STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 18, 2012

Steve Nyerere kupakua ‘Respect Nyerere’



WAKATI filamu yake ya 'Mr President' ikiendelea kutamba, mkali wa kuigiza sauti za watu, Steven Mengele 'Steve Nyerere', sasa yuko mbioni kufyatua filamu iitwayo 'Respect Nyerere'.
Filamu hiyo itakayotolewa na kampuni yake ya 'Nyerere the Power', itahusiana na mambo mbalimbali ya kisiasa pamoja na hotuba za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
Muigizaji huyo ambaye ni mmoja wa viongozi waandamizi wa Bongo Movie, alisema safari ya kwenda Butiama alipozaliwa Mwalimu Nyerere imeiva kwa ajili ya kufyatua kazi hiyo ambayo alidai kwamba itakuwa kali pengine kuliko ya 'Mr President'.
"Nipo katika maandalizi ya kufyatua kazi mpya ambayo itahusisha masuala ya siasa na baadhi ya hotuba za kusisimua za Mwalimu Nyerere, mmoja wa viongozi wa mfano duniani," alisema Steve Nyerere.
Muigizaji, huyo alisema kila kinachoendelea katika upakuaji wa kazi hiyo atawafahamisha mashabiki wake.

No comments:

Post a Comment