STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 4, 2013

Masheikh wauwawa Mombasa, kanisa lachomwa moto katika ulipizaji kisasi

Sheikh Abuu Rogo enzi za uhai wake, huyu aliuwawa mwaka jana

POLISI Kenya imetangaza kuwa, watu wanne akiwemo Sheikh Ibrahim Ismail Rogo wameuawa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana ndani ya gari dogo jana usiku huko mjini Mombasa.

Taarifa ya Polisi Kenya imeeleza,  Sheikh Ibrahim Rogo alikuwa mrithi wa Sheikh Aboud Rogo ambaye  naye aliuawa na familia yake kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana mwezi Agosti 2012.

Mauaji ya Sheikh Ibrahim Rogo ambayo yameutikisa mji wa Mombasa, yametokea  baada ya kupita takriban wiki mbili tokea kundi la al Shabab lilipovamia  na kuua  watu wasiopungua 63 na kujeruhi mamia ya wengine kwenye jengo la maduka ya biashara la Westgate jijini Nairobi.

Baadhi ya wananchi wa Mombasa wanakituhumu kikosi  maalumu cha kupambana na ugaidi kuwa ndicho kilichotekeleza  mauaji hayo.

Sheikh Ibrahim Rogo ambaye alikuwa akitoa mihadhara kwenye Msikiti wa Musa mjini Mombasa alituhumiwa na jeshi la polisi kuwa anawachochea vijana wa Kiislamu kujitumbukiza kwenye makundi  ya kigaidi.

Polisi Kenya imesema kuwa, Gaddafi Mohammad, Issa Abdallah  na Omar Abu Rumeisa ni miongoni mwa waliouawa, naye Salim Aboud alinusurika kwenye shambulio hilo.

=========

Protestors on Friday engaged armed police in running battles in Mombasa following killing of a Muslim cleric, and three others.

The rioting youths in Majengo area set a church on fire.

Earlier in the morning, hundreds of armed police were deployed across islamist strongholds in Majengo and Kisauni  as authorities anticipated riots from slain Sheikh Ibrahim Rogo’s militant supporters.

Tension which has been building up since Thursday’s blood end of Sheikh Rogo and his three friends was expected to reach boiling point at the afternoon Friday prayers in areas like Majengo especially at Musa Mosque where the slain preacher delivered controversial ceremonies.

Reports show that Sheikh Ibrahim delivered a lecture at the mosque at about 8.00pm on Thursday before  embarking on his last journey to meet his end in a drive by shooting near the Butterfly Pavillion afew minutes before 10.00pm long the Mombasa-Malindi road.

Unconfirmed reports indicate  the four were buried in the early hours of Friday at the same cemetery where slain radical islamist Sheikh Aboud Rogo Mohamed was buried on August 27 last year.

It is not clear whether the two Rogos are related.

Reports indicate the four victims were buried in a single grave at the Tudor Muslim Cemetery and accorded the rites of martyrs.

Supporters have identified the other victims as Abu Rumaysa Omar and others identified only as Issa and Shebe Gaddafi.

Salim Aboud who was with them escaped unscathed but with brief facial injuries after playing dead among the slumped corpses inside a bullet ridden car.

Militant islamist Sheikh Abubakar Shariff alias Makaburi who was among the first people to reach the scene of crime declared Thursady’s events as “an assassination” claiming state agents slew the four muslims “in retaliation” for the terrorist carnage at the Westgate Mall in Nairobi last month.

Makaburi who is facing terrorist charges and was  an ally of slain islamist Sheikh Aboud Rogo Mohamed claimed Sheikh Ibrahim Rogo was the target of Thursday’s shooting because of his past links to the former Rogo who was killed on August 27 last year.

And Makaburi denounced the Kenya government and  muslims collaborating with it following the Westgate massacre and in light of Thursday’s events.

He further warned that muslims are now justified to disobey Kenyan laws “because we cannot sit back and be slaughtered or see our sheikhs killed everyday.”

As they descended on the scene where the four were killed militant supporters of the slain preacher swore to avenge the killing.

According to Kisauni OCPD Julius Wanjohi who covers Bamburi where the killings took place, the four were killed when a “vehicle with unknown occupants sped past the car which was carrying Sheikh Ibrahim and four others and slowed a few metres from the vehicle.”

