STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, October 22, 2014

Newz Alert! Diamond ajisalimisha Polisi

Baada ya wacheza shoo wake kukamatwa, hatimaye Diamond naye ajisalimisha polisi Kituo cha Polisi cha Oyster Bay, alihojiwa kwa masaa kadhaa kisha kuachiwa kwa dhamana baada ya kukabidhi sare za JWTZ  kituoni hapo.
 0
 
 0 0Di - See more at: http://ubalozini.blogspot.com/2014/10/wacheza-show-wa-wakamtwadiamond-diamond.html#sthash.Rlfknl9k.dpuf
Baada ya wacheza shoo wake kukamatwa, hatimaye Diamond naye ajisalimisha polisi Kituo cha Polisi cha Oyster Bay, alihojiwa kwa masaa kadhaa kisha kuachiwa kwa dhamana baada ya kukabidhi sare za JWTZ  kituoni hapo.
 0
 
 0 0Di - See more at: http://ubalozini.blogspot.com/2014/10/wacheza-show-wa-wakamtwadiamond-diamond.html#sthash.Rlfknl9k.dpuf
http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/10/Diamond-na-Nay-wa-Mitego1.jpg
Diamond akiwa na magwanda ya jeshi sambamba na Nay wa Mitego
HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa msanii Diamond amejisalimisha mikononi mwa Polisi baada ya wanenguaji wake kutiwa mbaroni kutokana ns kupanda jukwaani wakiwa na sare zinazodaiwa za kijeshi, saa chache baada ya meneja wake, Babu Talle naye kukamatwa kwa mahojiano na Polisi.
Inadaiwa Diamond alijisalimisha kwenye kituo cha Oysterbay na baada ya kuhojiwa sambamba na kukabidhi magwanda hayo ya jeshi aliachiwa kwa dhamana.

Di Maria aleta Man Utd, kuivaa Chelsea

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/09/14/1410722741170_wps_53_epa04400505_Manchester_Un.jpg
Angel di Maria anayekuwa kuwa fiti tayari kuwavaa Chelsea Jumapili
KLABU ya Manchester United ina uhakika kuwa Angel Di Maria atakuwa fiti kwa ajili ya mchezo wa Jumapili dhidi ya Chelsea pamoja na kupata majeruhi katika mchezo wa jana dhidi ya West Ham United. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina alikuwa akisumbuliwa na maumivu katika kifundo cha mguu na kutolewa nje katika dakika ya 76 ya mchezo huo huku akionekana kuwekea barafu katika eneo hilo wakati akiwa benchi. 
Hata hivyo imedaiwa kuwa Di Maria amefanyiwa vipimo katika uwanja wa mazoezi wa United jana kwa ajili ya tahadhari lakini nyota huyo wa zamani wa Real Madrid anatarajiwa kuwa fiti katika mchezo dhidi ya Chelsea. 
Di Maria, 26 amekuwa katika kiwango bora toka atue Old Trafford ambapo tayari ameshatengeneza nafasi nne katika mechi sita huku akitengeneza nafasi ya bao alilofunga Marouane Fellaini katika mchezo wa juzi uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya West Bromwich Albion.

Babu Talle asekwa ndani, kisa magwanda ya jeshi aliyovaa Diamond

http://freemedia.co.tz/daima/wp-content/uploads/2014/10/diamond3.jpg
Diamond alipokuwa jukwaani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdRSS40VGBurMM50yz-gdx7STKAY29i40JtSVGBIUZ2GZMmvGuARHUWQov3RTD1gqfNOBA2SFa5EbQh8Q2Vq-FZnP0aRsAzkkBZRLHJUXKiO9P9x1uJQHl_4fOp6URxuRiRYI49a1Ju3E/s1600/talee.jpg
Meneja wa Diamond, Babu Talle
http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/08/babu-tale.jpg
Mtu na Meneja wake
  KUFUATIA tukio la Diamond Platinumz kuonekana akipanda katika onyesho la Fiesta akiwa na sare zinazoaminika kuwa za jeshi la Wananchi (JWTZ), imeelezwa kuwa jeshi la Polisi limemshikilia meneja wa Diamond, Babu Tale na inaelezwa kuwa alilala selo.


Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichokuwa katika eneo la kituo cha polisi cha Osterbay, Dar es Salaam jana (October 21), Babu Tale alifikishwa katika kituo hicho ambapo maafisa kadhaa wa jeshi na polisi walionekana katika eneo hilo.


Chanzo hicho kimeeleza kuwa Uongozi wa Diamond ulipewa muda wa kujieleza kabla ya saa mbili asubuhi, October 21 lakini haukufanya hivyo na ndipo hatua hiyo ikachukuliwa.


