STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 15, 2014

Manchester City waikalisha Chelsea FA Cup

Manchester City celebrate
Samis Nasir akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao la pili lililoizamisha Chelsea kwenye FA Cup hivi punde
Daa Chuma hichooo! Petr Cech na beki wake hawaamini kama Jovetic amefunga bao la kuongoza

MABAO mawili ya  Steven Jovetic na jingine la Samir Nasir yametosha kuzima ndoto za kocha Jose Mourihno kuitambia kwa mara ya pili Manchester City baada ya timu yake ya Chelsea kuondoshwa kwenye michuano ya Kombe la FA muda mfupi uliopita.
Jovetic alifunga bao la kwanza dakika ya 16 kwa pasi ya Edin Dzeko kabla ya Samir Nasir kuongeza la pili katika kipindi cha pili akimalizia kazi ya David Silva katika dakika ya 67 na kuipeleka Manchester City hadi Robo Fainali ya michuano hiyo.
Wiki mbili zilizopita Chelsea iliitambia City nyumbani kwao kwa kuilaza bao 1-0 na leo ilitarajiwa labda wangerejea kitendop hicho, lakini vijana wa Etihad walikuja kivingine na kuibana Chelsea na kuendelea kuweka hai matumaini ya kunyakua mataji nne msimu huu.
City tayari imetinga fainali ya Kombe la Ligi (Capital One) na inashiriki pia Ligi ya Mabingwa Ulaya na ipo kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England.

Wigan Athletic yaifuata Sunderland FA Cup

Wigan midfielder Ben Watson (second left) powers in a goal against Cardiff in their FA Cup tie
Wigan midfielder Ben Watson
KLABU ya Wigan Athletic imeifuata Sunderland katika hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Kombe la FA baada ya kuing'oa Cardiff City kwa mabao 2-1 katika mechi iliyomalizika muda mchache uliopita.
Wigan walipata ushindi huo ugenini kwa mabao Chris McCann katika dakika ya 18 na Ben Watson aliyefunga bao dakika ya 40, licha ya wenyeji ilipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 27 kupitia Fraizer Campbell.
Pambano lingine la michuano hiyo kati ya Manchester City dhidi ya Chelsea limeshaanza na wenyeji City wameshafunga bao moja lililofungwa na Stevan Jovetickatika dakika ya 16 na kwa sasa mchezo huo upo ndani ya dakika ya 20.






Azam wapo tayari kuwavaa Wamakonde, KMKM kufanya maajabu kwa Wahabesh?, KMKM

Azam Fc watakaokuwa ugenini nchini Msumbiji
KMKM ipo nyumbani kurudiana na Wahabeshi

