STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 6, 2018

Cheki Ratiba, Msimamo wa Kombe la Mapinduzi 2018

RAHIM JUNIOR
BAADA ya mechi za jana za makundi ya Kombe la Mapinduzi, cheki ratiba na msimamo wa michuano hiyo inayozidi kushika kasi visiwani Zanzibara na itakayofikia tamati Januari 13 ambapo bingwa wa mwaka huu atafahamika.
Kwa sasa Azam ndio wanaoshikilia taji hilo baada ya kuipokonya Simba katika fainali za mwaka jana. Timu hizo zitakutana tena katika mechi kali itakayopigwa usiku wa leo kwenye Uwanja wa Amaan, Unguja.

RATIBA:

Leo Jumamosi
JKU v Singida United
Simba v Azam

Kesho Jumapili

Zimamoto v Yanga

Jumatatu

Simba v URA
Yanga v Singida United

Jumatano, Jan 10, 2018
NUSU FAINALI

Kinara Kundi A v
Mshindi wa Pili Kundi B

Kinara Kundi B v
Mshindi wa Pili Kundi A
Saa 2:15 usiku

Jan 13, 2018
FAINALI

Saa 2:15 usiku

Msimamo:

Kundi A
               P    W    D    L    F    A    Pts
1.Singida  3    3    0    0    9    3    9
2.Yanga    3    3    0    0    5    1    9
3.M'ndege 5    2    0    3    5    7    6
4.Taifa      5    1    1    3    3    7    4
5.JKU       4    1    1    2    2    3    4
6. Z'moto 3    1    0    2    3    4    3

Kundi B
               P    W    D    L    F    A    Pts
1.URA      3    2    1    0    3    1     7
2.Azam    3    2    0    1    6    1    6
3.Simba   2    1    1    0    4    1    4
4.Mwenge4    1    1    2    2    4    4
5.Jamhuri4    0    1    3    2    9    1


Dk Mwakyembe azindua tamthilia zitakazorushwa DStv, Maisha Magic Bongo

Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice-Tanzania, Maharage Chande (kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Habari, Utamadunia, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe kabla ya uzinduzi wa tamthilia mbili jana usiku Mlimani City jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu, Joyce Fisoo.
MWANDISHI WETU
WASANII wametakiwa kufaidika na kazi zao za sanaa, ambapo Serikali pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, wako tayari kuwasaidia.
Waziri aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Sarafu na Kampuni, ambazo zitaoneshwa na kisimbuzi cha DStv.
Tamthilia hizo zitakuwa zikionekana kupitia chaneli ya Maisha Magic Bongo ili kuwapa burudani zaidi wateja wa DStv.
Mwakyembe alisema kuwa amefurahishwa na kiwango cha hali ya juu kilichooneshwa katika tamthilia hizo mpya, ambazo zote zimebuniwa na kutengenezwa hapa nchini na waigizaji wake, wahariri na waongozaji wote ni Watanzania.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harishon Mwakyembe (katikati) akiwa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Joyce Fisoo (wa pili kulia), Mtendaji Mkuu wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mwuingereza (kulia) Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania Maharage Chande (wa pili kushoto) na Mbunge wa Makete Prof. Norman Sigalla King wakifuatilia kwa makini tamthilia mpya za Kitanzania – SARAFU na KAPUNI 
Pia amewaasa wasanii kuhakikisha kuwa wanazingatia maadili ya jamii wakati wote wanapofanya kazi zao za sanaa, kwani sanaa ni kioo cha jamii na kwamba ikitumika vibaya inaweza kuwa na athari mbaya kwa jamii yetu.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice-Tanzania, Maharage Chande alisema Kapuni ni tamthilia iliyojaa vituko na misukosuko, ambavyo ni kivutio kwa watazamaji. Alisema Kapuni imeandaliwa na muandaaji maarufu wa filamu nchini, Leah Mwendamseke na vituko na misukosuko ya mahusiano na usaliti wa kimapenzi.
Tamthilia hizo zitaanza kurushwa hewa kuanzia wiki ijayo katika DStv chaneli 160 – Maisha Magic Bongo.
Tamthilia hiyo imechezwa na waigizaji maarufu akiwemo, Jacqueline Wolper, Gabo, Kajala, Masanja, Jenifer Kyaka (Odama),
Mwanamuziki Quick Rocka, DJ maarufu Rommy Jones na mastaa wengine wengi. 