The OCPD says the occupants of the unknown car opened fire on the right side of the approaching car carrying Sheikh Ibrahim.

Wanjohi further says Sheikh Ibrahim and three others were killed “on the spot and the vehicle sped away” apparently towards Bamburi.

According to the OCPD Sheikh Ibrahim’s car was heading towards Mtwapa where he is believed to live.
Source: Standard

Kaburi ya anayedaiwa kufufua lafukuliwa kuchunguza viungo vilivyokuwepo ndani yake

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida kaburi ambalo alizikwa mtoto Shabani Maulidi (15), ambaye anadaiwa kufariki dunia miaka mitatu iliyopita na kuonekana akiwa hai hivi karibuni, jana lilifukuliwa na viungo vya mwili wake kukutwa ndani.
Kazi hiyo iliyofanyika chini ya ulinzi mkali wa polisi pamoja na Mtafiti wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Mkoa wa Mwanza, Lucas Ndungulu, ilizua taharuki kwa umati wa watu waliokuwa eneo hilo, baada ya nyumba ya jirani lilipo kaburi hilo, Masanja Marwa, kubomoka ghafla wakati ufukuaji huo ukiendelea, huku mwanamke mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja naye akianguka na kuzirai.
Kwa sasa mtoto huyo ambaye alionekana hai, amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita kwa uangalizi wa kitaalamu.
Akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio, Ndungulu alisema kuwa wameamua kufukua kaburi hilo ili kupata sehemu ya viungo vya mwili kwa ajili ya vipimo.
“Lengo la kufukua kaburi hili ni kutaka tupate kiungo chochote cha mwili wa marehemu ili tufanye utafiti wa kitaalamu ili tujue kama ni kweli huyu anayedaiwa kuwa ni mtoto wao ndiye,” alisema.
Alisema kuwa ufukuaji huo umemalizika na kwamba wamepata baadhi ya viungo vya mwili wa marehemu na kuchukua baadhi ya mifupa ya mapaja yote mawili ambayo itapelekwa katika hospitali ya rufaa kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Kwa mujibu wa Ndugulu, majibu ya vipimo hivyo yatatolewa baada ya wiki mbili kama hakutakuwa na tatizo lolote la kukatika kwa umeme.
Naye Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Geita, Adamu Sijaona, alisema kuwa pamoja na kuchukua viungo hivyo, pia watachukua damu ya wazazi na mtoto mwenyewe.
“Tumechukua pia damu ya mama na baba wa Maulidi mwenyewe ili tukapime vinasaba (DNA) na kama alivyosema mtafiti, majibu yatatoka baada ya wiki mbili,” alisema.
Akizungumza baada ya kazi ya ufukuaji kumalizika, baba mzazi wa mtoto huyo, Maulidi Shabani, alisema kuwa endapo majibu yatakuja tofauti au vile wanavyokusudia, wapo tayari kuyapokea na kwamba ikigundulika huyo aliyeonekana ni Maulidi, pia watampokea na kuendelea kumtunza.
“Lakini nina imani kuwa huyu aliyeonekana ni mwanangu Maulidi kabisa, kwa sababu anazo alama zote,” alisema mzazi huyo.
Mtoto Maulidi aliyefariki dunia miaka mitatu iliyopita na kufanyiwa matanga, alionekana akiwa hai baada ya kukutana na mama yake ana kwa ana mapema wiki hii asubuhi wakati akienda kwenye shughuli zake za biashara.
Ilidaiwa na wazazi wake kuwa Maulidi alitoweka ghafla na kushindwa kurudi nyumbani kwao Januari mosi 2011, wakati alipokuwa amewapeleka mbuzi malishoni na mwili wake kuonekana baada ya siku tatu akiwa amefia kwenye kisima cha maji.
Kwa mujibu wa baba yake, Maulidi hakurudi nyumbani siku hiyo, ambapo waliendelea kumtafuta bila mafanikio na ndipo baada ya siku tatu walimkuta akiwa amefia ndani ya kisima cha maji kilicho maeneo ya Kijiji cha Nyankumbu, Kitongoji cha Mwembeni.
Tukio hili ni la tatu kutokea mkoani hapa ambapo wilayani Kasamwa, mwanamke aliyefariki dunia miaka mitano iliyopita alionekana hai na kutambuliwa na ndugu yake. Tukio la pili lilitokea Wilaya ya Chato, wakati kijana aliyefariki dunia miaka miwili iliyopita alionekana akiwa hai.
Tanzania Daima

