STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 21, 2014

'Uelewa Mdogo, Posho yavuruga wajumbe Bunge la Katiba'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEip-Tppcjw3lFnVUNKp9lt1kTz9VZYN2JeRPqecyYFQbXFvbP_UWM0k5Z_EMMpq7P7cFgofZMnDj2VrCpPqQRkIhhFCu9MSjXzlOnvnQnPkFBJsqCJofL-OvEbgaIKzCxbXs8ri7uqRKRw/s1600/NCCR.JPG
Samuel Ruhuza (kulia)
Na Suleiman Msuya
ALIYEWAHI kuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha NCCR Mageuzi Samuel Ruhuza amesema uelewa mdogo na posho wanaopokea wajumbe wa Bunge la Katiba ndicho chanzo kikubwa kinachosababisha kutohairishwa kwa bunge hilo linaloendelea Mkoani Dodoma.
Ruhuza alisema hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam ambaye alitaka kujua nini mtazamo wake juu ya Bunge la Katiba.
Alisema uelewa wa katiba ni changamoto kwa wananchi walio wengi ila inatia shaka pale ambapo wawakilishi wao katika bunge lao wanakuwa na uelewa mdogo zaidi na kinyume chake ni kutoa kauli za kashfa na sio za kujenga hoja ambazo zinaweza kuleta katiba nzuri.
Katibu Mkuu huyo wa zamani alisema kwa asilimia kubwa ya wajumbe wa bunge hilo wanaonekana ni watu ambao wanafikiria maslahi yao jambo ambalo linaweza kupatikana kwa katiba isiyo na tija kwa wananchi na nchi kwa ujumla.
Alisema wapo wajumbe hasa wa chama tawala (CCM) ambao wanaonekana kuwa wameambiwa maneno ya kusema jambo ambalo si haki kutokana na ukweli kuwa kilichopo kwenye rasimu ni maoni ya wananchi na sio chama.
“Mimi nimekuwa nikifuatilia tangu Bunge hilo lilivyo anza tatizo kubwa ni baadhi ya wajumbe hasa kutoka CCM wanaonekana kuwa hawajaenda pale kama wao ila wapo kutokana na msimamo wa chama jambo ambalo sahihi.”, alisema Ruhuza.
Ruhuza alisema pamoja na uelewa mdogo juu ya utengenezaji katika posho pia ni sababu kubwa ambayo inachangia kutohairishwa kwa bunge hilo ambalo limekosa mvuto kwa jamii ya Watanzania.
Alisema iwapo posho isingekuwepo ni dhahiri baadhi ya wajumbe ambao sio wanachama wa CCM wasingeendelea kujadili lakini ni ukweli kuwa 300,000 sio ndogo kwa siku hivyo ni vigumu kuikataa kama huna uzalendo na nchi yako.
Aidha alisema katika kuthibitisha hilo ni katika suala la muda wa wabunge kuwepo katika madaraka kwa kipindi cha miaka kumi na tano ambapo wamekiondoa na kusahau kuwa Rais yeye ana kikomo cha uwepo wa nafasi hiyo.
Ruhuza alisema ni wazi kuwa wabunge wengi waliopo katika bunge hilo wanatetea maslahi yao na sio jambo ambalo linaweza kukosekana au kupatikana katiba ambayo itakuwa na maslahi kwa jamii.
Katibu huyo alisema  ni vigumu rasimu ya katiba iliyopendekezwa na tume ya katiba kukubalika kwa wanasiasa kutokana na ukweli kuwa inagusa maslahi ya wanasiasa wengi ambao wapo katika Bunge la Muungano kutokana na mazingira yasiyovutia watu wengi.
Alisema rasimu inataka kuwepo kwa wabunge wawili kila mkoa na kuondolewa kwa viti maalum hivyo ni wazi kuwa wajumbe waliowengi wataendelea kuipinga kwa kila njia kwa dhana kuwa fulani akiingia madarakani atampatia nafasi.
Kuhusiana na sintofahamu iliyopo juu ya idadi ya serikali ambazo zimependekezwa alisema ni vema wananchi na viongozi wote wakatambua kuwa muungano hauwezi ukawa kwa kila kitu hasa muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao ulizaa Tanzania.
Alisema ni ngumu kuamni kuwa muungano upo wakati ni wazi kuwa Rais wa Zanzibar analindwa na mwanajeshi kama anavyolindwa Rais wa Muungano.
Katibu huyo wa zamani alisema ni vigumu kwa wazanzibar kukubaliana na rasimu iliyopo kwani inawanyanganya madaraka ambayo wamepewa na Katiba ya Zanzibar iliyopo sasa.
Ruhuza alitoa rai kwa Watanzania kutambua kuwa wao ndio wanatakiwa kusimamia maslahi yao wenyewe kwani wanasiasa hawawezi kuwa sahihi kwa kila jambo ambapo alitolea mfano katika suala hilo la katiba wananchi wamekuwa wakiambiwa mambo ambayo hayana tija kwa maslahi yao.

