STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 4, 2013

Kwa Mombeki Soka kwanza blabla baadaye


MSHAMBULIAJI mrefu wa Simba, Betram Mombeki amesema yeye kazi yake kubwa katika klabu hiyo ni kucheza mpira na siyo kuzungumza na vyombo vya habari.
Alisema iwapo kutakuwa na watu wanaotaka kumpamba au kumponda basi wapime uwezo wake uwanjani wakati anaitumikia Simba.
Akizungumza na gazeti hili katika mazoezi ya Simba, Mombeki aliyesajiliwa akitokea Pamba ya Mwanza, alisema huwa hapendi kuzungumza na vyombo vya habari kwa sababu siyo kazi yake.
"Unajua kazi yangu ni kucheza soka, ndiyo kazi yangu pekee ninayoijua yaani kujipanga vyema kuisaidia timu yangu iwe ni kwa kufunga au kutoa pasi ya mwisho, lakini siyo kuzungumza na wanahabari kila mara," alisema.
Mombeki alisema kama kuna mtu anataka kujua sifa na ubaya wake wampime kwa majukumu yake uwanjani badala ya kuzungumza au kutaka kujisifia yeye mwenyewe.
Mkali huyo ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa Simba tangu atue katika klabu hiyo akionyesha makali yake kwenye mechi za kirafiki na hata kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kutoa pasi za mwisho kwa Amisi Tambwe.
Mombeki, alisema kama mchezaji anajua majukumu yake ni kucheza kwa bidii ili mwishowe Simba imalize vyema ligi hiyo.
Mchezaji huyo mpaka sasa ametupia bao moja tu kimiani, huku mchezaji ambaye amekuwa akimpa pasi za mwishjo, Tambwe akiwa na mabao saba akiwa ndiye kinara wa mabao mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment