STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 22, 2014

Manji awapa mtihani mgumu wanaompinga Yanga

bejo
Mwenyekiti wa Klabu ya Young Africans Bw Yusuf Manji amesema wanachama wanaopinga maamuzi ya mkutano mkuu uliofanyika Juni Mosi 2014 katika Bwalo la Polisi Osyterbay ya kuwaongezea muda wa mwaka mmoja, wafike makao makuu ya klabu na kujiorodhesha majina yao kwa Katibu Mkuu.
 
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu, Manji amesema sisi sote tunajenga nyumba  hatuna haja ya kugombania fito, wanaopinga maamuzi yale ni vyema wakajiorodhesha majina yao ili kuweza kupata idadi yao na kama itafikia idadi ya waliohudhuria mkutano ule watu 1522 basi tutaitisha mkutano mwingine.
 
Vyombo vya Habari vimekua vikiripoti kuwa baadhi ya wanachama hawakubaliani na maamuzi ya mkutano mkuu, na mie ni mfuata Demokrasia namuagiza Katibu Mkuu kuweka reja hapa makao makuu kwa siku 5 kuanzia jumatatu mpaka ijumaa saa 11 jioni hivyo wale wote wanaosema/wanaopingana na maamuzi ya mkutano mkuu wapate kujioorodhesha.
 
Pili kwa yoyote ambaye anaona anaweza kuiongoza Yanga kwa sasa milango iko wazi, anaweza kufika makao makuu na kuongea na katibu mkuu kisha anaweza kunadi sera zake/kuongea na waandishi wa habari na baadae tutapeleka jina lake kwa Bodi ya Wadhamini wakiridhika nitaitisha mkutano mkuu wa Uchaguzi.
 
Zoezi la kujiorodhesha wanachama makao makuu litakua na usalama wa kutosha kutoka kwa jeshi la Polisi ambapo patakua na askari wa usalama watakao kuwa wakilinda usalama wa wanachama wanaofika kujiorodhesha kwenye reja hiyo.
 
Jumamosi ijayo Katibu Mkuu atatoa ripoti ya idadi ya wanachama walijiorodhesha kwenye reja na kama idadi ifikia 1522 kama ya waliohudhuria mkutano mkuu basi uongozi utaitisha upya mkutano mkuu, na kama idadi yao haitafikia baadhi demokrasia itatawala kwa kufuata maamuzi ya watu wengi.
Chanzo: Tovuti ya Yanga

No comments:

Post a Comment