STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 30, 2014

Miili ya waliokufa ajali ya Singida waanza kutambuliwa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3HAzgI5ejXZIyNcqMJaTT85XjZvOu2bov0tWDiQnia54biJdpoDHHWW0xYFF75HuMykuls7TOCKVf843bs4_U_60SbULAnYrqhsrxDbBOguGfwBnOHWDTHZRWU8-CxwzgdZkBPuTnO7o/s1600/1.jpg
Baadhi ya miili ya watu waliokufa kwenye ajali iliyosababishwa na basi la Sumry
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEicj2zByf8m-xK1qel4ADrQklEgUEenqOL_dhOswXFx3_FS3FE-RfUGdKF6RvS0-8JPmbot7v-ZvJp6amixQ029lnaoZFqBmhCoDrQ-r7TxE-2l8fsPCRVsJd1DYmAUce3Lu2ffVOYf5Yg/s1600/2.jpg
Ndugu, jamaa na familia za marehemu wa ajali iliyosababishwa na basi la Sumry wakiwa nje ya hospitali kusubiri kutambua miili ya ndugu zao
MIILI ya watu waliofariki kwenye ajali iliyosababishwa na basi la Sumry, iliyoaua watu 19 wakiwamo trafiki wanne imeanza kutambuliwa.
Ajali hiyo ilitokea juzi kwa basi la Sumry lililokuwa linatokea Kigoma kwenda Dar baada ya kuwaparamia watu waliokuwa wakitoa msaada ya mwendesha baiskeli aliyekuwa amekufa kwa kugongwa katika kijiji cha kijiji cha Utaho, wilayani Ikungi, barabara kuu ya Singida- Dodoma.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa Singida, Geofrey Kamwela, alisema siku ya tukio hilo wananchi wakiwa na askari polisi wa doria walikuwa wamekusanyika pembezoni mwa barabara kuupakia mwili wa mwendesha baiskeli, Gerald Zefania, aliyegongwa na lori na kufa papo hapo siku hiyo saa 1:30 jioni.
Alisema wakati wakiupakia mwili huo kwenye gari la polisi namba PT 1424 huku likiwa limeegeshwa pembeni mwa barabara, basi hilo lilitokea ghafla kwa kasi na kuwagonga watu 15 na kufariki dunia papo hapo, wengine wanne walikata roho wakati wakipelekwa hospitalini.
Kamanda Kamwela alisema dereva wa basi hilo, Paulo Njilo, mkazi wa jijini Dar es Salaam baada ya kukaribia eneo hilo aliliona gari la polisi likiwa limeegeshwa pembeni kushoto mwa barabara, lakini wakati akijaribu kulikwepa ndipo alipoliparamia kundi la watu waliokuwa na askari.
 Aidha, alisema dereva wa basi hilo baada ya ajali hiyo aliendelea na mwendo hadi aliposimama kilomita 25 katika makao makuu ya Wilaya ya Ikungi na kutokomea kusikojulikana, lakini juhudi za kumtafuta zinaendelea.
Kamanda huyo aliwataja askari waliokufa kuwa ni F.849 D/CPL Boniface Magubika wa CID Wilaya ya Singida, F.6837 Pc Jumanne Mwakihaba wa FFU Singida, G.7993 Pc, Novatus Tarimo wa ofisi ya RCO na G.8948 Pc, Michael Mwakihaba wa FFU Singida.
Wengine ni Ofisa Mtendaji Kijiji cha Utaho, Ramadhan Mjengi; Mwenyekiti wa Kijiji Utaho, Paul Hamis; Mwenyekiti wa Kitongoji cha Utaho, Ernest Salanga; Said Rajab, Usirika Itambu, Chima Mughenyi, Salim Juma, Abeid Ramadhan, Mwinyi Hamis na Issa Hussein, wote wakazi wa kijiji cha Utaho.
Kamanda Kamwela alisema miili ya marehemu wengine wanne bado haijatambuliwa na ndugu zao na imehifadhiwa kwenye chumba cha maiti katika Hospitali ya Mkoa wa Singida.
Kamanda Kamwela alisema majeruhi wawili kati ya nane wa ajali hiyo  wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa Singida na wengine sita wapo hospitali ya Misheni Malikia wa Ulimwengu iliyopo Puma.
Aliongeza kuwa  miili ya askari polisi inatarajiwa kusafirishwa kwenda katika mikoa wanakotoka wakati wowote baada ya taratibu za kipolisi kukamilika ikiwamo kuwasiliana na ndugu zao walioko mikoa ya Kilimanjaro, Pwani, Mbeya na Iringa.

Chelsea wapata afueni, Terry, Cech warejea dimbani

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Petr+Cech+John+Terry+Blackburn+Rovers+v+Chelsea+jBW-c2W_Ow3l.jpg
Terry na Cech wakipongezana katika moja ya michezo yao
KIPA tegemeo wa Chelsea Petr Cech na nahodha John Terry wanatarajiwa kucheza mechi ya leo na nusu fainali ya Ligi ya mabingwa Ulaya kati yao na Atletico Madrid baada ya wachezaji hao kufanya mazoezi ya timu hiyo tangu juzi.
Ilisemekana Cech asingeweza kucheza tena msimu huu baada ya kuteua bega lake katika mchezo wa kwanza wakati Terry alitolewa nje kutokana na kuumia kifundo cha mguu katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya 0-0. 
Eden Hazard na Samuel Eto’o ambao walikuwa majeruhi wao pia walionekana kuwa fiti kwa kufanya mazoezi  jana, huku viungo John Mikel Obi na Frank Lampard wote hawatakuwepo katika mchezo huo wa marudiano utakaofanyika katika Uwanja wa Stamford Bridge kutokana na kutumikia adhabu ya mechi moja.
Kwa sasa imebaki maamuzi ya kocha Jose Mourinho kuona kama anaweza kuwatumia wachezaji waliorejea toka kwenye majareha kwa ajili ya mechi hiyo kuwania nafasi ya kutinga fainali kuifuata Real Madrid iliyotangulia usiku wa jana kwa kuizabua waliokuwa watetezi, Bayern Munich kwa kwa mabao 4-0.

Malawi yatua kuifuata Stars Mbeya

http://www.malawidemocrat.com/wp-content/uploads/2012/06/Flames-e1339493490888.jpg
Malawi the Flames wanaotua leo kuivaa Taifa Stars
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXy4DjvygUby0tzSChTVErun58_E3LDqa5xJ_i2zWfMLszWFaSyC9gFEfrYDK13Z3ay7OtaoFftdVKgyeW0ng6kOwB9SLKwda42hmSDnjKljVaRMR3dk2Wg9ugd3lFENkSbBF8-a-GegEK/s1600/FKB_1718.JPG
Taifa Stars itakayoikaribisha Malawi ikiwa na kocha mpya Mart Nooij
TIMU ya soka ya taifa ya Malawi (Flames) inatarajiwa kuwasili nchini kesho kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumapili hii kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Mbeya.
Boniface Wambura, Ofisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), alisema jijini Dar es Salaam  kuwa Flames yenye msafara wa watu 31 utakaoongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Soka cha Malawi (FAM) itaingia Mbeya kwa usafiri wa barabara. Wachezaji katika msafara huo watakuwa 20.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ikiwa chini ya Kocha mpya, Mart Nooij tayari ipo jijini Mbeya tangu juzi kujiwinda kwa mechi hiyo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mashindano ya kuwania kufuzu fainali zijazo za Afrika (AFCON) dhidi ya Zimbabwe itakayochezwa jijini Dar es Salaam kati ya Mei 16 na 18 mwaka huu.
Mwishoni mwa wiki Taifa Stars iliyofinyangwa na TFF, ilitia doa sherehe za miaka 50 ya uwapo wa Tanzania baada ya kuchapwa  magoli 3-0 dhidi ya timu ya taifa ya Burundi (Intamba Murugamba) kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

As Vita, Mazembe wapangwa kundi moja Afrika

http://www.adunagow.net/main/wp-content/uploads/Mazembe.jpg
Tp Mazembe

Al Ahly
KLABU za TP Mazembe na AS Vita za DR Congo zimepangwa kundi moja la  A katika Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa pamoja Al Hilal ya Sudan na Zamalek ya Misri.
Kundi B la michuano hiyo limezikutanisha timu za waarabu watupu, Esperance na C.S Sfaxien za Tunisia  E.S Setif ya Algeria na Ahly Benghazi ya Libya.
Katika droo iliyotolewa inaonyesha michezo za makundi hayo zitaanza kuchezwa kati ya Mei 16 na 18 na 23 na 25, Juni 6 na 8, Julai 25 na 27, Agosti 8 na 10 na  22 na 24 huku timu zitakazoshika nafasi mbili za juu kwenye makundi zikisonga Nusu Fainali.

