STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, November 11, 2014

Edin Dzeko azidi kuipa presha Man City

http://i4.mirror.co.uk/incoming/article2937913.ece/alternates/s615/Leicester-City-v-Manchester-City.jpgMSHAMBULIAJI wa klabu ya Manchester City, Edin Dzeko yupo katika hatihati ya kukosa pambano la nchi yake Bosnia-Herzegovina dhidi ya Israel kuwania kufuzu Fainali za Ulaya kutokana na kupata jeraha akiwa na timu hiyo ya taifa.
Mfumania nyavu huyo aliumia vibaya msuli wa kigimbi katika mguu wake wa kulia na Daktari wa timu ya taifa ya Bosnia-Herzegovina Reuf Karabeg amesema Dzeko, 28 anatarajiwa kukosa mchezo huo.
Karabeg alikaririwa akidai kuwa nyota huyo ameumia vibaya na atahitaji matibabu ambayo yatachukua muda mpaka kuja kupona.
Dzeko amefunga mabao manne katika mechi 17 katika kikosi cha City msimu huu lakini mpaka sasa ameshacheza mechi nane bila kufumania nyavu na kuumia kwake kutazidi kumtia tumbo joto kocha Manuel Pellegrini kutokana na kikosi cha timu yake kusuasua katika Ligi Kuu ya England na Ligi ya Mabingwa Ulaya ikiwa mguu ndani mguu nje kutupwa mashindanoni.

Make Money at : http://bit.ly/best_tips

Bonny Mwaitege Soma Mwanangu!

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AKh2imIAABEXVGJUjAXviN2%2B%2FFg&midoffset=2_0_0_1_3276571&partid=1.2&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Bonny Mwaitege
MUIMBAJI nyota wa muziki wa Injili, Bonny Mwaitege ameachia wimbo mpya uitwao 'Soma Mwanangu' ukiwa katika miondoko ya Reggae alioimba na mkali mwenzie Bahati Bukuku.
Kwa mujibu wa Mwaitege anayetamba na nyimbo za 'Utamjuaje', 'Mama', 'Mke Mwema' na nyingine wimbo huo umerekodiwa kwa Kameta.
Ndani ya wimbo huo, inasimulia kisa cha Baba anayemhimiza mwanae kusoma kwa bidii na kuacha kucheza ili kujenga mustakabali wa maisha yake ya baadaye na familia yao kwa ujumla.
"Baba yako napenda mwanangu kusoma....Maisha bila kusoma ni magumu...mama yako pia anapenda mwanangu usome..."

AFCON 2015 ipo haipo? Morocco yajivua rasmi

http://en.africatopsports.com/wp-content/uploads/2014/04/caf-logo.jpgSHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF limetangaza kusaka mwenyeji mpya wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON, baada ya nchi ya Morocco kuigomea.
CAF sasa inatarajiwa kutangaza mwenyeji mpya wa kuandaa michuano hiyo baada ya Morocco kushikilia msimamo wake wa kutoandaa kwa hofu ya Ebola.
Hata hivyo hofu imetanda kwamba huenda michuano hiyo isiwepo kabisa kwa mwaka ujao kutokana na nchi kadhaa zilizoombwa kuandaa kuchomoa.
CAF inafanya mazungumzo na nchi za Algeria, Angola, Equatorial Guinea, Ghana, Afrika Kusini na Misri, ambapo nchi za Ghana na Afrika Kusini zilishaonyesha kutokuwa tayari kubeba mzigo huo. 
Kwa hali hiyo ni kwamba hata mechi za kuwania kufuzu fainali hizo zilizosalia miongoni mwa timu zinazocheza makundi zinaweza zisiwe na maana yoyote.
Timu zinazochuana katika hatua ya makundi zilitarajiwa kushuka dimbani wikiendi hii kabla ya kumalizia mechi zao za mwisho wiki ijayo ambapo timu 15 zitafuzu kuungana na wenyeji wake.
Mpaka sasa nchi za Algeria na Cape Verde zimeshafuzu hatua hiyo baada ya kung'ara katika makundi yao kabla mechi hazijafikia tamati.

