STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 11, 2014

Chelsea yaiengua Arsenal kileleni

 Eden Hazard scores for Chelsea
MABAO mawili moja kutoka kwa Ezen Hazard na jingine la Fernando Torres 'El Nino' yameiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 ugenini na kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England kwa muda.
Chelsea ilipata ushindi huo dhidi ya Hull City kwenye pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Kingstons Communication na kuifanya kufikisha pointi 46, moja zaidi ya Arsenal ambao watashuka dimbani keshokutwa.
Hazard alifunga bao la kwanza dakika ya 56 akimalizia kazi nzuri ya Ashley Cole kabla ya Torres kuongeza la pili dakika ya 87 na kuwakatisha tamaa wenyeji.
Jioni hii kuna mechi nyingine zinazoendelea katika ligi hiyo na baadaye Manchester United itaikaribisha Swansea City waliowatoa nishai kwenye michuano ya Kombe la FA katika dimba hilo hilo.

No comments:

Post a Comment