Haijafahamika bado kwa nini jeshi la Polisi lilimshikilia Babu Tale peke yake bila Diamond lakini vyanzo vimeeleza kuwa mwanamuziki huyo yuko safarini.


Hadi habari hii inaenda hewani, namba ya simu ya Babu Tale ilikuwa haipatikani.


Tovuti ya Times Fm imeongea na kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni, Dar es Salaam, Camillus Wambura ambaye amesema bado hajawasiliana na kituo cha Osterbay kuhusu suala hilo na hajapata taarifa kwa kuwa kesi hiyo inachunguzwa na iko chini ya mkuu wa upelelezi wa Mkoa.


“Mimi ninachojua kuwa suala hilo liko chini ya uchunguzi. Habari ya kushikiliwa watu na nini bado sijafahamu. Najua tu  suala hilo liko chini ya uchunguzi na linafanyiwa uchunguzi. Hiyo ni kesi ambayo iko chini ya mkuu wa upelelezi wa Wilaya, chini ya mkuu wa upelelezi wa Mkoa. Kwa hiyo sijapokea taarifa ya uchunguzi huo ulipofika.” Ameiambia tovuti ya Times Fm.


Akijibu kuhusu taarifa za uongozi wa Diamond na Diamond kupewa muda wa kujieleza, Kamanda Wambura alijibu:


“Uchunguzi unafanywa huko. Kwa sasa hivi sina taarifa hiyo nina mambo mengi sana. Kwa hiyo kwa sasa hivi uchunguzi unafanywa chini ya Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa. Kwa hiyo sijapata nafasi ya kujua wamefikia wapi katika uchunguzi wa suala hilo,”ameongeza kamanda Wambura.


Mapema wiki hii, jeshi la wananchi Tanzania lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari likipiga marufuku raia kuvaa sare za jeshi.


Chanzo:timesfm

Hatimaye YP apumzishwa nyumba yake ya milele

  MWILI wa Marehemu Yesaya Ambikile Mwakalekamo  'YP', aliyekuwa msanii wa kundi la TMK Wanaume Family,  amezikwa hii leo katika makaburi ya Changombe jijini Dar es salaam.

Marehemu YP alifariki jana baada ya kuugua kifua na kulazwa katika Hospitali ya Temeke hadi mauti yalipo mkuta.

Awali kabla ya maziko hayo YP aliagwa na ndugu jamaa na marafiki zake katuika viwanja vya sigara Chang'ombe ambapo wasanii mbalimbali wa muziki wa Bongo fleva na Bongo muvi walihudhuria.
 
 YP kabla ya kuhamia katika sanaa ya uimbaji na kuibuka na kundi la wanaume Family alikuwa akifanya sanaa ya maigizo na vichekesho akiwa kundi moja na wasanii, Masanja Mkandamizaji, Mpigapicha maarufu na Blogger Mroki Mroki, Kiwewe, Dokii enzi hizo wakiwa na kundi la Get Well Generation lililokuwa chini ya Dokii na kurusha michezo yake Star Tv.



YP enzi za uhai wake aklitamba na nyimbo kama 'Ulipenda Pesa', 'Pumzika', 'Shemsha' na nyimbo nyingi za TMK Wanaume Family kama 'Twende zetu' ya Chege, 'Dar mpaka Moro', 'Kichwa kinauma', 'Tufurahi' na nyimbo nyingi za TMK Wanaume family pia alivuma na wimbo wa Binadamu Visa alioimba na swahiba wake, Y-Dash.
 Kiongozi wa kundi la Mkubwa na Wanae na TMK, Mkubwa na Wanawe, Saidi Fella akizungumza wakati wa msiba huo. 
 Juma Nature kutoka TMK Wanaume Halisi akizungumza.
 Mh Temba nae akizungumza...
 Mmoja wa waigizaji aliyehudhuria mazishi hayo, Jacob Steven 'JB' akizungumza.
Ilikuwa ni vilio kutoka kwa kila mtu aliyehudhuria mazishi hayo.  
Credit: FK

Miss Tanzania, Lundenga wapatwa kigugumizi, waahidi

 Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga (kati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya sakata la umri halali wa Mrembo alietwaa taji hilo Mwaka huu, Sitti Abbas Mtemvu (kushoto),katika mkutano huo Lundenga alitolea ufafanuzi swala la umri wa Mrembo huyo kulingana na vilelezo alivyopewa na mrembo huyo wakati akijiunga na mashindano hayo 

"Katika mashindano ya yetu,Washiriki wote hujaza fomu maalum zilizoandaliwa na Kamati ya Miss Tanzania,katika fomu alizojaza mrembo wa Miss Tanzania 2014 Sitty Abbas Mtemvu amejaza tarehe yake ya kuzaliwa ambayo ni Mei 31,1991 na hivyo kuwa ni sahihi kushiriki mashindano yetu" Alisema Lundenga mbele ya wanahabari hao.