Hatimaye Steve Nyerere afichua kilichomkimbiza Bongo Movie

http://lh4.ggpht.com/-z3q6Yev48RI/UxCqZWH-0zI/AAAAAAAAcjA/lQdNJxQOeKA/clip_image002_thumb%25255B2%25255D.jpg?imgmax=800
Steve Nyerere
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhjgvhq5QcHwD8q_oqHw6tPmZpvwtkdaYDMLvqfAu18cEi6mJ5rEXvMZICO8G3ufPKtT1dh_6Q56pqtZyM3026LlLzDX2hP0-mlDpFjrvDhueTGXzk6ygYlYh2fzhyASjsH6Tn-v20lfIk/s1600/12.jpg
Steve Nyerere alipochanguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bongo Movie akiwa na viongozi wenzake kabla ya kujiuzulu hivi karibuni

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steve Nyerere amefichua kilichomkimbiza kwa kujiuzulu katika Umoja huo wa Waigizaji wa filamu.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Steve Nyerere ambaye majina yake kamili ni Steven Mengele alisema, misimamo yake ya kutetea na kujenga nidhamu katika umoja huo sambamba na kuweka mizani sawa kwa wasanii wanachama ndicho kilichomponza, mbali na tofauti za kiitikadi za kisiasa baina yake na viongozi wenzake.
Steve Nyerere alisema baadhi ya viongozi wenzake walikuwa wakimuona kama alikuwa akiitumia Bongo Movie kujijenga kisiasa, bila kujua umaarufu wake kwa baadhi ya viongozi na wanasiasa wameisaidia Bongo Movie kuwaomboleza na kuwazika wasanii wenzao bila ya aibu licha ya umoja huo kutokuwa na fedha.
"Unajua nilikuwa najenga nidhamu na kutaka kila mwanachama kujiona sawa ndani ya Bongo Movie, hilo halikuwapendeza wenzangu na kuanzisha majungu, wakati naingia hakukuwa na akaunti wala fedha, lakini tumeweza kuwazika bila ya kutia aibu wenzetu, Rachel Haule 'Recho', Adam Kuambiana na George Otieno 'Tyson," alisema.
Muigizaji huyo alisema licha ya kujivua uenyekiti, bado anaendelea kuwa mwanachama muaminifu wa Bongo Movie na kuwa tayari kujitolea kwa jambo lolote, licha ya kukiri kwamba ni vigumu kuondoa itikadi zake kwa CCM, kama ambavyo hawezi kumuingilia Prof Jay ambaye ni rafiki yake kwa uaminifu na mapenzi yake kwa CHADEMA.
"Ni mambo madogo madogo ambayo wenzangu wameshindwa kuyavumilia kwa sababu ya kiitikadi na misimamo ya kuwajali hata wasanii chipukizi mradi ni wanachama wa Bongo Movie, lengo likiwa kujenga misingi imara ya kundi hilo hata wale wazoefu watakapokuwa wameachana na fani hiyo," alisisitiza.
Steve Nyerere alisema yeye atakuwa tayari kutoa ushauri na mambo mengine ya maendeleo hata akiwa nje ya uongozi kwa nia ya kuhakikisha Bongo Movie inafika mbele na katu hana kinyongo na yeyote.

Super Nyamwela amaliza Yangele

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEinhFA11RKfXYKXJhdY5A98fj4E_6AsMQSnWd-jfNHQ1UYvIhpDQW5VuYNOTNo_CPjYYEfsQtcdJdh9EKHlwfMZ8rSGGo321nHeAim1NkgfS42mOm1N_6-q5f6WHOModop9Dokm8P24Gw8/s1600/Nyamwela+2.jpgDANSA kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Hassan Mussa 'Super 'Nyawela' amekamilisha 'audio' na video ya wimbo wake mpya uitwao 'Yangele Yangele' anaojiandaa kuutambulisha kwa mashabiki wakati wowote kuanza sasa.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Nyamwela alisema wimbo huo umetengezwa kwenye studio za C9 Records  na vuideo yake imefanywa na Mkenya anayefahamika kwa jina la Yfeel.
Nyamwela alisema amechelewa kuitambulisha 'ngoma' yake hiyo kutokana na kuwa kwenye majonzi mazito ya kuondokewa na mama Mlezi wao, Mama Shuu, aliyekuwa Mke wa Mkurugenzi wa bendi yao, Ally Choki.
"Tumetoka kumaliza 40 ya Mama Shuu jana (juzi), tuliamua kupumzika kabisa masuala ya muziki kuomboleza kifo cha mama yetu na sasa tumerejea upya, nikiwataka mashabiki wangu wajiandae kuipokea kazi yangu mpya ya 'Yangele Yangele' ambayo imekamilika 'audio' na video yake," alisema Nyamwela.
Kabla ya kazi hiyo, dansa huyo wa zamani wa bendi ya African Star, alikuwa akitamba na nyuimbo kama 'Duvele Duvele', 'Tumechete', Maneno Maneno' na nyingine zilizokuwa katika albamu zake mbili za awali za 'Master of the Tample' na 'Afrika Kilomondo'.