Kuziona Simba na Ruvu Buku 5 tu, Mohammed Theofil kuzihukumu Taifa

Ruvu Shooting wakataokuwa wenyeji wa Simba
Vinara wa Ligi Kuu, Simba watakaovaana na Ruvu Shooting kesho jijini Dar
Na Boniface Wambura
KITIMTIM cha michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kinatarajiwa kuingia raundi ya saba kesho (Oktoba 5 mwaka huu)  kwa mechi nne ambapo Ruvu Shooting itakuwa mwenyeji wa vinara Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Viingilio katika mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Mohamed Theofil kutoka Morogoro kuanzia saa 10 kamili jioni vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000. Tiketi zitauzwa uwanjani kuanzia saa 4 asubuhi.

Mechi nyingine za kesho ni JKT Ruvu itakayoumana na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam huku Coastal Union ikiwa mwenyeji wa Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha ndiyo utakaotoa fursa kwa timu za Oljoro JKT na Mbeya City kuoneshana ujuzi katika kusaka pointi tatu.

Ligi hiyo itaendelea Jumapili (Oktoba 6 mwaka huu) kwa mechi kati ya Yanga na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Mgambo Shooting itaialika Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Maamuzi ya Kamati y Maadili TFF kufanyiwa mapitio upya, kisa...!

MCHAKATO wa Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) unaelekeo ukingoni ambapo Maamuzi ya Kamati ya Maadili yanatarajiwa kupitiwa kabla ya kuelekea kwenye uchaguzi huo utakaofanyika Okt 26/27 jijini Dar es Salaam.

Hivi sasa, wagombea wanasubiri vyombo vya juu vya uamuzi kwa ajili ya kutoa uamuzi wa mwisho kabla ya kuanza kampeni na hatimaye uchaguzi.

Hata hivyo, baada ya Kamati ya Maadili kufanya uamuzi dhidi ya kesi nane zilizowasilishwa mbele yake, Sekretarieti imeona kuwepo kwa ukakasi katika utekelezaji wa uamuzi huo kutokana na ukweli kuwa kuna baadhi ya mambo yanaonekana kuwa na ugumu katika kuyatekeleza.

Sekretarieti si chombo chenya mamlaka ya kutafsiri uamuzi wa vyombo huru vya Shirikisho, kazi yake kubwa ni kupokea uamuzi na kuutekeleza, hivyo kwa kuwa kuna ukakasi huo imeamua kuwasilisha uamuzi huo kwenye Kamati ya Rufani ya Maadili kwa ajili ya kuufanyia mapitio (revision) na pia kutoa mwongozo kabla ya kurejesha uamuzi huo kwenye Kamati ya Uchaguzi kwa ajili ya kuendelea na mchakato.

Sekretarieti imefanya hivyo kwa lengo la kusaidia wagombea ambao wengi wanaonekana kuwa njia panda baada ya kupokea uamuzi wa Kamati ya Maadili na kuiuliza Sekretarieti kuwa inakuwaje Kamati ya Maadili iwaone hawana hatia, lakini hapo hapo ikubaliane na uamuzi wa kuwaengua, jambo ambalo kwa kweli limetufanya tukose majibu sahihi na hivyo kuamua kuomba revision na mwongozo.

Pia mwongozo utakaotolewa na Kamati ya Rufani ya Maadili utasaidia kuweka mwelekeo mzuri wa masuala ya Maadili katika siku zijazo.

Miongoni mwa mambo yanayoonekana kuwa na ukakasi ni kuwaona watu wote ambao kesi zao ziliwasilishwa kwenye Kamati ya Maadili hawana hatia, lakini hapo hapo kukubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi wa kuwaengua baadhi yao kwa sababu za kinidhamu ikisema haiwezi kuwahukumu mara mbili kwa kuwa wameshaadhibiwa kwa kuenguliwa kwenye uchaguzi.

