MSHAMBULIAJI
wa klabu ya Liverpool, Luis Suarez ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwezi
Desemba wa Ligi Kuu nchini Uingereza huku meneja wa Manchester City
Manuel Pellegrini akitajwa kama kocha bora wa mwezi. Suarez ambaye
anakipiga katika klabu ya Liverpool alianza mwezi vibaya baada ya timu
hiyo kukubali vipigo kutoka kwa Hull City, Manchester City na Chelsea
lakini alionyesha kiwango cha juu baadae kwa kufunga mabao 10 katika
mechi nne pekee.

Mabao hayo alifunga katika mechi dhidi ya Norwich City ambapo alifunga manne, West Ham United mabao mawili, Totehham Hotaspurs mabao mawili na mengine mawili katika mchezo dhidi ya Cardiff City. Mabao hayo yaliisaidia Liverpool kushika usukani wa ligi katika kipindi cha Christmas iangwa baadae waliteleza mpaka nafasi ya tano katika kipindi cha mwaka mpya. Naye Pellegrini mwezi Desemba ulikuwa mzuri kwake baada ya kushinda mechi zote sita kati ya saba walizocheza huku mmoja wakitoka sare ya kufungana bao 1-1 na Southampton.