Oscar aongezwa miaka 5 zaidi Darajani

Oscar
KLABU ya Chelsea imetangaza kumuongeza mkataba mpya wa miaka mitano kiungo wake mahiri Oscar. Kiungo huyo wa kimataifa wa Brazil amekuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Chelsea toka alipojiunga nao akitokea klabu ya Internacional ya Brazil mwaka 2012.
Oscar, 23 amecheza mechi 15 na kufunga mabao manne katika mashindano yote msimu huu akiwa na Chelsea ambao hawajafungwa mpaka sasa.
Nyota huyo aliuambia mtandao wa klabu hiyo kuwa anafurahi kusaini mkataba mpya kwani anafurahia kuitumikia Chelsea na kuishi nchini Uingereza.
Sasa Oscar ambaye ameitumikia Brazil mechi 40 na kufunga mabao 11, ataendelea kuwepo Stamford Bridge mpaka mwaka 2019.

Marefa 23 wateuliwa kushiriki semina ya FIFA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifK0Ir0eMKHnBlb0rlOEKXM0IzeBuyw_3cgWPyRyAnzQLjK1RFMKyti6j2Mj_dIj4s0X3dXHRq0UuFIJRbA4gMuAGimsyjPYjL8bgDB16zX2azcV47vpbT2aiaWgfNZlTMgYeXZ7Y-nk3D/s1600/DSC_0823.jpg
WAAMUZI 23 wa daraja la kwanza wakiwemo wenye beji la Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wameteuliwa kushiriki semina itakayofanyika Novemba 16 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Washiriki wa semina hiyo ambayo pia itakuwa na mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) wanatakiwa kuripoti Novemba 15 mwaka huu kwenye hosteli ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.
Wakufunzi wa semina hiyo wanaotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) ni Riziki Majala na Soud Abdi.
Waamuzi watakaoshiriki semina hiyo ni Ahmed Juma Simba (Kagera), Arnold Bugado (Singida), Charles Peter Simon (Dodoma), Dalila Jafari Mtwana (Zanzibar), Ferdinand Chacha Baringenge (Mwanza), Florentina Zabron (Dodoma) na Frank John Komba (Pwani).
Grace Wamara (Kagera), Hellen Joseph Mduma (Dar es Salaam), Israel Mujuni Nkongo (Dar es Salaam), Issa Bilali Ali (Zanzibar), Issa Haji Vuai (Zanzibar), John Longido Kanyenye (Mbeya), Jonesia Rukyaa Kabakama (Kagera) na Josephat Deu Bulali (Tanga).
Kudra Omary (Tanga), Martin Eliphas Saanya (Morogoro), Mary Kapinga (Ruvuma), Mfaume Ali Nassoro (Zanzibar), Mgaza Ali Kinduli (Zanzibar), Samwel Hudson Mpenzu (Arusha), Soud Iddi Lila (Dar es Salaam) na Waziri Sheha Waziri (Zanzibar).

Taifa Stars yawasili salama 'Bondeni'

http://www.jaramba.co.tz/wp-content/uploads/2014/05/Taifa-stars.jpgKIKOSI cha wachezaji 23 wa Taifa Stars tayari kimewasili Johannesburg, Afrika Kusini tayari kwa maandalizi ya mechi dhidi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) dhidi ya Swaziland.
Mechi hiyo itafanyika Jumapili (Novemba 16 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa wa Somhlolo jijini Swaziland. Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwepo Johannesburg hadi Ijumaa itakapoondoka kwenda Mbabane.
Wachezaji wote walioitwa na Kocha Mart Nooij wapo kwenye msafara huo isipokuwa kiungo mshambuliaji Mrisho Ngasa ambaye amebaki Dar es Salaam kutokana na matatizo ya kifamilia.
Taifa Stars inatarajia kurejea nyumbani Jumatatu (Novemba 17 mwaka huu) saa 12.45 jioni kwa ndege ya South Africa Airways.
Wakati huo huo, kikosi cha maboresho cha Taifa Stars kitacheza mechi ya kirafiki na timu ya Taifa ya Rwanda kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 23. Mechi hiyo itachezwa Desemba 9 mwaka huu nchini Tanzania.
Kikosi cha maboresho cha Taifa Stars kinachoundwa na wachezaji wenye umri chini ya miaka 23 kitakuwa kinakutana mara moja kila mwezi hadi Mei mwakani kwa ajili ya mazoezi na kucheza mechi moja ya kirafiki.
Kocha Mart Nooij atatangaza kikosi kwa ajili ya mechi hiyo na programu nzima mara atakaporejea kutoka Swaziland.

