STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 17, 2012

AVB azuga, eti hakuwa na presha yoyote Spurs

Tottenham manager Andre Villas-Boas has insisted he did not feel under any pressure before recording his first Spurs win at Reading.
The Portuguese was the subject of speculation about his future, having not won any of his first three games.
But Villas-Boas dismissed such talk after his team's impressive 3-1 Premier League success at the Madejski Stadium.
"I talk to the chairman Daniel Levy every day. I didn't feel under any pressure at all," he said.
He also refused to react to comments by his predecessor Harry Redknapp,  appearing to criticise modern managers in the mould of Villas-Boas who present players with "70-page dossiers".
Play media
Cannot play media. You do not have the correct version of the flash player. Download the correct version
Reading 'will learn from mistakes'
Villas-Boas said: "It is not about the manager, it is about the players. It is the players that take us to success. Different managers have different leadership styles and the way they go about their business.
"I don't know if Harry was mentioning that about Jose Mourinho but it seems strange. I don't use those situations but in the end the most important thing is for your team and your players to reach a level that is needed for success.
"It doesn't matter if a manager is modern, old-fashioned or old school. The most important thing is you have to feel what is right, feel your convictions. Then you can sell your ideas better and take your players to success."
Villas-Boas admitted there had been anxiety in the Spurs dressing room after a defeat and two draws in their opening three games, but he insisted: "I am extremely happy because the players showed tremendous responsibility, commitment and concentration.
"They have been working so hard and deserve to get this first win. We managed to mix the result and the performance and come out of Reading very satisfied."

Kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya kuanza rasmi kesho

KINYANG'ANYIRO cha Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya kinatarajiwa kuanza rasmi hatua ya makundi kesho kwa mechi kadhaa ambapo Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England wataanzia ugenini mjini Madrid, Hispania kuumana na mabingwa wa nchini, Real Madrid katika mechi ya kundi D.
Tayari timu hizo zimeanza kutoleana tambo kuhusiana na mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa kandandfa duniani kote kutaka kuona kikosi cha Manchester City itavuna nini mbele ya vijana wa Jose Mourinho ambayo timu yao imeanza na 'mwaka wa tabu' katika ligi ya nchini mwao.
Mechi nyingine zinazotarajiwa kuchezwa kesho itazikutanisha timu za Ac Milan inayoyumba ligi ya Seria A kwa kupokea vipigo mfululizo kama Real Madrid kwa kuumana na Anderlecht, mjini MIlan.
Vijana wa Arsene Wenger ambao imetoka kupata ushindi wa kishidno katika ligi ya nchini mwao kwa kuialaza Southampton kwa mabao 6-0, yenyewe nayo itakuwa ugenini kuumana na Montpellier ya Ufaransa.
Mechi nyingine kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo hatua ya makundi ni kama ifuatavyo:

Tuesday, 18 September 2012
AC Milan v Anderlecht, GpC, 19:45
Borussia Dortmund v Ajax, GpD, 19:45
Dinamo Zagreb v FC Porto, GpA, 19:45
Malaga v Zenit St Petersburg, GpC, 19:45
Montpellier v Arsenal, GpB, 19:45
Olympiakos v Schalke 04, GpB, 19:45
Paris SG v Dynamo Kiev, GpA, 19:45
Real Madrid v Man City, GpD, 19:45

Wednesday, 19 September 2012
Barcelona v Spartak Moscow, GpG, 19:45
Bayern Munich v Valencia, GpF, 19:45
Braga v CFR 1907 Cluj-Napoca, GpH, 19:45
Celtic v Benfica, GpG, 19:45
Chelsea v Juventus, GpE, 19:45
Lille v BATE Borisov, GpF, 19:45
Man Utd v Galatasaray, GpH, 19:45
Shakhtar Donetsk v FC Nordsjaelland, GpE, 19:45

Tuesday, 2 October 2012
Spartak Moscow v Celtic, GpG, 17:00
BATE Borisov v Bayern Munich, GpF, 19:45
Benfica v Barcelona, GpG, 19:45
CFR 1907 Cluj-Napoca v Man Utd, GpH, 19:45
FC Nordsjaelland v Chelsea, GpE, 19:45
Galatasaray v Braga, GpH, 19:45
Juventus v Shakhtar Donetsk, GpE, 19:45
Valencia v Lille, GpF, 19:45

Wednesday, 3 October 2012
Zenit St Petersburg v AC Milan, GpC, 17:00
Ajax v Real Madrid, GpD, 19:45
Anderlecht v Malaga, GpC, 19:45
Arsenal v Olympiakos, GpB, 19:45
Dynamo Kiev v Dinamo Zagreb, GpA, 19:45
FC Porto v Paris SG, GpA, 19:45
Man City v Borussia Dortmund, GpD, 19:45
Schalke 04 v Montpellier, GpB, 19:45