Lundenga aliendelea kusema kuwa Mashindano ya Miss Tanzania hayaruhusu mshiriki yeyote mwenye mtoto kushiri,hivyo katika swala la Sitti Mtemvu kuwa ana mtoto,hilo kalina ukweli wowote bali ni uvumi tu wa kwenye mitandao ya kijamii baada ya Mrembo huyo kuonekana akiwa katika picha na mtoto aliyeomba kupiga nae.
 Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga akionyesha nakala ya cheti cha kuzaliwa cha Mrembo Sitti Mtemvu alicholetewa na wakazazi wake.
 Nakala halisi ya Cheti hicho inayoonyesha Mrembo huyo amezaliwa Mei 31,1991.
Miss Tanzania 2014,Sitti Abbas Mtemvu akizungumza machache na waandishi wa habari. Video ya alichokisema Miss Tanzania itawajia muda si mrefu.

Yanga kuadhibiwa na TFF, kisa...!

http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/08/YANGA-SC-2014.jpgSHIRIKISHO la  Soka Tanzania (TFF), kupitia Bodi ya Ligi limesema huenda likailima faini ya Sh 500,000 klabu ya Yanga kwa kitendo cha kususia kutumia chumba cha kubadilishia nguo katika mchezo wao dhidi ya Simba SC uliofanyika Jumamosi iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.
Katika mchezo huo Yanga hawakukitumia chumba hicho na badala yake kukitumia chumba cha mikutano na waandishi wa habari, huku kukiwa na tetesi kuwa waliamua kufanya hivyo baada ya kuwahisi wapinzani wao waliwafanyia vitendo vya kishirikina.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Ligi, Silas Mwakibinga, alisema kuwa wamezisikia taarifa hizo ambazo kwao siyo rasmi hivyo wanasubiri ripoti ya mchezo huo ili kuijadili na kuitolea ufafanuzi.
Alisema kuwa sheria zinaonyesha wazi kuwa, iwapo Yanga itabainika kufanya kitendo hicho lazima ikumbwe na rungu hilo la faini kama sheria zinavyosema.
“Sheria zipo wazi na kama kweli walifanya hivyo lazima waadhibiwe, kabla ya wiki hii kumalizika kamati itakaa kuijadili ripoti ya mechi hiyo na faini ya shilingi laki tano itawakumba iwapo tutalikuta suala hilo,” alisema Mwakibinga.

Steven Gerrard afichua siri nzito

NAHODHA wa Liverpool, Steven Gerrard amefichua siri kwamba aliwahi kuwinda na wapinzani wao wanaoumana leo kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, Real Madrid.
Gerrard alisema alikuwa akiwinda na mabingwa hao watetezi wa Ulaya kwa siku za nyuma na kudokeza kuwa hata sasa akipata nafasi hiyo anaweza kuigomea.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 alikuwa akikaribia kujiunga na Chelsea 2005, huku Jose Mourinho akiweka pembeni kiasi cha pauni milioni £30 kabla ya wekundu hao kupata nafasi ya kucheza Ulaya na kumfanya kusalia.
Gerrard ametanabaisha kuwa miaka miwili Mourinho alimfuata alipokuwa meneja Santiago Bernabeu, lakini akasema kuwa alikataa kuondoka Anfield.
Timu hizo usiku wa leo zinakutana katika pambano kwenye uwanja wa Anfield, ambapo kocha Brendan Rodgers akitamba kupata ushindi ili kujiweka pazuri katika mbio za kusonga mbele kwenye makundi.

Huzuni! Muigizaji Sherry Magari afariki Morogoro

Shery Charles Magari enzi za uhai wake
Marehemu sheri akiwa kapoz enzi za uhai wake
Hapa akiwa na wasanii wenzake wa kundi la vituko show
WAKATI wadau wa muziki wakijiandaa kumzika msanii YP, tasnia ya filamu nayo imepata pigo baada ya aliyekuwa Aliyekuwa muigizaji na mchekeshaji wa Shery Magari kufariki jana kwenye Hospitali ya Rufaa ya Morogoro alikokuwa amelazwa kwa muda mrefu.
Kwa mujibu zilizotolewa na mmoja wa wachekeshaji wenzake, Robert Augustine 'Kiwewe' ni kwamba Sherry anayetajwa kama mtoto wa muingizaji mwingine nyota nchini, Charles Magari alifariki jana saa 4 baada ya kufahamishwa na Afisa Habari wa TDFAA, Kaftany.
Taratibu za mazishi bado hazijafahamika ila inaelezwa huenda akazikwa leo huko mjini Morogoro na MICHARAZO itaendelea kuwaelezea kinachoendelea, ingawa taarifa hizi zilichelewa kuletwa kwenu kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo tangu tulipofgahamishwa mapema jana asubuhi.