Ili haki itendeke na ionekane inatendeka, Sekretarieti imeona ni vizuri masuala hayo yakafanyiwa revision (mapitio) na kutolewa mwongozo ili kuondoa ukakasi uliojitokeza miongoni mwa wagombea, Shirikisho na wadau na hivyo kujenga hisia kuwa kuna mbinu zimefanyika dhidi ya baadhi ya wagombea.

Uamuzi huu haumaaniishi kuwa Sekretarieti inapingana na uamuzi wa Kamati ya Maadili, bali ni utaratibu wa Sekretarieti kuomba ufafanuzi au mwongozo kutoka vyombo husika pindi inapotokea ukakasi katika utekelezaji wa uamuzi wa vyombo vya uamuzi vya Shirikisho.

Sekretarieti imeshamwandikia Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani za Maadili ili aitishe kikao kwa manajiri ya kufanya mapitio na kutoa mwongozo ambao utasaidia Shirikisho kuendelea na uchaguzi bila ya ukakasi.

TFF yaipigia goti serikali, taasisi kuisaidia U20 WanawakeSerikali, T

Lina Kessy
Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeiomba Serikali, taasisi na kampuni mbalimbali kuisaidia timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 inayojiwinda kwa mechi ya Kombe la Dunia dhidi ya Msumbiji.

Timu hiyo hivi sasa iko kambini Mlandizi mkoani Pwani chini ya Kocha Rogasian Kaijage kujiandaa kwa mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza itakayochezwa Oktoba 26 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mpira wa Miguu ya Wanawake ya TFF, Lina Kessy amesema hiki ndio kipindi muafaka cha kuisaidia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Ameitaka jamii kujitokeza kuisaidia timu hiyo ambayo haina mdhamini wala mfadhili, kwani timu za Taifa ni za Watanzania badala ya kusubiri ifanye vibaya na kusema ni kichwa cha mwendawazimu.

Kessy ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA), ameishukuru kambi ya JKT Ruvu kwa kutoa fursa ya kambi kwani timu hiyo hailipii malazi badala yake inalipia huduma nyingine inazopata hapo.

Vilevile amewashukuru wadau mbalimbali ambao wamekuwa wakijitolea kutokana na ukweli kuwa tangu kuanza mashindano ya mpira wa miguu wa wanawake kumekuwepo uungwaji mkono mkubwa.

“Shukrani za kipekee kwa wazazi kukubali watoto wao wachezee timu ya Taifa, kwani wengi bado wanasoma na wapo chini ya uangalizi wa wazazi. Pia tunawaomba wazazi wajitokeze mazoezini ili kuwajenga kisaikolojia wachezaji wetu,” amesema.

Fainali za Dunia za U 20 kwa wanawake zitafanyika mwakani nchini Canada. Iwapo Tanzania itaitoa Msumbiji katika raundi hiyo, raundi inayofuata itacheza na mshindi kati ya Botswana na Zimbabwe.

TFF, Polisi wapiga mkwara 'wakora' viwanjani

http://reluctantgourmet.com/media/k2/items/cache/2e2c1711fe12b24ae23d95c35bfd21c2_XL.jpg
Kisu, moja silaha hatari inayowezwa kutumiwa vibaya na mashabiki uwanjani kuleta maafa
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia Jeshi la Polisi kuanzia sasa halitashikilia silaha za washabiki, na badala yake litawazuia kabisa kuingia viwanjani wakati wa mechi.

Jeshi la Polisi limekuwa likihifadhi silaha za washabiki wanaokwenda viwanjani, na baadaye kuwarejeshea baada ya mechi kumalizika kwa vile Kanuni za Usalama Viwanjani za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) zinakataza silaha viwanjani.

Wikiendi iliyopita katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Jeshi la Polisi lilikamata bastola 17 katika upekuzi wa washabiki waliokwenda kushuhudia mechi kati ya Yanga na Ruvu Shooting na ile kati ya JKT Ruvu na Simba. Wote waliokutwa na silaha hizo walikuwa na leseni za kuzimiliki.

Hivyo, kwa washabiki wanaomiliki silaha hatawaruhusiwa kabisa kuingia viwanjani, na badala yake tunawashauri kuzihifadhi huko wanakotoka kabla ya kufika viwanjani.

