STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 11, 2014

SUAREZ, PELLEGRINI WASHINDA TUZO ZA MWEZI.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Liverpool, Luis Suarez ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba wa Ligi Kuu nchini Uingereza huku meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini akitajwa kama kocha bora wa mwezi. Suarez ambaye anakipiga katika klabu ya Liverpool alianza mwezi vibaya baada ya timu hiyo kukubali vipigo kutoka kwa Hull City, Manchester City na Chelsea lakini alionyesha kiwango cha juu baadae kwa kufunga mabao 10 katika mechi nne pekee. 


Mabao hayo alifunga katika mechi dhidi ya Norwich City ambapo alifunga manne, West Ham United mabao mawili, Totehham Hotaspurs mabao mawili na mengine mawili katika mchezo dhidi ya Cardiff City. Mabao hayo yaliisaidia Liverpool kushika usukani wa ligi katika kipindi cha Christmas iangwa baadae waliteleza mpaka nafasi ya tano katika kipindi cha mwaka mpya. Naye Pellegrini mwezi Desemba ulikuwa mzuri kwake baada ya kushinda mechi zote sita kati ya saba walizocheza huku mmoja wakitoka sare ya kufungana bao 1-1 na Southampton.

YANGA YAANZA KAMBI VEMA KWA KUICHAPA 3-0 ANKARA SEKERSPOR

Kikosi cha Young Africans kilichoanza leo dhidi ya Ankara Sekerspor
Young Africans imeanza vizuri katika kambi yake ya mafunzo nchini Uturuki baada ya kuifunga timu ya Ankara Sekerspor kwa mabao 3-0 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika pembeni kidogo ya eneo ililofikia katika mji wa Manavgat Antalya.

Kocha wa Young Africans aliwatumia wachezaji 18 jumla katika mchezo huo ambao wenyeji mara baada ya mchezo walimpongeza kwa timu yake kwa kucheza vizuri katika mchezo huo wa kirafiki.
Dakika ya 10 ya mchezo shuti lililopigwa na mganda Emmanuel Okwi lilishinda mlinda mlango wa Ankara Sekerspor ambapo aliutema mpira huo na kumkuta Didier Kavumbagu aliyeukwamisha mpira huo wavuni na kuhesabu bao la kwanza.

Timu zote ziliendelea kushambuliana kwa zamu na mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Ankara Sekerspor i0 - 1 Young Africans .
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na iliwachukua dakika moja Young Africans kujipatia bao la pili la mchezo kupitia kwa Emmanuel Okwi aliyeitumia vyema pasi ya mwisho ya kiungo Mrisho Ngasa aliywatoka walinzi wa Ankara Sekaspor na kumpasia mfungaji ambaye hakufanya makosa na kuukwamisha mpira wavuni.
Dakika ya 58 kocha Mkwasa alifanya mabadiliko, ambapo waliingia Hamis Kizza na Nizar Khalfani kuchukua nafasi za Didier Kavumbagu na kiungo Hassan Dilunga.

Hamis Kizza aliipatia Young Africans bao tatu la mchezo na la ushindi dakika ya 61 ya mchezo baada mpira aliogongewa na Domayo kuwapita walinzi wa Ankara Sekerspor na kumkuta Kizza ambaye alipiga shuti liliomgonga mlinzi wa Ankara Sekerspor wakati akiokoa na kujaa wavuni.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Ankara Sekerspor 0 -3 Young Africans.
Mara baada ya mchezo kaimu kocha mkuu wa Young Africans Charles Boniface Mkwasa alisema anashukuru vijana wake walicheza vizuri kwa kufuata malekezo na ndio maana wakaweza kupata ushindi huo,makosa yapo machache yaliyojitokeza na ataendelea kuyafanyia kazi.

"Mechi ilikua ni nzuri ukizingatia ndo mchezo wetu wa kwanza wa kirafiki tukiwa na siku ya tatu tangu tufike hapa Uturuki, kwa mazoezi ya jana vijana wameosha mabadiliko na leo wameweza kucheza vizuri na kuweza kupata ushindi, kikubwa naamini kwa siku zilizobakia nitaendelea kufanya marekebisho na kukifanya kikosi kuendelea kuwa bora pindi kitaporejea nchini tayari kwa mzunguko wa pili wa Lig Kuu ya Vodacom" alisema Mkwasa 

Kikosi cha Young Africans kilichocheza leo ni:
1.Juma Kaseja/Ally Mustafa "Barthez" (dk65), 2.Juma Abdul, 3.Oscar Joshua/David Luhende(dk 82), 4.Mbuyu Twite (C), 5.Kelvin Yondani, 6.Frank Domayo/Ibrahim Job(dkk 80), 7.Haruna Niyonzima/Saimon Msuva (dk72), 8.Hassan Dilunga/Nizar Khalfan (dk58), 9.Didier Kavumbagu/Hamis Kizza (dk58), 10.Mrisho Ngasa/Jerson Tegete (dk 68), 11. Emmanuel Okwi/Said Bahanuzi (dk 85)

Chelsea yaiengua Arsenal kileleni

 Eden Hazard scores for Chelsea
MABAO mawili moja kutoka kwa Ezen Hazard na jingine la Fernando Torres 'El Nino' yameiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 ugenini na kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England kwa muda.
Chelsea ilipata ushindi huo dhidi ya Hull City kwenye pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Kingstons Communication na kuifanya kufikisha pointi 46, moja zaidi ya Arsenal ambao watashuka dimbani keshokutwa.
Hazard alifunga bao la kwanza dakika ya 56 akimalizia kazi nzuri ya Ashley Cole kabla ya Torres kuongeza la pili dakika ya 87 na kuwakatisha tamaa wenyeji.
Jioni hii kuna mechi nyingine zinazoendelea katika ligi hiyo na baadaye Manchester United itaikaribisha Swansea City waliowatoa nishai kwenye michuano ya Kombe la FA katika dimba hilo hilo.

Simba yavunja mwiko, Kiemba we acha tu

 
AMRI Kiemba amezidi kudhihirisha kuwa yupo kikazi zaidi kama alivyopwahi kunukuliwa na Blogu hii baada ya usiku wa jana kuhusika na mabao mawili yaliyotosha kuvunja mwiko wa URA wa kutofungwa na Simba kwenye mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi.
Kiemba, alitengeneza bao la kwanza lililofungwa na beki Joseph Owino kabla ya kuongeza jingine na kuipa Simba ushindi wa mabao 2-0 na kuivusha hadi Fainali ya michuano hiyo.
Mabao yote mawili yalifungwa kwenye kipi8ndi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kuisha timu zikiwa hazijafungana na URA wakicheza punguyfu baada ya nyota wao Oweni Kasule kutolewa kwa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu Ramadhani Singano 'Messi'.
Kwa ushindi huo asmbao umeifanya Simba kuweka rekodi kwa kuondoa uteja kwa URAnma kutinga Fainali bila kupoteza mchezo zozote wala kufungwa bao lolote katika lango lao, limeifanya Simba sasa kukutana na KCC ya Uganda iliwatemesha taji waliokuwa watetezi, Azam.
Azam walikumbana na lkipindi cha mabao 3-2 katika mechi ya kwanza iliyochezwa jioni kwenye dimba la Amaan licha ya kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-1, mabaoi yake yakiwekwa kimiani na kinda, Joseph Kimwaga.
Fainali ya michuano hiyo itachezwa Jumatatu kwenye uwanja huo wa Amaan.