STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 22, 2014

Yanga yaua Taifa, Mbeya City yafa Mkwakwani

Emmanuel Okwi akimtoka kipa wa Ruvu Abdallah Ramadhani na kuifungia Yanga bao la tatu (Picha: Francic Dande)


Coastal walioifanyizia Mbeya City Mkwakwani Tanga

Mbeya City waliopoteza mechi yao ya pili katika ligi msimu huu baada ya kuwa wagumua duru la kwanza
MABINGWA watetezi Yanga wametuma salamu na kujibu mapigo ya wapinzani wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri baada ya jioni hii kuinyuka Ruvu Shooting kwa mabao 7-0 jijini Dar es Salaam.
Yanga na Al Ahly zitavaana Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa katika mechi ya mkondo wa kwanza ya raundi ya kwanza huku Wamisri hao wakitoka kutwaa taji la Super Cup kwa kuilaza CS Sfexien ya Tunisia.
Al Ahly ilitoa kipigo cha mabao 3-2 kwa Watunisia wakishuhudiwa na kocha msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa aliyetumwa kwenda kuifanyia ushushushu ambaye alitua Taifa Yanga ikiua Ruvu.
Yanga iliyopiga kambi yake Bagamoyo iliisambaratisha Ruvu iliyo chini ya Mkenya, Tom Olaba kwa mabao ya haraka haraka ya kipindi cha kwanza kupitia kwa Didier Kavumbangu na Simon Msuva.
Wachezaji hao waliofunga mabao mawili kila mmoja katika mechi hiyo walifunga mabao hayo ndani ya dakika mbili tu za kuanza kwa mchezo huo kabla ya Mrisho Ngassa na Emmanuel Okwi kuongeza mengine mawili na kufanya waende mapumziko wakiongoza 4-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Yanga kuongeza bao la tano kupitia tena kwa Didier kabla ya Hamis Kiiza 'Diego' kuongeza jingine la sita dakika ya 69 na Msuva akamalizia kazi.
Kwa ushindi huo Yanga imerejea kileleni ikiing'oa Azam ambayo itashuka dimbani kesho dhidi ya Prisons kwa kufikisha pointi 38 na mabao 41 ya kufunga, huku Didier na Kiiza wakifikisha mabao 9.
Pia ushindi huo umeifanya Yanga kuweka rekodi ya kipigo kikubwa kutolewa msimu huu ikipiku vile vya Simba na Mgambo JKT na Prisons dhidi ya JKT Ruvu zilizoisha kwa mabao 6-0 kila moja.
Katika mechi nyingine iliyochezwa mjini Tanga, Mbeya City imekuwa urojo kwa Coastal Union kwa kulazwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Mabao ya washindi yamefungwa na Mohammed Miraji dakika nane za mwisho kabla ya kumalizika kwa pambano hilo na kuifanya Coastal kuwa timu ya pili kuidungua Mbeya City baada ya Yanga na kufikisha pointi 25.

No comments:

Post a Comment