Tuesday, 23 October 2012
Spartak Moscow v Benfica, GpG, 17:00
BATE Borisov v Valencia, GpF, 19:45
Barcelona v Celtic, GpG, 19:45
FC Nordsjaelland v Juventus, GpE, 19:45
Galatasaray v CFR 1907 Cluj-Napoca, GpH, 19:45
Lille v Bayern Munich, GpF, 19:45
Man Utd v Braga, GpH, 19:45
Shakhtar Donetsk v Chelsea, GpE, 19:45

Wednesday, 24 October 2012
Zenit St Petersburg v Anderlecht, GpC, 17:00
Ajax v Man City, GpD, 19:45
Arsenal v Schalke 04, GpB, 19:45
Borussia Dortmund v Real Madrid, GpD, 19:45
Dinamo Zagreb v Paris SG, GpA, 19:45
FC Porto v Dynamo Kiev, GpA, 19:45
Malaga v AC Milan, GpC, 19:45
Montpellier v Olympiakos, GpB, 19:45

Tuesday, 6 November 2012
AC Milan v Malaga, GpC, 19:45
Anderlecht v Zenit St Petersburg, GpC, 19:45
Dynamo Kiev v FC Porto, GpA, 19:45
Man City v Ajax, GpD, 19:45
Olympiakos v Montpellier, GpB, 19:45
Paris SG v Dinamo Zagreb, GpA, 19:45
Real Madrid v Borussia Dortmund, GpD, 19:45
Schalke 04 v Arsenal, GpB, 19:45

Wednesday, 7 November 2012
Bayern Munich v Lille, GpF, 19:45
Benfica v Spartak Moscow, GpG, 19:45
Braga v Man Utd, GpH, 19:45
CFR 1907 Cluj-Napoca v Galatasaray, GpH, 19:45
Celtic v Barcelona, GpG, 19:45
Chelsea v Shakhtar Donetsk, GpE, 19:45
Juventus v FC Nordsjaelland, GpE, 19:45
Valencia v BATE Borisov, GpF, 19:45

Tuesday, 20 November 2012
Spartak Moscow v Barcelona, GpG, 17:00
BATE Borisov v Lille, GpF, 19:45
Benfica v Celtic, GpG, 19:45
CFR 1907 Cluj-Napoca v Braga, GpH, 19:45
FC Nordsjaelland v Shakhtar Donetsk, GpE, 19:45
Galatasaray v Man Utd, GpH, 19:45
Juventus v Chelsea, GpE, 19:45
Valencia v Bayern Munich, GpF, 19:45

Wednesday, 21 November 2012
Zenit St Petersburg v Malaga, GpC, 17:00
Ajax v Borussia Dortmund, GpD, 19:45
Anderlecht v AC Milan, GpC, 19:45
Arsenal v Montpellier, GpB, 19:45
Dynamo Kiev v Paris SG, GpA, 19:45
FC Porto v Dinamo Zagreb, GpA, 19:45
Man City v Real Madrid, GpD, 19:45
Schalke 04 v Olympiakos, GpB, 19:45

Tuesday, 4 December 2012
AC Milan v Zenit St Petersburg, GpC, 19:45
Borussia Dortmund v Man City, GpD, 19:45
Dinamo Zagreb v Dynamo Kiev, GpA, 19:45
Malaga v Anderlecht, GpC, 19:45
Montpellier v Schalke 04, GpB, 19:45
Olympiakos v Arsenal, GpB, 19:45
Paris SG v FC Porto, GpA, 19:45
Real Madrid v Ajax, GpD, 19:45

Wednesday, 5 December 2012
Barcelona v Benfica, GpG, 19:45
Bayern Munich v BATE Borisov, GpF, 19:45
Braga v Galatasaray, GpH, 19:45
Celtic v Spartak Moscow, GpG, 19:45
Chelsea v FC Nordsjaelland, GpE, 19:45
Lille v Valencia, GpF, 19:45
Man Utd v CFR 1907 Cluj-Napoca, GpH, 19:45
Shakhtar Donetsk v Juventus, GpE, 19:45


Orodha ya makundi:
Kundi A: Porto, Dynamo Kiev, Paris St Germain, Dinamo Zagreb
Kundi B: Arsenal, Schalke, Olympiakos, Montpellier
Kundi C: AC Milan, Zenit St Petersburg, Anderlecht, Malaga
Kundi D: Real Madrid, Manchester City, Ajax, Borussia Dortmund
Kundi E: Chelsea, Shakhtar Donetsk, Juventus, FC Nordsjaelland
Kundi F: Bayern Munich, Valencia, Lille, BATE Borisov
Kundi G: Barcelona, Benfica, Spartak Moscow, Celtic
Kundi H: Manchester United, Braga, Galatasaray, CFR Cluj

Cheka kucheza mara ya mwisho na Nyilawila, kisa...!