WAKATI ya Yanga na Chuoni yameshafahamika baada ya kucheza jioni ya leo, wawakilishi wengine wa Tanzania, Azam na KMKM zitakuwa kibaruani kesho kwenye mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho katika viwanja viwili tofauti.
Azam wenyewe watakuwa ugenini mjini Beira, Msumbiji kukabiliana na wenyeji wao, Ferroviario de Beira katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika wakati KMKM watakuwa uwanja wa Amaan Zanzibar dhidi ya wageni wao kutoka Ethiopia, Dedebit.
Katika mechi zao za awali wiki iliyopita Azam ilipata ushindi mwembamba nyumbani wa bao 1-0 wakati KMKM inayoiwakiliza Zanzibar kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika ilifungwa mabao 3-0.
Msemaji wa Azam, Jafar Idd amesema kikosi chao kipo imara kwa ajili ya mechi ya kesho ambapo wanatarajiwa kupata sapoti kubwa ya mashabiki wa Kitanzania kutoka miji mingine ya nchi hiyo iliyopo Kusini mwa Tanzania.
Jafar alisema jiji la Beira kwa sasa gumzo kubwa ji nyota wa Azam, Salum Abubakar, John Bocco 'Adebayor' na Kipre Tchetche ambao kesho watashuka dimbani kuihakikishia Azam ikitinga raundi ya kwanza ya michuano hiyo inayoishiriki kwa mara ya pili mfululizo.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo ya Afrika timu ya KCCA ya Uganda imesonga mbele licha ya kulala nyumbani kwa mabao 2-1 dhidi ya El Merreikh ya Sudan baada ya mechi ya awali kushinda ugenini 2-0, Kabuscop ya Angola imeing'oa Cote d'Or ya Seychelles kwa jumla ya mabao 7-2 baada ya leo kuilaza 2-1 wiki moja baada ya kuikung'uta mabao 5-1 mjini Luanda.
Nkana Red Devils ya Zambia iitandika Mbabane Swallows ya Swaziland kwa jumla ya mabao 5-4 baa ya leo kuilaza 5-2, wiki moja baada ya kulazwa 2-0 ikiwa ugenini, huku Rayon Sports ya Rwanda ikishindwa kutamba nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 na AC Leopards ya Congo na kung'olewa kwa faida ya mabao ya ugenini kwani wiki iliyopita walitoka suluhu ya 0-0 ugenini.Hizo ni mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika wakati mechi za Kombe la Shirikisho ukiacha Chuoni kung'oka pia Gaborone United ya Botswana imetolewa na Super Sports kwa jumla ya mabao 3-0 baada ya leo kulala nyumbani bao 1-0 wiki moja baada ya kufungwa ugenini 2-0, Club Kamsar ya Guinea imelazimishwa sare ya 1-1 na Douanes ya Togo na kung'olewa kwa jumla ya mabao 3-1 baada ya wiki iliyopita kulazwa 2-0 ugenini.
Nayo Cob ya Mali imefanikiwa kusonga mbele kwa jumla ya mabao 2-1 baada ya leo kushinda 1-0 baada ya sare ya awali ya 1-1 dhidi ya Al Ahli Tripoli, mechi nyingine zinazochezwa leo bado matokeo yake hayajapatikana mpaka sasa, ila MICHARAZO itawaeletea matokeo mara yatakapopatikana.

Sunderland yatangulia robo fainali FA England

Craig Gardner
Sunderland ikifunga bao lake pekee dhidi ya Southampton

SUNDERLAND imeendelea kuonyesha maajabu baada ya kuwa klabu ya kwanza kutinga hatua ya Robo Fainali ya Michuano ya FA baada ya kuitandika Southampton kwa bao 1-0 katika pambano lililochezwa mapema leo.
Vijana hao wa Gustav Poyet waliokuwa wakichechemea kwenye  Ligi Kuu ya England, tayari imeshatinga fainali ya Kombe la Ligi (Capital One) itakapoumana na Manchester City mwezi ujao na ushindi huo wa leo umeipa uhakika wa kuendelea kuonyesha maajabu chini ya kocha huyo.
Bao lililoizamisha Southampton katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Light (Stadium of Light) liliwekwa kimiani katika kipindi cha pili na Craig Gardner.
Gardner alifunga bao hilo katika dakika ya 49 na kuipa wakati mgumu wageni wao kutafuta bao la kusawazisha lakini dakika 90 zilipoisha wenyeji walikuwa washindi na kutangulia robo fainali.
Usiku huu kutakuwa na mechi nyingine za michuano hiyo Cardiff City dhidi ya Wigan Athletic na Manchester City itaikaribisha Chelsea na mechi nyingine iliyokuw aichezwe jioni hii kati ya Sheffield Wedn dhidi ya Charlton Athletic umeahirishwa kutokana na hali mbaya ya hewa.