Wakati huo huo ratiba ya makundi kwa michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika nayo imepangwa ambapo wababe wa Yanga, Al Ahly ya Misri imepangwa kundi B linalotajwa kama la kifo.
Kundi hilo linajumuisha timu za  Sewe Sport ya Ivory Coast, Etoile du Sahel ya Tunisia na Nkana Red Devils ya Zambia.
Kundi A lenyewe lina timu za Coton Sport ya Cameroon, ASEC Mimosas ya Ivory Coast, AS Real ya Mali na AC Leopards ya Kongo Brazzaville.
Mechi za michuano hiyo zinatarajiwa kuchezwa kuanzia kati ya Mei 16 na 18 na Juni 23 na 25, Juni 6 na 8, Julai 25 na 27, Agosti 8 na 10 na 22-24 na washindi wawili wa kila kundi watasonga Nusu Fainali.
Makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika
Kundi A: TP Mazembe (DRC), Al-Hilal (Sudan), Zamalek (Misri) na AS Vita (DRC)
Kundi B: Esperance (Tunisia), CS Sfaxien (Tunisia), Entente Setif (Algeria) na Al-Ahly Benghazi (Libya).
Makundi Kombe la Shirikisho Afrika:
Kundi A: Coton Sport (Cameroon), ASEC Mimosa (Ivory Coast), AS Real Bamako (Mali) na AC Leopards (Congo)
Kundi B: Al Ahly (Misri), Sewe Sport (Ivory Coast) Etoile du Sahel (Tunisia) na Nkana Red Devils (Zambia)

Bayern chali yapigwa 4-0 kwao na kuvuliwa taji

* Leo zamu ya Chelsea na Atletico Madrid

UNAWEZA usiamini ila ndivyo ilivyo, mabingwa watetezi wa Ligi ya Ulaya Bayern Munich wamevuliwa taji hilo baada ya kukandikwa mabao 4-0 na Real Madrid na kuwafanya wababe hao wa Hispania kutinga fainali.
Mpango wa kocha Carlo Ancelotti wa kuwapanga washambuliaji wake watatu Karim Benzema, Gareth Bale na Cristiano Ronaldo ulizaa mpango baada ya Real kuisambaratisha Bavarians nyumbani kwao bila kutarajiwa na kuzima ndoto za Pep Guardiola kubadilisha matokeo ya kipigo cha bao 1-0 ilichopewa timu yake katika  mechi ya kwanza.
Mabao mawili ya Sergio Ramos na mengine ya Cristiano Ronaldo yalitosha kukwamisha safari ya wababe hao wa Ujerumani kwenye uwanja wao wa Allianz Arena na kukubali kulitema taji hilo.
Ramos alianza kufunga bao la kwanza dakika ya 16 kwa pasi ya Luka Modric kabla ya kuongeza jingine dakika nne baadaye akimalizia pasi ya Pepe na Ronaldo alikuja kupigilia msumari katika dakika ya 34 kwa pasi ya Bale na kumalizia udhia dakika ya 90 kufunga bao la nne.
Real Madrid sasa inasubiri mshindi kati ya Chelsea ya England na Atletico Madrid wanaoumana leo katika mechi ya marudiano nyingine ya nusu fainali, mechi itakayochezwa mjini London.
Katika mechi ya kwanza timu hizo ziliotoka suluhu ya kutofungana na yeyeote eatakayetumia vyema karata yake ataifuata Real kwenye fainali ya Mei 24 mjini Lisbon Ureno.

Tuesday, April 29, 2014

UEFA yazitia hatiani Man City, PSG

KLABU za Manchester City ya Uingereza na Paris Saint-Germain ya Ufaransa watakabiliwa na adhabu baada ya kukiuka maadili ya sheria ya matumizi ya fedha ya Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA. 
Mbali na hao vilabu vingine vipatavyo 20 vinaaminika kukutwa na hatia ya kuvunja sheria hiyo. 
UEFA itatoa ofa maalumu kwa vilabu hivyo vilivyokiuka sheria hiyo kuelekea katika mkutano wao utakaofanyika Alhamisi. 
Adhabu kubwa ambayo ni timu husika kuenguliwa katika michuano ya Ulaya haitarajiwi kuwepo ingawa pia hawakuweka wazi ni adhabu zipi zitaazotolewa kwa timu hizo.

Rais wa Brazil amuunga mkono Dani Alves Hispania

Dani Alves aliebaguliwa Hispania na shabiki wa Villarreal
Rais wa Brazil  Dilma akiwa na Rais wa FIFA
RAIS Dilma Rousseff, amesifu kitendo cha mchezaji wa kimataifa wa Brazil, na Barcelona Dani Alves kutokana na tukio la ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya ligi kuu ya Uhispania, La Liga kati ya Barcelona na Villareal .
Mchezaji huyo wa Barcelona aliokota ndizi aliyokuwa ametupiwa na kuila kabla ya kuitupa na kuendelea na mchezo.
Bi Rousseff aliandika katika mtandao wake wa twitter kuwa Dani Alves alionyesha ujasiri wa kukabiliana na ubaguzi wa rangi katika kandanda na kuwa ni tukio la kuigwa .
Klabu ya Villarreal inasema kuwa imempiga marufuku mwanaume ambaye alitupa ndizi hiyo uwanjani na kuwa hatohudhuria mechi zote za nyumbani za klabu hiyo maishani.
Mamia ya watu na wachezaji maarufu duniani wameonyesha upendo wao kwa mchezaji huyo kwa kuweka picha zao kwenye mitandao wa kijamii wakila ndizi.
Mchezaji wa Manchester City Sergio Aguero alipachika picha akila ndizi sawa na nyota ya soka ya wanawake Marta .
Wengine ni Luiz Suarez wa Liverpool,Oscar, David Luiz na Willian wote wa Chelsea .
Rais wa Fifa sepp Blatter ameongezea sauti yake katika tukio la hivi punde akisema ni vibaya kwa dhulma hizo kuendelea katika karne hii.
BBC

Elias Maguli ajinadi Simba, Yanga, Azam

Elias Maguli
MSHAMBULIAJI nyota wa Ruvu Shooting, Elias Maguli amesema yupo tayari kutua klabu yoyote kati ya Simba, Yanga au Azam, iwapo ataridhishwa na dau atakalowekewa mezani na klabu hizo.
Maguli aliyeshika nafasi ya pili kwa ufungaji sambamba na Kipre Tchjetche na Mrisho Ngassa, wakiwa nyuma ya Amissi Tambwe aliyeibuka Mfungaji Bora, alisema haoni tatizo kuihama Ruvu Shooting kama kuna klabu inayomhitaji.
Alisema, ingawa mpaka sasa hakuna timu yoyote iliyomfuata kumshawishi kujiunga nayo kwa msimu ujao, lakini amekuwa akisoma na kusikia tetesi tu kuwa Simba inamnyemelea na kusema milango i wazi kwao kama wanamtaka.
Maguli, alisema siyo Simba tu bali hata kama ni Yanga, Azam au Mbeya City inamhitaji yupo tayari kujiunga nayo mradi taratibu zifuatwe na masilahi yawe ya kuridhisha kwa sababu maisha yake yanategemea soka kama ajira.
"Nisiwe muongo zijafuatwa na klabu yoyote mpaka sasa, lakini nasikia tu tetesi za kuhitaji na moja ya klabu kubwa nchini, ila mimi nategemea soka klabu yoyote iliyoridhishwa nami milango i wazi waje tuzungumze," alisema.
Kuhusu kushindwa kuendelea na kasi ya ufungaji kama ilivyokuwa kwenye msimu wa kwanza, Maguli alisema matatizo aliyokuwa nayo kwenye duru la pili ikiwamo kuuguliwa na mama yake na sakata lake la kutimka umangani kusaka soka la kulipwa lilichangia kumfanya aachwe mbali na Tambwe.
Maguli aliyekuwa akishika nafasi ya pili nyuma ya Tambwe katika duru la kwanza wakitofautiana bao moja, Tambwe akiwa na 10 yeye akiwa na 9 alijikuta akiachwa mbali na mpinzani wake huyo aliyefunga bao 19 huku yeye na wenzake wawili wakimaliza msimu na mabao 13 tu.
Aidha Maguli amesema anamshukuru Mungu kwa kuweza kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa, chini ya kocha mpya kutoka Uholanzi, Mart Nooij, akidai ni furaha kwake na kuahidi kutomuangusha.
"Namshukuru Mungu, nilikuwa likizo nyumbani Mara na sasa naelekea Mbeya kwenye kambi, nimefurahi sana kocha mpya kunijumuisha kikosini.

