STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 22, 2014

Arsenal, Man City, West Ham 'zaua' England


Olivier Giroud
Wachezaji wa Arsenal wakishangilia moja ya mabao yao leo
Carlton Cole
Wachezaji wa West Ham United wakishangilia mabao yao

Yaya Toure scores for Man City against Stoke
Yaya Toure akifunga bao lililoipa ushindi Manchester City
ARSENAL imeendelea kuifukuzia Chelsea kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England baada ya muda mfupi uliopita kuichabanga Sunderland mabao 4-1, huku Manchester City nayo ikiibuka na ushindi.
Vijana wa Gunners wakiwa uwanja wa nyumbani wa Emirates ilipatra ushindi huo ikitoka kulala mabao 2-0 dhidi ya Bayern Munich katika Ligi ya mabingwa wa Ulaya.
Mabao ya Oliver Giroud aliyefunga mawili katika dakika ya tano na 31 kabla ya Tomas Rosicky kufunga la tatu dakika ya 42 na kwenda mapumziko wakiongoza kwa mabao 3-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa Arsenal kuongeza bao la nne likifungwa Laurent Koscielny katika dakika ya 57 na bao pekee la Sunderland likifungwa na Giaccherini'  katika dakika ya 81.
Ushindi huo umeifanya Arsenal kubaki nafasi ya pili nyuma ya Chelsea kwa tofauti ya pointi moja, Arsenal ikiwa na 59 na Chelsea 60 huku wakifuatiwa na Manchester City ilipata ushindi wa 1-0 nyumbani dhidi ya Stoke City.
Bao hilo pekee katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa Etihad lilifungwa na Yaya Toure katika dakika yua 70.
Katika mechi nyingine Hull City imepata ushindi mnono ugenini kwa kuilaza Cardiff City mabao 4-0, huku West Bromwich ikilazimishwa sare ya 1-1 na Fulham waliotangulia kupata bao mapema.
Nayo West Ham United ikiwa nyumbani iliishindilia Southampton kwa mabao 3-1.
Mechi inayotarajiwa kuchezwa muda mfupi ujao ni kati ya mabingwa watetezi, Manchester United iliyopo ugenini dhidi ya Crystal Palace.

No comments:

Post a Comment