Simba bado gonjwa, Coastal yakaa Mlandizi

* Mtibwa Sugar nayo yanyukwa nyumbani, kwingine sare tupu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg2BTfXkwh4BZ5f8ZQ6Ys5ZFz04K7rM7SUvMVEKPecWJHyoL_6pe1P9_Fq3AmPV0Pc1iw1uB7AqBm1WTQ9nq2JJISFutKaNXFzEqLWQWOL5g9cNxO1mG8cimYRISmeLknTq4KPU6zXFmFFi/s1600/Simba+Vs+Mbeya+City.jpg
Deo Julius wa Mbeya na Haruna Chanongo wa Simba leo wote wamehusika na mabao ya jijini Mbeya. Hii ni mechi yao ya kwanza iliyoisha kwa sare ya 2-2

VIJANA wa Msimbazi, Simba jioni ya leo imeigomea Mbeya City nyumbani kwao kukweka kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuchomoa bao na kulazimisha sareya 1-1 katika pambano kali lililochezwa kwenye uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya.
Wakati Simba ikilazimisha sareugenini, Mtibwa Sugar imejikuta ikichezea kichapo toka kwa Prisons ya Mbeya, huku Mgambo JKT na  Rhino Rangers zikitoka sare ya 1-1 kama ilivyokuwa kwa Oljoro JKT dhidi ya JKT Ruvu na Coastal Union ikishindwa kuonyesha makali wa Oman kwa kulala kwa Ruvu Shooting.
Katika pambano la Mbeya, Simba walishtukizwa na bao la penati katika dakika 13 baada ya William Lucian 'Gallas' kunawa mpira  langoni mwake na Deogratius Julius kukwamisha na kudumu hadi wakati wa mapumziko licha ya kosa kosa za hapa na pale toka kwa timu zote.
Dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, Amissi Tambwe aliisawazishia Simba bao kwa kichwa na kuwa goli lake la 15 la mshambuliaji huyo kutoka Burundi baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Haruna Chanongo aliyepiga krosi murua.
Timu ziliendelea kushambuliana na kufanya mabadiliko ya wachezaji, lakini hakuna kitu kilichobadilika na kufanya mechi kuisha kwa sare ya 1-1 na timu hizo kugawa pointi moja moja na kuiacha Simba ikibakia nafasi ya nne ikiwa na pointi 32 na Mbeya ikifikisha pointi 35 na kulingana na Yanga, lakini uwiano wa mabao umeifanya kubaki nafasi ya tatu.
Kwa sare hiyo imeikwamisha Mbeya City kukwea kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo nafasi waliyokuwa nayo katika mchezo huo kwani ingefikisha pointi 37 na kuzishinda Azam na Yanga ambao wikiendi hii wana majukumu ya kimataifa ugenini nchini Comoro na Msumbiji.
Katika mechi nyingine, Mgambo JKT ilishindwa kuendeleza ubabe katika ligi hiyo baada ya kufungana bao 1-1 na Rhino Rangers mjini Tabora. Wenyeji walianza kuandika bao dakika ya 29 kupitia Gideon Mlami na Mgambo kusawazisha kipindi cha pili dakika ya 51 na Ajali Boli. huku Oljoro JKT kubanwa  nyumbani jijini Arusha mbele ya JKT Ruvu kwa kutoka 0-0 nayo Coastal Union ikisulubiwa na Ruvu Shooting Mlandizi-Pwani kwa kulazwa bao 1-0, bao lililofungwa na Said Dilunga.
Nao Ashanti United ikiwa uwanja wa nyumbani wa Chamazi, wakilazimishwa sare na Kagera Sugar ya kutofunga bao lolote, huku Mtibwa Sugar ikiwa uwanja wa Manungu imelazwa  bao 1-0 na wageni wao Prisons ya Mbeya.

Ngassa azidi kung'ara Afrika apiga hat trick nyingine Comoro, Chuoni yang'oka Shirikisho Afrika yalala kwa Wazimbabwe

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi11gBZHuo7IUZ3uKTJrVrdmUFUir9Z5Oc8ElaQAwQWFmHZj3LJsWXh3x8O43owD9f_7o29fg8A7vqq25rErMvJHI8g06ph2VmhSTCkbJ79-BBwiQgjqAnxZw_YyvPZoNyZUwzusu5h8FIf/s640/blogger-image-1980253589.jpg
Ngassa alipoinyanyasa Komorozine jijini Dar na leo kaifanyia hivyo hivyo kwa kupiga hat trick