Wasanii mbalimbali wa tasnia ya filamu hapa nchini wakifuatilia kwa makini tamthilia mpya za Kitanzania – SARAFU na KAPUNI zitakazoonekana katika chanel ya Maisha Magic Bongo kuanzia mwezi huu wakati wa uzinduzi wa tamthilia hizo jana katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Tamthilia hizo zimeigizwa na wasanii maarufu kama Jacquline Wolper, Gabo, Kajala, Mwanamuziki Quick Rocka, Mohammed Funga Funga ( Mzee Jengua), Irene Uwoya, Idris Sultan na wengineo.
Chande aliongeza kusema kuwa tamthilia ya Sarafu iliyoandaliwa na John Samwel Isike, nayo ni maridadi iliyobeba marafiki wawili ambao wanaingia kwenye chuki na uadui mkubwa mpaka kuingiza familia zao kwenye hatari, kisa ni fedha zinazozaa kiburi, dharau na anasa za kupitiliza.
Waigizaji maarufu akiwemo Mohammed Funga Funga ( Mzee Jengua), Mzee Chilo, Elizabeth Michael (Lulu), Hemed Suleiman, Irene Uwoya, Idris Sultan, Yusuph Mlela na mastaa wengineo wamo kwenye tamthilia hiyo.
DStv kupitia chaneli yake mahsusi ya maudhiu ya Kitanzania ya Maisha Magic Bongo imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa tasnia ya Sanaa inakua na kuifanya iwe moja ya vyanzo muhimu vya mapato kwa wasanii na hatimaye kuchangia katika uchumi wa nchi yetu.
Chanel ya Maisha Magic Bongo ilianzishawa tarehe 1 Octoba 2015, kwa lengo kuu la kuinua na kukuza vipaji na Sanaa hapa Tanzania na pia kuongeza maudhui ya kitanzania kwa wateja wa DStv.
Kwa kipindi chote hiki Chanel hii imekuwa kwa haraka sana, ambapo kwa sasa ni miongoni mwa Channel zenye watazamaji wengi zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki. Channel hii imekuwa kitovu cha maendeleo ya wasanii hapa nchini, huku mamia ya wasanii wakipata fursa mbalimbali kutokana na kazi zao kurushwa katika channel hii na pia kupata mafuzo na kipato kupitia Sanaa.
Kwa upande wa tasnia ya filamu na uigizaji, Maisha Magic Bongo imeleta mapinduzi makubwa na miongoni mwa filamu zinazotikisa katika soko kwa sasa ni pamoja na Tamthila ya HUBA,ambayo ilipokelewa vizuri sana na Watanzania, pia kuna filamu na vipindi vingine kama MWANTUMU, HARUSI YETU, KITIMTIM ambazo zote zinazidi kuwa maarufu kila uchao.
Kuingizwa kwa tamthilia mpya za Kapuni na Sarafu, nu muendelezo wa mkakati wa Chaneli hii kuongeza maudhui ya kitanzania, na kuwapa watanzania burudani inayoendana na wakati na yenye kuakisi maisha halisi ya kitanzania.
Credit:MLEKANI

Wenger apewa kibano, kisa kumkoromea refa

Kiocha Arsene Wenger akikoromeana na mwamuzi
LONDON, England
MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya Pauni 40,000 kwa kumtolea maneno makali refa kwenye chumba cha kubadilishia nguo baada ya mchezo dhidi ya West Bromwich Jumapili iliyopita.
Kocha huyo alifanya kitendo hicho baada ya kukasirikia kitendo cha mwamuzi huyo Mike Dean kuwazawadia The Baggies penalti ya dakika ya mwisho baada ya mpira uliopigwa na Kieran Gibbs kumfikia mkononi Calum Chambers.
Alimfuata Dean baada ya mechi na kuanza kumtolea maneno ya kulaumu uamuzi wake baada ya Jay Rodriguez kufunga penalti hiyo kuipatia timu yake sare ya 1-1.
Wenger alifunguliwa mashitaka na Chama cha Soka England mapema wiki hii na sasa atakosekana kwenye mechi ya Raundi ya Tatu Kombe la FA dhidi ya Nottingham Forest Jumapili na mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya Kombe la Ligi, maarufu kama Carabao dhidi ya Chelsea.

Liver, Man Utd watakata, Lukaku, Virgil watupia

Virgil akishangilia bao lake
Lukaku akishiangilia bao akiwa na Lingard
Man United wakipongezana