HII NDIYO RATIBA YA LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015



Snake Boy Jr, Nassib kurudiana Dar

Bondia Mohamed Matumla kushoto na Nassibu Ramadhani wakitunishiana misuli 
Na Mwandishi Wetu
 MABONDIA Nassibu Ramadhani pamoja na Mohamed Matumla 'Snake Boy Jr' wameingia makubaliano ya kuzipiga kwa mara ya pili siku ya septemba 27 katika ukumbi wa Friends Corner, Manzese Dar es salaam.

Akizungumzia mpambano huo mratibu wake Yassin Abdallah 'Ustadhi' amesema mabondia hao wamekubaliana na kusaini mkataba wa kuzipiga siku hiyo, ambapo ni marudiano baina yao kwani walishakutana mapema mwaka huu na Matumla kumshinda mpinzani wake kwa pointi.

Ustaadh alisema siku ya pambano hilo ambalo ameshindwa kutabiri kama ni Nassib atalipa kisasi au Matumla kuendeleza ubabe kutakuwa na michezo kadhaa ya utangulizi.

Baadhi ya michezo hiyo ni pamoja na lile pambano la

  Issa Omardhidi ya Juma Fundi katika uzani wa kg 53 raundi nane, Sadiq Momba vs Tasha Mjuaji kg 59 raundi nane, huku Juma Mustafa atamkabili Bakari Dunda kg 61 raundi sita.

Pia siku hiyo wanadada Lulu  Kayage atapambana na Fatma Yazidu kg 51 raundi nne.

siku hiyo pia kutakuwa na huuzwaji wa  DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.

Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Paquaio,Floyd Maywether,Amir Khani, Mohamed Ali ,Mike Tayson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani
kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi

Azam yakwama Sudan, yang'oka Kagame kwa matuta

http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/08/AZAM-FC-KIKOSI-1-546x291.jpg
WAWAKILISHI pekee wa Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa AfrikaMashariki na Kati, Kombe la Kagame,  Azam FC ya Chamanzi jijini Dar es Salaam imetupwa nje ya michuano hiyo mikubwa kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati baada ya kucharazwa mikwaju 4-3 dhidi ya El Marreikh ya Sudani katika mchezo wa pili wa robo fainali.Wachezaji ambao walielezwa awali kuwa wanasumbuliwa na vyama za paja lakini wakashuka katika dimba la Nyamirambo mjini Kigali Rwanda ndio walioigharimu Azam FC licha ya mlinda mlango  Mwadin Ally kufanya kazi nzuri ya kupangua penati ya wapinzani wao. 

Wachezaji walioipa tiketi ya kurejea nyumbani Azam FC kujiandaa na mchezo wao wa Ngao ya Hisani dhidi ya Yanga SC ni beki Shomary Kapombe na mshambuliajiLionel Saint- Preux kutoka Haiti.
Aidha kocha wa mabingwa hao wapya wa soka la Tanzania, Mcameroon JosephMarious Omog ameonekana amekuwa akiandaa Azam FC kitaalamu mnokuelekea mchezo huo, ambapo mbali na mambo mengine aliwaelekeza mifumona aina tofauti ya uchezajiikiwa ni pamoja na kutumia mipira mirefu na mifupi.
Omong aliwaandaa wachezaji wake pia kwa kupiga penaltilakini hakuna kilichofua dafu kutokana na upigaji wa kimakosa uliofanywa na Kapombe aliyepaisha penati yake juu na gonga mwamba na Preux aliyepiga mpira mwepesi na kumwezesha mlinda mlango wa Merreikh kuificha bila shaka.

