STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 22, 2014

HII NDIYO TOP 10 YA WALIONG'ARA KIDATO CHA NNE

http://1.bp.blogspot.com/-SUcYdsp6pq0/UU7zJboieNI/AAAAAAAAdo4/5fAU57VdG3M/s1600/NECTA.jpg
WASICHANA Wasichana waliofanya vizur kwenye mtihani huo wameongozwa na Robina Nicholaus (Marian Girls), Magrath Kakoko (St Francis), Joyceline Leonard Marealle (Canossa), Safarina W Mariki, Abby T Sembuche na Janeth Urassa (Marian Girls). Wengine ni Angle Ngulumbi (St Francis), Getrude James Mande wa Precious Blood (Arusha), Violet Mwasenga wa St Francis na Catherine Swai kutoka Marian Girls.
WAVULANA
Wavulana waliofanya Vizuri ni Sunday Mrutu wa Anne Marie, Nelson Rugola Anthony na Emanuel Mihuba Gregory wote kutoka Kaizirege, Razack Hassan wa St Matthew’s (Pwani) na Hamis Msangi kutoka Eangles (Pwani).
Wengine ni Joshua Zumba wa Uwata (Mbeya), Brian Laurent na Mohamed Ally wa Marian Boys (Pwani), Shahzill Msuya wa St Amedeus (Kilimanjaro) na Shabani Hamisi Maatu wa Mivumon Islamic Seminary (Dar es Salaam).

Simba, Azam kuvuna nini kesho Dar?

Simba itavuna nini kwa JKT Ruvu?
JKT Ruvu itaendelea kuwa urojo kesho katika ligi kuu mbele ya Simba?
Azam watahimili vishindo vya Prisons baada ya kung'oka Kombe la Shirikisho Afrika?
Prisons wataendeleza ubabe wao walioonyesha kwenye mechi za duru la pili kesho kwa Azam au...?!
BAADA ya kupata ushindi wa mechi tatu mfululizo na sare moja katika duru la pili, Prisons ya Mbeya kesho itavaana na timu ambayo haijapoteza mechi yoyote katika Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam huku Simba wakivaana na maafande wa JKT Ruvu waliochabangwa mabao 6-0 katika mechi yao iliyopita.
Mechi hizo mbili zitachezwa kesho jijini Dar es Salaam zikiwa ndiyo pekee katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania bara kukamilisha mzunguko wa 19.
Azam wanaorejea kwenye ligi baada ya kung'olewa kwenye Kombe la Shirikisho la Ferroviario de Beira wataivaa Prisons kwenye uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya jiji, huku Simba itaikaribisha Ruvu inayonolewa kwa sasa na kocha Fred Minziro kwenye uwanja wa Taifa.
JKT walikuwa wahanga wa Prisons kwa kukubali kipigo cha 6-0 na kuweka rekodi ya kufungwa mabao nande katika mechi mbili zilizopita, kipigo kingine walipewa na ndugu zao Ruvu Shooting ambayo leo imekumbana na dhahama kwa kulazwa mabao 7-0 na watetezi Yanga.
Mechi hizo zinasubiriwa kwa hamu kwa sababu ndizo zinazoweza kubadilisha msimamo wa ligi hiyo kwa timu zilizopo kwenye Nne Bora, kwani Azam ikishinda itarejea kwenye nafasi yake ya kwanza ambayo imechukuliwa na Yanga jioni ya leo baada ya ushindi wake dhidi ya Ruvu.
Simba nayo ikishinda itaiengua Mbeya City na kukalia nafasi ya tatu baada ya vijana hao wa Juma Mwambusi kuchezea kipigo toka kwa Coastal Union jijini Tanga jioni ya leo.
Simba ina pointi 32, tatu nyuma ya Mbeya City, lakini ikiwa na uwiano mzuri ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Azam wenyewe wana pointi 36, mbili zaidi ya Yanga wanaoongoza sasa kwa pointi 38, hali inayofanya mechi za kesho kuwa na msisimko mkubwa mashabiki wakitaka kuona Prisons itaendeleza rekodi yake ya kukusanya pointi 10 katika mechi zake nne za duru la pili na kuvunja mwiko wa Azam kupoteza mchezo!
Wana Lambalamba ndiyo timu pekee ambayo haijapoteza mechi yoyote katika ligi ya msimu huu na katika mechi zake za duru la pili imekuwa ikigawa dozi nene hali inayoifanya Prisons kuwavaa wapinzani wao hao kwa tahadhari kubwa.
Tayari timu zote nne zimekuwa zikitambiana kila moja ikidai imejiandaa kushinda, lakini matokeo ya mwisho yatategemea baada ya dakika 90 kwa namna timu hizo zilivyopigana katika kuwakabili wapinzani wao.
Simba ambayo imekuwa na mwenendo mbovu tangu duru la pili lianze itataka ushindi ili kutuliza munkari wa mashabiki na wanachama wao baada ya kujikuta wakipoteza pointi saba kati ya tisa katika mechi zao tatu zilizopita ikiambulia sare mbili dhidi ya Mtibwa Sugar na Mbeya City na kulazwa na Mgambo JKT.
Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014     
                                      P    W     D     L     F    A   GD  PTS
01.Yanga                        17   11    05   01   41   12   29  38
02.Azam                         16  10    06   00   29   10   19   36
03.Mbeya City                19   09    08   02   24   16   08  35
04.Simba                        18   08    08   02   33   16   17  32
05.Kagera Sugar             19   06    08   05   16  15   01  26
06.Coastal Union            19   05    10    04  14  09   05  25
07.Mtibwa Sugar            19   06    07    06   23  23   00  25
08.Ruvu Shooting            19   06   07   06    20  26  -06  25
09.Mgambo                    19   05    05    09   12  27  -15  20
10.Prisons                       17   04    07    05   15  16  -01  19
11. JKT Ruvu                  18   06    01    11   13  27  -14  19
12.Oljoro                        20   02    09    09   15  30  -15  15
13.Ashanti                       18   03    05    10   15  30  -15  14
14.Rhino Rangers            19   02    07    10   12  23 -11  13