Francis Cheka (kulia) alipokuwa 'akimsulubu' Karama Nyilawila katika pambano lao lililofanyika mapema mwaka huu na mjini Morogoro na Cheka kuibuka mshindi wa pointi dhidi ya mpinzani wake.

BONDIA nyota wa ngumi za kulipwa nchini, Francis Cheka 'SMG' amesema huenda pambano lake dhidi ya Karama Nyilawila 'Captain' ndilo likawa la mwisho kwake kupigana na mabondia wa Tanzania.
Cheka anatarajiwa kuzipigana na Nyilawila katika pambano la kuwania ubingwa wa UBO litakalofanyika Septemba 29 kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mara ya tatu kwa mabondia hao kukutana.
Katika michezo yao ya awali, wawili hao walitoka sare mechi moja na nyingine iliyochezwa mapema mwaka huu, Cheka aliibuka kidedea kwa kumpiga mpinzani wake kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Cheka alisema anaamini pambano hilo alilodai ana hakika ya kuibuka na ushindi mbele ya Nyilawila, huenda likawa la mwisho kwake kuzipiga na mabondia wa Tanzania.
Alisema, awali alishasema asingecheza tena nchini kwa kukosa mpinzani wa kweli kufuatia kuwachakaza karibu mabondia wote wakali akiwemo Rashid Matumla, Mada Maugo, Japhet Kaseba na hata Nyilawila mwenyewe.
"Iwapo nitaendeleza mkong'oto kwa Nyilawila, japo nina hakika kwa hilo kutokana na ubora nilionao na uwezo mkubwa katika ngumi, sitacheza tena na mabondia wa nchini, nitaelekeza nguvu zangu kwa mabondia wa nje ili kujenga zaidi jina," alisema.
Alisema kwa sasa anaendelea vema na maandalizi yake dhidi ya pambano hilo lililoandaliwa na Robert Ekerege na litakalosindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi na kutamba ataendelea kuwapa raha mashabiki wake.
"Naendelea vema kujifua chini ya kocha wangu Abdallah Saleh 'Komando', sitawangusha mashabiki wangu kwa namna nitakavyomchapa Nyilawila," alisema.
Pambano hilo la uzani wa Super Middle raundi 12, litaamuliwa na mwamuzi wa kimataifa wa Malawi Jerome Waluza na litasindikizwa na michezo ya utangulizi ambapo Juma Kihiyo dhidi ya Ibrahim Maokola, Seba Temba wa Morogoro dhidi ya Stam Kesi.
Michezo mingine ni kati ya Sadik Momba dhidi ya Amos Mwamakula, huku Anthon Mathias wa Morogoro atacheza na Shaban Kilumbelumbe na Deo Samwel akipambana na Hassan Kidebe.
          
Mwisho

Mbio za Uchaguzi Mkuu SPUTANZA zaanza rasmi


MBIO za kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu wa Chama cha Umoja wa Wacheza Soka Tanzania, SPUTANZA, zimeanza rasmi kwa fomu za uchaguzi huo kuanza kutolewa jijini Dar.
Uchaguzi huo wa SPUTANZA unatarajiwa kufanyika Oktoba 20 na fomu hizo zimeanza kutolewa leo ambapo wanamichezo wanaotaka kugombea nafasi za juu watapaswa kulipia kiasi cha Sh 100,000 na zile za ujumbe kwa sh 50,000.
Katibu Msaidizi wa chama hicho, Abeid Kasabalala aliiambia MICHARAZO nafasi zitazowaniwa kwenye uchaguzi huo ni Uenyekiti, Umakamu Mwenyekiti, Ukatibu Mkuu na Msaidizi wake, Mhazini na Msaidizi wake ambao gharama za fomu ni Sh 100,000.
Kasabalala aliyewahi kutamba zamani na timu za Plisners na Mecco ya Mbeya, alisema nafasi nyingine katika uchaguzi huo ni Ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF na nafasi saba za Kamati ya Utendaji ambazo gharama zake ni sh. 50,000.
"Zoezi la uchukuaji na urudishaji wa fomu za uchaguzi mkuu wa SPUTANZA linaanza rasmi leo (jana) fomu zinapatikana eneo la Magomeni, " alisema.
Kasabalala alisema mwisho wa zoezi hilo la kuchukua na kurudisha fomu ni siku ya Ijumaa kabla ya zoezi la kuyapitia majina, pingamizi na usaili kufanyika takati kwa uchaguzi huo utakaoiwezesha SPUTANZA kupata viongozi wapya.
Katibu huyo alisema wakati zoezi hilo la uchaguzi wa taifa ukianza rasmi, chaguzi za vyama vya mikoa inaendelea kufanyika na kusema mikoa yote imetakiwa iwe imaliza chaguzi zao kabla ya Oktoba 10.
"SPUTANZA Taifa tumewashawaeleza vyama vyote vya mikoa iwe imeshafanya chaguzi zao kabla ya Oktoba 10 ili kuwawezesha viongozi wao kushiriki uchaguzi wa taifa utakaofanyika siku kumi baadae," alisema.

