sababu ya kupata elimu...hilo ni onyesho la taaluma







Watoto wakikabidhiwa vyeti na zawadi zao

SHULE za Montesory na Ulongoni B zilizopo wilaya ya Ilala zimepewa kwa nyakati tofauti misaada ya tani moja ya Saruji sambamba na fedha taslim kwa ajili ya kuboresha majengo ya shule hizo.
Misaada hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa kampuni ya Zugo Gold Mining ambaye pia ni Mwakilishi wa Wanawake na Maendeleo ya Vijana na Ajira kwa Wachezaji wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), Zuwena Idd Kipingu, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali ya shule hizo mwishoni mwa wiki.
Akizungumza kwenye mahafali ya 35 ya wanafunzi wa awali wa Shule ya Montesory, Zuwena alisema kwa ajili ya kuhakikisha wanafunzi wanapoa wasaa wa kusoma katika mazingira mazuri anajitolea tani moja ya simenti na Sh,. Mil. 1 kwa ajili ya kuendelez aujenzi wa shule hiyo iliyopo Ilala Boma.
Zuwena aliyemwakilisha Mwenyekiti wa Mfuko wa Fursa Sawa Kwa Wote (EOTF), Anna Mkapa katika mahafali hayo kama mgeni rasmi na kutangaza kutoa msaada huo ikiwa ni siku moja tu tangu akabidhi msaada kama huo katika Shule ya Ulongoni B.
"Bila kusubiri kuombwa nimeona majengo yenu hayajamalizika, hivyo najitolea kuwapa tani moja ya saruji na Jumatatu tuwasiliane ili niwakabidhi pamoja na Sh Milioni 2 za vifaa vya michezo na Sh Mil 1 ya kusaidia ujenzi huo," alisema.
Aliongeza kuwa, kama mmoja wa wanawake waliofanikiwa kujiendeleza kimaisha kupitia michezo anawasihi wazazi nchini kutowakataza watoto wao wenye vipaji mbalimbali kujihusisha na vitu vinavyohusiana na vipaji vya ili kuwatengenezea mazingira mazuri ya kujiajiri kupitia fani hizo.
Alisema yeye wakati akiwa mtoto alikuwa akichapwa mno na baba yake kwa kupenda kwake michezo, lakini alikuja kuwa mwanamke wa kwanza kunyakua mkanda mweusi katika karate na taekwondo na kuwa mfanyabishara mkubwa kwa sasa kutokana na fursa aliyopata kupitia kwenye michezo.
"Wazazi wasikazanie watoto wao kusoma tu, pia wawasaidie kuendeleza vipaji vyao kwa nia ya kuwatengenezea ajira wanapokuwa wakubwa," alisema Zuwena.
Katika mahafali hayo jumla ya wanafunzi 75 walihitimu masomo yao ya awali na kukabidhiwa vyeti pamoja na zawadi na mgeni rasmi huyo Zuwena Idd Kipingu, sambamba na kutoa burudani mbalimbali za taaluma na michezo.