Liverpool wakipongezana
MANCHESTER, England
MANCHESTER United imeendelea kugawa dozi baada ya usiku wa kuamkia leo kuitungua Derby Count kwa mabao 2-0, huku LIverpool wakiitoa nishai Everton kwa kuichapa mabao 2-1 katika mchezo mwingine mkali wa michuano hiyo.
Romelu Lukaku aliifungia Man United bao la pili dakika ya 90 huku Jesse Lingard akitupia kambani bao la kuongoza dakika ya 84 katika mechi kali iliyopigwa Uwanja wa Old Trafford.
Katika pambao jingine Liverpool ikiwa uwanja wa nyumbani wa Anfield iliitandika wapinzani wao wa jadi Everton kwa mabao 2-1 na kuing'oa kwenye michuano hiyo.
Beki wa Liverpool, Mholanzi Virgil van Dijk akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Wenyeji walitangulia kufunga bao la kwanza kwa mkwaju wa penalti kupitia James Milner dakika ya 34 kabla ya Gylfi Sigurosson kuisawazisha Everton katika dakika ya 65 na kwenye dakika ya beki mpya wa Liverpool, Virgil van Dijk alitupia kambani bao la ushindi dakika sita kabla ya kumalizika kwa pambano hilo.
Ushindi huo umeifanya Liverpool kuungana na Man United kutinga Raundi ya Nne ya michuano hiyo na leo Jumamosi na kesho Jumapili michezo mingine kibao itapigwa katika mfululizo wa michuano hiyo mikongwe nchini England.

Yanga hiyooo, Simba, Azam mechi ya kisasi

Azam FC itakayovaana na Simba usiku wa leo
Simba watakaokuwa na kibarua mbele ya watetezi wa Mapinduzi, Azam FC

Yanga waliotangulia nusu fainali ya Mapinduzi usiku wa jana
RAHIM JUNIOR
WAKATI Simba usiku huu ikishuka uwanjani katika mechi ya kisasi dhidi ya Azam, watani zao usiku wa kuamkia leo wametangulia nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi wakiungana na Singida United.
Singida inayoongoza Kundi A ikiwa na alama 9 sawa na Yanga ila ikiwa na faida ya mabao ya kufungwa na kufungwa, itashuka tena uwanjani jioni ya leo kuvaana na JKU katika pambano jingine linalotarajiwa kuwa kali itakayochezwa Uwanja wa Amaan mjini Unguja.
Maafande wa JKU wataivaa Singida ikiwa inauguza kidonda cha kutunguliwa bao 1-0 na Yanga katika mechi yao iliyopita na itakuwa ikikamilisha ratiba tu kwani hata kama itaifunga Singida itafikisha pointi 7 ambazo zimeshapitwa na wapinzani wao.
Yanga ilitinga nusu fainali baada ya kuifunga Taifa Jang'ombe kwa mabao 2-0, mabao yaliyowekwa kimiani katika vipindi vyote. La kwanza likifungwa na Ibrahim Ajib dakika chache kabla ya mapumziko na jingine la Yohana Mkomola kwenye dakika ya 60 na kuifanya Yanga kukata tiketi ya kucheza nusu fainali ikiwa na michezo miwili mkononi dhidi ya Zimamoto na Singida United zitakazopigwa kati ya kesho Jumapili na Jumatatu mtawalia.
Hata hivyo Yanga na Singida zikitangulia mapema nusu fainali, wapinzani wao Simba watakuwa na kibarua kizito usiku wa leo kwa kuvaana na Azam katika mechi ya kisasi na inayorejesha kumbukumbu ya fainali ya michuano iliyopita.
Simba ilicharazwa na Azam kwa bao 1-0 katika fainali ya mwaka jana ya michuano hiyo na kuwaacha matajiri hao wa Chamazi wakibeba taji kwa mara ya tatu wakifikia rekodi ya Wekundu wa Msimbazi.
Mchezo wa leo ni vita baada ya Azam jana kulala 1-0 mbele ya URA wanaoongoza kundi lao la B na ushindi pekee ndio utakawanusuru wasiliteme taji hilo la sivyo itawaacha Simba wakiungana na Waganda kucheza hatua hiyo itakayoanza Januari 10.
Simba kupitia Kocha wake, Masudi Djuma imetamba kukata tiketi hiyo kwa sababu imepanga mwaka huu kubeba kila taji baada ya kutemeshwa taji lao la Kombe la FA na timu ya Green Warriors iliyopo Ligi Daraja la Pili (SDL).
Simba ipo nafasi ya tatu nyuma ya URA na Azam ikiwa na alama nne baada ya kupata sare moja na kushinda mchezo mwingine wa mwisho na kama itaichapa Azam, licha ya kulipa kisasi cha mwaka jana, lakini itafuzu nusu fainali.
Watetezi ambao walipoteza mchezo wao wa kwanza msimu huu na kufungwa bao la kwanza katika Mapinduzi tangu mwaka jana walipobeba taji bila kupoteza wala kufungwa bao, imetamba tiketi yao ya nusu fainali wanayo Simba na lazima wawape. Ngoja tuone itakavyokuwa baada ya kipyenga cha mwisho usiku wa leo.

