STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 15, 2014

Sunderland yatangulia robo fainali FA England

Craig Gardner
Sunderland ikifunga bao lake pekee dhidi ya Southampton

SUNDERLAND imeendelea kuonyesha maajabu baada ya kuwa klabu ya kwanza kutinga hatua ya Robo Fainali ya Michuano ya FA baada ya kuitandika Southampton kwa bao 1-0 katika pambano lililochezwa mapema leo.
Vijana hao wa Gustav Poyet waliokuwa wakichechemea kwenye  Ligi Kuu ya England, tayari imeshatinga fainali ya Kombe la Ligi (Capital One) itakapoumana na Manchester City mwezi ujao na ushindi huo wa leo umeipa uhakika wa kuendelea kuonyesha maajabu chini ya kocha huyo.
Bao lililoizamisha Southampton katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Light (Stadium of Light) liliwekwa kimiani katika kipindi cha pili na Craig Gardner.
Gardner alifunga bao hilo katika dakika ya 49 na kuipa wakati mgumu wageni wao kutafuta bao la kusawazisha lakini dakika 90 zilipoisha wenyeji walikuwa washindi na kutangulia robo fainali.
Usiku huu kutakuwa na mechi nyingine za michuano hiyo Cardiff City dhidi ya Wigan Athletic na Manchester City itaikaribisha Chelsea na mechi nyingine iliyokuw aichezwe jioni hii kati ya Sheffield Wedn dhidi ya Charlton Athletic umeahirishwa kutokana na hali mbaya ya hewa.

No comments:

Post a Comment