STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 22, 2014

Jahazi la timu ya Babi Malaysia majanga matupu

BAADA ya kugangamala katika mechi yake iliyopita kwa kupata sare ya 2-2 ikitokea kupokea kipigo cha mabao 4-0 katika Ligi Kuu ya Malaysia, timu ya UiTM anayoichezea kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Abdi Kassim 'Babi' imekutana na kiama baada ya kunyukwa mabao 8-0 na Felda United.
Hicho ni kipigo cha kwanza kikubwa kwa timu hiyo ikiwa na Babi aliyewahi kung'ara na timu za Yanga, Azam, Mtibwa Sugar, KMKM na Taifa Stars.
UiTM ilikumbana na pigo hicho uwanja wa ugenini wa Majlis Perbandaran, mjini Selayang baada ya Jumatatu iliyopita kupata sre ya 2-2 kwenye uwanja wake wa nyumbani dhidi ya PBAPP ikitokea ugenini kuchezea kichapo cha 4-0 toka kwa DRB-Hicom.
Katika mchezo huo wa juzi wakati UiTM ikizama kwa 8-0 magoli ya washindi yalifungwa naMohd Raimi katika dakika ya 20, Edward Junior Wilson aliyefunga mawili katika dakika ya  44 na 47 kabla ya Indra Putra Mahayuddin kufunga hat trick kwa magoli ya dakika za 62', 88' na 90 na mengine yakifungwa na '
Ndumba Makeche dakika ya  83' na Mohd Syahid Zaidon dakika moja baadaye.
Kwa matokeo hayo ya juzi, UiTM imeendelea kusaliwa na pointi 21 ikikamata nafasi ya 9 baada ya kushuka dimbani mara 21 mpaka sasa.

Magoli 76 yafungwa Brazili, mbio za kiatu cha dhahabu hatari

van Persie

Benzema
Valencia
Robben

Muiller

WAKATI ngwe ya mwisho ya mechi za raundi za pili zikitarajiwa kufikia tamati leo kwa mechi za Kundi F na H, mpaka sasa jumla ya mabao 76 yamefungwa kwenye Fainali za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini Brazili.
Idadi hiyo imefika baada ya mechi za jana kushuhudia mabao sita yakifungwa katika mechi za kundi G na F ambapo Argentina ya Lionel Messi iliifunga Iran bao 1-0, Ghana na Ujerumani kutoshana nguvu kwa kufungana mabao 2-2 na Nigeria kuizodoa Bosnia ya Edin Dzeko kwa bao 1-0.
Mpaka sasa nyota kadhaa wanafukuzana kwenye mbio za kuwania kiatu cha Dhahabu wakiongoza wakiwa na mabao matatu kila mmoja na wengine wakifuata wakiwa na magoli mawili mawili.
Wachezaji wanaoongoza katika orodha hiyo ni Karim. Benzemawa Ufaransa, Thomas  Mueller wa Ujerumani, Enner Valencia wa Ecuador na Arjen Robben na Robin  van Persie wote wa Uholanzi.
Wachezaji wenye mabao mawili kila mmoja mpaka sasa ni pamoja na Tim  Cahill wa Australia, Neymar wa Brazili, Gervinho wa Ivory Coast, Lionel Messi wa Argentina, James Rodriguez wa Colombia, Luis Suarez wa Uruguay na Mario Mandzukic wa Croatia, wakifuatiwa na utitiri wa waliofunga bao moja moja.