Muumin & Double M Sound kujitambulisha Kigoma

Muumin
BAADA ya kukonga nyoyo za mashabiki wa mikoa ya Shinyanga na Kagera wakati wa sikukuu ya Pasaka, bendi iliyorejeshwa upya ya Double M Sound mwezi ujao inatarajiwa kwenda kujitambulisha kwa wakazi wa Kigoma.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Prince Mwinjuma Muumini aliiambia MICHARAZO kuwa, wanatarajia kwenda kuitambulisha bendi yao katika miji ya Kibondo na Kasulu iliyopo mkoani Kigoma.
Muumin alisema onyesho la kwanza mkoani humo watalifanya Mei 9 mjini Kibondo kabla ya siku inayofuata watahamia Kasulu kabla ya kurejea maskani kwao Kahama-Shinyanga kwa ajili ya kufanya mazoezi za uzinduzi rasmi.
"Tunashukuru tumerejea salama kutoka kwenye maonyesho yetu wakati wa sikukuu ya Pasaka kwa kutambulisha bendi eneo la Kakola, Ushirombo, Ruzewe, Ngara na Katoro. Kwa sasa tupo kambini mjini Kahama kujiandaa na ziara ya mkoani Kigoma mapema mwezi ujao," alisema Muumin.
Muumin aliongeza kuwa uongozi wao unajipanga kufanya uzinduzi na onyesho la kwanza kuitambulisha na kuizindua Double M Sound mjini Kahama mwishoni mwa mwezi ujao.
"Pamoja na watu kujua Double M Sound ipo Kahama, lakini hawajawahi kuiona hadharani kwa sababu tunapanga kuizindua rasmi mwishoni mwa Mei na kisha ndipo tuanze kuifanya maonyesho mjini hapa," alisema Muumin.
Double M Sound iliyowahi kutamba na nyimbo mbalimbali ilisambaratika mara baada ya uzinduzi wa albamu yao ya Titanic mwaka 2004 na Muumin ameamua kuifufua upya na kujichimbia Kahama kama maskani yake kwa sasa.

Kamanda Kova afunguka vifo vya watoto Bwawa la Kuogolea Dar

Picha haihusiani na habari, ila watoto wakifurahia kuoga kwenye bwawa la kuogolea kama wanavyuoonekana
KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum  Suleiman Kova amefafanua juu ya taarifa ya vifo vya watoto watatu
waliofariki wakati wakiongolea kwenye bwawa la hoteli.
Kamanda Kova alisema April 27  kulitokea vifo vya watoto 3 ambao walikua na birthday party nyumbani lakini baada ya kukamilika kwa taratibu za party ya nyumbani waliamua kuimalizia party hiyo hotel ya Landmark,walipofika walienda kuogelea kwenye swimming pool ya watoto lakini baadae watoto hao walitoka kwenye pool ile ya watoto wakaingia kwenye pool ya wakubwa na kwa bahati mbaya waliingia sehemu yenye kina kirefu.
Watoto wenzao walipoona wenzao wanazama walianza kuwavuta kuwatoa nje lakini hali zao tayari zilikua mbaya, mmoja wapo hali yake ilikua kidogo afadhari lakini kwa bahati mbaya nayeye alifia hospital wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Masana na kufanya Idadi ya watoto waliofariki kuwa 3 majina yao ni Janet Zacharia, Eva na Ndimbuni.
Kamanda Kova amesema; "’Kusema kweli sio mara ya kwanza kutokea, mara nyingi vifo vya watoto vinatokana na uangalifu au uzembe kutoka kwa wale wanaotakiwa kuwaangalia hao watoto wao, hizi hotel zote zenye swimming pool lile eneo la kuogelewa basi wasiruhusiwe watoto wadogo kuogelea au kuwe na mtu ambaye anajua kuogelea au kuokoa ambaye yupo pale’
‘Unajua watoto wana tabia ya kuigana mmoja akiingia akiogelea pengine anafahamu kidogo wengine wote wanafata mkumbo wanaona wanaweza,sisi kama jeshi la Polisi tumeamua hili kosa la uzembe kusababaisha kifo kisheria mtu anaweza kushtakiwa kwa kuzembea kwa kutochukua tahadhari mpaka watoto kama wale ambao hawana hatia uwezo wao mdogo wa kufikiri au kuijiokoa’
‘Tunafatilia kwa umakini lakini jukumu la kufatilia maisha ya watoto ni la wazazi mia kwa mia wasipofanya hivi wakiwa hawapo makini matokeo yake ni haya watoto 3 wamefariki,tunaendelea na uchunguzi na baadae tutatoa taarifa kamili’.

Ubingwa mweupe kwa Juventus, yaifumua Sassuolo 3-1

Wachezaji wa tatu wa Juve (jezi za njano) wakiwania mpiura na beki wa Sassuolo walipoikandika timu hiyo mabao 3-1 ugenini
JUVENTUS imebakisha mechi moja tu kutangazwa tena kuwa mabingwa wa Italia baada ya usiku wa kuamkia leo kupata ushindi mnono wa mabao 3-1 ugenini dhidi ya Sassuolo katika mfululizo wa Ligi Kuu ya nchini hiyo Seria A.
Mabingwa hao watetezi ambao Alhamis hii watakuwa nyumbani kwao kuwakaribisha Benfica ya Ureno kwenye mechi ya marudiano ya Nusu Fainali ya Ligi Ndoigo ya Ulaya (UEFA Europa League) ili kujaribu kupindua matokeo ya kipigo cha mabao 2-1, ilishtukiza kwa bao la mapema la dakika 9 la wenyeji liliwekwa kimiani na Simone Zaza.
Hata hivyo wakati wakitafakari jinsi ya kulirudisha bao hilo wenyeji hao waliwasaidia  kulisawazisha wenyewe baada ya Alessandro
Longhi kujifunga dakika ya 34.
Juventus maarufu kama kibibi kizee cha turin, iliongeza bao la pili katika dakika ya     58 kupitia Claudio Marchisio kabla ya Llorente kufunga bao la tatu katika dakika ya 76 na kuifanya timu hiyo kufikisha pointi 93, nane zaidi na ilizonazo wanaoshikilia nafasi ya pili Roma wenye pointi 85 na kila timu ikiwa imesaliwa na mechi tatu kabla ya kufunga msimu huu.

Arsenal yapumua, yaifumua Newcastle United 3-0

KLABU ya soka ya Arsenal imefufua matumaini yake ya kuwepo kwenye Top 4 na kushiriki moja kwa moja Ligi ya Mabingwa ya Ulaya bada ya usiku wa kuamkia kuitandika Newcastle United kwa mabao 3-0 kwenye uwanja wa wa Emirates, mjini London.
Mabao ya Laurent Koscielny katika dakika ya 26, Mesut Ozil aliyefunga dakika ya 42 na jingine la Olivier Giroud yaliweka Arsenal pazuri ikiwa imepata ushindi wa tatu mfululizo na kuzidi kuikimbia Everton wanaoifukuzia nafasi yao.
Arsenal waliokuwa vinara wa ligi ya England kwa muda mrefu kabla ya kuporomoka, itasubiri kujua hatma yake ya kutwaa nafasi ya nne baada ya pambano la Everton na Manchester City mwishoni mwa wiki, kama Everton itateleza kama ilivyofanya katika mechi zake zilizopita basi vijana wa Gunners watakuwa wamejihakikisha kutwaa nafasi hiyo na kucheza ligi ya mabingwa moja kwa moja.
Vijana hao wa Arsene Wenger wamekusanya jumla ya pointi 73 nne zaidi na iliyonazo Everton waliopo nyuma yao na pointi 69.

Ajali tena! Zaidi ya 15 wafariki ajalini usiku wa kuamkia leo Singida

Picha haihusiani na habari hii, lakini ni miongoni mwa mabasi ya Sumry lililowahi kupata ajali siku za nyuma.
WATU 13 akiwemo askari wa kikosi cha usalama barabarani (Trafiki) wamepoteza maisha baada ya kugongwa na basi la kampuni ya Sumry lililokuwa likitoka Kigoma kwenda Dar katika kijiji cha Ikungi mkoani Singida usiku wa kuamkia leo.
Ajali hiyo ilitokea baada ya ajali ya kwanza iliyolihusisha lori lililomgonga mwendesha baiskeli aliyepoteza maisha papo hapo na wakati wananchi wakiwa wamekusanyika eneo hilo la ajali huku trafiki akiendelea kupima ajali hiyo, lilitokea basi la kampuni ya Sumry na kuwagonga watu hao pamoja na trafiki na kupelekea jumla ya watu 14 kupoteza maisha eneo hilo.
Basi hilo lililokuwa likitokea Kigoma kwenda Dar halikuweza kusimama eneo hilo mpaka dereva wake alipokwenda kujisalimisha kituo cha polisi Ikungi, Singida. 
Miili 14 ya waliopoteza maisha katika ajali hiyo imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa mkoani Singida pamoja na majeruhi wawili waliopelekwa hospitalini hapo.
MUNGU AZILAZE ROHO ZA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!