Friday, January 5, 2018

Dk 70 Yanga bado ipo mbele ya kwa mabao 2-0


AJIB anakosa bao la wazi dakika ya 70, matokeo bado ni yale yale, Yanga inaongoza mabao 2-0. Pambano ni kali kwelikweli Uwanja wa Amaan.

Mkomola anaiandikia Yanga bao la pili

Yohana Mkomola
STRAIKA Yohana Mkomola ameiandikia Yanga bao la pili muda mfupi uliopita kutokana na uzembe wa mabeki wa Taifa. Yanga 2 Taifa 0. Dakika ya 63.

Dakika ya 60 matokeo bao 1-0 Yanga inaongoza

Kikosi cha Yanga
PAMBANO la Yanga na Taifa linaendelea kwenye Uwanja wa Amaan, Unguja na mpaka sasa matokeo bado yakiwa ni bao 1-0, Yanga ikiendelea kuongoza.

Simba kazi wanayo kwa Azam

Kocha Masudi Djuma akimkumbatia nahodha msaidizi, Mohammed Hussein 'Tshabalala', huku aliyekuwa Kocha Mkuu Joseph Omog na Mratibu, Abbas Ali wakishuhudia
Wachezaji wa Simba wakijifua mazoezini

RAHIM JUNIOR
HAKUNA namna ila kushinda tu. Ndivyo ambavyo Simba inapaswa kufanya wakati kesho Jumamosi itakaposhuka Uwanja wa Amaan, mjini Unguja kupepetana na Azam katika mechi ya kisasi itakayoamua hatma yao ya kutinga nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani hapa.
Simba ambayo ilipata ushindi wa kishindo usiku wa jana kwa kuikandika Jamhuri Pemba kwa mabao 3-1, itavaana na Azam usiku wa kesho na timu yoyote ikishinda itajihakikishia nafasi ya kutinga nusu fainali na kusubiri kujua itaungana na nani.
Azam inayotetea taji hilo ililolipata mwaka jana kwa kuichapa Simba kwa baoa 1-0 katika fainali, huo utakuwa ni mchezo wao wa mwisho na kwa sasa ikiwa na alama sita baada ya mechi tatu, kutokana na kupigwa 1-0 jioni ya leo na URA ya Uganda.
Simba yenyewe ipo nafasi ya tatu katika Kundi B ikiwa na alama nne baada ya mechi mbili, huku URA wakiongoza msimamo na pointi zao saba baada ya mechi tatu. Pambano la mwisho la Waganda hao litakuwa ni dhidi ya Simba  litakalopigwa Jumatatu jioni.
Hata hivyo Simba chini ya Kocha, Masudi Djuma imeonyesha kuwa na mabadiliko makubwa kulinganisha na ilipokuwa chini ya Mcameroon, Joseph Omog aliyetimuliwa na kama itacheza kama ilivyocheza mechi yao iliyopita, Azam ni lazima ijipange kwa Vijana hao wa Msimbazi.
Mrundi huyo aliyewapa taji Rayon Sports ya Rwanda, anatarajiwa kuendelea kumtegemea nahodha wake, John Bocco 'Adebayor' kuongoza mashambulizi akisaidiana wa nyota wengine, huku beki kiraka, Asante Kwasi aliyetupia kambani jana katika mechi yake ya kwanza akiwa na uzi wa Simba akitarajiwa kufanya yake.
Kwasi alisajiliwa na Simba hivi karibuni akitokea Lipuli na ameanza kuonyesha makeke yake na kuwafanya mashabiki wa Simba kutabasamu kwa kuamini kuwa timu yao inazidi kunoga, ikiwa siku chache tangu watolewa na kutemeshwa taji la Kombe la FA kwa kufungwa na timu ya Daraja la Pili, Green Warriors.
Azam iliyokuwa haijafungwa bao lolote katika michuano hiyo tangu mwaka jana walipobeba taji bila kupoteza, sio ya kubeza kwanui ukuta wake unaoongozwa na Mghana, Yakubu Mohammed na safu kali ya ushambuliaji chini ya Mghana mwingine, Bernard Arthur na chipukizi Paul Peter na Zayd na Shaaban Idd huenda isikubali kirahisi kupoteza mchezo huo na kutemeshwa taji la michuano hiyo.
Mbali na mchezo huo mapema jioni Singida United itakuwa uwanjani kupepetana na JKU katika mechi nyingine.

