STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 4, 2013

Kombe la Dunia kutua tena nchini

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgtYbw_PVUbcO_y9ZUz619vY3Dxe-PLUHAYUtbg8x3y3D2kWnWTEvxppaVj2MmA6Zy7h4v99re623LlokJlXKcD0CQqtsodC3_tcN5WDErf8x5XPBjxrP7VdMznSlJHIm3K8EpMlZgZYNw/s400/FIFA+World+cup+_trophy.jpg
KOMBE la Dunia ambalo litashindaniwa mwakani nchini Brazil, linatarajiwa kutua nchini mwishoni mwa mwezi huu na watanzania watapata fursa ya  kupiga nalo picha.
Kombe hilo litatatua nchini ikiwa ni mara ya tatu na kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Leonard Thadeo litatua Novemba 29-30 likitokea Kenya.
Ziara hiyo ya Kombe hilo la Dunia inadhaminiwa na kampuni ya Coca Cola na kwamba itahusisha nchi kadhaa na itaendelea hadi April kwa kutua Brazil tayari kwa kujiandaa na fainali za michuano hiyo zitakazofanyika nchini humo mwaka 2014.
Tanzania na Kenya ni nchi pekee za Ukanda wa afrika mashariki zilizobahatika kuwepo kwenye ratiba ya ziara ya Kombe hilo kwani baada ya kutoka Tanzania taji hilo linaloshikiliwa kwa sasa na Hispania litatua Afrika Kusini na kuendelea kwenye mataifa mengine.
Baadhi ya nchi za Afrika zilizobahatika kupangwa kulipokea Kombe hilo ni Misri, Algeria, Ghana, Morocco na Tunisia.

TFF yamchinja Msafiri Mgoyi, Kidau aula


Simba yawarejesha Redondo, Henry kikosini kuiua Ashanti Utd


Henry Joseph
Redondo
 BENCHI la Ufundi la Klabu ya Simba limewarejesha kikosini viungo wake nyota, Ramadhani Chombo 'Redondo' na Henry Joseph kwa ajili ya mechi yao ya kumalizia duru la kwanza dhidi ya Ashanti United.
Wachezaji hao waliokuwa wameshushwa katika kikosi cha pili cha timu hiyo, wamejumuishwa na wenzao na kuingia kambini Bamba Beach, Kigamboni nje kidogo ya jijini la Dar kwa ajili ya pambano hilo la Jumatano.
Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, wachezaji hao wamewaridhisha benchi lao la ufundi ndiyo maana wamewarejesha kikosi cha kwanza na huenda wakashuka dimbani keshokutwa dhidi ya Ashanti.
Kamwaga alisema kikosi chao kinajiandaa vyema kwa lengo la kupata ushindi kwa Ashanti ili kumaliza duru la kwanza wakiwa katika nafasi nzuri baada ya kutetereka hivi karibuni na kushika nafasi ya nne.
Pia aliongeza kuwa wachezaji Zahoro Pazi na Nassor Masoud 'Chollo' wameshindwa kuingia kambini kwa ajili ya pambano hilo la Ashanti kutokana na matatizo mbalimbali.
Alisema Pazi ameshindwa kuungana na wenzake kwa kusumbuliwa na homa ya Malaria wakati Chollo ni majeruhi.
Katika hatua nyingine uongozi wa Simba umekanusha taarifa ya mpango wa kufanya mabadiliko ya benchi lao la ufundi kwa kutaka kuwaondoa makocha wao wa sasa, Abdallah Kibadeni na Jamhuri Kihwelu 'Julio'.
Kamwaga alisema taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari leo ni uzushi na zenye lengo la kutaka kuwachanganya wanasimba kwa sababu Kamati yao ya uetndajni haijakutana siku za karibuni kujadili lolote.
Kibadeni na Julio wamekuwa wakielezwa wapo kwenye kitimoto ndani ya Simba kutokana na matokeo mabaya yaliyoipata timu yao na kuporomoka toka nafasi yua kwanza hadi ya nne, japo nna tayari wachezaji hao naki ukweli Simba haipo pabaya kiasi cha kuanza kupandwa na presha.