Ronaldo, Bale, Benzama kuanza pamoja 'kuiua' Bayern, Klopp atabiri

Bale na Ronaldo
WAKATI kocha hasimu wa Bayern Munich, Jurgen Klopp wa Borussia Dortmund akiwapa nafasi kubwa mabingwa watetezi hao kutinga fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya, miamba wa soka wa Hispania, Real Madrid timu yenye mafanikio zaidi katika historia ya michuani hiyo  wakitwaa taji hilo mara tisa wamepania safari hii kuondokana na mzimu wa kulikosa kila mara kwa miaka 12  sasa.
Madrid imeangukia katika hatua ya nusu fainali katika michuano yote mitatu iliyopita, mara mbili ikitolewa dhidi ya timu za Ujerumani.
Borussia Dortmund waliwafunga jumla ya magoli 4-3 katika nusu fainali ya mwaka jana wakati Bayern waliwatoa kwa 'matuta' katika nusu fainali ya msimu wa 2011-12 lakini wanaingia katika mechi ya leo ya marudiano kwenye Uwanja wa Allianz Arena kwa ushindi wa 1-0, kufuatia kiwango cha juu walichoonyesha katika mechi yao ya awali mjini Madrid.
Karim Benzema alifunga goli pekee la mechi hiyo, kuipa timu ya kocha Carlo Ancelotti uongozi, lakini, licha ya hilo, watatakiwa kuwachunga Bayern ambao wamekuwa na mafanikio chini ya kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola.
Mabingwa hao wa Bundesliga wanafukuzia kutwaa makombe matano chini Guardiola baada ya kutwaa Uefa Super Cup na Kombe la Dunia la Klabu, huku pia wakiwasubiri Borussia Dortmund katika fainali ya Kombe la 'FA' la Ujerumani la DFB-Pokal.
Bayern wamepoteza mechi nne tu nyumbani tangu mwanzo wa msimu huu, huku Manchester City na Arsenal zikiwa ni timu pekee za Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya zilizoonja mafanikio kwenye Uwanja wa Allianz Arena katika kipindi hicho, lakini Ancelotti amesisitiza timu yake itakwenda kwenye mechi hiyo ikijiamini wakati wakidhamiria kutwaa makombe matatu katika msimu wa kwanza chini ya kocha huyo Muitalia.
"Nina imani na wachezaji na nadhani kila mmoja anapaswa kuwa hivyo pia," aliuambia mkutano na waandishi wa habari wa Hispania. "Mpango wetu mjini Munich ni kufunga, kuliko kujilinda."
Ancelotti alibainisha kuwa washambuliaji watatu wa Madrid, Benzema, Cristiano Ronaldo na Gareth Bale, wote wataanza mjini Munich.
Alvaro Arbeloa, Jese Rodriguez na Sami Khedira (wote goti) ndiyo wachezaji pekee watakaokosa Real.
Beki Rafinha amerejea kwa Bayern baada ya kutumikia adhabu ya kadi katika mechi ya ligi wikiendi lakini, wakati Thiago amerejea mazoezini, Holger Badstuber (goti), Xherdan Shaqiri (paja) na Tom Starke (kiwiko) wote bado wako nje ya uwanja.
Bayern wamekuwa wakitajwa kama timu inayopewa nafasi kubwa zaidi ya kutwaa taji hilo kwa muda wote wa michuano na Guardiola anaamini kwamba mabingwa hara tano wa Ulaya wanaweza kupindua matokeo ya mechi yao ya awali.
"Ninaiamini kwa asilimia 100 timu yangu," Mcatalunya huyo aliiambia tovuti rasmi ya klabu hiyo ya mjini Munich. "Tunaweza kama tutafanya kazi pamoja."
Mshambuliaji wa Bayern, Mario Mandzukic na nyota wa Madrid, Sergio Ramos, Xabi Alonso na Asier Illarramendi watakosa fainali kama watapigwa kadi za njano katika mechi hiyo ya leo.
Licha ya kuwa bado na nafasi ya kutwaa taji hilo, staili ya uchezaji inayofundishwa na Guardiola imezidi kupoteza umaarufu na haiwavutii wakosoaji wa Bayern.
"Kumiliki mpira hakuna maana yoyote pale mpinzani wako anapotengeneza nafasi bora zaidi yako. Tuna bahati walifunga goli moja tu," alisema rais wa heshima wa Bayern, Franz Beckenbauer katika ukosoaji wake mpya alioutoa karibuni dhidi ya staili ya kucheza ya Guadiola ya tiki-taka la Kijerumani.
Katika hatua nyingine meneja wa klabu ya Borussia Dortmund, Jurgen Klopp ameipa nafasi Bayern Munich kugeuza matokeo ya kufungwa bao 1-0 na Real Madrid katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Bao la Karim Benzema lilitenganisha timu hizo mbili katika mchezo huo uliofanyika wiki iliyopita katika Uwanja wa Santiago Bernabeu baada ya Madrid kucheza mchezo wa tahadhari kubwa.
Hata hivyo, Klopp ambaye timu yake ilienguliwa na Madrid katika mzunguko wa mwisho anaamini mahasimu wao Bayern watashinda mchezo huo.
Klopp amesema bado anashawishika kuamini kuwa Bayern wanaweza kushinda hususani kwa mchezo maridadi waliouonyesha mara ya kwanza pamoja na kufungwa. Bayern na Madrid zinatarajiwa kukwaana kesho katika mchezo wa marudiano kutafuta nafasi ya kucheza fainali ya michuano hiyo itakayofanyika jijini Lisbon, Ureno.

Chelsea ilipaki mabasi mawili Anfield, kocha Liver alia

Makocha wanaofukuzana kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England
MENEJA wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers amemtuhumu meneja wa Chelsea Jose Mourinho kwa kupaki mabasi mawili na kuipa ushindi wa mabao 2-0 katika Uwanja wa Anfield. 
Katika mchezo huo mabao ya Chelsea yalifungwa na Demba Ba aliyetumia vyema makosa ya nahodha Steven Gerrard kipindi cha kwanza na lingine la Willian katika majeruhi. 
Kocha Rodgers amesema wapinzani wao walipaki mabasi mawili langoni mwao akimaanisha walikuwa wakizuia kipindi chote cha mchezo huo hivyo kuwapa wakati mgumu kupenya ngome yao ingawa walijitahidi kujaribu. 
Rodgers amesema walijitahidi kushinda mchezo huo lakini walishindwa kupenya ngome ya wapinzani wao ambayo ilikuwa ikilindwa vizuri. 
Pamoja na ushindi huyo Mourinho bado ameendelea kudai kuwa hawana nafasi ya kunyakuwa ubingwa wa Ligi Kuu na kudai kuwa mbio hizo wamewaachia Manchester City na Liverpool. 
Mreno huyo amesema kitu cha msingi alichokuwa akihitaji ni kupata alama tatu hizo muhimu ambazo zitawasaidia kujihakikishia nafasi tatu katika msimamo wa ligi hivyo kufuzu moja kwa moja bila kucheza mechi za mtoano katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.
Timu hiyo ya Mourinho kesho itakuwa na kibarua kizito mbele ya Atletico Madrid katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya nusu fainali.
Katika mchezo wa kwanza timu hizo zilitoka suluhu bila kufungana mjini Madrid na hivyo Chelsea inapatakiwa kuhakisha inapata ushindi au sare isiyokuwa na mabao iwapo inataka kufuzu hata kwa mikwaju ya penati.

Neymar akemea ubaguzi wa rangi Hispania

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Neymar amesema atapambana na ubaguzi wa rangi baada ya mchezaji mwenzake Dani Alves kurushiwa ndizi wakati wa mechi yao waliyoshinda 3-2 ugenini dhidi ya Villarreal juzi.
"Sisi sote tuko sawa, sisi sote ni nyani, sema hapana kwa ubaguzi wa rangi," Neymar aliandika katika ukurasa wa mtandao wake wa kijamii, akiweka 'hashtag' #SisiSoteNiNyani.
"Ni aibu kwamba hadi mwaka 2014 bado kuna matendo kama haya. Ni wakati sasa wa watu kuinua sauti zao kukemea. Njia yangu ya kusapoti ni kufanya alichofanya Dani Alves.
"Kama nawe unasapoti kampeni hii, jipige picha ukila ndizi nakisha tutaitumia katika kupinga ubaguzi huu."

Del Piero atundika daluga zake

MCHEZAJI mkongwe Alessandro Del Piero ameamua kutundika daruga kuitumikia klabu ya Sydney FC lakini anaweza kurejea kwa shughuli nyingine. 
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Juventus amekuwa akihusishwa na tetesi za kuwa kocha katika klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu nchini Australia baada ya Frank Farina kutimuliwa. 
Del Piero, 39 na klabu hiyo wanataka kuendelea na mahusiano lakini haijabainika wazi ni uhusiano wa namna gani. 
Akiwa amefunga jumla ya mabao 24 yakimfanya kuwa mfungaji bora wa klabu katika misimu yote miwili aliyoitumikia, mkali huyo aliandika ujumbe kushukuru na kuaga kupitia mtandao wake. 
Del Piero amesema katika ujumbe huo ule wakati umewadia safari yake akiwa na Sydney FC inakaribia ukingoni ingawa inasikitisha lakini amekuwa na muda mzuri katika kipindi chote alichoitumikia.