Ajibu atupia kambani, Yanga 1-0 Taifa Jang'ombe

RAHIM JUNIOR
IBRAHIM Ajib ameitanguliza Yanga mguu mmoja kwenye nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuifungia bao la kuongoza dakika chache kabla ya kwenda mapumziko akimalizia mpira wa shuti kali ha Yohana Nkomola kuokolewa na kipa wa Jang'ombe.
Kwa sasa pambano hilo lipo mapumziko na kama matokeo yatasalia hivyo, basi Yanga itaifuata Singida United iliyotangulia mapema leo mchana kwa kuilaza Mlandege.
Katika mchezo wa leo unaochezwa Uwanja wa Amaan usiku huu, Yanga imechezesha kikosi cha vijana zaidi, huku wakongwe kama kina Youthe Rostand, Nadir Haroub 'Cannavaro', Amissi Tambwe, Papy Kabamba Tshishimbi wakiwa jukwaani.

Chirwa apigwa stop, Kocha Mbao ala kibano

Obrey Chirwa
Kocha wa Mbao, Etienne Ndayiragije
RAHMA WHITE
MZAMBIA Obrey Chirwa ambaye ameididia klabu ya Yanga kucheza na kutimkia kwao Zambia, amesimamishwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuitimulia timu yake kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu.
Chirwa ameasimamiwa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi maarufu kama Kamati ya Saa 72 iliyokutana jana Alhamisi na kujadili mechi mbalimbali za Ligi Kuu (VPL) Daraja la Kwanza (FDL) na Daraja la Pili (SDL).
Soma maamuzi ya kamati hiyo na adhabu zake katika ligi hizo;

LIGI KUU YA VODACOMMechi namba 72 (Mbeya City 0 vs Simba 1).Kamishna wa mechi hiyo Billy Mwilima amepewa Onyo Kali kwa kuruhusu mchezaji Hamisi Msabila wa Mbeya City kucheza mechi bila kuonyesha leseni, hivyo kukiuka Kanuni ya 14(16 na 17) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. 
Mechi namba 81 (Ndanda 1 vs Njombe Mji 1). Klabu ya Ndanda imepigwa faini ya sh 500,000 (laki tano) kwa kutowasilisha orodha ya wachezaji wake (team match list) kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre- match meeting) kama ilivyoainishwa katika Kanuni ya 14(2k) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu dhidi ya Ndanda katika mechi hiyo iliyofanyika Novemba 24, 2017 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu.
Pia Kamati imeiomba Sekretarieti ya Bodi ya Ligi kutoa Waraka mwingine kwa klabu kuzikumbusha kuhusu kutoa orodha ya wachezaji kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting).
Mechi namba 83 (Yanga 1 vs Tanzania Prisons 1). Tanzania Prisons imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting) ikiwa na maofisa watatu badala ya wanne, hivyo kwenda kinyume na Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.
Adhabu dhidi ya Tanzania Prisons katika mechi hiyo iliyochezwa Novemba 25, 2017 Uwanja wa Azam Complex ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(3) ya Ligi Kuu.
Wachezaji Lambart Sabiyanka wa Tanzania Prisons na Obrey Chirwa wa Yanga wamesimamishwa kwa kuzingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Kuu kutokana na kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu, wakisubiri malalamiko dhidi yao kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF.
Pia Kamati imeiomba TFF iipatie Bodi ya Ligi uamuzi (ruling) wa Kamati ya Nidhamu juu ya mchezaji wa Yanga kusimamishwa baada ya mechi dhidi ya Mbao FC wakati akisubiri mashtaka yake ili kuufanyia kazi kwa ajili ya mapendekezo ya marekebisho ya Kanuni.
Mechi namba 84 (Mbao 1 vs Mwadui 0). Klabu ya Mbao FC imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kuruka uzio wa ndani na kwenda kushangilia katika eneo lisiloruhusiwa katika mechi iliyochezwa Novemba 25, 2017 Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Adhabu dhidi ya Mbao FC ni uzingativu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 90 (Lipuli 0 vs Tanzania Prisons 1).Mtunza Vifaa wa Lipuli FC, George Mketo amesimamishwa akisubiri suala lake la kuwatukana waamuzi katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 30, 2017 Uwanja wa Samora mjini Iringa kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu. Uamuzi wa kumsimamisha umezingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Kuu kuhusu Usimamizi wa Ligi.
Mechi namba 94 (Mbao 2 vs Yanga 0). Kocha wa Mbao FC, Etiene Ndayiragije amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuondolewa kwenye mchezo (ordered off) na Mwamuzi kwa kushindwa kuheshimu taratibu na kuonywa mara tatu.
Adhabu hiyo dhidi ya Kocha Ndayiragije katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 31, 2017 Uwanja wa CCM Kirumba imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(11) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Pia klabu ya Mbao FC imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo. Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(10) kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 96 (Mwadui 2 vs Ruvu Shooting 1).Klabu ya Mwadui imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo iliyochezwa Januari 1, 2018 Uwanja wa Mwadui Complex. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 42(10) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Klabu