Real Madrid yapanda kileleni Hispania


Real Madrid's Gareth Bale
MABAO matatu yaliyofungwa na Illaramendi katika dakika ya 34, Gareth Bale la dakika ya 72 na lile la Isco la dakika ya 81 yalitosha kuipaisha Real Madrid hadi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) walipoifumua Elche mabao 3-0.
Madrid wakiwa uwanja wa nyumbani wa Santiago Bernabeu ilionyesha dhamira ya kupata ushindi kwa Illarramendi kufunga bao kwa pasi ya Pepe, bao lililodumu hadi mapumziko.
Bale mchezaji ghali kuliko wote katika usajili, alitupia bao la pili akimalizia kasi ya Xabi Alonso kabla ya Karim Benzema kumtengea Isco kufunga bao la tatu.
Kwa ushindi huo, Madrid imefikisha pointi 63 na kuziengua kileleni Barcelona na Atletico Madrid zenye pointi 60 kila moja ambazo zina mchezo mmoja mkononi, Barca wakitarajia kushuka dimbani muda mchache baadae ugenini dhidi ya Real Sociedad, huku wenzao wakitarajiwa kucheza kesho.




Arsenal, Man City, West Ham 'zaua' England


Olivier Giroud
Wachezaji wa Arsenal wakishangilia moja ya mabao yao leo
Carlton Cole
Wachezaji wa West Ham United wakishangilia mabao yao

Yaya Toure scores for Man City against Stoke
Yaya Toure akifunga bao lililoipa ushindi Manchester City
ARSENAL imeendelea kuifukuzia Chelsea kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England baada ya muda mfupi uliopita kuichabanga Sunderland mabao 4-1, huku Manchester City nayo ikiibuka na ushindi.
Vijana wa Gunners wakiwa uwanja wa nyumbani wa Emirates ilipatra ushindi huo ikitoka kulala mabao 2-0 dhidi ya Bayern Munich katika Ligi ya mabingwa wa Ulaya.
Mabao ya Oliver Giroud aliyefunga mawili katika dakika ya tano na 31 kabla ya Tomas Rosicky kufunga la tatu dakika ya 42 na kwenda mapumziko wakiongoza kwa mabao 3-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa Arsenal kuongeza bao la nne likifungwa Laurent Koscielny katika dakika ya 57 na bao pekee la Sunderland likifungwa na Giaccherini'  katika dakika ya 81.
Ushindi huo umeifanya Arsenal kubaki nafasi ya pili nyuma ya Chelsea kwa tofauti ya pointi moja, Arsenal ikiwa na 59 na Chelsea 60 huku wakifuatiwa na Manchester City ilipata ushindi wa 1-0 nyumbani dhidi ya Stoke City.
Bao hilo pekee katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa Etihad lilifungwa na Yaya Toure katika dakika yua 70.
Katika mechi nyingine Hull City imepata ushindi mnono ugenini kwa kuilaza Cardiff City mabao 4-0, huku West Bromwich ikilazimishwa sare ya 1-1 na Fulham waliotangulia kupata bao mapema.
Nayo West Ham United ikiwa nyumbani iliishindilia Southampton kwa mabao 3-1.
Mechi inayotarajiwa kuchezwa muda mfupi ujao ni kati ya mabingwa watetezi, Manchester United iliyopo ugenini dhidi ya Crystal Palace.

