STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 24, 2013

Breaking News: OCD-Kilindi apigwa risasi

TAARIFA zilizotufikia muda huu zinasema kuwa, Mkuu wa Kituo cha Polisi (OCD) Wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga, Inspekta Lusekelo Edward amejeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi na kundi la watu wasiojulikana.
Inadaiwa kuwa watu hao kabla inadaiwa walimuua Mgambo aliyekuwa akiendesha zoezi la ushuru wa mazao na ndipo Polisi walipoenda kwa ajili ya kutuliza ghasia na kuwakamata wauaji hao na ndipo akafyatuliwa risasi zilizomjeruhi tumboni na mkononi.
Kwa sasa majeruhi huyo amelazwa Hospitali ya mkoa wa Bombo, huku ikielezwa watu wawili wanashikiliwa kuhusiana na tukio hilo, lililotokea siku chache mkoani humo baada ya Mpelelezi wa Makosa ya Jinai wa wilaya ya Lushoto, Ufoo Maanga kushambuliwa na mapanga na wanakijiji waliokerwa na kitendo cha Polisi walioenda kumkamata mtuhumiwa wa mgogoro wa Ardhi kufytulia mtu risasi na kumuua.