STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 18, 2012

Madame V awakumbuka wajane, yatima




MSANII mahiri wa muziki wa Zouk, ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Geita, Vicky Kamata amejitosa kwenye huduma za kijamii akiunda asasi yake binafsi inayoshughulikia kuwasaidia wajane, yatima na wasiojiweza.
Akizungumza na MICHARAZO, Kamata maarufu kama 'Madam V' alisema asasi hiyo inafahamika kwa jina la Victoria Foundation ambayo tayari imeshaanza kuendesha shughuli zake tangu mwishoni mwa mwaka jana.
Kamata aliyetamba na nyimbo kama 'Wanawake na Maendeleo' na 'Mapenzi na Shule', alisema ameianzisha asasi hiyo kutokana na kuguswa na matatizo ya baadhi ya watu hususan yatima na wajane waliopo ndani ya wilaya ya Geita unaotarajiwa kuwa mkoa.
Alisema kama mwanaharakati kijana anaona ni wajibu wake kujitolea kwa hali na mali kusaidia jamii hiyo ili nao angalau wajione ni wenye kuthaminiwa na kuongeza kuwa kila mtu ambaye ana uwezo wa kuwapiga tafu wenye matatizo wasisubiri kusukumwa.
"Hii ni njia ya kurudisha fadhila kwa jamii kutokana na kukubalika kwa kazi zangu kisanii na kuchaguliwa kwangu kuwa kama Mbunge, hivyo na wengine wenye uwezo wa kuwasaidia wenye matatizo wasisubiri kusukumwa kwani ni jukumu letu," alisema.
Kamata alisema kwa sasa anajiandaa kugawa baiskeli 50 na misaada mingine kwa watu wa tarafa nyingine za Geita baada ya awali kufanya hivyo tarafa ya Bugando, ambapo aligawa baiskeli 30 na kugawa vyakula na magodoro kwa vituo vya kulelea yatima vya Lelea na Feed & Tent International.

No comments:

Post a Comment