STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 29, 2014

Arsenal yapumua, yaifumua Newcastle United 3-0

KLABU ya soka ya Arsenal imefufua matumaini yake ya kuwepo kwenye Top 4 na kushiriki moja kwa moja Ligi ya Mabingwa ya Ulaya bada ya usiku wa kuamkia kuitandika Newcastle United kwa mabao 3-0 kwenye uwanja wa wa Emirates, mjini London.
Mabao ya Laurent Koscielny katika dakika ya 26, Mesut Ozil aliyefunga dakika ya 42 na jingine la Olivier Giroud yaliweka Arsenal pazuri ikiwa imepata ushindi wa tatu mfululizo na kuzidi kuikimbia Everton wanaoifukuzia nafasi yao.
Arsenal waliokuwa vinara wa ligi ya England kwa muda mrefu kabla ya kuporomoka, itasubiri kujua hatma yake ya kutwaa nafasi ya nne baada ya pambano la Everton na Manchester City mwishoni mwa wiki, kama Everton itateleza kama ilivyofanya katika mechi zake zilizopita basi vijana wa Gunners watakuwa wamejihakikisha kutwaa nafasi hiyo na kucheza ligi ya mabingwa moja kwa moja.
Vijana hao wa Arsene Wenger wamekusanya jumla ya pointi 73 nne zaidi na iliyonazo Everton waliopo nyuma yao na pointi 69.

No comments:

Post a Comment