STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 24, 2013

PSG, Baravania 'waua' Ulaya, Man U, City nazo zapetaZlatanZla

Zlatan Ibrahimovic akionyesha makeke yake uwanjani
ZLATAN Ibrahimovic jana aliiongoza PSG kufanya maajabu ya 'Shalobela' ugenini baada ya kufunga mabao manne wakati mabingwa hao wa Ufaransa wakiizabua Anderlecht kwa mabao 5-0, huku Cristiano Ronaldo na Sergio Aguero 'Kun' wakizibeba timu zao za Real Madrid na Manchester City zikishinda mechi zao za Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Zlatan alifunga mabao hayo manne na kuondoka na mpira wake huku mkali mwingine wa kikosi hicho cha Matajiri wa Ufaransa Edinson Cavani akifunga bao jingine.
Katika mechi nyingine Cristiano Ronaldo  aliisaidia Real Madrid kupata ushindi baada ya kufunga mabao mawili yaliyoiua Juventus ya Italia kwa 2-1, huku bao la pili akilifunga kwa mkwaju wa penati na kumfanya kufikisha jumla ya mabao 7 na kuongoza oprodha ya wafungaji bora kwa sasa mbele ya  Zlatan mwenye mabao sita.
Mechi hiyo ilikuwa ya kuvutia zaidi katika zilizochezwa jana kwani Juventus pamoja na kucheza ugenini lakini ilipiga soka la uhakika mbele ya wenyeji wao ikisawazisha bao la dakika nne la Ronaldo kupitia kwa Fernanod Llorente, kabla ya Ronaldo kuongeza jingine na kudumu hadi kipindi cha kwanza kinaisha na cha pili vilevile.
Nao mabingwa watetezi Bayern Munich aliendeleza rekodi yao ya kushinda michezo yake kwa 100% baada ya kuipasua Viktoria Plzeƈ kwa mabao 5-0, huku mchezaji bora Ulaya, Frank Ribery akipiga mabao mawili.
Mechi nyingine iliwashuhudia Didier Drogba akiiongoza Galatasaray nyumbani kuwachapa Copenhagen kwa mabao 3-1. Drogba akitupia moja huku Melo na Sjneider wakiongeza mengine.
Nao mabingwa watetezi wa Ligi ya England, Manchester United ikaenda kileleni mwa Kundi A baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Real Sociedad, shukurani kwa bao la kujifunga la Inigo Martnez. huku mahasimu wao wa jiji hilo la  Manchester, Manchester City wakishinda ugenini mabao 2-1, shukrani ikiwa ni kwa Kun Aguero aliyefunga yote dhidi ya CSKA Moscow.
Matokeo ya michezo hiyo ya jana ni kama ifuatavyo:
Bayern Munich 5-0 Viktoria Plzen
Man United 1-0 Sociedad
Galatasaray 3-1 Copenhagen
Real Madrid 2-1 Juventus
Anderlecht 0-5 PSG
Benfica 1-1 Olympiakos
Beyer Leverkusen 4-0 Shakhtar
CSKA Moscow 1-2 Manchester City.
Leo barani humo kutakuwa ni patashika ya michuano ya Ligi Ndogo ya UEFA 'Europa League'

No comments:

Post a Comment