WINGA machachari wa kimataifa, Mrisho Ngassa ameendelea kuweka rekodi Afrika baada ya jioni ya leo nchini Comoro kufunga hat trick nyingine na kuondoka na mpira wakati Yanga ikiilaza Komorozine de Domoni kwa mabao 5-2.
Ngassa alifunga mabao matatu katiuka mchezo wa kwanza wakati Yanga ikishinda mabao 7-0 na kuondoka na mpira uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kurudia kitendo hicho leo inamfanya kufikisha jumla ya mabao 6 na kuongoza kwenye orodha ya wafungaji wa michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mabao mengine ya Yanga katika mchezo huo wa marudiano yaliwekwa kimiani na Simon Msuvah na Hamis Kiiza 'Diego'.
Kwa ushindi huo Yanga imefuzu raundi ya kwanza kwa jumla ya mabao 12-2 na kupata nafasi ya kuvaana na mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Al Ahly ya Misri katika mechi mbili kazi inayoonekana ngumu kwa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Nao wawakilishi wa Tanzania Zanzibar katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika Chuoni, imehitimisha safari yake katika michuano hiyo baada ya kulazwa mabao 2-1 na How Mine ya Zimbabwe katika mchezo uliochezwa uwanja wa Amaan Zanzibar.
Chuoni walitangulia kupata bao kabla ya wageni kurejesha na kuongeza la ushindi na kufanya isonge mbele kwa jumla ya mabao 6-1 baada ya mechi ya awali Wazimbabwe hao kushinda nyumbani mabao 4-0.

Hiki ndicho kikosi cha Yanga kitakachoanza Comoro



1. Deogratias Munish "Dida" - 30
2. Mbuyu Twite - 6
3. Oscar Joshua - 4
4. Nadir Haroub "Cannavaro" - 23
5. Kelvin Yondani - 5
6. Athuman Idd "Chuji" - 24
7. Saimon Msuva - 27
8. Haruna Niyonzima - 8
9. Didier Kavumbagu - 7
10. Mrisho Ngasa - 17
11. Hamis Kizza - 20

Subs:
Barthez, Juma Abdul,Luhende, Rajab, Domayo, Dilunga n Bahanuzi

Simba, Mbeya City hapatoshi leo Sokoine

* Mbeya City kukalia kiti cha uongozi leo?
* viwanja vingine vitano kuwaka moto wikiendi hii
Ilivyokuwa hekaheka ya mechi ya kwanza kati ya Simba na Mbeya City

Simba
Mbeya City

Ashanti Utd
JKT Ruvu wapo ugenini jijini Arusha
 
Kagera Sugar watakuwa jiji Dar kuivaa Ashanti
Prisons wageni wa Mtibwa mjini Manungu