LIGI DARAJA LA KWANZAMechi namba 37 Kundi B (JKT Mlale 1 v Mufindi United 0). Klabu ya Mufindi United imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na Kiongozi wake Hussein Turuka kutoa lugha chafu kwa Mwamuzi katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 31, 2017 mjini Songea. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 40 Kundi B (Mawenzi Market 1 v Polisi Dar 0). Klabu ya Mawenzi Market imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kutaka kuwapiga waamuzi na kuwashawishi ball boys kuchukua mipira iliyotoka nje na kuwapelekea jukwaani.  Adhabu hiyo katika mechi hiyo iliyochezwa Desemba 31, 2017 ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Pia Kocha Mkuu wa Mawenzi Market amepewa Onyo Kali kwa kuchelewa kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre-macth meeting) kwa dakika saba. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo.
Mechi namba 39 Kundi C (Dodoma FC 3 v Alliance Schools 2). Klabu ya Alliance Schools imepigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) kwa timu yake kuonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 30, 2017 mjini Dodoma. Adhabu hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(10) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mchezaji Shaban William wa Alliance Schools amesimamishwa, hadi suala lake la kumpiga Mwamuzi litakaposikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya TFF. Uamuzi wa kumsimamisha umezingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Usimamizi wa Ligi.
Waamuzi wote wanne; Andrew Shamba, Abdallah Mkomwa, Athuman Athuman na Omari Juma wamefungiwa miaka mitatu kila mmoja kwa kuchezesha mechi hiyo chini ya kiwango. Adhabu dhidi ya waamuzi hao imezingatia Kanuni ya 38(1a) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Waamuzi.
Pia Kamishna wa mechi hiyo Mackshem T. Nzunda amefungiwa miaka mitatu kwa kushindwa kutoa taarifa ya mchezo kwa usahihi. Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 39(1) ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Udhibiti wa Kamishna.
Kamati imeomba suala la waamuzi hao ambao baadhi yao ni wa Ligi Kuu, kupitia TFF liwasilishwe kwenye chombo chenye dhamana ya kisheria ya rushwa kufanyiwa uchunguzi zaidi.

LIGI DARAJA LA PILIMechi namba 18 Kundi B (Africans Sports 1 v Kitayosce 2). Kitayosce imepigwa faini ya sh. 50,000 (elfu hamsini) baada ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya mechi (pre-match meeting) ikiwa na maofisa watatu badala ya wanne, hivyo kwenda kinyume na Kanuni ya 14(2b) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Taratibu za Mchezo.
Adhabu dhidi yao katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 29, 2017 jijini Tanga imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu taratibu za Mchezo.
Mechi namba 16 Kundi C (Mighty Elephant 1 v Green Warriors 3). Kocha wa Green Warriors, Azish Kondo amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 300,000 (laki tatu) baada ya kuondolewa kwenye mchezo (ordered off) na Mwamuzi kwa kutumia lugha chafu.
Adhabu hiyo dhidi ya Kocha Kondo katika mechi hiyo iliyofanyika Desemba 29, 2017 mjini Songea imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(10) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Mechi namba 18 Kundi C (Mkamba Rangers 0 v Boma 1). Klabu ya Mkamba Rangers imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kutokana na washabiki wake kuingia uwanjani (pitch).  Adhabu hiyo katika mechi hiyo iliyochezwa Desemba 29, 2017 ni kwa mujibu wa Kanuni ya 42(1) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Udhibiti wa Klabu.
Mechi namba 16 Kundi D (Area C v Nyanza). Timu ya Nyanza FC imeshushwa madaraja mawili na matokeo ya michezo yako yote imefutwa kwa kutofika uwanjani bila kutoa sababu yoyote na kusababisha mechi yao dhidi ya Area C iliyokuwa ichezwe Desemba 29, 2017 mjini Dodoma isifanyike.
Uamuzi huo dhidi ya Nyanza FC umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 28(1) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Kutofika Uwanjani. Pia kwa mujibu wa Kanuni ya 28(2) ya Ligi Daraja la Pili kuhusu Kutofika Uwanjani, imepigwa faini ya sh. 2,000,000 (milioni mbili) ambapo sh. 1,000,000 (milioni moja) itachukuliwa na Bodi ya Ligi, na sh. 1,000,000 (milioni moja) italipwa timu pinzani.
Vilevile Kamati imeiomba Sekretarieti kukiandikia barua Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Manyara (MARFA) ili kujua tatizo la timu hiyo.

MVUVUMWA VS FRIENDS Kamati imeipa Friends Rangers ushindi wa pointi tatu na mabao matatu baada ya Mvuvumwa kuchezesha wachezaji ambao hawajasajiliwa (non qualified) katika mechi ya Kundi A Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya timu hizo iliyochezwa Oktoba 29, 2017. Mvuvumwa ilishinda mechi hiyo mabao 4-1.
Uamuzi huo dhidi ya Mvuvumwa umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(18) na 42(20) za Ligi Daraja la Kwanza. Nayo Friends Rangers imepewa ushindi kwa kuzingatia Kanuni ya 14(37) na ya Ligi Daraja la Kwanza kuhusu Taratibu za Mchezo. 
Vilevile viongozi wa Mvuvumwa waliohusika kughushi leseni zilizotumiwa na wachezaji hao ambao hawakusajiliwa watafikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya TFF kwa ajili ya hatua zaidi.

ALLIANCE SCHOOLSKamati imepitia malalamiko ya Alliance Schools kupinga uchezeshaji wa Mwamuzi wa mechi yao dhidi ya Dodoma FC iliyofanyika Desemba 30, 2017 Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Baada ya kupitia hoja zote, Kamati haikukubaliana na malalamiko hayo kwa vile hayakuwa na vielelezo wala kanuni za kuyathibitisha. Pia kwa suala la muda, Kamati imejiridhisha kuwa kazi ya kutunza muda ni ya Mwamuzi.



Yanga, Azam, Singida wasipojipanga wamekwisha Kombe la FA


Kikosi cha Yanga

Azam FC
RAHMA WHITE
VIGOGO wa Ligi Kuu Bara, Yanga, Azam na Singida United, lazima zijipange baada ya kupewa wababe katika mechi za Raundi ya Tatu ya michuano ya Kombe la FA.
Katika droo ya michuano hiyo iliyofanyika asubuhi ya leo ikihusisha timu 32 zilizopenya hatua hiyo, Yanga imepewa wababe wa Mbeya City, Ihefu FC ya Mbalali, huku Singida wakikabidhiwa watemi wea Simba, Green Warriors.
Azam yenyewe imepangwa kupepetana na Shujaa FC katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Mkamba CCM, mjini Morogoro ili kusaka tiketi ya kuingia Robo fainali.
Katika raundi hiyo ya imehusisha timu nne za Mabingwa wa Mikoa (RCL), tatu za Ligi Daraja la Pili (SDL), 12 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na klabu 13 za Ligi Kuu zilizopenya kwenye mechi zao za raundi ya pili zilizochezwa mwishoni mwa mwaka jana.
Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mechi za raundi hiyo zitachezwa kati ya Januari 31 na Febaruari Mosi kwenye miji tofauti kulingana na ratiba ilivyo.
Kabla ya mechi hizo za raundi ya tatu kuchezwa tayari zimechezwa mechi 59 na magoli 137 yamefungwa.

Cheki ratiba kamili ilivyo na viwanja vyake:

Kagera Sugar     v Buseresere FC- Kaitaba, Bukoba
Shupavu FC       v Azam FC- Mkamba CCM, Morogoro
Majimaji Rangersv Mtibwa Sugar - Ilulu, Lindi
Kariakoo Lindi     v Mbao FC- Ilulu, Lindi
Prisons               v Burkina Fc- Sokoine, Mbeya
Green Warriors    v Singida FC-Azam Complec, Dar
Mwadui FC          v Dodoma FC- Mwadui, Shinyanga
Ihefu FC              v Yanga SC-Sokoine, Mbeya
JKT Tanzania        v Polisi Dar- Uhuru, Dar
Polisi Tanzania      v Friends- Ushirika, Moshi
Pamba SC            v Stand United-Kirumba, Mwanza
Ndanda FC           v Biashara United-Nangwanda Kiluvya United      v JKT Oljoro-Mabatini, Pwani
Njombe Mji          v Rhino Rangers-Sabasaba Njombe
Majimaji Fc          v Ruvu Shooting -Majimaji, Songea
KMC                    v Toto Africans- Uhuru, Dar

Singida United yatangulia nusu fainali, Azam yatibuliwa Mapinduzi Cup

Kikosi cha Azam ambacho jioni hii kimelala mbele ya URA

Wachezaji wa Singida wakipongezana katika mechi yao ya Kombe la Mapinduzi

Danny Usengimana akijiandaa kupioga penalti iliyoiandikia Singida bao la kuonmgoza jioni ya leo
TARIQ JUNIORVIJANA wa Hans Pluijm, Singida United sio wa mchezo mchezo, baada ya jioni ya leo kuwa timu ya kwanza kutinga nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi 2018 kwa kuichakaza Mlandege kwa mabao 3-0, huku Azam ikitenguliwa udhu na Watoza Ushuru wa Uganda.
Singida imefikisha pointi 9 ikiwa imecheza mechi tatu na kukata tiketi moja ya Kundi A ambalo lina timu ya Yanga inayoshuka dimbani usiku huu kuumana na Taifa Jang'ombe katika mechi nyingine kali ya michuano hiyo.
Walima Alizeti hao wamejihakikishia nafasi hiyo kutokana na ukweli timu zilizopo nyuma yake ni Yanga pekee inayoweza kuzipiku pointi ilizonazo, huku pia ikiwa na michezo miwili mkononi ya kufungia makundi.
Mabao ya Danny Usengimana aliyefungwa kwa penalti dakika ya 29 na mengine Kenny Ally la dakia ya 37 na lile la Lubinda Mundia la dakika ya 56 yalitosha kuipa ushindi Singida inayoshiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza mwaka huu.
Wakati Singida ikichekelea kutangulia nusu fainali, watetezi wa taji hilo, Azam ilinyooshwa na URA ya Uganda kwa bao 1-0 na kutenguliwa rekodi yao iliyokuwa ikishikilia kwa kutoruhusu bao lolote tangu michuano ya 2017.
Azam ilibeba taji hilo Januari mwaka jana kwa kucheza mechi zake zote bila kuruhusu bao lolote achilia mbali kupoteza mchezo, lakini URA wakiwa na utulivu mkubwa waliwaotea Matajiri nao na kuwatengua 'udhu' kwa bao la dakika ya 32 lililofungwa na Nicholaus Kabaga akipiga tobo kipa Razak Abalora.
Hata hivyo Azam bado ina nafasi ya kupenya hatua ya nusu fainali kama itapata matokeo mazuri katika mechi yao ya mwisho kesho dhidi ya Simba ambayo inafuatia nyuma yao kwa alama zao nne baada ya kucheza mechi mbili.
URA imefikisha pointi saba na kuongoza msimamo wa kundi hilo la B, kisha Azam ikifuata na alama zao 6. Timu zote tatu zina nafasi sawa ya kutinga nusu fainali kupitia kundi hilo na zinatarajiwa kukutana zenyewe kuamua hatma yao.
Cheki matokeo ma msimamo mzima wa michuano hiyo inayoingia mwaka wa 11 tangu kuasisiwa kwake mnamo Mwaka 2007;
Kombe la Mapinduzi 2018
Kundi A
Mlandege, JKU, Zimamoto, Yanga, Taifa Jang'ombe, Singida United

Kundi B
Jamhuri, Mwenge, Simba, Azam, URA

Des 29, 2017
Mlandege 2-1 JKU
Jamhuri 0-1 Mwenge
Zimamoto 2-1 Taifa Jang’ombe

Des 30, 2017
Zimamoto 0-1 JKU
Taifa Jang’ombe 1-0 Mlandege

Des 31, 2017
Azam 2-0 Mwenge
Jamhuri 1-1 URA

Jan 01, 2018
Mlandege 2-1 Zimamoto
JKU 0-0 Taifa Jang’ombe

Jan 02, 2018
Singida United 3-2 Zimamoto
Simba 1-1 Mwenge
Yanga 2-1 Mlandege

Jan 03, 2018
URA 1-0 Mwenge
Azam 4-0 Jamhuri
Taifa Jang’ombe 1-3 Singida United

Jan 04, 2018
JKU 0-1 Yanga
Simba 3-1 Jamhuri

Jan 05, 2018
Mlandege 0-3 Singida United
URA 1-0 Azam
Yanga v Taifa Jang’ombe

Jan 06, 2018JKU v Singida United
Simba v Azam

Jan 07, 2018Zimamoto v Yanga

Jan 08, 2018Simba v URA
Yanga v Singida United

Nusu FainaliJan 10, 2018Kinara Kundi A v
Mshindi wa Pili Kundi B

Kinara Kundi B v
Mshindi wa Pili Kundi A
Saa 2:15 usiku

FAINALIJan 13, 2018Saa 2:15 usiku

Msimamo:
Kundi A
               P   W   D    L   F   A    Pts
 

1.Singida 3    3    0    0    9    3    9
2.Yanga   2    2    0    0    3    1    6
3.M'ndege5   2    0    3    5    7    6
4.Taifa     4    1    1    2    3    5    4
5.JKU      4    1    1    2    2    3    4
6. Z'moto 3    1    0    2    3    4    3

Kundi B
              P   W    D   L    F   A    Pts
 

1.URA     3    2    1    0    3    1     7
2.Azam   3    2    0    1    6    1    6
3.Simba  2    1    1    0    4    1    4
4.Mwenge4    1    1    2    2    4    4
5.Jamhuri4    0    1    3    2    9    1