Haya ndiyo makundi ya AFCON 2015

Kocha Steven Keshi akiwa amebebwa baada ya kuipa Nigeria taji la AFCON 2013 nchini Afrika Kusini

WAKATI Tanzania itaanzia katika hatua ya awali ya michuano ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2015, mabingwa watetezi Nigeria watawakabili Afrika Kusini na Sudan katika kundi lao la kuwania kutinga katika fainali hizo zitakazofanyika Morocco.
Kikosi cha kocha Stephen Keshi kilitwaa kombe hilo kwa mara ya tatu mwaka 2013 kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Burkina Faso na watakutana na wenyeji wa mwaka huo, Afrika Kusini, katika kuwania kufuzu kwa fainali za 2015.
Timu hizo mbili zinaungana na Sudan katika Kundi A, wakati timu nafasi moja ya mwisho ya kufuzu kuingia katika kundi hilo kutokea katika hatua ya awali itagombewa na timu za Namibia, Congo, Libya au Rwanda.
Burkina Faso watakabiliana na Angola na Gabon katika Kundi C, na nafasi moja ya mwisho itagombewa na timu za Liberia, Lesotho, Kenya na Comoro.
Ivory Coast na Cameroon, ambao wataungana na Nigeria katika fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil, wamepangwa pamoja katika Kundi D la kuwania kufuzu pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Ghana - taifa jingine litakaloenda kwenye Kombe la Dunia - litakabiliana na mahasimu wao wa Afrika Magharibi, Togo katika Kundi  E, wakati Algeria, wawakilishi wengine wa Afrika nchini Brazil, watakuwa na mechi dhidi ya Mali na Ethiopia katika Kundi B.
Mabingwa mara saba Misri watawavaa Tunisia na Senegal katikaKundi G.

Makundi yote ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika 2015 kwa ujumla:

Kundi A: Nigeria, Afrika Kusini, Sudan na moja kati ya Namibia, Congo, Libya na Rwanda

Kundi B: Mali, Algeria, Ethiopia na moja kati ya Sao Tome na Principe, Benin, Malawi na Chad

Kundi C: Burkina Faso, Angola, Gabon na moja kati ya Liberia, Lesotho, Kenya na Comoros

Kundi D: Ivory Coast, Cameroon, DR Congo na moja kati ya Swaziland, Sierra Leone, Gambia na Shelisheli

Kundi E: Ghana, Togo, Guinea na moja kati ya Madagascar, Uganda, Mauritania na Equatorial Guinea

Kundi F: Zambia, Cape Verde, Niger na moja kati ya Tanzania, Zimbabwe, Msumbiji na Sudan Kusini

Kundi G: Tunisia, Misri, Senegal na moja kati ya Burundi, Botswana, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Guinea Bissau.

Monday, April 28, 2014

Bayern Munich kutema taji la Ulaya kesho kwa Real Madrid?

* Chelsea kujiuliza upya kwa Atletico Jumatanohttp://static.goal.com/389000/389072_heroa.jpgMABINGWA watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich ya Ujerumani kesho itakuwa na kibarua cha kuamua kusuka au kunyoa, watakapoikaribisha Real Madrid katika mechi ya mkondo wa pili wa Nusu Fainali ya michuano hiyo kabla ya Chelsea na Atletico Madrid  wakijiuliza siku ya Jumatano.

Watetezi hao walicharazwa bao 1-0 katika mechi ya mkondo wa kwanza iliyochezwa wiki iliyopita nchini Hispania ambao mabingwa wa kihistoria, Real Madrid walikosa mabao mengi ya wazi na kuwapa presha kubwa Bavarians.
Bayern italazimika kubadilisha matokeo hayo mbele ya vijana wa Carlo Ancelotti ambao wana kiu ya kutaka kunyakua taji la michuano hiyo baada ya kulikosa kwa miaka 12 na pia wakitaka kufikia idadi ya kulibeba mara 10.
Hofu ya Bavarians watakaokuwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Allianz Arena ni kurejea tena kwa Cristiano Ronaldo ambaye katika mechi ya kwanza aliicheza akiwa na maumivu kabla ya kutolewa kipindi cha pili kumpisha Gareth Bale aliyekuwa akisumbuliwa na mafua.
Hata hivyo Bayern chini ya Pep Guardiola haitabali kufanywa daraja na wapinzani wao kuelekea kwenye fainali zitakazofanyika nchini Ureno katikati ya mwezi ujao.
Ikiwategemea nyota wake kama Franck Ribery, Arjen Robben, Mario Gotze, Mario Mandzukic, Dante, Thomas Muller na kiungo matata Bastian Schweinsteiger ina uhakika na kuivusha tena timu hiyo katika mchezo wa fainali kama ilivyokuwa mwaka uliopita ilipoenda kukumbana na Borussia Dortmund na kubeba taji hilo baada ya kulikosa mikononi mwa Chelsea mwaka 2012.
Kivumbi kingine cha nusu fainali kitakuwa siku ya Jumatano mjini London wakati Chelsea itakapokuwa uwanja wa Stanford Bridge kuikaribisha vinara wa La Liga, Atletico Madrid ambao wiki iliyopita wakiwasimamisha na kwenda nao suluhu ya kutofungana mjini Madrid.
Chelsea iliyofufua tumaini la kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu ya England baada ya jana kuizabua Liverpool wanaoongoza msimamo watashuka Stanford Bridge ikiwakosa baadhi ya wachezaji wake nyota akiwamo kipa Petr Cech na nahodha John Terry walioumia katika pambano la awali.
Hata hivyo mbinu za kocha Jose Mourinho katika kukabiliana na wapinzani wake inawapa matumaini mashabiki wa Chelsea kuamini kuwa wanaweza kuwasimamisha vijana wa Diego Simeone ambayo msimu huu imekuwa moto wa kuotea mbali.
The Blues watakuwa na kazi ya kuwachunga nyota wa Atletico, Diego Costa, Diego, Koke, Thiago, David Villa, Gabi na Raul Garcia ambao wameifanya timu yao msimu huu kuzima ubabe wa Real Madrid na Barcelona nchini Hispania.
Mashabiki wana hamu kubwa ya kutaka kujua ni timu zipi mbili zitakazofuzu hatua fainali na kushuhudia moja wapo ikitawazwa kuwa bingwa mpya mjini Lisbon Ureno mnamo Mei 24.
Je Bayern itakubali kuvuliwa taji na Real Madrid au Chelsea itatepeta nyumbani dhidi ya Atletcio Madrid? Tusubiri tuone.

Newz Alert! Polisi Mbeya yatimua askari 6 kisa...!

Kamanda wa Polisi  Mkoani Mbeya  Ahmed Msangi
JESHI la Polisi Mkoani Mbeya limewafukuza kazi Askari 6 wa kikosi cha Usalama barabarani  Wilaya za Rungwe na Mbeya kwa tuhuma za kuomba,kushawishi na kupokea rushwa.

Kamanda wa Polisi  Mkoani Mbeya  Ahmed Msangi amewatataja Askari hao kuwa ni pamoja na waliokuwa wakifanya kazi wilaya ya Mbeya barabara ya Mbeya/Tunduma eneo la Songwe ni Copro Jonson,PC Rymond na PC Simon.

Msangi amewataja wengine kuwa ni pamoja Sajini Hezron,PC Shaban na PC Kajolo ambao walikuwa wanafanya kazi barabara ya Mbeya/Rungwe wilaya ya Rungwe.

Askari hao walikuwa wanakabiliwa na makosa hayo na walifikishwa katika Mahakama ya Kijeshi na Hukumu kutolewa Aprili 24 mwaka huu na kupewa adhabu ya kufukuzwa kazi.

Aidha Kamanda Msangi amesema Jeshi lake halitasita kuwafukuza kazi Askari watakaokwenda kinyume na maadili ya Jeshi la Polisi na Askari yeyote atakayekwenda kinyume atakumbwa na adhabu kali ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi au kufikishwa mahakamani.

Askari wengine waliofukuzwa kazi hivi karibuni ni pamoja na PC James Kagomba ambaye amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa kutumia silaha,WP Prisca Kilwai anayekabiliwa na kesi ya wizi wa mtoto.

Wengine wliohukumiwa kifungo cha mwaka mmoja baada ya kukutwa na hatia ya kuua bila kukusudia ni DC Marcelino Venance mwenye namba 8084,PC Juma Idd mwenye namba 3117 na Askari wa Mgambo MG Jackson Mwakalobo ambao walidaiwa kusababisha kifo cha mwanafunzi Dentho Kajigili aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari Ivumwe ya Jijini Mbeya. 