Pia tunatoa mwito kwa shabiki ambaye atamuona mwenzake akiwa na silaha uwanja kutoa taarifa kwa mamlaka husika likiwemo Jeshi la Polisi ili aweze kuchukuliwa hatua.

Viwanja 10 kutimka vumbi FDL wikiendi hii

Polisi  Moro, moja ya timu inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza
Na Boniface Wambura
KIVUMBI cha Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kuwania tiketi za kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao (2014/2015) inaendelea wikiendi hii (Jumamosi na Jumapili) kwa kuzikutanisha timu 20 zitakazopambana katika viwanja kumi tofauti.

Jumamosi kutakuwa na mechi kati ya Green Warriors na Friends Rangers (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi), Kimondo na Burkina Faso (Uwanja wa CCM Vwawa, Mbozi), Mlale JKT na Mkamba Rangers (Uwanja wa Majimaji, Songea) na Kurugenzi dhidi ya Polisi Morogoro (Uwanja wa Wambi, Mafinga).

Polisi Dodoma na Stand United (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma), Toto Africans na JKT Kanembwa (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza), Mwadui na Polisi Mara (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga) na Polisi Tabora na Pamba (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora).

Keshokutwa (Jumapili) kutakuwa na mechi kati ya African Lyon na Transit Camp (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi) na Villa Squad dhidi ya Polisi Dar es Salaam (Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam).

Uhuru Seleman awataka 'Wagosi wa Kaya' kuwaiga wenzao wa Mbeya

Uhuru Seleman akiwa na taji la ubingwa la Ligi Kuu alipokuwa Simba
KIUNGO wa Coastal Union, Uhuru Seleman amesema amekunwa na mashabiki wa soka wa mkoa wa Mbeya kwa namna wanavyoisapoti timu yao ya Mbeya City kiasi cha kuzisahau Simba na Yanga na kuwataka mashabiki wa Coastal Union na Tanga kwa ujumla kuiga mfano huo.
Uhuru ambaye ni mwenyeji wa Mbeya, alisema wiki iliyopita Coastal ilipoenda kuumana na Mbeya City alishangazwa na namna wakazi wa mkoa huo walivyoungana pamoja na kuishangilia timu yao mwanzo mwisho kitu alichodai hajawahi kukiona Tanga na kuwataka 'Wagosi wa Kaya' kuzinduka.
Kiungo aliyewahi kuzichezea Mtibwa Sugar, Simba na Azam, alisema kwa namna mashabiki wa mkoa Mbeya wanavyoungana na kuzisahau kabisa Simba na Yanga inawatia moyo na kuwapa nguvu wachezaji wa timu hiyo kujituma uwanjani.
"Huwezi amini ukiwa Mbeya husikii habari za Simba na Yanga wao na Mbeya City na Prisons, kitu ambacho nilikuwa napenda kuwaomba mashabiki wa soka wa mkoa wa Tanga kuiga jambo hilo na kuwa na uzalendo kwa timu zao na hasa Coastal Union iliyopo Ligi Kuu," alisema.
Alisema sapoti wanayopewa wachezaji wa Mbeya City inawatia moyo na kupata nguvu ya kuipigania timu yao kuweza kuwa na matokeo mazuri licha ya ugeni wake katika ligi hiyo inayozidi kushika kasi.
"Uzalendo wa namna hiyo wa kuziunga mkono timu za nyumbani husaidia kuwatia nguvu wachezaji badala ya utamaduni wa mashabiki kugawanyika kwa unazi wa Simba na Yanga na kuzisahau timu zao ambazo zinawapelekea mechi kubwa na kuziona timu wanazoziota," alisema Uhuru.
Kiungo huyo na wachezaji wenzake watakuwa uwanja wa Mkwakwani Tanga kesho kwa ajili ya kuwakabili Azam katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, timu hizo zote zinatokea Mbeya walipoumana na wenyeji wao Mbeya City na Prisons na kuambulia sare ya bao 1-1 kila moja.

