STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 22, 2014

Simba, Azam kuvuna nini kesho Dar?

Simba itavuna nini kwa JKT Ruvu?
JKT Ruvu itaendelea kuwa urojo kesho katika ligi kuu mbele ya Simba?
Azam watahimili vishindo vya Prisons baada ya kung'oka Kombe la Shirikisho Afrika?
Prisons wataendeleza ubabe wao walioonyesha kwenye mechi za duru la pili kesho kwa Azam au...?!
BAADA ya kupata ushindi wa mechi tatu mfululizo na sare moja katika duru la pili, Prisons ya Mbeya kesho itavaana na timu ambayo haijapoteza mechi yoyote katika Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam huku Simba wakivaana na maafande wa JKT Ruvu waliochabangwa mabao 6-0 katika mechi yao iliyopita.
Mechi hizo mbili zitachezwa kesho jijini Dar es Salaam zikiwa ndiyo pekee katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania bara kukamilisha mzunguko wa 19.
Azam wanaorejea kwenye ligi baada ya kung'olewa kwenye Kombe la Shirikisho la Ferroviario de Beira wataivaa Prisons kwenye uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya jiji, huku Simba itaikaribisha Ruvu inayonolewa kwa sasa na kocha Fred Minziro kwenye uwanja wa Taifa.
JKT walikuwa wahanga wa Prisons kwa kukubali kipigo cha 6-0 na kuweka rekodi ya kufungwa mabao nande katika mechi mbili zilizopita, kipigo kingine walipewa na ndugu zao Ruvu Shooting ambayo leo imekumbana na dhahama kwa kulazwa mabao 7-0 na watetezi Yanga.
Mechi hizo zinasubiriwa kwa hamu kwa sababu ndizo zinazoweza kubadilisha msimamo wa ligi hiyo kwa timu zilizopo kwenye Nne Bora, kwani Azam ikishinda itarejea kwenye nafasi yake ya kwanza ambayo imechukuliwa na Yanga jioni ya leo baada ya ushindi wake dhidi ya Ruvu.
Simba nayo ikishinda itaiengua Mbeya City na kukalia nafasi ya tatu baada ya vijana hao wa Juma Mwambusi kuchezea kipigo toka kwa Coastal Union jijini Tanga jioni ya leo.
Simba ina pointi 32, tatu nyuma ya Mbeya City, lakini ikiwa na uwiano mzuri ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Azam wenyewe wana pointi 36, mbili zaidi ya Yanga wanaoongoza sasa kwa pointi 38, hali inayofanya mechi za kesho kuwa na msisimko mkubwa mashabiki wakitaka kuona Prisons itaendeleza rekodi yake ya kukusanya pointi 10 katika mechi zake nne za duru la pili na kuvunja mwiko wa Azam kupoteza mchezo!
Wana Lambalamba ndiyo timu pekee ambayo haijapoteza mechi yoyote katika ligi ya msimu huu na katika mechi zake za duru la pili imekuwa ikigawa dozi nene hali inayoifanya Prisons kuwavaa wapinzani wao hao kwa tahadhari kubwa.
Tayari timu zote nne zimekuwa zikitambiana kila moja ikidai imejiandaa kushinda, lakini matokeo ya mwisho yatategemea baada ya dakika 90 kwa namna timu hizo zilivyopigana katika kuwakabili wapinzani wao.
Simba ambayo imekuwa na mwenendo mbovu tangu duru la pili lianze itataka ushindi ili kutuliza munkari wa mashabiki na wanachama wao baada ya kujikuta wakipoteza pointi saba kati ya tisa katika mechi zao tatu zilizopita ikiambulia sare mbili dhidi ya Mtibwa Sugar na Mbeya City na kulazwa na Mgambo JKT.
Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014     
                                      P    W     D     L     F    A   GD  PTS
01.Yanga                        17   11    05   01   41   12   29  38
02.Azam                         16  10    06   00   29   10   19   36
03.Mbeya City                19   09    08   02   24   16   08  35
04.Simba                        18   08    08   02   33   16   17  32
05.Kagera Sugar             19   06    08   05   16  15   01  26
06.Coastal Union            19   05    10    04  14  09   05  25
07.Mtibwa Sugar            19   06    07    06   23  23   00  25
08.Ruvu Shooting            19   06   07   06    20  26  -06  25
09.Mgambo                    19   05    05    09   12  27  -15  20
10.Prisons                       17   04    07    05   15  16  -01  19
11. JKT Ruvu                  18   06    01    11   13  27  -14  19
12.Oljoro                        20   02    09    09   15  30  -15  15
13.Ashanti                       18   03    05    10   15  30  -15  14
14.Rhino Rangers            19   02    07    10   12  23 -11  13

No comments:

Post a Comment