Na Mbeya yetu

Subira ya Shaa apewa Adam Juma

MTAYARISHAJI mahiri wa video za muziki wa kizazi kipya nchini, Adam Juma wa Visual Lab, amepewa shavu la kurekodi video ya wimbo mpya wa mwanadada Sarah Kais 'Shaa' uitwao 'Subira'.
Wimbo huo ambao awali ulikuwa ukifahamika kama 'Sifa Ujinga' kabla ya kubadilishwa jina, unatarajiwa kurekodiwa video yake wiki ijayo.
Mmoja wa mabosi wa Shaa ambaye anafanya kazi na Mkubwa na Wanae kwa mkataba maalum, Said Fella aliiambia MICHARAZO kuwa, wameamua kumpa 'shavu' Adam Juma kuiandaa video ya wimbo huo ambao umekamilika tangu mwishoni mwa mwaka jana.
"Baada ya kutafakari kwa kina tumeamua kumpa nafsi nyingine mkali Adam Juma kufyatua video ya wimbo mpya wa Shaa uitwao 'Subira' na kazi ya kurekodi inatarajiwa kuanza wiki ijayo hapa jijini Dar es Salaam," alisema.
Fella alisema wanatarajia video hiyo iwe kali kufunika hata ile ya wimbo wa 'Sugua Gaga' ambao umekuwa ukifanya vyema kwenye vituo vya runinga nchini ikiwa ni kati ya kazi za kwanza za Shaa chini ya Mkubwa na Wanae.

Simba yaomboleza kifo cha Muchacho, yafafanua suala la katiba

http://sundayshomari.files.wordpress.com/2014/04/simba-300x286.jpg 
MWENYEKITI wa Simba SC, Mhe; Ismail Aden Rage, ametuma salamu za rambirambi kwa ndugu, jamaa, marafiki na familia ya Marehemu Abdulrahman Muchacho (66), aliyefariki dunia jijini Dar es Salaam na kuzikwa juzi katika makaburi ya Kisutu jijini.
Muchacho ni miongoni mwa wanachama wenye historia ya kipekee ndani ya klabu kwani akiwa Timu Meneja wa Timu ya Simba mwaka 1976, Simba iliifunga Yanga mabao 6-0, ambao ndiyo mshindi mnono zaidi kuwahi kutokea katika historia ya mechi za Watani wa Jadi na akiwa Mweka Hazina wa Timu katika miaka ya 1990, Simba ilicheza katika Fainali ya Kombe la CAF.
Mwanachama huyu ndiye pia chachu ya kuanzishwa kwa kundi la ushangiliaji la Muchacho ambalo ndilo chimbuko la makundi yote ya ushingilijiaji katika viwanja vya soka hapa nchini.
"Kwa kweli msiba huu umenigusa sana hasa ukizingatia kwamba niliona utendaji wake wakati mimi nikiwa mchezaji wa Simba na baadaye katika uongozi. Msiba wa Muchacho ni mkubwa kwa klabu kwa sababu jina lake litabaki kuwa sehemu ya historia iliyotukuka ya Simba SC.
"Muchacho anatoka katika familia ya wana Simba. Baba yake alikuwa shabiki mkubwa wa Sunderland na mrehemu alikuwa mrithi mzuri wa mapenzi haya ya baba yake. Kwa sababu ya mambo ambayo wameifanyia klabu, jina la Muchacho na Simba vitaendelea kudumu, daima na milele," alisema Rage.

MSAJILI.
KLABU ya Simba inapenda kukanusha upotoshaji unaofanywa na baadhi ya watu kupitia vyombo vya habari kwamba Katiba ya Simba bado haijapelekwa katika Ofisi za Msajili.
Katiba ya tayari iko kwa Msajili kwa Zaidi ya wiki moja sasa na kilichobaki ni taratibu za kawaida za serikali kuhakikisha kwamba mchakato huu unamalizika kwa faida ya pande zote.
Simba SC inatumia nafasi hii kuwaomba wanachama na wapenzi wake kuwa watulivu wakati wakisubiri Ofisi ya Msajili wa Vyama na Vilabu kufanya kazi yake. 

Tangu mwanzo tulikubali kwamba Katiba yetu itatumika mara tu baada ya kupitishwa na TFF na Ofisi ya Msajili ambao wanafanya kila kitu kwa taratibu zao.
Ni vema pia watu wakaacha kueneza maneno ya uongo kuhusu Katiba kutopelekwa kwa Msajili kwa vile taarifa kama hizo zina lengo tu la kupotosha na kutaka kusababisha rabsha hata pasipo na sababu.
Mchezo wa mpira ni wa kistaarabu na ni vema wastaarabu wote wakatulia na kusubiri majibu kutoka katika Ofisi ya Msajili.

Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Katibu Mkuu
Simba SC

Barca chupuchupu, Messi aibeba yaiengua Real Madrid

http://e2.365dm.com/14/04/660x350/Lionel-Messi-Barcelona-2014_3132310.jpg?20140427222759
http://peruzonatv.com/wp-content/uploads/2014/03/Barcelona-vs-Osasuna-en-vivo.jpg?0e806a
Messi akishangilia bao lake na wachezaji wenzake wa Barcelona
KLABU ya Barcelona usiku wa kuamkia leo imeponea tundu la sindano baada ya kupata ushindi wa mabao 3-2 ugenini dhidi ya Villarreal na kuzidi kuendelea kuwepo kwenye mbio za ubingwa.
Bao la dakika ya 83 kupitia kwa Lionel Messi akimalizia kazi nzuri ya Cesc Fabregas na mawili ya kujifunga ya wachezaji ya Villarreal ndiyo yaliyoibeba Barca waliotanguliwa kufungwa na wenyeji wao.
Cani aliifungia Villarreal bao la kuongoza dakika ya 45 akimalizia kazi nzuri ya Jonathan Pereira kabla ya Trigueros kuongeza la pili dakika ya 55 baada ya kumegewa pande na Aquino.
Hata hivyo mabao mawili ya kujifunga kupitia kwa Gabriel Paulista dakika ya 65 na jingine la dakika ya 78 kupitia kwa Musacchio yalifanya matokeo kuwa mabao 2-2 kabla ya Messi kufunga bao la ushindi dakika ya 83 na kuwapa Barca ushindi huo muhimu.
Matokeo hayo yameifanya Barca kufikisha jumla ya pointi 84 na kuchupa toka nafasi ya tatu hadi ya pili wakiishusha Real Madrid yenye pointi 82, na pointi nne nyuma ya vinara Atletico Madrid.

Suarez ndiye Mwanasoka Bora England


MSHAMBULIAJI nyota wa Liverpool, Luis Suarez ambaye jana alishindwa kuinusuru timu yake kuepuka kipigo toka kwa Chelsea ameteuliwa kuwa Mwanasoka Bora wa Mwaka.
Eden Hazard wa Chelsea alishika nafasi ya pili katika tuzo hiyo ya wachezaji wa kulipwa PFA Player of the Year na kiungo wa Manchester City, Yaya Toure alinyakua nafasi ya tatu.
Suarez ambaye anakumbukwa kwa vituko alivyofanya kwa msimu uliopita anakuwa mchezaji wa pili wa Liverpool kunyakua tuzo hiyo katika miaka 25 iliyopita baada ya nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard kufanya hivyo mwaka 2006. Klabu hiyo ilishawahi kunyakua tuzo hizo nne kati ya mwaka 1980-88 kupitia wachezaji wake wa zamani Terry McDermott, Kenny Dalglish, Ian Rush na John Barnes.
Suarez kufikia mafanaikio hayo baada ya kuifungia timu yake mabao 30 na ndiye anayeongoza matumaini ya timu yake kukatisha ukame wa miaka 24 ya kunyakua taji la Ligi Kuu ya England.Kabla ya kutwaa tuzo hiyo, Suarez alipamba vyombo vya habari za England na matukio aliyowahi kuyafanya siku za nyuma ikiwamo kumng'ata beki wa Chelsea  Chelsea Branislav Ivanovic na lile tukio la kudaiwa kumfanyia ubaguzi nahodha wa Manchester United, Patrick Evra na kutozwa faini na kusimamishwa mechi kadhaa.
Mchezaji huyo toka Uruguay pia alijumuishwa kwenye kikosi cha msimu sambamba na Eden Hazard wa Chelsea aliyetajwa kama mchezaji mchanga wa mwaka huu, Daniel Sturridge na nahodha wa Liverpool Steven Gerrard.
Wengine katika kikosi hicho ni; Kipa wa Chelsea aliye majeruhi kwa sasa Petr Cech, Gary Cahil, Yaya Toure, Vincent Kompany, Luke Shaw, Adam Lallana, Seamus Coleman wa Everton.