Julio aitisha Ruvu Shooting, wawili kulikosa pambano kesho Taifa

Julio akitetea na Mombeki na Henry Jospeh akiwa kando yake
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, wanatarajiwa kushuka kesho dimbani kuvaana na Ruvu Shooting bila ya wachezaji wake, Miraj Adam na Abdallah Seseme ambao ni majeruhi huku wakiwa hana hakika ya kumtumia Issa Rashid 'Baba Ubaya' ambaye hali yake bado haijatengemaa vyema.
Hata hivyo kitu cha kufurahisha ni kwamba nahodha wake msaidizi, Nassoro Masoud 'Chollo' na mkongwe Henry Joseph wenyewe wapo fiti tayari kuwakabili maafande hao wanaonolewa na kocha Charles Boniface Mkwasa.
Akizungumza na MICHARAZO  kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' alisema Simba ipo kamili kuivaa Ruvu licvha ya kuwakosa Abdallah Seseme na Miraji Adam ambao wote wamefungwa plasta gumu (POP) miguuni.
Julio alisema ukiondoa wachezaji hao wengine wanaendelea vyema japo hali ya Baba Ubaya aliyeanza mazoezi na wenzake bado haijatengemaa vizuri na hivyo kutokuwa na hakika ya kumtumia katika mechi hiyo itakayochezwa kwenye uwanja wa Taifa na kudai itakuwa ngumu na yenye ushindani mkubwa.
"Kikosi kipo tayari kwa vita dhidi ya Ruvu Shooting, japo tunasikitika kusema kuwa hatutakuwa na Seseme na Miraj ambao wote wamefungwa POP huku Baba Ubaya akitupa mashaka, japo Henry Joseph na Chollo wamerejea dimbani kuungana na wenzao ambao wana ari ya ushindi," alisema.
Kuhusu mfungaji wao bora, Amisi Tambwe ambaye majuzi alishindwa kuendelea na mazoezi na wenzake kutokana na kusumbuliwa na tumbo, Julio alisema anaendelea vyema na Jumamosi ataendelea kuongoza 'mauaji' kwa Ruvu.
"Aaah alichafukwa na tumbo tu na wala halikuwa tatizo kubwa na panapo majaliwa ataendelea kuongoza mauaji dhidi ya wapinzani wetu katika Ligi Kuu," alisema Julio beki wa zamani wa Plisner, Simba na Taifa Stars.
Mbali na mechi ya Simba na Ruvu, kesho kutakuwa na mechi nyingine nne zitakazozikutanisha timu za JKT Ruvu dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa Chamanzi, Coastal Union kuialika Azam jijini Tanga na Oljoro JKT kuikaribisha Mbeya City kabla ya Jumapili Yanga kupepetana na Mtibwa Sugar na Mgambo JKT kuumana na Prisons kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga

Gari laacha njia na kuua wawili Mbeya, wengine wanaswa na bangi gramu 900

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbSKddVeeyHTyKf5ybVJhtXhjjGjgBrBwlffjXY7411udEf3xhx7lKaamyX8nf6GDoTTpcl46_dmR43D3Qz68E3q_lkYa3MX0qj0z7BBK8jJTKBwPpBBG6g038Al0GJJShhP09FkJnDXU/s640/Kamanda+wa+Polisi+Mbeya+.JPG

WATEMBEA kwa miguu wawili wamepotea maisha yao baada ya kugongwa na gari lililoacha njia mjini Mbeya huku watu wengine wawili wakinaswa na dawa za kulevya aina ya Bangi yenye uzito wa gramu 900.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi la Polisi mjini humo inayosemeka hapo chini ni kwamba watu hao walipatwa na ajali hiyo jana saa 1 usiku. Isome mwenyewe taarifa hiyo.