TCRA yawafunda Bloggers kuhusu Uchaguzi Tanzania

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, TCRA, Prof John Nkoma akifungua mkutano dhidi yao na Bloggers
Maafisa wa TCRA wakiwa makini kufuatilia mkutano huo leo Mlimani City
Wana Blogu wakiwa makini ni Peter Mwenda na Super D
Mkongwe Beda Msimbe alikuwa makini kufuatilia mada iliyowasilishwa katika mkutano huo
Wana Blogu wakifuatilia
Wanahabari waandamizi wakijadiliana wakati wa mkutano huo
 


 
Injinia Andrew Kasaka akiwasilisha mada ya Muongozo wa Utangazaji wa Uchaguzi
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Assa Mwambene akizungumza wakati wa kufunga mkutano huo
Assa Mwambene akizungumza na wanablogu
Viongozi wa Kamati ya Muda ya Chama cha Wamiliki wa Blogu
Mwenyekiti Joacquim Mushi (kati) akiwa na viongozi wenzake
 

William Malecela mmoja wa jumbe wa Kamati ya Muda wa Wamiliki wa Blogu
Mwenyekiti Mushi akizungumza na wanablogu baada ya kuteuliwa kuongoza chama hicho

Wa Micharazo Mitupu naye alikuwapo kupata ujuzi zaidi
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania, TCRA wamekutana na wamiliki wa mitandao ya kijamii (bloggers) na kuwapa semina juu ya misingi ya kuendesha mitandao yao kipindi cha chaguzi zijazo.
Mkutano huo wa pamoja umefanyika kwenye ukumbi wa mikutano ya Mlimani City, ambapo Afisa Mwandamizi wa Utangazaji wa TCRA, Injinia Andrew Kasaka, aliwasilisha mada maalum.
Katika uwasilishaji wake, Injinia Kasaka alisema ni vyema wamiliki wa Blogu kuzingatia miiko, maadili ya taaluma ya habari kutokana na ukweli blogu zimekuwa na mchango mkubwa katika fani hiyo.
Aidha aliwahimiza wamiliki wa mitandao hiyo kuwa na uzalendo ili kuepusha kutumiwa na kuvuruga amani na utulivu wa nchi kama ilivyowahi kutokea katika mataifa mengine.
"Pia aliwataka wamiliki hao kusajili blogu zao ili watambulike na kuwa rahisi katika kuaminika, sambamba na kuahidi kuendesha semina zaidi mikoani katika Kanda zao za TCRA kuwapa elimu wamiliki juu ya kufahamu mipaka inayowazunguka.
"Mnapaswa kuzingatia kuandika na kuchapisha Habari zenye ukweli, zisizoumiza wengine na zenye kuchochea maendeleo ya nchi sambamba na kuelimisha, kuhabarisha na kuburudisha, kwa sababu blogu zina nguvu kubwa kwa sasa katika teknolojia ya Mawasiliano," alisisitiza Injinia Kasaka.
Kabla ya kuwasilishwa kwa mada, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Prof John Nkoma, alisema mamlaka hiyo imehitisha mkutano huo baada ya kubaini nguvu kubwa zilizopo kwa mitandao hiyo baada ya awali kufanya mkutano kama huo kwa vyomo vya habatri ya utangazaji kwa maana ya redio na televisheni.
Naye Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Mawasiliano, Assa Mwambene alieleza namna ya baadhi ya mitandao ya kijamii inavyotumia uhuru uliopo kwa kujadili vitu ambavyo havijengi.
"Serikali tuliamua kuwahabarisha wananchi juu ya kuumwa kwa Rais na kwenda kutibiwa nje, lakini taarifa hii imekuwa chanzo cha mijadala isiyo na tija, kitu ambacho hakipendezi," alisema.
Aliongeza kuwa "Hatuko hapa kwa ajili ya kutaka kuwabana maana mnaweza kusema Mwambene anatoka serikalini hivyo labda ndiye niliyotoa wazo hili, hapa tunataka kusaidia kuendesha blogu zenu kwa umakini," alisema Mwambene wakati akifunga mkutano huo.
Pia alisistiza mitandao ya kijamii na wanahabari kutumia vyema uhuru wa habari kuepuka kuleta uchochezi au mambo yatakayoivuruga nchi akisema "Uhuru bila mipaka ni hatari".
Katika uchangiaji wa mada wanablogu walipendekeza kuwepo na utaratibu wa mikutano kama hiyo na elimu zaidi kwa wale ambao hawana taaluma ya habari kuepuka kuingia matatani kwa kutoa taarifa ambazo wakati mwingine huwa hazina ukweli na zinazoumiza.
Katika mkutano huo uliunda Kamati ya Muda ya Chama cha Bloggers, ambacho kinaongozwa na Mwenyekiti Joacquim Mushi, Makamu wake akiwa Francis Godwin, Katibu akiwa Khadija Kalili na wajumbe ni Aaron Msigwa, Shamim Mwasha, Henry Mdimu,  William Malecela na na Othman Maulid.
Baadhi wa wajumbe walitoa maoni yao na kusema semina hiyo ni nzuri ila hawajui ni vipi imekuja wakati huu wa kuelekea kwenye uchaguzi na siyo wakati mwingine wowote.
Hata hivyo hofu ilitolewa mapema na Prof Nkoma wakati akijibu maswali ya watu waliotaka kujua iweje kanuni hizo ziguse uchaguzi tu na kuelekeza mipaka ya blogu kufanya kazi zao.