Sunday, April 27, 2014

Atletico Madridi yazidi kupeta Hispania, Sevilla yapigwa 3-1


Atletico Madrid wakipongezana baada ya Raul Garcia kufunga bao pekee dhidi ya Valencia
Leading by example: The Atleti captain was too strong in the air for Valencia's defence to handle
Raul Garcia akishangilia bao lake
KLABU ya Atletico Madrid imezidi kujiimarisha kwenye harakati zao za kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu ya nchini Hispania baada ya usiku huu kupata ushindi wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Valencia.
Bao pekee la kichwa lililofungwa na Raul Garcia katika dakika ya 43 lilitosha kuipaisha Atletico kwa klufikisha pointi 88, sita zaidi ya wapinzani wao Real Madrid wanaowafukuzia kwenye nafasi ya pili.
Washindi hao wanaotarajiwa kushuka dimbani keshokutwa kuumana na Chelsea kwenye mechi ya mkondo wa pili ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya umeifanya kusaliwa na mechi mbili tu kati ya tatu kutawazwa kuwa mabingwa wapya.
Katika mchezo huo beki wa Atletico Juanfran alijikuta akitolewa nje dakika za lala salama kwa kadi nyekundu kutokana na madhambi aliyofanya.
Watetezi wa taji hilo Barcelona waliopo nafasi ya tatu watashuka dimbani baadaye kuumana na Villarreal ikiwa ugenini kujaribu kurejesha matumaini yao.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Athletic Bilbao ikiwa nyumbani ilipata ushindi mnono wa mabao 3-1 dhidi ya wageni wao Sevilla.
Mabao ya washindi yalitupiwa kimiani na Susaeta dakika ya tano kabla ya Muniain kuongeza la pili dakika ya 53 na Ander Herrera kufunga la tatu dakika ya 73 kabla ya wana nusu fainali wa Ligi Ndogo ya Ulaya Sevilla iliyocheza pungufu ya mchezaji mmoja kupata bao la kufutia machozi kupitia kwa  Gameiro katika dakika ya 79.
Ushindi huo umeifanya Bilbao kuzidi kujiweka pazuri katika mbio zao za kuwania ushiriki wa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya mtoani ikiishusha Sevilla katika nafasi ya nne.

Manchester City yatakata England

Pole position: Manchester City moved back into the driving seat in the title race with victory at Crystal Palace
Samir Nasir akishangilia bao la Dzeko aliyembeba
Yaya Toure gives Manchester City a 2-0 lead against Crystal Palace at Selhurst Park
Yaya Toure akifunga bao la pili la Man City
MBIO za ubingwa wa Ligi Kuu ya England zimezidi kuwa ngumu kutabirika baada ya usiku huu Manchester City kupata ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Crystal Palace na kuijongelea Chelsea iliyoisimamisha Liverpool ikiwa nyumbani jioni ya leo.
Bao la mapema la dakika ya nne lililofungwa na Edin Dzeko na lingine kupitia wa Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure dakika mbili kabla ya mapumziko ziliwafanya vijana wa Manuel Pellegrini kufikisha pointi 77, moja nyuma ya Chelsea yenye 78 na mbili pungufu na zile za Liverpool yenye pointi 80.
Manchester hata hivyo imecheza mechi pungufu zaidi ya wapinzani wao waliosaliwa na mechi mbili kila moja, huku wenyewe wakiwa na mechi tatu kabla ya kumalizia msimu wa ligi hiyo.
Kwa kipigo hicho cha nyumbani Crystal Palace imeendelea kusalia kwenye nafasi ya 11 ikiwa na pointi 43 kutokana na mechi 36.
Kipute cha ligi kitaendelea tena kesho kwa pambano moja tu litakalowakutanisha Arsenal watakaokuwa nyumani kuwakaribisha Newcastle United, wakiwa katika mbio za kujihakikisha nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani wakichuana na Everton ambayo jana ilifungwa na Southampton ikiwa kwao.

Ngorongoro Heroes yawafuta machozi Watanzania

* Waing'oa Kenya kwa mikwaju ya penati
Mchezaji Idd Suleimana Tanzania akichanja mbuga mbele ya wachezaji wa Kenya U20
TIMU ya soka ya taifa ya Vijana U20, Ngorongoro Heroes jioni hii imewafuta machozi Watanzania baada ya kuiodnosha patupu timu ya Kenya kwa kuifunga mkwaju ya penati 4-3 katika mechi ya kuwania kucheza Fainali za Afrika.
Ngorongoro imepata ushindi huo baada ya kushindwa kutambiana na vijana wenzo katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa ikiwa ni siku moja tangu kaka zao kunyukwa 3-0 na Burundi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki kuadhimisha sherehe za Muungano.
Katika mechi hiyo Tanzania ilipata penati kupitia kwa Kevin Friday, Mohammed Hussein, Mange Chagula na Iddi Suleiman, huku Mudathir Yahya alikosa yake.
Wakenya walipata penati zao kupitia Geofrey Shiveka, Timonah Wanyonyi na Victor Ndinya, huku Evans Makari na Harison Nzivo walipoteza.

Kwa kufuzu huko Tanzania sasa inatarajiwa kuvaana na Nigeria katika hatua inayofuata katika kuwania kucheza fainali hizo zitakazofanyika nchini Senegal.

Papa Francis aweke rekodi, ateua mapapa wawili kuwa watakatifu

Papa Francis, kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani
UMATI mkubwa wa watu wamekusanyika mjini Vatican kushuhudia tukio la kihistoria ambapo viongozi wawili wa zamani wa Kanisa Katoliki, Papa John Paul II na Papa John XXIII wametangazwa watakatifu.
Ibada iliyoendeshwa kwa pamoja kati ya Papa Francis na mtangulizi wake Papa Benedict XVI imeangaliwa na karibu mahujaji milioni moja na wengine mamilioni ya watu kupitia matangazo ya televisheni na redio.
Karibu ujumbe wa wageni 100 wamehudhuria sherehe hiyo, wakiwemo kutoka koo za kifalme na wakuu wa nchi na serikali.
Hii ni mara ya kwanza kwa papa wawili kutangazwa kwa wakati mmoja kuwa watakatifu.
Waandishi wa habari wanasema hatua hii inachukuliwa kama njia ya kuziunganisha kambi mbili za wapenda mageuzi na wasiotaka mabadiliko ya sheria katika Kanisa Katoliki.
Chanzo BBC Swahili

Kocha mpya Stars aita wapya tisa yumo Javu, Maguli

Hussen Javu aliyeitwa Stars ya kuivaa Malawi
Elias 'Magoli' Maguli naye kaongezwa na kocha mpya wa Stars
kochaaaa
Kocha mpya wa Stars
 KOCHA Mkuu mpya wa Taifa Stars, Mart Nooij amewaongeza wachezaji tisa katika kikosi cha timu hiyo kinachojiandaa kwa mechi ya kirafiki na timu ya Malawi(The Flames) ambayo itakachezwa Mei 4 mwaka huu katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Stars iliyonyolewa mabao 3-0 jana na Burundi huku kocha huyo akishuhudia uwanjani, ambapo Rais wa TFF, Jamal Malinzi alimtambulisha na kueleza wamemsainisha mkataba wa miaka miwili kuinoa timu hiyo.
Wachezaji walioongezwa na kocha huyo ni Edward Manyama (JKT Ruvu), Elias Maguli (Ruvu Shooting), Hassan Dilunga (Yanga), Hussein Javu (Yanga), John Bocco (Azam), Kelvin Friday (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na Shomari Kapombe (AC Cannes, Ufaransa).
Walioondolewa ni pamoja na beki Kelvin Yondani wa Yanga ambaye aliitwa awali na sababu za kuondolewa ni kushindwa kuripoti kambini.
Kikosi hicho cha Taifa Stars inategemewa kuingia kambini kesho Aprili 28 jijini Mbeya kujiandaa kwa mechi dhidi ya Malawi.
Wakati huo huo, Tanzania (Taifa Stars) imepangiwa kucheza na Zimbabwe katika raundi ya pili ya mechi za mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika (AFCON) zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.
Kwa timu ya Taifa Stars itaanzia nyumbani ambapo mechi ya kwanza itachezwa kati ya Mei 16 na 18 wakati ile ya marudiano itachezwa Harare kati ya Mei 30 na Juni 1 mwaka huu.

Chelsea yaizima Liverpool Anfield

Demba Ba akiiandikia Chelsea bao dakika ya 45 ya mchezo wao wa leo
Mimi ndiyo Only Special bwana!! Mourhino akijipiga kifua kuonyesha umahiri wake kwa kuzima Liverpool kwao kwa maba 2-0
Liverpool wakiwa hawamini kama wamelala nyumbani
 CHELSEA chini ya kocha wake, Jose Mourinho ikiwa ugenini kwenye uwanja wa Anfield imefanikiwa kuisimamisha Liverpool baada ya kuizamisha Liverpool kwa mabao 2-0 katika Ligi Kuu ya England.
Liverpool ambayo ilikuwa ikitarajiwa kujiandikishia rekodi ya kuelekea kunyakua taji la kwanza la Ligi Kuu baada ya miaka 24, ilishindwa kuamini kama imelala nyumbani kwao kwa vijana wa Mourinho.
Mabao ya 'jioni' katika kila kipindi kupitia kwa Demba Ba na Willian yalitosha kuipa ushindi huo Chelsea na kuwasogelea wapinzani wao kwenye mbio za kuelekea kwenye ubingwa wa ligi hiyo.
Demba Ba alifunga bao la uongozi dakika chache kabla ya timu kwenda mapumziko kabla ya Torres kuvunja mtego wa kuotea na kumpa pasi murua Willian aliyezamisha bao sekundu chache kabla ya mchezo huo kumalizika.
Chelsea iliyotumia muda mrefu 'kupaki basi' na kuinyima fursa Liverpool kuipenya ngome ya vijana hao wa The Blues ambap hawakutarajiwa kupata ushindi huo katika mechi yao leo.
Hii ni kwa sababu Mourinho alishatangaza mapema angekichezesha kikosi cha pili ili kuweka nguvu kwa mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa hatua ya nusu fainali dhidi ya Atletico Madrid watakaowafuiata Stanford Bridge siku ya Jumanne.
Kwa ushindi huo, Chelsea imeweza kupunguza pengo la pointi na kufikisha mbili nyuma ya wapinzani wao wanaoongoza msimamo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 80 wakati ligi imesaliwa na raundi mbili kabla ligi haijamalizika mwezi ujao.
Dakika chache zijazo Manchester City waliopo nafasi ya pili watakuwa ugenini kuvaana na Crystal Palace katika mfululizo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 74 kutokana na mechi 34.

