STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 15, 2014

Mario Balotelli aibeba Milan Seria A

The man: Balotelli is surrounded by his team-mates after scoring the winner over Bologna
Wachezaji wa AC Milan wakimpongeza Balotelli (45) baada ya kufunga bao pekee katika mechi ya Seria A jana usiku
MSHAMBULIAJI 'mtukutu', Mario Balotelli usiku wa kuamkia leo aliifungia bao pekee timu yake ya AC Milan na kuipa ushindi dhidi ya Bologna katika mechi ya Ligi Kuu ya Italia (Seria A).
Balotelli alifunga bao hilo dakika za lala salama likiwa ni bao lake la 10 msimu huu kwa shuti kali la mita karibu 30 na kuipa ushindi timu yake ambayo imekuwa ikichechemea kwenye ligi hiyo.
Nyota huyo anayeichezea pia timu ya taifa ya nchi hiyo alifunga dakika ya 86 akiwa ndani ya lango la wapinzani na kuifanya Milan kufikisha pointi  32 sawa na kurejea kwenye nafasi ya 10 nyuma ya Lazio.

No comments:

Post a Comment