STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 4, 2014

Ruvu Shooting kama Azam yatema sita

Kikosi cha Ruvu kitakachopanguliwa wachezaji sita kutokana na pendekezo la kocha Tom Olaba
KOCHA mkuu wa Ruvu Shooting, Tom Olaba amependekeza wachezaji sita watemwe katika kikosi chake kitakachoshirikishi Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu ujao kutokana na utovu wa nidhamu.
Msemaji wa timu hiyo, Masau Bwire, aliiambia MICHARAZO kuwa, kocha Olaba katika ripoti yake ya msimu wa 2013/14 wa ligi hiyo, amependekeza wachezaji sita watemwe kutokana na utovu wa nidhamu na kushuka kwa kiwango cha soka.

Bwire hakuwa tayari kuweka wazi majina ya wachezaji hao hata hivyo. 
“Tutawataja muda ukifika,”amesema Bwire huku rungu hilo likionekana wazi litawakumba wachezaji waliotoroka kambini na kukimbilia Oman kwa ajili ya kufanya majaribio na wale waliotoroka kambini wakati timu ya 'maafande' hao wa Pwani ikijiandaa na mechi iliyopita dhidi ya Azam FC.
Aidha, katika mikakati ya kukisuka upya kikosi chao cha U-20 na timu ya wakubwa, uongozi wa umesema kutakuwa na majaribio ya wachezaji kati ya Mei 15 na 28 kwenye makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo Mlandizi, Pwani.

“Mwenyekiti wa klabu, Kanali Nguge ameomba yeyote mwenye uwezo wa kucheza mpira, umri stahiki wa mpira, umbo na nidhamu kutoka sehemu yoyote nchini aje kushiriki majaribio hayo,” amesema Bwire.

Diamond, Jaydee wafunika tuzo za Kili Music Awards 2014

Diamond aliyeng'ara tuoz za Kill akimpita hata 20 Percent aliyetamba mwaka juzi

Comandoo Jide kama kawa
1. USIKU wa jana kulikuwa na utoaji wa tuzo za muziki ambapo kama kawaida Diamond amerejea kwa kishindo kwa kunyakua tuzo lukuki, sambamba na Jady Jaydee na Mzee Yusuph. Jisomee mwenyewe washindi wa tuzo hiyo kisha upime ukali wa wasanii hao watatu waliotajwa hapo juu.

WIMBO BORA WENYE VIONJO VYA ASILI YA TANZANIA - Bora Mchawi, Dar Bongo Massive
2. MSANII BORA CHIPUKIZI ANAYEIBUKA - Young Killer 
3. WIMBO BORA WA ZOUK - Yahaya, Lady Jaydee
4. WIMBO BORA WA AFRO POP - Number One, Diamond Platnumz
5. WIMBO BORA WA RAGGA / DANCEHALL - Nishai Chibwa Ft Juru
6. WIMBO BORA WA RAGGAE - Niwe na wewe, Dabo
7.WIMBO BORA WA TAARAB - Wasiwasi wako, Mzee Yusuf
8. KIKUNDI CHA MWAKA CHA TAARAB - Jahazi Modern Taarab
9. MWIMBAJI BORA WA KIKE  TAARAB - Isha Ramadhani
10. MWIMBAJI BORA WA KIUME TAARAB - Mzee Yusuf
11. WIMBO BORA WA KISWAHILI BENDI - Ushamba mzigo, Mashujaa Band
12. MWIMBAJI BORA WA KIKE BENDI - Luiza Mbutu
13. MWIMBAJI BORA WA KIUME BENDI - Jose Mara
14. RAPA BORA WA MWAKA BENDI - Furguson


15. BENDI YA MWAKA - Mashujaa Band
16. MWIMBAJI BORA WA KIKE, KIZAZI KIPYA - Lady Jaydee
17. MWIMBAJI BORA WA KIUME, KIZAZI KIPYA - Diamond
18. KIKUNDI CHA MWAKA CHA KIZAZI KIPYA - Weusi
19. WIMBO BORA WA RNB - Closer, Vanessa Mdee
20. WIMBO BORA WA HIP HOP - Nje ya Box, Nick wa Pili Ft Joh Makini & Gnako
21. MSANII BORA WA HIP HOP - Fid Q
22. WIMBO BORA WA KUSHIRIKISHA / KUSHIRIKIANA - Muziki Gani, Nay wa Mitego ft Diamond
23. WIMBO BORA WA AFRIKA MASHARIKI - Tubonge, Jose Chameleone
24. MTUNZI BORA WA MWAKA TAARAB - Mzee Yusuf
25. MTUNZI BORA WA MWAKA BENDI - Christian Bella
26. MTUNZI BORA WA MWAKA KIZAZI KIPYA - Diamond
27. MTUNZI BORA WA MWAKA HIP HOP - Fid Q
28. MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA, TAARAB - Enrico
29. MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA, BENDI - Amoroso
30. MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA, KIZAZI KIPYA - Man Water, Combination Sound
31. HALL OF FAME, INDIVIDUAL - Hassan BItchuka
32. HALL OF FAME, INSTITUTION - Masoud Masoud
33. VIDEO BORA YA MUZIKI YA MWAKA - Number One, Diamond
34.WIMBO WA MWAKA - Number One. Diamond
35. MTUMBUIZAJI BORA WA KIKE WA MUZIKI - Isha Ramadhani
36. MTUMBUIZAJI BORA WA KIUME WA MUZIKI - Diamond