Mwina Kaduguda afunguka Simba kuelekea Uchaguzi Mkuu

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiZr9zB8jynEIPYNspsH_GwAc4jaqA8REf2Q-oJCyB6nAKNQ2kgA75m-MIsYRtg2OI10zit1RxQuwsAYGdpBLXRovzv0G3Hjj-YfxjRNokWlOMH28psVc5VT2CReAAJu_QmISgPokUHzlw/s1600/DSC_6361.JPG
Mwina Kaduguda (kushoto) akiwa na aliyekuwa mwenyekiti wake, Hassan Dalali walipokuwa wakiukabidhi uongozi wa sasa wa Simba, chini ya mwenyekiti wake Ismail Rage
KATIBU Mkuu wa zamani wa Simba, Mwina Kaduguda ameyataka makundi yanayosigana ndani ya klabu hiyo kukaa pamoja na kumaliza tofauti zao kabla ya  kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu unaoatarajiwa kufanyika hivi karibuni.Kaduguda alisema lengo la makundi hayo kukaa meza moja ni kujenga umoja na mshikamano kwa lengo la kupata viongozi bora wanaokubalika.
Aidha amewakumbusha wanachama wa klabu hiyo kuhakikisha wanachagua viongozi ambao wataiwezesha Simba kuwa moja na itakayokuwa na uwezo wa kunyakua ubingwa wa Afrika.
Akizungumza kwenye kituo cha radio Clouds Fm leo mchana, Kaduguda alisema uzoefu alionayo katika kuongoza soka ndani ya klabu hiyo na kwingine umemfanya kuitambua kinachokwaza soka la Tanzania kusonga mbele mojawapo ikiwa ni mifarakano ya kuendekeza makundi.
Kaduguda aliyewahi kuwa Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kipindi ikiitwa FAT, alisema ndani ya Simba kuna makundi ambayo yamekuwa yakiwagawa wanachama kila upande ukitaka kundi lao litoe kiongozi kitu alichodhani kinapaswa kudhibitiwa mapema.
Alisema ni vyema makundi yaliyopo kukaa meza moja kwa nia ya kuijenga Simba kuelekea kwenye uchaguzi kwa kuiwezesha klabu hiyo kupata viongozi bora watakaoivusha mahali ilipo na kuja kutamba Afrika, la sivyo inaweza kukutwa na yaliyozikuta Gor Mahia au AFC Leopard za nchini Kenya, zilizopotea kwenye umaarufu wao wa soka kabla ya kuibuka tena.
"Hakuna siri ndani ya Simba kuna makundi kama ya Simba Taleban, Friend's of Simba na Banyamulenge ambalo hata hivyo limelegalega, nashauri wanayounga mkono makundi hayo yakae pamoja na kumaliza tofauti na kujadiliana kiongozi gani anayewafaa kuwaongoza."
Kaduguda alisema na kuongeza, pia makundi hayo yanapaswa kutowapuuza au kuwabeba watu kwa sababu ya haiba yao au uwezo wa kiuchumi, akieleza hata wasio na uwezo wa kifedha wana haki na nafasi kubwa ndani ya klabu hiyo.
Pia aliwakumbusha wanachama wa klabu hiyo kuwa makini katika uchaguzi huo ili kuipa Simba viongozi makini na bora watakaoiwezesha klabu yao kutamba kimataifa badala ya kuwabeba watu ambao watakuja kuwanyima raha kwa miaka minne ijayo.
Klabu ya Simba inaelekea kufanya uchaguzi mkuu baada ya uongozi wa sasa chini ya Mwenyekiti wao, Ismail Aden Rage kumaliza muda wao mwezi ujao.
Hata hivyo uchaguzi huo bado haujatangazwa rasmi na Kamati ya Uchaguzi ya klabu hiyo kwa sababu ya kusubiri kupitishwa kwanza kwa Katiba yao mpya na ofisi ya Msajili ili kuweka hadharani mchakato kamili ya kinyang'anyiro hicho.

PSG yakwama kutangaza ubingwa Ufaransa

http://static.goal.com/334600/334648hp2.jpg
KLABU ya PSG  inalazimika kusubiri hadi wiki ijayo kuona kama itatetea na kunyakua taji la Ligi Kuu ya Ufaransa mapema baada ya mpango huo kukwama mbele ya timu iliyopo mkiani Sochaux na kulazimishwa sare ya bao 1-1 katika ligi hiyo.
Bao la kujifunga la Mbrazil Thiago Silva liliinyima PSG fursa ya kutawazwa mabingwa wapya na kuwafanya wababe hao kufikisha pointi 83.
PSG ilionekana kama wangesherehekea ubingwa ikiwa ugenini baada ya Edinson Cavani kufunga bao dakika ya 24 na lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Cavani alifunga bao hilo kiufundi baada ya kupokea krosi pasi ya Thiago Motta kwa kifua kabla ya kujikunjua na kuiandikia PSG bao.
PSG itabidi wasubiri pambano lao lijalo dhidi ya Rennes kukamilisha kiu yao ya kunyakua taji kwa ya pili mfululizo mbelebya Monaco waliopo nafasi ya pili wakiwa na pointi 75 huku timu zote zikisaliwa na michezo mitatu kila moja.
Hata hivyo p

Hatma ya waliosimamia Ruvu kujulikana kesho

http://api.ning.com/files/RbGVjb*ZO54uy37SpnuBHdFW7xexpiQ8bPS114bo6aA*6lpw39ydLeFhzsy4HxtWhz99xUAiwN2Yp679VDZwThtXKHkwDf9M/kiijiko.JPG
Kijiko
HATMA ya wachezaji watatu wa timu ya Ruvu Shooting waliosimamishwa kwa muda usiojulikana siku moja kabla ya kuvaana na Azam katika mechi za mwishoni mwa msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara, inatarajiwa kujulikana kesho Jumatatu wakati Kamati ya Utendaji ya timu hiyo itakapokutana kuipitia na kuijadili ripoti ya kocha wao, Mkenya Tom Oloba aliyeiwasilisha kwao juzi Ijumaa.
Wachezaji hao beki Ibrahim Susan 'Chogo' kiungo Juma Seid 'Kijiko' na mshambuliaji Cosmas Lewis walisimamishwa na viongozi kwa tuhuma za utovu wa nidhamu baada ya kutoweka kambini bila taarifa zozote wakielekea kwenye mechi hiyo na Azam iliisha kwa mabingwa wapya wa msimu huu, Azam kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 na kuvunja mwiko wa Ruvu kufungwa Mabatini.
Afisa Habari wa Ruvu, Masau Bwire alisema licha ya awali uongozi kupanga kuwaita wachezaji hao ili wajieleze, suala hilo lilishindikana kutokana na kubanwa na ratiba ya mechi za kufungia msimu, hivyo watakutana Jumatatu kuamua hatma yao.
Bwire alisema wataamua hatma ya wachezaji hao kutegemeana na ripoti ya benchi la ufundi la timu hiyo iliyowasilishwa kwao na kocha wao Tom Olaba ambayo ina mapendekezo kwa ajili ya msimu ujao.
"Hatma ya wachezaji watatu na wengine ambao wataachwa au kubakishwa kwenye kikosi cha Ruvu kwa ajili ya msimu ujao itafahamika Jumatatu (kesho) wakati viongozi watakapokutana ili kuipitia na kuijadili kwa kina ripoti ya kocha iliyowasilishwa kwetu siku ya Ijumaa," alisema.
Aliongeza, uongozi huo pia utafanya tathimini ya msimu mzima wa ligi kwao kama wamefanikiwa katika malengo yao na kujipanga kwa msimu ujao ili kuhakikisha yale yaliyowaangusha msimu huu yasijirudie na Ruvu Shooting iendelee kuwa timu ya upinzani na siyo shiriki katika ligi hiyo ambayo iliyoshuhudia ushindani ya hali ya juu.
Ruvu Shooting imekuwa na msimu mzuri mwaka huu baada ya kufanikiwa kumaliza nafasi ya sita ikiwa na pointi 38 ikilingana na klabu ya Simba na Kagera Sugar waliotofautiana nao mabao ya kufunga na kufungwa.