Hakunaga kama Cristiano Ronaldo Hispania

Ronaldo na moja ya Di Stephano

Ronaldo na tuzo zake
Akikabidhiwa tuzo ya Pichichi na Rais wa Atletico Madrid

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amezidi kung’ara baada ya kukabidhiwa tuzo yake ya. Mfungaji Bora wa La Liga 'Pichichi' sambamba na ile ya Mchezaji Bora wa La Liga maarufu kwa jina la Di Stefano ikiwa ni mara ya tatu mfululizo tangu mwaka 2011 alipompoka mshindani wake kwa sasa dunia, Lionel Messi aliyekuwa akiishikilia kwa miaka miwili mfululizo pia.

Tuzo hizo alikabidhiwa na Rais wa Atletico Madrid Enrique Corezo, huku akisema ilikuewa huzuni kwa Alfredo Di Stefano kutukuwepo katika makabidhiano ya tuzo hiyo. Gwiji hilo la Real Madrid alifariki Julai mwaka huu akiwa na miaka 88.


WASHINDI:
TUZO YA PICHICHI
2009-10 Lionel Messi
2010-11 Cristiano Ronaldo 
2011-12 Lionel Messi
2012-13 Lionel Messi
2013-14 Cristiano Ronaldo 

TUZO YA DI STEFANO:
2009-10 Lionel Messi
2010-11 Lionel Messi
2011-12 Cristiano Ronaldo
2012-13 Cristiano Ronaldo
2013-14 Cristiano Ronaldo  

Rais JK anaendeleas vyema Marekani

Miraj AAHALI ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Jakaya Kikwete aliyepo Maryland Marekani kwa ajili ya matibabu, inaendelea vizuri na ameanza mazoezi ya kutembea ikiwa ni siku ya pili tangu afanyiwe upasuaji wa tezi dume.
Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imetoa taarifa hiyo na kuongeza kuwa itaendelea kutoa taarifa kadri hali yake itakavyokuwa inaendelea.
Kupitia ukurasa wa Instagram wa mtoto wa Rais Kikwete, Miraj Kikwete (@kikwete) ameweka picha muda mfupi uliopita inayomwonyesha Rais pamoja na maneno haya;- “… #26464 #we #good TABASAMU TU LEO . thank you everyone for your endless support, love and prayers. It means so much to Dad, myself and our family. You are a strength to us. TUNAWASHUKURU KWA KUJALI ….
Miraj


