STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 15, 2014

Manchester City waikalisha Chelsea FA Cup

Manchester City celebrate
Samis Nasir akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao la pili lililoizamisha Chelsea kwenye FA Cup hivi punde
Daa Chuma hichooo! Petr Cech na beki wake hawaamini kama Jovetic amefunga bao la kuongoza

MABAO mawili ya  Steven Jovetic na jingine la Samir Nasir yametosha kuzima ndoto za kocha Jose Mourihno kuitambia kwa mara ya pili Manchester City baada ya timu yake ya Chelsea kuondoshwa kwenye michuano ya Kombe la FA muda mfupi uliopita.
Jovetic alifunga bao la kwanza dakika ya 16 kwa pasi ya Edin Dzeko kabla ya Samir Nasir kuongeza la pili katika kipindi cha pili akimalizia kazi ya David Silva katika dakika ya 67 na kuipeleka Manchester City hadi Robo Fainali ya michuano hiyo.
Wiki mbili zilizopita Chelsea iliitambia City nyumbani kwao kwa kuilaza bao 1-0 na leo ilitarajiwa labda wangerejea kitendop hicho, lakini vijana wa Etihad walikuja kivingine na kuibana Chelsea na kuendelea kuweka hai matumaini ya kunyakua mataji nne msimu huu.
City tayari imetinga fainali ya Kombe la Ligi (Capital One) na inashiriki pia Ligi ya Mabingwa Ulaya na ipo kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England.

No comments:

Post a Comment