Prisons yafa nyumbani, duru la kwanza kufungwa wiki hii

Prisons Mbeya iliyolala jana Sokoine
Oljoro JKT iliyopifumua Prisons-Mbeya
WAKATI pazia la duru la kwanza la Ligi Kuu Tanzania Bara likitarajiwa kufungwa wiki hii kwa michezo saba ya raundi 13 kuchezwa kwenye viwanja tofauti, Prisons ya Mbeya imeendelea kuwa urojo baada ya jana kukubali kipigo cha bao 1-0 toka kwa Oljoro JKT.
Prisons ambayo ilikuwa imetoka kupokea kipigo cha bao 2-0 toka kwa 'ndugu' zao Mbeya City, jana ilikubali kipigo hicho kingine na kuwafanya wazidi kuchechemea kwenyue ligi hiyo inayofikia ukingoni kwa mechi za duru la kwanza.
Bao pekee lililoizima wajelajela hao na kuisaidia Oljoro kupanda kutoka nafasi ya 13 katika msimamo wa Ligi Kuu hjadi nafasi ya 11 ikiishusha Ashanti United katika nafasi hiyo, lilifungwa na Amir Omary.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena keshokutwa kwa mechi nne ambapo maafande wa JKT Ruvu wanaouguza kipigo cha mabao 4-0 toka kwa Yanga itaikaribisha Coastal Union kwenye uwanja wa Chamazi, huku Simba na Ashanti United zikiumana kwenye uwanja wa Taifa na Ruvu Shooting itakuwa kwenye dimba lake la nyumbani Mabatini-Mlandizi kuikaribisha Mtibwa Sugar na Kagera Sugar ikiwa Kaitaba mjini Bukoba itaumana na wageni wao Mgambo JKT.
Mechi za kufungia rasmi pazia la ligi hiyo litafungwa Alhamisi kwa mechi tatu kati ya mabingwa watetezi Yanga itakayocheza na Oljoro JKT uwanja wa Taifa, Azam na Mbeya City zitamaliza ubishi baina yao kwenye uwanja wa Chamazi na Rhino Ranger itakuwa mjini Tabora kuikaribisha Prisons katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.
Baada ya mechi hizo timu zitaenda mapumziko kupisha maandalizi ya timu ya taifa kwa ajili ya ushiriki wa michuano ya Kombe la Chalenji itakayoanza katikati ya mwezi huu, huku pia pazia la dirisha dogo la usajili likifunguliwa tayari kwa duru la pili litakaloanza mapema mwakani.

Diego Costa azidi kuchana nyavu A. Madrid ikiifukuza Barca

Diego Costa celebrates for Atletico Madrid
Diego Costa akishangilia bao lake la jana dhidi hya Athletic Bilbao
MSHAMBULIAJI nyota wa Atletico Madrid, Diego Costa ameendelea kudhihirisha ni moto wa kuotea mbali baada ya jana kufunga bao lake la 13 katika La Liga na kumkamata Cristiano Ronaldo wa Real Madrid, huku akiisaidia timu yake kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Athletic Bilbao.
Costa aliyekuwa ameachwa na Ronaldo baada ya nyota huyoi wa Kireno kufunga mabao mawili wakati timu yake ikiifunga Rayo Vallecano, alifunga bao hilo katika dakika ya 41 likiwa ni la pili kwa Atletico Madrid baada ya awali David Villa kutangulia kufunga bao la kuongoza dakika ya 33.
Ushindi huo wa Atletico umeifanya timu hiyo kuendelea kuifukuza mabingwa watetezi, Barcelona waliopo juu yao katika msimamo wa ligi hiyo kwa tofauti na pointi moja.
Barcelona yenywe ina pointi 34 na Atletico imekusanya pointi 33 timu zote zikiwa zimecheza michezo 12, nafasi ya tatu ikiwa inashikiliwa na Real Madrid yenye pointi 28.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo ya Hispania, Valencia ilipata ushindi wa ugenini wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Getafe nayo Granada ilipata ushindi kama huo ugenini dhidi ya Levante naMalaga ikiwa nyumbani iliinyuka Real Betis kwa mabao 3-2. Leo katika ligi hiyo kuna mchezo mmoja tu kati ya Elche dhidi ya Villarreal.

Monaco yaonja kipigo cha kwanza, ikiiacha PSG itambe kileleni

Nolan Roux scores Lille's first against Monaco
Roux akiifungia Lille moja ya mabao yaliyoizima Monaco jana
MABAO mawili yaliyofungwa na Nolan Roux wa Lille yamezima mbio za Monaco kufukuzana na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Ufaransa, PSG, baada ya kupata kipigo chao cha kwanza katika ligi hiyo msimu huu.
Monaco na PSG ndizo timu zilizokuwa zikichuana kwenye kilele cha msimamo wa ligi hiyo zikiwa pekee hazijapoteza, lakini kipigo hicho cha mabao 2-0 toka kwa Lille limneifanya Monaco kuiacha PSG itambe pekee yake kwa sasa.
Roux alianza 'kuwatengua' udhu, Monaco dakika ya 27 ya kipindi cha kwanza kwa bao lililotokana na kazi kubwa iliyofanywa na Basa na kudumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili pamoja na Monaco kucharuka na kuwakimbiza wenyeji wao kupitia mshambuliaji wake nyota Radamel Falcao, lakini walijikuta wakifungwa tena bao la pili na mshambuliaji huyo wa Kifaransa, Raux kwa mara nyingine katika dakika ya 71.
Kwa kipigo hicho Monaco imesaliwa na pointi 25 na kuiacha PSG iliyoshinda Ijumaa kwa mabao 4-0 dhidi ya Lorient itulie kileleni ikiwa na pointi 28 ikifuatiwa na Lille yenye pointi 26 baada ya kila timu kucheza mechi 12 mpaka sasa.

Rais amtembelea kumpa pole Dk Mvungi


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Mhe James na daktari wa zamu wakimwangalia Mjumbe wa Tume ya Katiba Dkt Sengondo Mvungi aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Mifupa (MOI) jana Novemba 3, 2013 kufuatia kujeruhiwa kwake na watu wanaosadikiwa ni majambazi juzi usiku Novemba 2, 2013
 
PICHA NA IKULU