Mgambo JKT wapo Tabora kuvaana na Rhino Rangers
Oljoro JKT kuvuna nini kwa JKT Ruvu jijini Arusha?
Ruvu Shooting kuifanyia nini Coastal Union
JIJI la Mbeya leo litasimama kwa muda wakati wenyeji Mbeya City watakapoikaribisha Simba kwenye uwanja wa Sokoine likiwa ni moja ya michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayochezwa leo nchini.
Mechi hiyo inavuta hisia kubwa kuliko hata mechi za kimataifa ambazo timu za Yanga na Azam zilizopo ugenini zitakuwa zikiiwakilisha Tanzania katika kutafuta nafasi ya kufuzu raundi ya kwanza.
Mvuto wa mechi hiyo ya Mbeya unatokana na ukweli kuwa Simba katika mechi zake mbili zilizopita ilionekana kupepesuka, huku Mbeya City inayotajwa kuwa tishio zaidi ikiwa uwanja wa nyumbani ikiwa na kumbukumbu ya kupata sare dhidi ya Mnyama katika mechi yao ya duru la kwanza jijini Dar es Salaam.
Mashabiki wa Mbeya wanaamini Simba leo haitatoka kama walivyoifanyia Mtibwa Sugar au ilipoibana Yanga ilipoenda kucheza nao kwenye uwanja huo mwaka jana.
Hata hivyo mashabiki wa Simba wenyewe wanaamini wameenda Mbeya ili kukata mzizi wa fitina wa kutofungika kwa timu hiyo kwenye uwanja wao wa nyumbani na kutaka kuendeleza ilichokifanya Yanga kwa 'kuitengua udhu' walipoumana nao wiki mbili zilizopita jijini Dar na kuzima rekodi ya kutofungika kabisa licha ya kucheza Ligi Kuu kwa maraya kwanza msimu huu.
Makocha wa timu zote mbili wamenukuliwa wakitambiana kwamba leo ni leo, lakini kwa kuwa mpira ni dakika 90 mashabiki watakuwa na hamu ya kuona mechi hiyo itaishaje.
Simba chini ya makocha Zdrakov Lugarusic na msaidizi wake, Seleman Matola wameapa kupata ushindi ili kurejea kwenye nafasi ya tatu waliyoikalia kwa muda kabla ya Mbeya City kuirejea na kuirudisha Simba nafasi ya nne iliyokuwa inaikamata tangu duru la kwanza lilipoisha.
Kupoteza mchezo huo kunaweza kuitoa Simba kwenye kinyang'anyiro cha ubingwa msimu huu kazi inayowapa wakati mgumu vijana wa Logarusic kukaza msuli Sokoine.
Mbeya City nayo chini ya kocha Juma Mwambusi wameapa kutaka kuizima Simba ili kunyakua pointi tatu na kuzidi kusonga nafasi za juu ili kutimiza ndoto za kutaka kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu katika msimu wao wa kwanza kama walivyowahi kufanya 'kaka' zao Tukuyu Stars mwaka 1987.
Pia ushindi wowote kwa vijana wa Mwmbusi itamaanisha wanaziengua Azam na Yanga zilizopo juu yao na kukalia kiti cha uongozi angalau wiki nzima kwa kuwa itafikisha pointi 37 moja zaidi ya za Azam wanaoongoza sasa na pointi 36 na mbili zaidi ya Yanga wanaokamata nafasi ya pili kwa sasa.
Timu zote zinawategemea nyota wao kadhaa, Simba ikimtambia kinara wa mabao Amissi Tambwe, Ramadhani Singano 'Mess' na Haruna Chanongo, wakati Mbeya City inayoundwa na vijana zaidi ikiwategemea 'wauaji' wao Mwagani Yeya, Paul Nonga, Jeremiah Michael na mkongwe Stephen Mazamba.
Mbali na mechi hiyo iliyo gumzo kwa mashabiki wa soka nchini kote kwa sasa, leo pia kutakuwa na mechi nyingine tano, ambapo Ruvu Shooting itaikaribisha Coastal Union kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi Pwani, huku Mgambo JKT itakuwa ugenini dhidi ya Rhino Rangers.
Mechi nyingine itazikutanisha timu za Oljoro JKT itakayokuwa uwanja wake wa nyumbani wa Sheikh Amri Abeid kuvaana na maafande wenzao wa JKT Ruvu, huku Ashanti Utd wataialika Kagera Sugar kwenye dimba la Chamazi  jijini Dar es Salaam na Mtibwa Sugar itaikaribisha Prisons-Mbeya uwanja wa Manungu.

Vita tupu Kombe la FA England

*Man City, Chelsea leo, Arsenal v Liverpool kesho

LIGI KUU ENGLAND Wikiendi hii itakuwa mapumzikoni ili kupisha michezo ya Raundi ya Tano za Kombe la FA ambapo kazi itaanza leo Jumamosi na kuendelea hadi Jumatatu.
Kubwa kwenye mechi hizo ni Big Match mbili leo Jumamosi na ile ya Jumapili ionayokumbushia mechi za Ligi Kuu ya England watu kutaka kulipizana kisasi. Leo Jumamosi, huko Etihad, Manchester City wataikaribisha Chelsea huku wakikumbuka kufungwa na Chelsea Bao 1-0, wiki iliyopita kwenye Mechi ya Ligi na Jumapili, ndani ya Emirates, Arsenal, watawaalika Liverpool ambao Jumamosi iliyopita waliinyuka Arsenal 5-1 huko Anfield kwenye Mechi ya Ligi.
Ni Kocha Yupi atalimwaga?? kati ya hawa! FA CUP
Raundi ya Tano