KILELE CHA MIAKA 10 YA ‘LADY IN RED’ KUFANYIKA NYUMBANI LOUNGE

* Kutolewa vyeti maalum
* Wadau kukata keki ya pamoja
* Slim kutumbuiza
https://thumbp4-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AMJ2imIAABG1UwdzPAAAAA91Vj0&midoffset=2_0_0_1_1606779&partid=2&f=1214&fid=Inbox&w=3000&h=3000
 
Na Andrew Chale
KILELE cha Miaka 10  na ‘After Party’ ya onesho la mavazi la ‘Lady in Red Super Brand’  kinatarajia kufikia tamati usiku wa Jumamosi, Februari 22, ndani ya Ukumbi ulio na mgahawa wa kisasa na hadhi ya juu wa kwa jiji la Dar es Salaam, wa Nyumbani Lounge, huku kukitarajiwa kuwa na surprise mbali mbali kwa wadau watakaojitokeza.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Fabak Fashions,  Asia Idarous Khamsin, wandaaji wa Lady in red, kila mwaka hapa nchini, alisema, ‘after party’  hiyo ni maalum kwa ajili ya kutoa  shukrani na  vyeti maalum kwa wadau wanaoliunga  mkono jukwaa la Lady in red kwa kipindi chote hadi kufikia hapo ambapo pia watapata wasaha wa kukata keki  ya ukumbusho.
“After party ya miaka 10 ya Lady in red, kwa mwaka huu itakuwa ya aina yake sambamba na surprise, hivyo nyote munakaribishwa na hakuna kiingilio na kwa watakaokuwa tayari kujiunga siku maalum pale  Nyumbani Lounge, wafike  katika duka la Fabak Fashion, lililopo  jirani na kituo cha Msasani, Kwa Mwalimu Nyerere au kwa kupiga simu namba 0713263363  ama 0784263363” alisema Asia Idarous.
Na kuongeza kuwa, pia tiketi maalum za bure zitatolewa mlangoni Nyumbani Lounge, kwa wadau watakaofika. Aidha, alisema msanii wa muziki wa kizazi kipya, Slim Guapo Sosa anayetamba na kibao cha ‘ LOVE YOU ’ na vingine vingi anatarajiwa kuwakonga nyoyo watakaojitokeza kwenye ‘after party’ hiyo.
 Party hiyo imedhaminiwa na  wadhamini mbali mbali wakiwemo Times fm, Michuzi media group, mo blog, Nyumbani Lounge, Darling air, G one Media na wengine wengi.
Mwisho

Mtibwa Sugar yaona mwezi yainyuka Ashanti, Mgambo haikamatiki

Ashanti United waliyolazwa na Mtibwa Sugar
Mtibwa Sugar iliyoona mwezi
Oljoro JKT waliogeuzwa asusa na Mgambo mjini Arusha
Mgambo inayoendelea kugawa dozi kwa wapinzani wao katika Ligi Kuu
MABINGWA wa zamani wa kandanda nchini, Mtibwa Sugar leo imeona mwezi baada ya kupata ushindi wake wa kwanza katika mechi za duru la pili kwa kuinyoa Ashanti Utd wa mabao 2-1.
Mabao ya Mohammed Mkopi na Abdallah Juma ya kila kipindi yalitosha kuipa Mtibwa iliyokuwa uwanja wa nyumbani wa Manungu Complex pointi tatu muhimu vijana hao wa Mecky Mexime katika ligi hiyo inayozidi kuchanja mbuga.
Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Mussa hassan Mgosi, alilimwa kadi nyekundu katika mchezo huo kabla ya timu yake kupata bao la ushindi lililofungwa na Abdallah Juma.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Rhino Rangers ikisafiri ugenini kuumana na wenyeji wa Kagera Sugar walishindiliwa bao 1-0 lililoifungwa na Suleiman Kibuta katika dakika ya nne na kuzidi kujiweka pabaya kwenye janga la kushuka daraja.
Nao Mgambo JKT ambao kwenye duru la pili wameonekana kuamka waliendeleza ubabe wao kwa kuichapa Oljoro JKT nyumbani kwao kwa mabao 2-1, mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha.

