STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 22, 2014

KILELE CHA MIAKA 10 YA ‘LADY IN RED’ KUFANYIKA NYUMBANI LOUNGE

* Kutolewa vyeti maalum
* Wadau kukata keki ya pamoja
* Slim kutumbuiza
https://thumbp4-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AMJ2imIAABG1UwdzPAAAAA91Vj0&midoffset=2_0_0_1_1606779&partid=2&f=1214&fid=Inbox&w=3000&h=3000
 
Na Andrew Chale
KILELE cha Miaka 10  na ‘After Party’ ya onesho la mavazi la ‘Lady in Red Super Brand’  kinatarajia kufikia tamati usiku wa Jumamosi, Februari 22, ndani ya Ukumbi ulio na mgahawa wa kisasa na hadhi ya juu wa kwa jiji la Dar es Salaam, wa Nyumbani Lounge, huku kukitarajiwa kuwa na surprise mbali mbali kwa wadau watakaojitokeza.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Fabak Fashions,  Asia Idarous Khamsin, wandaaji wa Lady in red, kila mwaka hapa nchini, alisema, ‘after party’  hiyo ni maalum kwa ajili ya kutoa  shukrani na  vyeti maalum kwa wadau wanaoliunga  mkono jukwaa la Lady in red kwa kipindi chote hadi kufikia hapo ambapo pia watapata wasaha wa kukata keki  ya ukumbusho.
“After party ya miaka 10 ya Lady in red, kwa mwaka huu itakuwa ya aina yake sambamba na surprise, hivyo nyote munakaribishwa na hakuna kiingilio na kwa watakaokuwa tayari kujiunga siku maalum pale  Nyumbani Lounge, wafike  katika duka la Fabak Fashion, lililopo  jirani na kituo cha Msasani, Kwa Mwalimu Nyerere au kwa kupiga simu namba 0713263363  ama 0784263363” alisema Asia Idarous.
Na kuongeza kuwa, pia tiketi maalum za bure zitatolewa mlangoni Nyumbani Lounge, kwa wadau watakaofika. Aidha, alisema msanii wa muziki wa kizazi kipya, Slim Guapo Sosa anayetamba na kibao cha ‘ LOVE YOU ’ na vingine vingi anatarajiwa kuwakonga nyoyo watakaojitokeza kwenye ‘after party’ hiyo.
 Party hiyo imedhaminiwa na  wadhamini mbali mbali wakiwemo Times fm, Michuzi media group, mo blog, Nyumbani Lounge, Darling air, G one Media na wengine wengi.
Mwisho

No comments:

Post a Comment