STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 11, 2014

SUAREZ, PELLEGRINI WASHINDA TUZO ZA MWEZI.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Liverpool, Luis Suarez ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba wa Ligi Kuu nchini Uingereza huku meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini akitajwa kama kocha bora wa mwezi. Suarez ambaye anakipiga katika klabu ya Liverpool alianza mwezi vibaya baada ya timu hiyo kukubali vipigo kutoka kwa Hull City, Manchester City na Chelsea lakini alionyesha kiwango cha juu baadae kwa kufunga mabao 10 katika mechi nne pekee. 


Mabao hayo alifunga katika mechi dhidi ya Norwich City ambapo alifunga manne, West Ham United mabao mawili, Totehham Hotaspurs mabao mawili na mengine mawili katika mchezo dhidi ya Cardiff City. Mabao hayo yaliisaidia Liverpool kushika usukani wa ligi katika kipindi cha Christmas iangwa baadae waliteleza mpaka nafasi ya tano katika kipindi cha mwaka mpya. Naye Pellegrini mwezi Desemba ulikuwa mzuri kwake baada ya kushinda mechi zote sita kati ya saba walizocheza huku mmoja wakitoka sare ya kufungana bao 1-1 na Southampton.

No comments:

Post a Comment