48, wengi wakiwa wanafunzi wauwawa kwa bomu Nigeria


_78894856_024676851-1WATU wapatao 48 wameuwawa katika shambulizi la bomu la kujitoa muhanga katika shule moja huko kaskazini mashariki mwa Nigeria wengi wao wakiwa wanafunzi.
Mlipuko huo ulitokea jana Jumatatu katika mji wa Potiskum katika jimbo la Yobe wakati wanafunzi wakiwa wamekusanyika kwenye uwanja wa shule katika shule mioja ya sekondari ya serikali.
Wafanyakazi wa huduma wanasema watu wapatao 79 walijeruhiwa katika mlipuko huo , wengi wao wameumizwa vibaya . Magaidi wanasema mlipuaji huyo alivaa kama mwanafunzi.
VOA

Taifa Stars yapaa kwenda Afrika Kusini

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/07/team-stars-1.jpg
Wakali wa Tanzania, Taifa Stars
KIKOSI cha timu ya taifa, Taifa Stars, kimeondoka alfajiri ya leo kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya kambi ya siku chache kabla ya kwenda kuvaana na Swaziland katika pambano la kirafiki la kimataifa linalotambuliwa na Shirikisho la Soka Dunia, FIFA litakalochezwa Novemba 16 mjini Mbabane nchini humo.
Kikosi cha wachezaji 24, benchi la ufundi na viongozi wengine wameambatana na timu hiyo kwa ajili ya kuhakikisha wanaendeleza rekodi nzuri dhidi ya Swaziland.
Stars mara ya mwisho kwenye mechi ya kimataifa waliifumua Benin mabao 4-1 uwanja wa Taifa na kuifanya timu hiyo ipae kwenye orodha ya viwango vya kimataifa vya soka vya FIFA.
Hata hivyo timu hiyo imekuwa na matokeo mabaya nje ya nchi kulingananisha ikiwa nyumbani kwani kabla ya kuvaana na Benin ilitoka kunyukwa mabao 2-0 na Burundi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliochezwa mjini Bunjumbura.

Rasmi, michuano yaota mbawa 2014

http://cecafafootball.org/wp-content/uploads/2014/07/cecafa-2013-winners-kenya-Harambee-stars.jpg
Kenya wataendelea kubaki na taji lao la Chalenji
BAADA ya Ethiopia kuchomoa uenyeji wa michuiano ya Kombe la Chalenji 2014 na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati, CECAFA kuiomba Sudan kuokoa jahazi, imethibitika safari hii haitakuwapo.
CECAFA imekwama kupata mwenyeji mpya baada ya Sudan nao kukataa ombi hilo.
Michuano hiyo ilitarajiwa kuanza Novemba 24 hadi Desemba 9, mwaka huu huko Ethiopia bingwa mtetezi akiwa ni Kenya.
Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka vya Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) Nicholas Musonye, alisema baada ya Ethiopia kujitoa, imekuwa ngumu kupata nchi mbadala ya kuandaa michuano kwa haraka.
“Hatukupenda, lakini imeshindikana kabisa, tulifanya kila juhudi lakini mambo yamekuwa ni magumu,” alisema Musonye.
Alisema  imekuwa ngumu kupata wadhamini pia kwani waandaaji walijitoa dakika za mwisho, hali iliyowachanganya.

Arsene Wenger 'alivulia' kofia Chelsea

http://i2.mirror.co.uk/incoming/article4513390.ece/alternates/s615/Manchester-United-v-Chelsea.jpg
Chelsea inayomkuna Wenger
http://www.independent.co.uk/incoming/article9850327.ece/alternates/w620/Arsene-Wenger.jpg
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger

KASI ya klabu ya Chelsea imemfanya, kocha wa Arsenal, Arsene Wenger kukiri kwamba hakuna klabu yoyote kwa sasa inayoweza kuisimamisha wakali hao wa Darajani.
Wenger amenukuliwa akisema kuwa hakuna timu inayoweza kuwapata vinara wa Ligi Kuu Chelsea msimu huu kwa jinsi ilivyo katika kiwango cha kuvutia zaidi.
Arsenal walichapwa mabao 2-1 ugenini na Swansea City juzi na kuteleza nyuma zaidi ya Chelsea ambao hawajafungwa msimu huu kwa tofauti alama 12.
Chelsea wameshinda michezo yao tisa kati ya 11 msimu huu na kujikusanyia alama 29, nne zaidi ya Southampton wanaoshika nafasi ya pili katika msimamo huo, ambao wamekuwa na mafanikio makubwa tofauti na ilivyotarajiwa na wengi baada ya kumpoteza kocha na wachezaji karibu 10 nyota waliosajiliwa timu mbalimbali za Ligi Kuu ya England.
Katika mahojiano, Wenger amesema kama Chelsea wakiendelea na makali yao hayo hadhani kama kuna timu ya kuwashika msimu huu kwani inaonekana hakuna timu inayoweza kupambana nao kwa sasa.
Chelsea walipambana na kuhakikisha wanatoka nyuma na kuifunga Liverpool mabao 2-1 katika Uwanja wa Anfield Juzi na Wenger anaamini kikosi chao kimejitengenezea hali ya kujiamini.
Hata hivyo kocha huyo aliwahi kunukuliwa wiki chache zilizopita akisema ni ngumu kwa Chelsea kuweza kufikia rekodi yao ya msimu wa 2003-2004 waliocheza mechi 49 bila kupoteza kwa madai ni mapema mno.