Mwisho

MKURANGA wapata viongozi wapya wa soka

CHAMA cha Soka Wilaya ya Mkuranga, MDFA, kimefanikiwa kupata viongozi wake wapya baada ya chama hicho kufanya uchaguzi wake mkuu jana Jumapili.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Soka Mkoa wa Pwani, COREFA, iliyosimamia uchaguzi huo wa Mkuranga, Masau Bwire, uchaguzi huo wa MDFA ulifanyika wilayani humo juzi Jumapili, ambapo Sudi Baisi alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa chama hicho.
Bwire, alisema Baisi alipata jumla ya kura 41 kati ya wajumbe 46 kutoka klabu 19 walioshiriki kinyang'anyiro cha uchaguzi huo ambao baadhi ya nafasi zilikosa wagombea wenye sifa za kuziwania.
Mwenyekiti huyo alisem, aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu ni Issa Kivyele aliyezoa kura 42, huku John Malata alichaguliwa kuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa COREFA na Mwakilishi wa Klabu nafasi hiyo ilitetewa vema na Rashid Selungwi.
Bwire, alisema nafasi nyingine katika uchaguzi huo hazikuwa na wagombea na hivyo chama hicho kitalazimika kuitisha uchaguzi mdogo kwa ajili ya kuziba mapengo hayo.
MDFA kimekuwa chama cha pili kufanya uchaguzi wake mkuu baada ya awali Chama cha soka Kisarawe, KIDAFA kuchaguana wiki mbili zilizopita, huku vyama vingine viwili vya Rufiji na Mafia vyenyewe zikitarajiwa kufanya Septemba 29 sambamba na kile cha Soka la wanawake mkoa wa Pwani, TWFA.
Chama cha soka Bagamoyo chenyewe kitaitisha uchaguzi wake Oktoba 8, siku chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa COREFA utakaofanyika Oktoba 14 wilayani Mafia.

Mwisho

Kipemba achezwa shere 'trela' la Injinia

Msanii Issa Kipemba
KATIKA hali ya kushangaza kabla filamu yenyewe haijaingizwa sokoni wala kutangazwa itatoka lini, tayari wajanja wachache wameanza kusambaziana 'trela' la filamu ya 'Injinia', kupitia simu za mikononi, huku mwenye filamu hiyo, Issa Kipemba akiwa hana taarifa zozote.
Mwandishi wa habari hizi alifanikiwa kuwaona baadhi ya abiria ndani ya daladala wakirushiana trela la filamu hiyo kupitia simu zao za mikononi na yeye kuomba arushiwe kwa nia ya kuwa na ushahidi wa kutosha kwa kile alichokishuhudia.
Walipododoswa walipoipata 'trela' hilo ambayo filamu yake inahaririwa kwa sasa, abiria hao walidai wamerushiwa na jamaa yao.
MICHARAZO liliwasiliana na Issa Kipemba ambaye ndiye mtunzi na mmoja wa waigizaji wa filamu hiyo kutaka kujua juu ya jambo hilo, alidai hata yeye ameshangazwa na taarifa hizo akidai amekuwa akipokea simu tangu wiki iliyopita juu ya kuonekana kwa trela la filamu hiyo.
Kipemba alisema japo ni kweli alitengeneza 'trela' la filamu hiyo ya Injinia kwa ajili yake mwenyewe na kumpa mmoja wa rafiki yake aliyoiona, cha ajabu limesambaa hata kwa watu ambao hawakuwa na habari juu ya filamu hiyo.
"Kwa kweli wewe ni mtu wa 10 kama sikosei kunipigia simu kuniuliza juu ya jambo hilo, sijajua nani anayesambaza hilo trela, ingawa nililitengeneza kwa ajili yangu binafsi na nikampa mmoja wa watu wangu wa karibu japo sijui kama ndiye aliyesambaza au imevujia wapi," alisema Kipemba.
Mchekeshaji huyo aliyevuma na kundi la Kaole kabla ya kutoweka katika fani miaka nane iliyopita, alisema atachunguza ajue aliyevujisha 'trela' hilo, ili kuweza kumchukulia hatua zinazostahili kwa kuhofia isije 'akaumizwa', hata kabla filamu hiyo haijatoka.
Filamu hiyo ya 'Injinia', iliyoongozwa na Leah Richard 'Lamata' imeshirikisha wakali kama Kipemba, Jacklyne Wolper, Lumole Matovolwa na 'stelingi' Castro Dickson.