STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 25, 2013

Majambazi waliopora fedha Dar wanaswa

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limewakamata watuhumiwa wa ujambazi watano wanaodaiwa kupora sh milioni 46 za mfanyabiashara wa bia wilayani Temeke, Ivon Urio.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Suleiman Kova, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa tano asubuhi na watuhumiwa wote wamekiri kuhusika na tukio hilo, na kumtaja mwenzao John Tesha kwamba ndiye aliyekimbia na fedha hizo.
Kova aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Bernards Mashamba, Steven Thadeo, Adams Isudor, Johns Benja na Sultanis Kipensa huku juhudi za kumtafuta mwenzao aliyekimbia zikiendelea.
Alisema pesa hizo zilikuwa zimewekwa katika boksi kwa ajili ya kupelekwa benki ya BOA ghafla mfanyabiashara huyo akavamiwa na watuhumiwa hao waliokuwa na bunduki kubwa moja na bastola mbili wakitumia pikipiki mbili aina ya Boxer mojawapo ikiwa na namba za usajili T 311 CGE rangi nyekundu.
Kova alitaja maeneo waliyokamatiwa majambazi hao ni Chamanzi, Manzese, Keko, Kongowe Kizinga na Mtoni Mtongani.
Katika hatua nyingine, Kova alisema pikipiki 300 zimekamatwa kati ya hizo 201 ni aina ya Boxer ambazo zinasadikiwa kuwa kwa kiasi kikubwa zinatumiwa na majambazi.
Aliongeza kuwa wanaandaa utaratibu wa kuzipaka rangi pikipiki zote kama zilivyo teksi ili zijulikane wilaya zinakotoka na wamiliki wake.
Kamanda Kova alisema mpango huo utasaidia kudhibiti uhalifu na ajali zinazotokea mara kwa mara.    

Ajuza watatu wachinjwa kama kuku Bunda wakituhumiwa uchawi

Matukio kama haya ya watu kujichukulia sheria mikononi na kuwauwa wenzao kwa kuwachoma moto yamekithiri katika jamii na ndiyo yaliyosababisha ajuza watatu kuuwawa kikatili usiku wa kuamkia leo huko Bunda, Mara
MAUAJI ya kikatili yametokea usiku wa kuamkia leo wilayani Bunda, mkoani Mara baada ya watu wenye hasira wa kijiji cha Kasaula kuwauwa kwa kuwachinja kama Kuku kisha kuwachoma moto ajuza watatu kwa kuwatuhumu wanajihusisha na vitendo vya kishirikina.
Pia watu hao mbali na kuwaua kikatili vibibi hivyo kwa tuhuma kwamba walimuua kijana mmoja aitwaye Sale Ligolo, walichoma moto na kuteketeza nyumba walizokuwa wakiishi wazee hao pamoja na kupora kuku waliokuwa wakiwafuga na kuatafuna kumaliza hasira zao.
Kwa mujibu wa wa taarifa ya mwandishi Masau Bwire aliyepo Bunda kwa sasa, tukio hilo limetokea usiku wa kumakia leo baada ya watu hao wenye hasira kuwasaka ajuza hao baada ya kuwepo tuhuma kwamba walishirikiana kumuua kijana huyo hivi karibuni.
Inaelezwa kijana huyo alikufa kwa kugongwa na gari, lakini dereva aliyemgonga alidai hakuona kama alimgonga mtu ila mbwa na pia inaelezwa  tangu azikwe kijana huyo alikuwa akirejea kwa mkewe na kumuita nyakati za usiku pamoja na kusumbua familia yao akitaka apewe chakula na ndipo wanafamilia hao walipoamua kwenda kwa mganga kuchunguza tukio hilo.
Inaelezwa ndipo walipotajiwa majina ya wanavijiji watatu wa kijiji hicho ambao hata hivyo walitoroka kwenda vijiji vya jirani pamoja na familia zao kabla ya usiku wa leo kuvamiwa walipokuwepo na kuangushiwa adhabu hizo za kinyama.
Wa kwanza kushambuliwa na kuuwa ni bibi aitwaye Bi Mgala ambaye alikimbilia kijiji cha jiorani kwa rafikie aitwaye Bi Laya, ambapo walimtaka miguu yote miwili na kumtenganisha kichwa na kiwiliwili kabla ya kumchoma moto ambapo hata hivyo kitu cha ajabu ni kwamba ziliungua nguo zake tu huku mwili ukiwa upo vile vile.
Baadaye walimgeukia Bi Laya aliyekuwa akitaka kuwatoroka na kumfanyia unyama kama rafikie kwa kile walichodai kwa kosa la kumhifadhi Bi Mgala kwa kuamini huenda wanafanya shughuli za kishirikina pamoja na baadaye kurudi Kasaula na kumnasa Bi Chausiku na kumfanyia kama walivyowafanyia ajuza hao wengine kisha kuchoma nyumba tatu.
Bibi wa tatu wanayemtuhumu pia kwa ushirikina, ametimka kijijini hapo, lakini nyumba yake imeteketezwa pamoja na kuku waliokuwa wakiwafuga kuporwa na watu hao na kutumia moto waliouwasha katika nyumba hizo kuwachoma na kuwala kwa hasira.
Kamanda wa Polisi wa Bunda, Mika David Nyange amethibitisha juu ya tukio hilo la kusikitisha na kwamba wanedelea na upelelezi kwa nia ya kuwasaka waliohusika na kitendo hicho cha kujichukulia sheria mikononi.