STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, August 21, 2014

Omar Katanga amfuata Kutenge EFM

Aliyekuwa mtangazaji wa Redio One katika kipindi cha “Spot Leo” Omary Katanga (pichani kushoto) naye pia ameamua kufuata nyayo za pacha wake Maulid wa Kitenge aliyejiunga na  kituo cha redio (93.7) E FM  mapema wiki hii.
Katanga, aliyeweka wazi na kuripoti katika kituo hicho, ameamua kumfuata pacha wake Maulid Kitenge, ikiwa ni siku ya tatu tu tangu Kitenge alipojitangaza kwenye ukurasa wake wa Facebook na mitandao mingine kuwa ameamua kujiuzulu kazi na saa chache kutangazwa kujiunga na kituo hicho.
Watangazaji haowaliokuwa wakipiga kazi pamoja kwenye kipindi cha michezo katika kituo cha Redio One, wanatarajiwa kuanza kusikika hewani E FM 93.7 kuanzia kesho katika kipindi cha michezo cha E Sports, ambacho kitakuwa kikiruka kila siku saa 7:00 – 7:30 jioni.
Watangazaji hao wanajiunga na watangazaji wengine maarufu kama Dennis Ssebo, Dickson Ponnela (Dizzo 1), DJ Majay, na Kanky.

No comments:

Post a Comment