RATIBA:
Jumamosi Februari 15

Sunderland v Southampton
Cardiff v Wigan
Sheff Wed v Charlton
Man City v Chelsea

Jumapili Februari 16
Everton v Swansea
Sheff Utd v Nottm Forest
Arsenal v Liverpool
Jumatatu Februari 17
Brighton v Hull

Yanga na kazi nyepesi Comoro leo


WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Yanga leo inatarajiwa kushuka dimbani ikiwa ughaibuni kwa kuumana na Komorozine ya Comoro katika pambano la marudiano la michuano hiyo.
Mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa Sheikh Said Mohamed International uliopo mji wa Mitsamihuli na Yanga ina kazi nyepesi ya kukamilisha ushindi mnono iliyopata katika mechi yao ya nyumbani ilipoisasambua Komorozine mabao 7-0.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Comoro zilizoripotiwa na mtandao wa klabu hiyo ni kwamba mara baada ya juzi jioni kufanya mazoezi mepesi katika uwanja mdogo wa hotel ya Retaj, Yanga ilijifua tena jana  asubuhi majira ya saa 5 ausbuhi katika Uwanja wa Sheikh Said kwa ajili ya kuuzoea tayari kwa ajili ya mchezo wa leo.
Kocha mkuu wa Young Africans Hans Van der Pluijm amesema anashukuru kikosi chake kipo vizuri kuelekea mchezo huo na hakuna mchezaji majeruhi hata mmoja hivyo anapata fursa ya kuchagua amtumie nani katika mchezo huo.
Akiongelea wapinzani timu ya Komorozine de Domoni amesema hawajaidharau kwa mechi ya leo kama watu wengi wanavyofikiria, kikubwa amewaandaa vijana wake waeze kufanya vizuri na kupata ushindi, "Kwangu mie hakuna mechi ndogo wala mchezo wa kirafiki" alisema Hans.
Young Africans itashuka dimbani kucheza mchezo huo wa marudiano ikiwa na kumbukumbu nzuri ya ushindi wa mabao 7-0 iliyoupata katika mchezo wa awali uliofanyika jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika mechi hiyo Mrisho Ngassa alitupia mabao matatu na kushika nafasi ya pili kwa wachezaji wanaoongoza kwa kufunga mabao mengi katika michuano hiyo, ambapo kama leo ataongeza jingine anaweza kujiweka pazuri katika kuwania kiatu cha dhahabu mwishoni ila kama Yanga itasonga mbele mbele ya Al Ahly ya Misri watakaoumana nao kwenye raundi ya kwanza.

Mario Balotelli aibeba Milan Seria A

The man: Balotelli is surrounded by his team-mates after scoring the winner over Bologna
Wachezaji wa AC Milan wakimpongeza Balotelli (45) baada ya kufunga bao pekee katika mechi ya Seria A jana usiku
MSHAMBULIAJI 'mtukutu', Mario Balotelli usiku wa kuamkia leo aliifungia bao pekee timu yake ya AC Milan na kuipa ushindi dhidi ya Bologna katika mechi ya Ligi Kuu ya Italia (Seria A).
Balotelli alifunga bao hilo dakika za lala salama likiwa ni bao lake la 10 msimu huu kwa shuti kali la mita karibu 30 na kuipa ushindi timu yake ambayo imekuwa ikichechemea kwenye ligi hiyo.
Nyota huyo anayeichezea pia timu ya taifa ya nchi hiyo alifunga dakika ya 86 akiwa ndani ya lango la wapinzani na kuifanya Milan kufikisha pointi  32 sawa na kurejea kwenye nafasi ya 10 nyuma ya Lazio.