Simba, Yanga kuonyeshana kazi Okt.12

Kikosi cha wakali wa Msimbazi
Vijana wa Jangwani
WATANI wa jadi Simba na Yanga watakutana mapema katika raundi ya nne ya ligi Oktoba 12 mwaka huu, kwa mujibu wa ratiba ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara 2014-15 iliyotolewa jana na shirikisho la soka nchini (TFF).
Miamba hao wa soka nchini watarudiana katika raundi ya 17 ya ligi hiyo Februari 8, 2015, ratiba hiyo imeonyesha.
Mabingwa Azam FC wataanza kampeni ya kutetea taji lao la kwanza kwa kuwakaribisha Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Azam Complex katika siku ya kwanza ya ufunguzi wa msimu Septemba 20, siku ambayo viwanja sita 'vitawaka moto'.
Yanga waliomaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita wataanza msimu mpya chini ya kocha mpya Mbrazil Marcio Maximo kwa kucheza ugenini dhidi ya timu inayozinyima usingizi timu kubwa ya Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Jamhuri wakati Mbeya City waliomaliza katika nafasi ya tatu watawakaribisha JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Simba waliomaliza wa nne msimu uliopita wataingia katika mtihani wa kwanza chini ya kocha mpya Mzambia Patrick Phiri kwa kuwakaribisha Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika siku hiyo ya ufunguzi wa msimu.
Mechi nyingine za siku ya ufunguzi zitakuwa ni wageni wa ligi hiyo Stand United watakaowakaribisha wageni wenzao Ndanda FC kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga huku Mgambo JKT ikiwa mwenyeji wa Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati Ruvu Shooting itawakaribisha Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Mabatini, mkoani Pwani.
Yanga watakuwa na mechi mbili ngumu zilizofuatana katika raundi ya nane na ya tisa ya ligi pale watakapowakabili mabingwa Azam Novemba 9 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa na kisha kusafiri hadi ugenini Mbeya kuwavaa Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine siku sita baadaye.
Simba watawakaribisha Mbeya City katika raundi ya 10 ya ligi kwenye Uwanja wa Taifa Desemba 20 mwaka huu kabla ya kuwavaa Azam katika raundi ya 12 siku ya Mwaka Mpya Januari 1, 2015 kwenye Uwanja wa Taifa. Ligi hiyo itafikia tamati Aprili 18, 2015.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, ratiba hiyo imezingatia michuano ya Chalenji itakayochezwa Novemba, usajili wa dirisha dogo Nov 15- Des 15, ushiriki wa klabu za Azam na Yanga kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa (CL) na Kombe la Shirikisho (CC).
Wambura alisema mechi za ligi hiyo zitachezwa wikiendi ili kuongeza msisimko/kuwapa fursa washabiki wengi zaidi kuhudhuria na kwamba katikati ya wiki imeachwa wazi kwa ajili ya mechi za Kombe la FA (Federation Cup).
"Vilevile kutakuwa na mechi Boxing Day na siku ya Mwaka Mpya," alisema Wambura.

Omar Katanga amfuata Kutenge EFM

Aliyekuwa mtangazaji wa Redio One katika kipindi cha “Spot Leo” Omary Katanga (pichani kushoto) naye pia ameamua kufuata nyayo za pacha wake Maulid wa Kitenge aliyejiunga na  kituo cha redio (93.7) E FM  mapema wiki hii.
Katanga, aliyeweka wazi na kuripoti katika kituo hicho, ameamua kumfuata pacha wake Maulid Kitenge, ikiwa ni siku ya tatu tu tangu Kitenge alipojitangaza kwenye ukurasa wake wa Facebook na mitandao mingine kuwa ameamua kujiuzulu kazi na saa chache kutangazwa kujiunga na kituo hicho.
Watangazaji haowaliokuwa wakipiga kazi pamoja kwenye kipindi cha michezo katika kituo cha Redio One, wanatarajiwa kuanza kusikika hewani E FM 93.7 kuanzia kesho katika kipindi cha michezo cha E Sports, ambacho kitakuwa kikiruka kila siku saa 7:00 – 7:30 jioni.
Watangazaji hao wanajiunga na watangazaji wengine maarufu kama Dennis Ssebo, Dickson Ponnela (Dizzo 1), DJ Majay, na Kanky.

Serikali kujenga kiwanda cha kuzalisha viua mbu

Frank Mvungi-Maelezo
Serikali kutumia Euro Milioni 16 katika ujenzi wa Kiwanda cha kuzalisha viuadudu vinavyoua viluwiluwi vya mbu wanaoambukiza malaria ulioko chini ya shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) unaotarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.
Hayo yamesemwa na Meneja Uhusiano wa Shirika hilo Bw. Abel Ngapemba wakati wa mkutano nawaandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
“Hivi sasa majengo yote yamekwisha kamilika katika eneo la Maili moja Kibaha Mkoani Pwani na mitambo yote imeshawasili na wataalamu wanaifunga ambapo kabla ya mwisho wa mwaka   uzalishaji  wa majaribio utaanza” Alisema Ngapemba.
Akifafanua zaidi Ngapemba alisema kiwanda hicho kitasaidia kuzalisha ajira  za moja kwa moja zipatazo 172 kwa watanzania.

Pia Ngapemba alibainisha kuwa kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha lita milioni sita za viadudu kwa mwaka ambapo asilimia 80 ya dawa hizo zitatumika nchini na asilimia 20 zitauzwa nchi za nje ambazo tayari zimeonyesha nia ya kuzitaka dawa hizo.
Viadudu hivyo vinatengenezwa kutokana na vimelea ambao wanakuzwa kwa kutumia viinilishe mbalimbali na kunyinyiziwa katika maeneo yenye mazalia ya mbu ambapo viluwiluwi wa mbu wanapovila wanakufa
Kulingana na ripoti ya upembuzi yakinifu wa mradi huu uliofanywa na NDC kwa kushirikiana na kampuni ya Labiofam ya Cuba mwaka 2010, mbali na malaria kusababisha vifo vya Watanzania wapatao 80,000 kwa mwaka,ambapo watu milioni 18 huugua ugonjwa huo kila mwaka ambapo Serikali imekuwa ikitumia kiasi cha dola za marekani zipatazo milioni 240 kwa mwaka katika kupambana na ugonjwa huu.
Ujenzi wa Kiwanda hicho ulianza miaka miwili iliyopita na kuwekwa jiwe la msingi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Jakaya Mrisho Kikwete October mwaka 2013 lengo likiwa kupambana na hatimaye kutokomeza mbu wanaoeneza malaria na magonjwa mengine yaenezwayo na mbu.

Taarifa za wabunge, wagombea watarajiwa Uchaguzi Mkuu kisasa zaidi

Uchaguzi Mkuu wa Wabunge na Rais unataraji kufanyika hapo mwakani, Wabunge na wanaotaka kuwania Ubunge katika majimbo mbalimbali nchini hata urais mnakaribishwa kuandaa TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA VYAMA VYENU. Kitabu kama hicho kitakuwezesha wewe Mgombea kuto tumia nguvu kuubwa ya kujinadi badala yake utavigawa kwa wananchi mbalimbali jimboni kwako nawe kuelewa nini umewafanyia katika kipindi ambacho ulikuwa madarakani. 

Pia wagombea wapya pia wanaweza andaa vitabu kama hivi kuonesha yale ambayo wameshiriki kuyafanya na wanataraji kuyafanya chini ya ilani za vyama vyao husika. 

Mawasiliano zaidi kwa wenye uhitaji: Mroki Mroki (pichani juu) 
+255 717 002303/0755 373999/0788207274 
au barua pepe: mrokim@gmail.com