Chelsea yazidi kujikita kileleni yailaza Everton

Quick off the mark: John Terry reacts first as Slyvain Distin, Leighton Baines and Phil Jagielka can only watch
BAO la dakika ya lala salama lililofungwa na nahodha, John Terry limeiwezesha Chelsea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England, EPL, baada ya kupata ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Everton.
Terry alifunga bao hilo katika dakika ya tatu ya nyongeza ya mchezo huo uliochezwa 'darajani' ambao ulionekana kama ungeisha kwa sare na kuweka reheni nafasi ya timu hiyo kuendelea kuongoza msimamo.
Ushindi huo umeifanya Chelsea kufikisha jumla ya pointi  60 baada ya mechi 27, na kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ambapo michezo mingine inaendelea jioni hii huku Arsenal ikiwa nyumbani inaongoza 3-0 mpaka sasa.

Yanga yaua Taifa, Mbeya City yafa Mkwakwani

Emmanuel Okwi akimtoka kipa wa Ruvu Abdallah Ramadhani na kuifungia Yanga bao la tatu (Picha: Francic Dande)


Coastal walioifanyizia Mbeya City Mkwakwani Tanga

Mbeya City waliopoteza mechi yao ya pili katika ligi msimu huu baada ya kuwa wagumua duru la kwanza
MABINGWA watetezi Yanga wametuma salamu na kujibu mapigo ya wapinzani wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri baada ya jioni hii kuinyuka Ruvu Shooting kwa mabao 7-0 jijini Dar es Salaam.
Yanga na Al Ahly zitavaana Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa katika mechi ya mkondo wa kwanza ya raundi ya kwanza huku Wamisri hao wakitoka kutwaa taji la Super Cup kwa kuilaza CS Sfexien ya Tunisia.
Al Ahly ilitoa kipigo cha mabao 3-2 kwa Watunisia wakishuhudiwa na kocha msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa aliyetumwa kwenda kuifanyia ushushushu ambaye alitua Taifa Yanga ikiua Ruvu.
Yanga iliyopiga kambi yake Bagamoyo iliisambaratisha Ruvu iliyo chini ya Mkenya, Tom Olaba kwa mabao ya haraka haraka ya kipindi cha kwanza kupitia kwa Didier Kavumbangu na Simon Msuva.
Wachezaji hao waliofunga mabao mawili kila mmoja katika mechi hiyo walifunga mabao hayo ndani ya dakika mbili tu za kuanza kwa mchezo huo kabla ya Mrisho Ngassa na Emmanuel Okwi kuongeza mengine mawili na kufanya waende mapumziko wakiongoza 4-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Yanga kuongeza bao la tano kupitia tena kwa Didier kabla ya Hamis Kiiza 'Diego' kuongeza jingine la sita dakika ya 69 na Msuva akamalizia kazi.
Kwa ushindi huo Yanga imerejea kileleni ikiing'oa Azam ambayo itashuka dimbani kesho dhidi ya Prisons kwa kufikisha pointi 38 na mabao 41 ya kufunga, huku Didier na Kiiza wakifikisha mabao 9.
Pia ushindi huo umeifanya Yanga kuweka rekodi ya kipigo kikubwa kutolewa msimu huu ikipiku vile vya Simba na Mgambo JKT na Prisons dhidi ya JKT Ruvu zilizoisha kwa mabao 6-0 kila moja.
Katika mechi nyingine iliyochezwa mjini Tanga, Mbeya City imekuwa urojo kwa Coastal Union kwa kulazwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Mabao ya washindi yamefungwa na Mohammed Miraji dakika nane za mwisho kabla ya kumalizika kwa pambano hilo na kuifanya Coastal kuwa timu ya pili kuidungua Mbeya City baada ya Yanga na kufikisha pointi 25.