STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 18, 2012

Mdogo wa Nsajigwa 'atua' Bandari Kenya



BEKI wa kutumainiwa wa timu ya 94 KJ inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara ya 94 KJ, ambaye ni mdogo wa nahodha wa Yanga, Shadrack Nsajigwa, Simon Joel Nsajigwa, ametua klabu ya Bandari Fc ya Kenya kwa ajili ya kufanyiwa majaribio.
Mchezaji huyo aliyefanana sura na umbo kama kaka yake, alienda kufanyiwa majaribio katika timu hiyo iliyoshuka daraja msimu huu toka Ligi Kuu ya Kenya, wiki mbili zilizopita baada ya mawakala wa timu kuvutiwa na soka lake.
Kocha wa timu ya 94 KJ, Mwinyimadi Tambaza, alisema walimruhusu mchezaji huyo kwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa na amekuwa akiwasiliana naye kila mara kujua kinachoendelea.
Tambaza alisema walipowasiliana naye juzi alimfahamisha kuwa majaribio yake yanaendelea vema na atarejea nchini wiki ijayo ili kusubiri kitakachofuata juu ya hatma yake ya kuichezea timu hiyo iliyodakiwa na kipa Ivo Mapunda kabla ya kuitema iliposhuka daraja na kwenda kujiunga na Gor Mahia.
"Ni kweli beki wetu ambaye ni mdogo wa Shadrack Nsajigwa, yupo Kenya akifanyiwa majaribio katika timu ya Bandari na anatazamiwa kurejea nchini wiki ijayo kuungana na wachezaji wenzake kwa ajili ya duru la pili la Ligi Daraja la Kwanza wakati akisubiri tararibu nyingine za kuichezea timu hiyo ya Kenya," alisema Tambaza.
Tambaza, alisema ana imani kubwa kwa Nsajigwa mdogo kusajiliwa Bandari kutokana na kuwa na uwezo mkubwa kwa nafasi yake ya ulinzi wa pembeni kama ilivyo kwa kaka yake ambaye ni maarufu nchini kama 'Fuso'.

Mwisho

No comments:

Post a Comment