Orodha kamili ya wafungaji;
 3-Karim. Benzema- France
Thomas  Mueller-Germany
Arjen Robben-Netherlands
Enner Valencia-Ecuador
Robin  van Persie-Netherlands

2-Tim  Cahill-Australia
Neymar- Brazil
Gervinho-Côte d'Ivoire
Mario Mandžukić-Croatia
Lionel Messi-Argentina
James Rodríguez-Colombia
Luis Suárez-Uruguay
Msimamo wa makundi:
Kundi A
                  P W D L F A PTS

Brazil          2  1  1  0  3  1  4
Mexico       2  1  1  0  1  0  4
Croatia       2  1  0  1  5  3  3
Cameroon  2  0  0  2  0  5  0

Kundi B
                    P W D L F A PTS

 Uholanzi       2  2  0  0  8  3  6
Chile            2  2   0  0  5  1  6
Australia       2  0   0  2  3  6  0
Hispania       2  0  0  2  1  7  0

Kundi C
                     P  W  D  L  F  A  PTS

 Colombia      2   2   0   0  5  1    6
Ivory Coast   2   1   0   1   3  3   3
Japan            2   0   1   1   1  2   1
Ugiriki           2   0   1   1   0  3   1   

Kundi D
                       P  W  D  L F A PTS

Costa Rica      2    2  0  0  4  1  6
Italia                2    1  0  1  2  2  3
Uruguay          2    1  0  1  3  4  3
England           2    0  0   2  2  4  0

Kundi E
                       P W D L F A PTS

Ufaransa          2  2  0  0  8  2  6
Ecuador           2  1  0  1  3  3  3
Uswisi              2   1  0  1  4  6  3
Honduras         2   0  0  2  1  5  0  

Kundi F
                             P W D L F A PTS

Argentina               2  2  0  0  3  1  6
Nigeria                  2  1  1  0  1  0  4
Iran                       2  0  1  1  0  1  1
Bosnia-Herze.       2  0  0  2  1  3  0

Kundi G
                           P W D L F A PTS

Ujeruman            2  1  1  0  6  2  4
Marekani            1  1  0  0  2  1  3
Ghana                 2  0  1  1  3  4  1
Ureno                 1  0  0  1  0  4  0

Kundi H
                  P W D L F A PTS

Belgium      1  1  0  0  2  1  3
Korea        1  0  1  0  1  1  1
Russia        1  0  1  0  1  1  1
Algeria       1  0  0  1  1  2  0

RATIBA :
LEO, Jumapili
Ubelgiji     v Russia        (1:00)
Korea Kusini     v Algeria    (4:00)
Marekani        v Ureno        (7:00)

KESHO, Jumatatu
Australia     v Hispania    (1:00)
Uholanzi     v Chile        (1:00)
Cameroon     v Brazili    (5:00)
Croatia        v Mexico        (5:00)

KESHOKUTWA, Jumanne

Costa Rica     v England    (1:00)
Italia         v Uruguay    (1:00)
Ugiriki         v Ivory C    (5:00)
Japani         v Colombia    (5:00)

JUMATANO, Juni 25
Bosnia        v Iran        (1:00)
Nigeria         v Argentina    (1:00)
Ecuador         v Ufaransa    (5:00)
Honduras     v Uswisi        (5:00)

ALHAMISI, Juni 26
Ureno        v Ghana        (1:00)
Marekani        v Ujerumani    (1:00)
Algeria        v Russia        (5:00)
Korea Kusini     v Ubelgiji    (5:00)

Watu 10 wauwawa nchini Nigeria

Kiongozi wa kundi la Boko Haram, Abubakar Shekau
TAKRIBAN watu kumi wameuawa katika shambulizi la kijiji kimoja kazkazini mashariki mwa Nigeria,karibu na eneo ambalo zaidi ya vijana 200 walitekwanyara mnamo mwezi Aprili.
Wakaazi wanasema kuwa watu waliojihami walivamia kijiji cha Korongi-nim kilichopo takriban kilomita 14 kutoka Chibok ambapo wasichana hao walitekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram.
Kiongozi moja wa eneo hilo ameiambia BBC kwamba wanamgambo hao walikichoma kijiji chote cha Koronginim.
Ripoti pia zinaarifu kuwa kundi hilo limedaiwa kuwatekanyara wanaume na wasichana kutoka kijiji chengine katika jimbo la Yaza siku ya alhamisi.
BBC