MNAMO TAREHE 03.10.2013 MAJIRA YA SAA 19:46HRS HUKO KATIKA ENEO LA SIMIKE JKT – ITENDE BARABARA YA MBEYA/TUNDUMA JIJI NA MKOA WA MBEYA.  GARI T.170 AUM AINA YA  TOYOTA CRESTA LIKIENDESHWA NA DEREVA MAHUNDI S/O KAPITI, MIAKA 27, KYUSA, MKAZI WA ITIJI LILIACHA NJIA NA KUWAGONGA WATEMBEA KWA MIGUU WAWILI  KISHA KUPINDUKA NA KUSABABISHA VIFO VYA WATU WAWILI AMBAO NI 1. DEREVA MWENYEWE 2. NEEMA D/O MWINUKA, MIAKA 32, MNDALI, MWALIMU AMBAYE ALIKUWA MTEMBEA KWA MIGUU MKAZI WA NZOVWE PIA KUSABABISHA MAJERUHI KWA WATU WAWILI AMBAO NI 1.TWINZA S/O MWAKIYOMA, MIAKA 36, KYUSA, MKAZI WA MAJENGO AMBAYE AMELAZWA HOSPITALI YA  RUFAA MBEYA NA 2. STIVIN S/O MWAKALINGA, MIAKA 36, KYUSA, MKAZI WA NZOVWE AMBAYE ALIPATIWA MATIBABU NA KURUHUSIWA.  MIILI YA MAREHEMU IMEHIFADHIWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. CHANZO NI MWENDO KASI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA  KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANAENDELEA KUTOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOENDESHA VYOMBO VYA MOTO KWA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUSHA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA. 


WILAYA YA  MOMBA – KUPATIKANA NA BHANGI.

MNAMO TAREHE 03.10.2013 MAJIRA YA  SAA 11:00HRS  HUKO KATIKA MTAA WA MAPOROMOKO TUNDUMA  WILAYA YA  MOMBA  MKOA WA MBEYA.  ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIWAKAMATA 1. IZDORI S/O PELLA, MIAKA 24, MKINGA, MFANYABIASHARA, MKAZI WA MAPOROMOKO NA 2. AMOS S/O ALISON MELLA, MIAKA 28, MNYIHA, MKULIMA, MKAZI WA MTAA WA MIGOMBANI WAKIWA NA BHANGI YENYE UZITO WA GRAM 900. MBINU NI KUFICHA BHANGI HIYO KATIKA KIBANDA CHA BIASHARA CHA IZDORI S/O PELLA. WATUHUMIWA NI WAVUTAJI NA WAUZAJI WA BHANGI. TARATIBU ZINAFANYWA ILI WAFIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA  KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA  WITO KWA  JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA   KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA  MTUMIAJI. AIDHA ANATOA RAI KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MTU/WATU WANAOJIHUSISHA NA BIASHARA HARAMU ZA MADAWA YA KULEVYA AZITOE KWENYE MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE.
Signed by:
                           [DIWANI ATHUMANI - ACP]
  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Kwa Mombeki Soka kwanza blabla baadaye


MSHAMBULIAJI mrefu wa Simba, Betram Mombeki amesema yeye kazi yake kubwa katika klabu hiyo ni kucheza mpira na siyo kuzungumza na vyombo vya habari.
Alisema iwapo kutakuwa na watu wanaotaka kumpamba au kumponda basi wapime uwezo wake uwanjani wakati anaitumikia Simba.
Akizungumza na gazeti hili katika mazoezi ya Simba, Mombeki aliyesajiliwa akitokea Pamba ya Mwanza, alisema huwa hapendi kuzungumza na vyombo vya habari kwa sababu siyo kazi yake.
"Unajua kazi yangu ni kucheza soka, ndiyo kazi yangu pekee ninayoijua yaani kujipanga vyema kuisaidia timu yangu iwe ni kwa kufunga au kutoa pasi ya mwisho, lakini siyo kuzungumza na wanahabari kila mara," alisema.
Mombeki alisema kama kuna mtu anataka kujua sifa na ubaya wake wampime kwa majukumu yake uwanjani badala ya kuzungumza au kutaka kujisifia yeye mwenyewe.
Mkali huyo ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa Simba tangu atue katika klabu hiyo akionyesha makali yake kwenye mechi za kirafiki na hata kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kutoa pasi za mwisho kwa Amisi Tambwe.
Mombeki, alisema kama mchezaji anajua majukumu yake ni kucheza kwa bidii ili mwishowe Simba imalize vyema ligi hiyo.
Mchezaji huyo mpaka sasa ametupia bao moja tu kimiani, huku mchezaji ambaye amekuwa akimpa pasi za mwishjo, Tambwe akiwa na mabao saba akiwa ndiye kinara wa mabao mpaka sasa.