STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 15, 2014

Vita tupu Kombe la FA England

*Man City, Chelsea leo, Arsenal v Liverpool kesho

LIGI KUU ENGLAND Wikiendi hii itakuwa mapumzikoni ili kupisha michezo ya Raundi ya Tano za Kombe la FA ambapo kazi itaanza leo Jumamosi na kuendelea hadi Jumatatu.
Kubwa kwenye mechi hizo ni Big Match mbili leo Jumamosi na ile ya Jumapili ionayokumbushia mechi za Ligi Kuu ya England watu kutaka kulipizana kisasi. Leo Jumamosi, huko Etihad, Manchester City wataikaribisha Chelsea huku wakikumbuka kufungwa na Chelsea Bao 1-0, wiki iliyopita kwenye Mechi ya Ligi na Jumapili, ndani ya Emirates, Arsenal, watawaalika Liverpool ambao Jumamosi iliyopita waliinyuka Arsenal 5-1 huko Anfield kwenye Mechi ya Ligi.
Ni Kocha Yupi atalimwaga?? kati ya hawa! FA CUP
Raundi ya Tano

RATIBA:
Jumamosi Februari 15

Sunderland v Southampton
Cardiff v Wigan
Sheff Wed v Charlton
Man City v Chelsea

Jumapili Februari 16
Everton v Swansea
Sheff Utd v Nottm Forest
Arsenal v Liverpool
Jumatatu Februari 17
Brighton v Hull

No comments:

Post a Comment