STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 10, 2012

Diamond ahukumiwa miezi sina anusurika kwa kulipa faini





MAMIA ya watu waliofurika kushuhudia hukumu ya msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini Naseeb Abdul a.k.a Diamond, walipigwa na butwaa baada ya kuhukumiwa kifungo cha miezi sita jela au kulipa faini ya Sh.50.000 kwa kosa la kumshambulia na kuharibu mali za mwandishi wa habari mkoani Iringa Francis Godwin.
Hatua hiyo imekuja baada ya msanii Diamond na wacheza shoo wake wawili kukiri kosa mbele ya mahakama yeye na wenzake kwa kuharibu Camera mbili, Lap top aina ya Accer pamoja na kumshambulia mwanahabari Francis Godwin Desemba 31 mwaka jana katika uwanja wa Samora mjini Iringa.
Akitoa hukumu hiyo hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Hakimu Masua alisema kulingana na watuhumiwa wote watatu kukiri kosa hilo anawahukumu kwenda jela miezi 6 au kulipa fidia ya shilingi elfu hamsini kila mmoja na huku wakilazimika kumlipa Godwin shilingi elfu 30 kila mmoja na kufanya kufikia kiasi cha shilingi 90000 Wakitoa utetezi wao watuhumiwa hao walisema mahakama iwapunguzia adhabu kwa kuwa hawakukusudia kufanya kosa hilo, na wao walikuja mkoani hapa kwa ajili ya kutoa burudani, na kuwa tukio hilo wamelifanya kwa ghadhabu.
Mheshimiwa Hakimu ninaomba unipunguzie adhabu licha ya kutenda kosa hilo, kwani nakili kuwa nilipatwa na hasira kama binadamu na kuamua kuchukua uamuzi wa kufanya hayo, mimi sikukusudia kuja Iringa kufanya vurugu bali hali hiyo ilikuja baada ya kupata ghadhabu kama walivyo binadamu wengine,” alisema Diamond.
Naye mwanasheria Evaristo Myovela alisema kesi hiyo hakimu ametimiza wajibu wake, huku akimshauri Francis kukata rufaa kama hajaridhika na maamuzi ili kuipeleka kesi hiyo katika Mahakama nyingine kwa kufuata utaratibu wa sheria katika kuchukua maamuzi hayo.
Wakati wanahabari wakijadili juu ya hukumu ya Diamond , mara Waziri wa sera na uratibu wa sheria za bunge Willium Lukuvi alikatiza katika mahakama hiyo ndipo wanahabari wakataka kupata mawazo na uelewa zaidi juu ya hukumu hiyo.
Hata hivyo Diamond alilipa fidia hiyo na kuachiwa huru licha ya Godwin kuamua kupeleka barua mahakamani ya kuomba nakala ya kesi na 13. ya 2012 kwa ajili ya kukata rufaa

VICKY KAMATA ALIVYOMWAGA MISAADA GEITA





Mbunge Vicky Kamata amwaga misaada kwa walemavu, yatima mkoani Geita







MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa Mpya wa Geita, Vicky Kamata, amemwaga msaada wa wenye thamani zaidi ya Sh Milioni 10, unaohusisha vyakula, mavazi, magodoro na viti vya walemavu (wheel chair) 30 kwa wakazi wa tarafa ya Bugando mkoani humo.
Misaada hiyo ambao ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi zake kwa wakazi wa Geita waliomsaidia kuchaguliwa kwake kuwa mbunge kupitia CCM, ulitolewa juzi katika tarafa hiyo na vituo vya kulelea na kutunzia yatima vya Lelea na Feed & Tend International.
Kwa mujibu wa Kamata, misaada hiyo imehusisha viti vya walemavu 30, magodoro 50, maziwa, vyakula na nguo vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Sh. Milioni 10 na kudai ugawaji huo umefanyika kwa awamu ya kwanza na utaendela kwa awamu nyingine mbili.
"Hii ni awamu ya kwanza ya utekelezaji wa ahadi zangu kwa wakazi wa Geita katika kuwasaidia wenye matatizo, natarajia kuendelea na ugawaji kama huo utakaohusisha baiskeli nyingine 50, ambazo tayari zimeshawasili toka nje ya nchi," alisema Kamata.
Mbunge huyo kijana, alisema misaada hiyo na mingine ambayo amekuwa akitoa kwa watu wenye matatizo mkoani mwake inafanywa chini ya mfuko wake wa Victoria Foundation ambayo yeye ni Mwenyekiti wake ikishirikiana na wafadhili wa nje ya nchi.
Alisema ukiondoa utekelezaji wa ahadi zake, lakini misaada hiyo inalenga kuwasaidia watu wenye matatizo waliopo mkoani humo, wanaondokana na adha walizonazo na kufurahia maisha kama watu wengine.

Mwisho