Marehemu YP kuzikwa leo Chang'ombe

10724259_1561586274078135_315827170_n
MWILI wa marehemu Yesaya Ambilikile 'YP', 28, msanii wa kundi la TMK Wanaume Family, anatarajiwa kuzikwa leo jioni kwenye makaburi ya Chang'ombe Maduka Mawili.
Msanii huyo alifaraiki usiku wa kuamkia jana kutokana na kusumbuiliwa na maradhi ya kifua yaliyomlaza katika Hospitali ya Temeke.
Marehemu YP aliyewahi kutamba na nyimbo kadhaa akiwa na msanii mwenzake Y Dash na wenzake wa TMK Wanaume kama 'Twende Zetu', 'Tufurahi', Dar Mpaka Moro na nyingine alizaliwa Novemba 10, 1986.
Mungu Ailaze Roho Yake Mahali Pema Ameen.

Chelsea, Bavarian, Barca zaua Ulaya, kivumbi leo

Didier Drogba in Chelsea action
Drogba akifunga mkwaju wa penati kuiandikia Chelsea bao la pili
Messi akishangilia bao lake dhidi ya Ajax jana
Bayern Munich celebrateChelsea scored three goals in the first half against MariborKLABU za Chelsea na Bayern Munich zimefanya mauaji katika mechi zao za Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya, huku Barcelona nayo wakitakata nyumbani katika mfululizo wa mechi hizo.
Bayern iliitambia As Roma nyumbani kwao kwa kuilaza mabao 7-1, wakati Chelsea ikiiua Malboro kwa mabao 6-0 huku mkongwe Didier Drogba akishuhudiwa akifunga bao kwa mkwaju wa penati.
Mabao mengine ya Chelsea katika mchezo wao yalifungwa na Loic Remy dakika ya 13 kabla ya kuumia na kutoka dakika tatu baadae na kuingia Drogba aliyefungwa bao la pili dakika ya 23 kwa penati.
Beki John Terry aliiongezea Chelsea bao la tatu dakika ya 31 akimalizia kazi ya Cesc Fabregas mabao yalidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa Waswidish kujifunga kupitia mchezao wao Viler dakika ya 54 na Eden Hazard akaongeza mengine mawili dakika ya 77 kwa mkwaju wa penati na dakika ya 90.
Katika pambano jingine Bayern Munich ilitoa kipigo kikali kwa AS Roma ikiwa kwao Italia kwa mabao 7-1 Arjen Robben akianza kuandika bao dakika ya 8 akimalizia kazi nzuri ya Phillip Lahm kabla ya Mario Gotze kuongeza la pili dakika ya 23 kwa pande la Thomas Muller.
Dakika mbili baadaye Robert Lewandowski aliongeza bao la tatu kwa pande la Juan Bernat kabla ya Robben kurudi tena kambani kwa mabao la nne kwa kazi nzuri ya Lewandowski na mkwaju wa pwanti uliopigwa na Thomas Muller uliifanya wageni iende mapumziko ikiwa mbele kwa 5-0.
Gervinho aliifuta machozi Roma kwa kufunga bao dakika ya 66 kabla ya Wajerumani kurudi tena kuwaadhibu kwa mabao mawili mengine ya Franck Ribery aliyefunga dakika ya 78 na Xherdan Shaqiri dakika ya 80.
Katika mechi nyingine ya kundi hilo la E, Manchester City iling'ang'aniwa na CSKA Moscow na kutoka nao sare ya 2-2.
Katika mfululizo wa mechi nyingine PSG ikiwa ugenini ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya APOEL, huku Barcelona ikishinda nyumbani mabao 3-1 dhidi ya Ajax, Schalke 04 ikitamba nyumbani mabao 4-3 dhidi ya Sporting na Shakhtar Donetsk ikishinda ugenini mabao 7-0 dhidi ya BATE na Porto iliitambia Athletic Bilbao 2-1.
Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea tena usiku wa leo kwa michezo kadhaa ya kusisimua.
Atlético Madrid itakuwa nyumbani kuvaana na Malmö FF, wagiriki wa Olympiakos Piraeus itaikaribisha Juventus, Ludogorets itaumana na Basel wakati Liverpool itaumana na Real Madrid katika pambano la aina yake, huku Bayer Leverkusen itaikaribisha Zenit.
Klabu ya Monaco ambayo bado haijasimama vema itavaana na Benfica wakati Anderlecht itakuwa wenyeji wa Arsenal na Galatasaray itaumana na Borussia Dortmund.