Yaya, Enyeama, Gervinho kuwania tuzo ya BBC

https://pbs.twimg.com/media/Baf0_7GCMAAYkTD.jpg:large
Yaya Toure akiwa na tuzo ya BBC aliyotwaa mwaka jana, mwaka huu ataibuka tena kidedea?
YAYA Toure, Kiungo nyota wa kimataifa wa Ivory Coast na klabu ya Manchester City ameteuliwa tena kwa mara ya sita mfululizo kugombea tuzo ya Mchezaji Bora wa mwaka wa Afrika inayotolewa na Shirika la Utangazaji la Uingereza, BBC. 
Yaya ambaye pia Mwanasoka Bora wa Afrika, ameteuliwa kutetea tuzo hiyo ya BBC pamoja na Emerick Aubameyang kutoka Gabon na klabu ya Borussia Dortmund, Yacine Brahimi kutoka Algeria, Vincente Enyeama wa Nigeria na Gervinho wa Ivory Coast. 
Katika orodha hiyo wachezaji wanne walicheza katika michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika nchini Brazil ambapo kwa mara ya kwanza katika historia timu mbili kutoka Afrika zilifanikiwa kuvuka hatua ya makundi. 
Golikipa Enyeama alicheza katika hatua ya timu 16 bora katika michuano hiyo akiwa na Nigeria wakati Brahimi naye alifikia hatua hiyo akiwa na timu yake ya taifa ya Algeria. 
Yaya licha ya kutofanikiwa kuivusha nchi ya Ivory Coast hatua ya makundi ya Kombe la Dunia yeye na Gervinho wamekuwa na msimu mzuri katika vilabu vyao hivyo kuwapata nafasi ya kuwepo katika orodha hiyo. 
Yaya ameisaidia City kunyakuwa taji lake la pili la Ligi Kuu katika kipindi cha miaka mitatu wakati Gervinho amekuwa sehemu muhimu ya kikosi cha AS Roma toka alipondoka Arsenal kwa kuifungia timu hiyo mabao 10 katika mechi 39 za Serie A. 
Kwa upande wa Aubameyang pamoja na kutocheza Kombe la Dunia kwa sababu ya nchi yake ya Gabon kutofuzu michuano hiyo amewekwa katika orodha hiyo kutokana na kuwa katika kiwango kizuri katika klabu yake ya Borussia Dortmund ya Ujerumani. 
Mshindi wa tuzo hiyo natarajiwa kutangazwa Desemba mosi mwaka huu.

Make Money

TCRA, Wanablogu kutetea asubuhi hii


MAMLAKA ya Mawasiliano nchini Tanzania, TCRA, asubuhi hii inatarajiwa kuteta na wamiliki wa mitandao ya kijamii ili kupeana miongozo kuelekea chaguzi zilizopo mbeleni.
Mkutano huo wa pamoja unatarajiwa kuanza saa 3 asubuhi kwenye ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam ambapo kwa mujibu wa 'bango' la TCRA lengo kuu ni kupeana muongozo wa kuandika taarifa za uchaguzi wa serikali za mitaa na ule wa mkuu wa Rais, wabunge na madiwani.
Hata hivyo mbali na hilo, pia mkutano huo utatoa muongozo kwa wanablogu mingine juu ya kuzingatia maadili na miiko ya taaluma ya mawasiliano.
Kwa kipindi kirefu baadhi ya mitandao na blogu zimekuwa zikiweka taarifa au picha zinazokiuka maadili ya taaluma pamoja na miiko na desturi za kitanzania.
Nini kitakachojadiliwa na kuamuliwa, MICHARAZO itawajuza wasomaji wake bila ya shaka!